Kitengo cha Pension Hazina Rais Magufuli akimulike

Mshangai

JF-Expert Member
Feb 16, 2008
468
1,086
Moja ya vitengo vilivyo sahauliwa na kuleta mateso kwa watumishi wa Umma waliotumikia nchi hii kwa uadilifu mkubwa ni PENSION SECTION pale Wizara ya Fedha.

Kitengo hiki ukianzia pale Registry hadi katika kuandaa malipo ni kero kubwa sana. Watu hawawajibiki na wamejawa na dharau kwa vile wanahudumia wazee ambao wanaona hawana uwezo wa kuwafanya kitu tena.

Registry kuna wamama pale wanaweza kupokea claim za watu na kukaa nazo hata miezi miwili eti faili halionekani na hawajali kitu. Jee huo ndio utendaji wa awamu ya tano? Au ni kwa vile waziri Mpango ni mpole sana hivyo hajihusishi na yanayoendelea kitengo hicho?

Au Katibu mkuu wa Fedha naye anaona kitengo hicho ni kama kushughulikia maiti? Ikumbukwe hao wanaodharauliwa kama maiti ndio walio jitoa kutumikia nchi hadi kuifikisha hapa ilipo na wengi wao hawakuwa mafisadi ndio maana kwao pension wanaiona ni heshima kwao japo ni ndogo.

Majuzi nimeenda pale kushughulikia mzee wangu mgonjwa sasa lakini nikajiuliza mbona Magufuli alikomesha utendaji wa aina hii Muhimbili na idara zingine kwa nini hapa Pension Hazina mambo ni kama yale ya zamani?

Umefika wakati sasa tuwataje kwa majina watumishi wa pale Pension ambao wanasumbua wazee na kuwataka wengine watoke huko mikoani kuja hapo kufuatilia visenti vyao ilihali kila kitu kipo na kingeweza kufanyika bila ya wao kuja.

Dr Mpango kama umeshindwa basi tumuite Magufuli atembelee hapo ajionee jinsi pending za kazi zilivyo na UTUKUFU wanaojifanya wanao watumishi husika.
 
Pension ni tatizo linaendelea kuota sugu. Mfano pspf huko ndio imekuwa balaa,wastaafu wanakaa zaidi ya miezi 6 kusubilia mafao yao. Viambatanisho vyote vimekamilika kabla ya kustafu na vipo lakini bado usumbufu huu niwa nini.
 
Pension ni tatizo linaendelea kuota sugu. Mfano pspf huko ndio imekuwa balaa,wastaafu wanakaa zaidi ya miezi 6 kusubilia mafao yao. Viambatanisho vyote vimekamilika kabla ya kustafu na vipo lakini bado usumbufu huu niwa nini.
Ni bora huko PSPF ambako kunajulikana hali ya kifedha sio nzuri na pia pamoja na kuchelewesha malipo bado kuna lugha nzuri. Usiombe Pension section ya Hazina mkuu! Kila mtu ana majibu yake tena ya kebehi hakuna mfano.
Kutafutiwa faili hasa kwa watumishi wa zamani ni kama mtu anaomba kufufua maiti. Hili jambo nimepanga kulifikisha kwa Katibu mkuu mwenyewe pamoja na majina ya watumishi wasiofuata maadili ya kazi zao na kuleta mateso kwa wengine.
Hawa sifa waliyo baki nayo ni KUFUKUZWA kazi tuu
 
Saidia watanzania wenzako wanaoteswa na hawa wanaojiona miungu watu,chukua hatua tusiishie hapa jf pekee.
 
Hapo nomaa mkuu sie mzee wetu kafa tumelipwa milioni tisa tu na mtu katumikia taifa kwa miaka 40, kafikia cheo cha kamishna msaidizi.
 
hao wahudumu hawajui nao ipo siku watastaafu na watasumbuliwa kupata haki yao
 
na hawa Azania nao ni jipu japo sio serikali!!!

Habarini za mchana wananchi wa inji hii. Hii benki yetu ya Azania sasa inaelekea kuwa "Jipu" kwa sisi wateja. Imekuwa na matatizo makubwa ya network karibu kila siku lakini leo hakuna network tangu asubuhi haijafanya kazi na hakuna mteja aliyeweza kutoa senti tano wala kujya salio lake. Huwezi kutazama salio wala kuchukua pesa. Si kwenye ATM, si kaunta. Unaweza kuweka tu lakini watakuingizia pesa baadaye.

Nadhani kuna tatizo lililojificha nyuma ya hili. Hakuna anayewaambia w...ateja jambo lolote na wateja wanakwenda na kurudi wakinung'unika bila chembe ya wafanyaiazi kuonesha kujali.

Benki Kuu iwamulike haraka na ikibidi warekebishe hali hii kama ilivyokuwa kwa Benki nyingine pale Samora Avenue (Twiga Bancorp).

Benki kadhaa zinatumia Umoja Switch lakini ni wateja wa Azania tu wamekuwa wanasuffer kila siku. BOT chungulieni pale. Mtagundua mengi zaidi yaliyofichika nyuma ya pazia.

Kwa hali hii ni ngumu sana wateja kuwashauri ndugu, jamaa na marafiki wajiunge na huduma za benki za aina hii.
 
hao wahudumu hawajui nao ipo siku watastaafu na watasumbuliwa kupata haki yao
Kuna watu wanapenda kujenga tabia mbaya tuu. Muhimu ni kuwafichua kwa uwazi tuu ili wafukuzwe kazi kabisa wasipate hata nafasi ya kulipwa pension ili wajue thamani ni mtu ni utu.
Hawana huruma kabisa utadhani ni wanyama na bahati mbaya hata wakubwa wao hawajui kitu gani kinaendelea kitengo hicho maana wanakiona kama motuary ya watumishi
 
Kuna watu wanapenda kujenga tabia mbaya tuu. Muhimu ni kuwafichua kwa uwazi tuu ili wafukuzwe kazi kabisa wasipate hata nafasi ya kulipwa pension ili wajue thamani ni mtu ni utu.
Hawana huruma kabisa utadhani ni wanyama na bahati mbaya hata wakubwa wao hawajui kitu gani kinaendelea kitengo hicho maana wanakiona kama motuary ya watumishi

Kumbe tunakiri JPM hakurupuki.Akichukua hatua kuna watu wanaanza kulia haki za binadamu,fuata taratibu.Unafuatwa na mtu mzima mwenye umri sawa na baba au mama yako kwa jambo lililo haki yake unataka akupigie magoti,ukifukuzwa unalia.JPM usilegeze Kamba.Mh.Dr.Mpango wapuuzi hawa wasichafue sifa zako.Agiza tu uchafu utoke utatoka.
 
Usipende kutumia neno"wametumikia taifa kwa uadirifu". Watanzania wengi ni mafisadi, hao unaowasema ungewakuta enzi zao ofisini ungejua
 
Usipende kutumia neno"wametumikia taifa kwa uadirifu". Watanzania wengi ni mafisadi, hao unaowasema ungewakuta enzi zao ofisini ungejua
Kwa hiyo unaunga mkono vitendo vya unyanyasaji wanavyofanyiwa wazee wastaafu kwa vile unadhani nao walikuwa ni mafisadi? Hivi kweli mtu aliyekuwa fisadi anaweza kwenda toka Bukoba hadi Dar kusotea kwa wiki kadhaa shilingi milioni 10? Think again!
 
Watumishi hao wachunguzwe na kama kweli wana tabia hizo wapewe adhabu zinazowastahili ikiwepo kufukuzwa kazi kama inavyotokea katika sekta zingine. Mambo ya kufanya kazi kwa mazoea hayapo sasa hivi.
 
Tusiwahukumu moja kwa moja nahisi wengine wanataka njia za mkato kupata pension zao au wapendwa wao. tatizo tukiambiwa vielelezo vyote vikamilike tunaanza kulalamika kuwa tunaonewa! Nao hao staff wa kitengo cha pension huenda wanaogopa wasije kuwalipa 'wastaafu hewa' wakatumbuliwa, lazima wajiridhishe jamani tuache mihemko!
 
Tusiwahukumu moja kwa moja nahisi wengine wanataka njia za mkato kupata pension zao au wapendwa wao. tatizo tukiambiwa vielelezo vyote vikamilike tunaanza kulalamika kuwa tunaonewa! Nao hao staff wa kitengo cha pension huenda wanaogopa wasije kuwalipa 'wastaafu hewa' wakatumbuliwa, lazima wajiridhishe jamani tuache mihemko!
Kwa hiyo hata hizo lugha za dharau na kukaa na pending bila kuzifanyia kazi muda mrefu ni kutaka vielelezo? Kwanza uhakiki huo huwa unafanywa na maofisa walioko katika ofisi za Sub Treasure huko mikoani sasa sababu ya ucheleweshaji huko ni dhaifu. Usikute wanataka rushwa kutoka kwa hao wazee.
 
Hili jambo limezungumzwa leo sana PB clouds. Kumbe fedha zinadaiwa waziwazi na hakuna anayejali. Dr Mpango tunajua kuna mengi yanakushinda lakini hata hili huwezi kulipatia credit?
 
Ni bora huko PSPF ambako kunajulikana hali ya kifedha sio nzuri na pia pamoja na kuchelewesha malipo bado kuna lugha nzuri. Usiombe Pension section ya Hazina mkuu! Kila mtu ana majibu yake tena ya kebehi hakuna mfano.
Kutafutiwa faili hasa kwa watumishi wa zamani ni kama mtu anaomba kufufua maiti. Hili jambo nimepanga kulifikisha kwa Katibu mkuu mwenyewe pamoja na majina ya watumishi wasiofuata maadili ya kazi zao na kuleta mateso kwa wengine.
Hawa sifa waliyo baki nayo ni KUFUKUZWA kazi tuu
Weka majina yao hao watumishi mizigo wanokwamisha pension za waliomtangulia, ujumbe utamfikia magufuli.
 
Back
Top Bottom