Dullo
JF-Expert Member
- Oct 24, 2009
- 251
- 64
Hivi hawa CHADEMA hawana kitengo cha habari? Mimi nashindwa kuelewa kwanini hawatoi picha kutoka katika mikutano yao ambayo watu wengi wanapenda kuona na kufahamu kinachoendelea katika mikutano hiyo, yaani ukitaka kupata picha unahangaika sana na wakati mwingine hatupati picha hata moja kutoka katika mikutano hiyo.
Cha kushangaza zaidi wanakuwa wanazunguka na waandishi na kuwalipa posho wakati wangekuwa wanatembea na Blogger mmoja ambapo akawa anatoa picha kwa wakati maana watu tunakuwa na hamu ya kuona kinachoendelea lakini hatupati.
Ushauri kwa Viongozi wa CHADEMA ni bora wakawa na Bloggers wakawa wanatoa picha kwa wakati kuliko kutembea na kundi la waandishi ambao habari zao zinapatikana siku ya pili bila ya kuwa na picha za kutosha. Hebu jaribuni kujifunza toka kwa Serengeti Breweries, Tigo na Vodacom ambao mara nyingi picha zao zinapatikana kwa wingi sana na kutoa coverage za kutosha.
Jamani jitahidini mtupatie picha za kutosha kutoka mikutano yenu.
Cha kushangaza zaidi wanakuwa wanazunguka na waandishi na kuwalipa posho wakati wangekuwa wanatembea na Blogger mmoja ambapo akawa anatoa picha kwa wakati maana watu tunakuwa na hamu ya kuona kinachoendelea lakini hatupati.
Ushauri kwa Viongozi wa CHADEMA ni bora wakawa na Bloggers wakawa wanatoa picha kwa wakati kuliko kutembea na kundi la waandishi ambao habari zao zinapatikana siku ya pili bila ya kuwa na picha za kutosha. Hebu jaribuni kujifunza toka kwa Serengeti Breweries, Tigo na Vodacom ambao mara nyingi picha zao zinapatikana kwa wingi sana na kutoa coverage za kutosha.
Jamani jitahidini mtupatie picha za kutosha kutoka mikutano yenu.