Kitokeacho Baada ya Mwanamke Kumfumania Mumewe

busness

Member
May 1, 2014
27
9
Kuna kautafiti nimefanya nikagundua kwenye mahusiano kuna mambo mengi ikiwemo kuchepuka. Cha kushangaza wanawake wengi pindi wafumaniapo waume zao utamwona anakurupuka na kumvagaa mke/binti anaye kutwa naye.

Hii ni tofauti kwa wanaume akifumania mkewe mara nyingi anatoa adhabu kwa mkewe si kwa aliye mfumania.

Je hii ni sawa na kusema adui wa mwanamke ni mwanamke?

Au naombeni ufafanuzi kiroho safi.
 
Simple, mara nyingi mwizi wa mwanamke ni mtu yuko nae close!! So anampiga mwanamke mwenzie coz alijifanya rafikiye kumbe anamuibia mumewe
 
Hili suala hadi nichepuke kwanza ndo nitakuja kujibu lakini awali ya yote hakutakua na "uaminifu"
 
Kuna kautafiti nimefanya nikagundua kwenye mahusiano kuna mambo mengi ikiwemo kuchepuka. Cha kushangaza wanawake wengi pindi wafumaniapo waume zao utamwona anakurupuka na kumvagaa mke/binti anaye kutwa naye.

Hii ni tofauti kwa wanaume akifumania mkewe mara nyingi anatoa adhabu kwa mkewe si kwa aliye mfumania.

Je hii ni sawa na kusema adui wa mwanamke ni mwanamke?

Au naombeni ufafanuzi kiroho safi.

Sio kweli

Huu utafiti wako ni uongo

Kila uchao tunaona Wanaume wanachinjana kisa tu amemfumania mkewe

Watu wanaingiliwa kinyume na maumbile kwa kufumaniwa na waume za wake waliowafumania nao halafu wewe unaleta hapa hii ndoto yako!
 
Kwa mawazo yangu, japo haimaanishi nafurahishwa na kitendo cha watu kufumaniana au kuchepuka.

Nafikiri ikitokea umemfumania mwenzi wako, hangaika na mkeo/mmeo na wala sio yule uliyemkuta nae.

Huenda mtu kadanganya hajaolewa au hajaoa, kwa nini niangaike na huyo ambae sina mkataba nae? Hata nikimpiga haisaidii kitu.
 
Sion umuhimu wa kupiga chepuko....
Hujui alichomwambia au kumdanganya huenda alimwambia Sina mume/ mke

Beba mumeo/ mkeo baada ya kumfumania nenden nyumban
 
Mhhh Best atarudia tena huyo

Harudii tena ukimya unaumiza zaid ya kibano

Kuna mdada alifumaniwa mumewe hukuongea lolote zaid ya kumwambia twende nyumban nakupenda mke wangu
kesho ake jamaa kaacha pesa ya matumiz kaishia zake job jion karud kakuta mwanamke kaondoka

Heeee mke alijipa talaka mwenyewe akaondoka kwao
 
Sion umuhimu wa kupiga chepuko....
Hujui alichomwambia au kumdanganya huenda alimwambia Sina mume/ mke

Beba mumeo/ mkeo baada ya kumfumania nenden nyumban
Kama hakujua sawa lakini ambaye hakujua utamuona tu maana mwenyewe hatokuwa na raha na huyo mwanaume, mtamchangia wote huyo mwanaume. Ila kuna michepuko mingine haina ustaarabu. Si umenyamaza ukasema mkamalizane na mumeo, yeye anaona umemuogopa. Basi simu mpaka usiku anapiga hana wasiwasi. Kimada kinatawala kama ndo mke. Saa nyingine inabidi kukitishia kijue kama bwai na iwe bwai bwana, some things are off limit. Ukimwachia sana itakula kwako kumbuka mume yeye anapenda kula kote kote so hawezi kumkoromea kivile. Aibe sawa, lakini ndo ajue yeye ni mwizi na akikutwa lazima asepe kabla haijawa noma
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom