Kitengo cha habari CHADEMA mmelala sana, mnastahili lawama

Dullo

JF-Expert Member
Oct 24, 2009
251
64
Hivi hawa CHADEMA hawana kitengo cha habari? Mimi nashindwa kuelewa kwanini hawatoi picha kutoka katika mikutano yao ambayo watu wengi wanapenda kuona na kufahamu kinachoendelea katika mikutano hiyo, yaani ukitaka kupata picha unahangaika sana na wakati mwingine hatupati picha hata moja kutoka katika mikutano hiyo.

Cha kushangaza zaidi wanakuwa wanazunguka na waandishi na kuwalipa posho wakati wangekuwa wanatembea na Blogger mmoja ambapo akawa anatoa picha kwa wakati maana watu tunakuwa na hamu ya kuona kinachoendelea lakini hatupati.

Ushauri kwa Viongozi wa CHADEMA ni bora wakawa na Bloggers wakawa wanatoa picha kwa wakati kuliko kutembea na kundi la waandishi ambao habari zao zinapatikana siku ya pili bila ya kuwa na picha za kutosha. Hebu jaribuni kujifunza toka kwa Serengeti Breweries, Tigo na Vodacom ambao mara nyingi picha zao zinapatikana kwa wingi sana na kutoa coverage za kutosha.

Jamani jitahidini mtupatie picha za kutosha kutoka mikutano yenu.
 
Nakubaliana na wewe, Mh.Regia alikuwa mstari wa mbele sana wakati CHADEMA wakifanya ziara Lake zone, lakini anatusikitisha sana kwa kutowatendea haki wana-kanda ya kusini kwa sasa, yawezekana Mh.Regia alibaka wajibu wa chombo kingine ndani ya CDM matokeo yake kumekuwepo na ubishani juu ya nani atoe taarifa na picha.

CDM hamtutendei haki wanachama na wakereketwa wa CDM. Tafadhali onyesheni tofauti yenu na CCM ktk kutoa habari.
 
Silalamiki ila nataka kuonyesha kwamba tunahitaji kuona wanaangalia kwa mapana zaidi kitengo cha habari maana tunahitaji sana kupatikana kwa picha zao, maana kazi yetu sie ni kuwakumbusha wanapokuwa wanajisahau.
 
Dullo,

Naomba utusaidie kwa kufanikisha hili.......badala ya kulalama
Hajalalamika mkuu, anachoongea nadhani yupo sahihi.

CDM naona Regia anajitahidi yeye kuwa ana-update hapa JF panapokuwa na issues lakini sidhani kama alitakiwa yeye kubeba msalaba huu.

Chama kina ruzuku, kusaidiwa kwa sasa wasidhani ni jambo la kukimbilia, badala yake watumie resources wanazopata kuhakikisha habari na picha vinasambaa haraka.

Vipi mbona humshauri akajitolee kuwasaidia CCM? Hii kuwashtua CDM pekee ni msaada mkubwa, yawezekana CDM wanajiona wanavyofanya ni sahihi lakini uhalisia ndio huu, wanajisahau sana
 
Hivi hawa CHADEMA hawana kitengo cha habari? Mimi nashindwa kuelewa kwanini hawatoi picha kutoka katika mikutano yao ambayo watu wengi wanapenda kuona na kufahamu kinachoendelea katika mikutano hiyo, yaani ukitaka kupata picha unahangaika sana na wakati mwingine hatupati picha hata moja kutoka katika mikutano hiyo.

Cha kushangaza zaidi wanakuwa wanazunguka na waandishi na kuwalipa posho wakati wangekuwa wanatembea na Blogger mmoja ambapo akawa anatoa picha kwa wakati maana watu tunakuwa na hamu ya kuona kinachoendelea lakini hatupati.

Ushauri kwa Viongozi wa CHADEMA ni bora wakawa na Bloggers wakawa wanatoa picha kwa wakati kuliko kutembea na kundi la waandishi ambao habari zao zinapatikana siku ya pili bila ya kuwa na picha za kutosha. Hebu jaribuni kujifunza toka kwa Serengeti Breweries, Tigo na Vodacom ambao mara nyingi picha zao zinapatikana kwa wingi sana na kutoa coverage za kutosha.

Jamani jitahidini mtupatie picha za kutosha kutoka mikutano yenu.

picha za chadema ziko moyoni na akilini mwangu.

picha zengine ni furahisha macho tu.

lakini ni wazo zuri
 
Tayari dalili za CDM kulewa sifa zimeanza kushika kasi, ni aibu kwa chama kinachojijenga kushindwa kutoa taarifa kwa walengwa, yawezekana pia CDM wameanza kulewa na muitikio wa watu kwenye mikutano huku wakijisahau walengwa wanaohitaji kupata elimu juu ya CDM wanahitaji picha, habari, nyimbo na vyombo vingine vinavyoweza kufikisha ujumbe.

Wakumbuke kuwa wtanzania wanapitia sana internet kwa sasa kiasi kwamba kila taarifa zinazotoka ktk mtandao wakuwa nazo mapema na hivyo kutowafanya CCM waweweseke. Please fikisha ujumbe kwa wakati
 
Naungana na mleta hoja..........CHADEMA you need to wake up now!
 
CCM Mafisadi siwapendi, lakini nawaheshimu sana katika kutafuta udhaifu wa chama pinzani, CDM walituahidi kuwa watatwanga kote kote, lakini inaonekana wanatwanga kwenda mbele tu. Wanasahau kuwa wanayoyafanya mikoani wanatakiwa walete feedback hapa jijini kwa njia ya Photos na taarifa kwa njia ya internet ili na sisi tuwasambazie wengine duniani, siasa za leo ni universal kuna watanzania wako Ulaya na Marekani wanapataje taarifa bila kutupatia soft copies za matukio?

WAKE UP CDM. Tunaamini wengi wengi wenu no dot.com generation, Mh.Regia ni shahidi wa dot com
 
Habari ni kitu muhimu sana ktk kutangaza kitu.

Cha msingi kama wapo wadau wa Chadema humu ndani JF ujumbe umefika mkalifanyie kazi
 
Hajalalamika mkuu, anachoongea nadhani yupo sahihi.

CDM naona Regia anajitahidi yeye kuwa ana-update hapa JF panapokuwa na issues lakini sidhani kama alitakiwa yeye kubeba msalaba huu.

Chama kina ruzuku, kusaidiwa kwa sasa wasidhani ni jambo la kukimbilia, badala yake watumie resources wanazopata kuhakikisha habari na picha vinasambaa haraka.

Vipi mbona humshauri akajitolee kuwasaidia CCM? Hii kuwashtua CDM pekee ni msaada mkubwa, yawezekana CDM wanajiona wanavyofanya ni sahihi lakini uhalisia ndio huu, wanajisahau sana
Kwa kifupi hao watu kama wapo they need to be fired immediately. CDM need to think of this very fast, mfano kufanya live internet broadcasting ya mikutano yao itawagharimu sh. ngapi? Au wanasubiri wawe wanatokea bure TBC na ITV? Ilitakiwa kitengo hicho pia kiwe na kina Nape wakati huo huo wako na akina Slaa. Mnafanya instant reporting huku na kule hata kabla wao hawajaingia hewani.

Another opportunity ni kuanza kutengeneza clips kwa kuanzia ziwekwe you tube... Mfano hii juzi JK alivyosema maneno ya Nape ni yake pia what an opportunity? Zingetengenezwa clip za kutosha mpaka sasa. Namna hii watacontrol hata namna wapinzani wao wanavyosema. They would need to think twice.
 
Nakushukuru sana mleta mada,

Chadema waamke wajue dunia sasa ni kijiji. Kinachoendelea mikoani na vijijini duna inatakiwa ijue.Napenda wakiongezee nguvu kitengo cha habari Chadema.

Inavyoonekana mkuu wa kitengo hiki Erasto Tumbo kazidiwa majukumu. Napendekeza aongezwe Regia Mtema katika idara hii. Kwani ndiye amekuwa akifanya kazi kama mkuu wa idara hii kwa muda mrefu sasa........
 
CHADEMA wako sahihi kutembea na waandishi wa habari, vyombo vya habari vya Tanzania vina nguvu ya coverage kuliko hizo blogs unazozifikiria.

Magazeti na redio yanafika mbali na yana impact kubwa kuliko hizo blogs. Wasipotembea na waandishi hawatapata coverage kwenye magazeti
ukiwa unafikiria siasa za tz lazima ujaribu kuifikiria kitanzania zaidi na siyo ki-ulaya ulaya. Very few people have got access to internet na hata kati ya hao wenye access na internet ni % ndogo tu wanatumia internet.

Wazo lako sio baya ila ningependa kulifanyia marekebisho kidogo kama utaniruhusu', viongozi wa chadema wangekuwa na camera kila kwenye mikutano yao wanawapa watu wanaombatana nao wapige picha halafu mikutano ikiisha wanazi upload kwenye website ya chadema. Zitto anafanya hivyo na huwa ana upload kwenye blog yake
 
Kila mtu ana wajibu katika kusaidia katika kuleta harakati hizi, Tanzania pia kama vipi wote kuna wajibu wa kuwasaidia CHADEMA
 
CHADEMA wako sahihi kutembea na waandishi wa habari, vyombo vya habari vya Tanzania vina nguvu ya coverage kuliko hizo blogs unazozifikiria.

Magazeti na redio yanafika mbali na yana impact kubwa kuliko hizo blogs. Wasipotembea na waandishi hawatapata coverage kwenye magazeti
ukiwa unafikiria siasa za tz lazima ujaribu kuifikiria kitanzania zaidi na siyo ki-ulaya ulaya. Very few people have got access to internet na hata kati ya hao wenye access na internet ni % ndogo tu wanatumia internet.

Wazo lako sio baya ila ningependa kulifanyia marekebisho kidogo kama utaniruhusu', viongozi wa chadema wangekuwa na camera kila kwenye mikutano yao wanawapa watu wanaombatana nao wapige picha halafu mikutano ikiisha wanazi upload kwenye website ya chadema. Zitto anafanya hivyo na huwa ana upload kwenye blog yake
Mkuu unachoongea ni sahihi kabisa lakini kumbuka ukifanya live broadcasting unatoa nafasi hata kwa redio Ngara, au gazeti la kigoma au TV ya Peramiho kukunukuu exactly ulivyosema.

Cha msingi ni kutengeneza official site which can be reffered to. Tena this is cheaper kuliko hata kutembea na hao waandishi ambao sometimes ni hodari wa kupindisha habari iwe kusudi au bahati mbaya.
 
Semilong nimekuelewa lakini na nimependa comment zako lakini katika upigaji wa picha nitapingana nawe kwani hiyo nayo ni taaluma inabidi wawe na wataalam wa kupiga picha!! lakini tuko pamoja!!
 
picha za chadema ziko moyoni na akilini mwangu.

picha zengine ni furahisha macho tu.

lakini ni wazo zuri

Ukiona umefikia hali hiyo basi ujue umekua kichaa,.. Kauli za "mimi ni mwanachama damu" sijui wa chama gani ni utumwa! Hautaruhusu kifikiri hata siku moja,kisa ni damu yako,...

Chadema wanafanya uzembe na kuna mtu aliwahi kuwaambia wasipotumia nafasi hii ipasavyo kutokana na vyombo vya habari na media mbali mbali kuwavuta vijana na wasomi hawata pata nafasi kama hii tena!

Unadhani CCM hawapendi kuweka picha zao humu? CUF je?

Lakini hazina mvuto sasa, CHADEMA mnajua na Marando aliwahi waambia (indirectly)kwamba chama cha siasa kinazaliwa, kinakua na kinakufa,... CHADEMA mnakua sasa hivi lakini hamtumii kukua kwenu vizuri, mtakufa haraka kwani kiu ya watu kupata habari kwa undani hamuikati,... siku kiu ikiondoka, mkaanza kubandika updates zenu hapa itakuwa too late!
 
Semilong nimekuelewa lakini na nimependa comment zako lakini katika upigaji wa picha nitapingana nawe kwani hiyo nayo ni taaluma inabidi wawe na wataalam wa kupiga picha!! lakini tuko pamoja!!

kabisaaaa,..
Chuo kinafundisha watu kushika kamera,... ku-upload images kwenda mtandaoni kabisaaaa?

Chuo gani hiko kinatoa taaluma ya namna hiyo? So huko kwenye maadamano woote hawajui kushika kamera ni regia tu?haha
 
Mkuu unachoongea ni sahihi kabisa lakini kumbuka ukifanya live broadcasting unatoa nafasi hata kwa redio Ngara, au gazeti la kigoma au TV ya Peramiho kukunukuu exactly ulivyosema. Cha msingi ni kutengeneza official site which can be reffered to. Tena this is cheaper kuliko hata kutembea na hao waandishi ambao sometimes ni hodari wa kupindisha habari iwe kusudi au bahati mbaya.
NIliwahi kutoa suggestion ya chadema ku-redesign website yao na kuwa wanatoa updates kwa kila wanacho fanya hapa,..

Kwamba wajitofautishe na Chama Cha Magamba kwani website yao ni hovyoooo,...lakini wapi; wote CCM na CHADEMA wanazidiwa hata na CUF!
 
Back
Top Bottom