Kitenge Pande Nne!

Rev. Kishoka

JF-Expert Member
Mar 7, 2006
4,526
1,529
Kila kukicha kunafunuliwa jipya kuhusu Ufisadi na kigugumizi cha Chama Twawala kushika hatamu na kuwajibika.

Butiama tumekwenda, tumefuta mwafaka, tukamhani Julius, tukaunyamazia uhujumu, tukaapiana kushikamana, tukumbushane Mei, kujipanga kula kupya.

Left and right you hear same stories of Uhujumu. Sasa kisima kingine cha pesa za umma Benki ya Posta kimevumbuliwa, lakini kila siku CCM wako kimya.

Je wako wapi wale wanaojiita CCM Safi? Kwa nini mnaendelea kulelea Uhujumu, Ufisadi, Uzembe na kukosekana na Uwajibikaji? Ikiwa mnakerwa na Udhalimu, inakuwaje mnaendelea kukumbatiana na Madhalimu?

Mama Kilango, Mwakyembe, Seleli, na wengine mliopigia baragumu Richimondi na na uhakika mnanguruma chinichini kuhusu EPA, Chenge na uhujumu mwingine. Kwa nini mnaendelea kuwa wanachama na waumini wa Chama ambacho kinakataa kujisafisha kwa dharura na kwa maendeleo kwa manufaa ya Taifa?

Je viapo vyenu vya Utii kuitii Katiba ya Tanzania vimekwenda wapi? Au ni kiapo cha kuitii CCM na maslahi yake kwanza? Mwamkiri mwamkubali na kumtumikia Shetani na mambo yake yote? Mmelewa mvinyo gani mpaka kila siku na kila saa mnaimba "Nasadiki"?

Nyerere mwasisi wa Chama Chenu alisema kuwa CCM si Mama yake, anaweza achana nacho saa yeyote ile. Je mnaogopa nini kuachana na CCM? Ni maslahi gani mnaogopa kuyapoteza kwa kuiacha CCM Solemba?

Wakulu msifikirie nawashikilia bango kina Kilango na Mwakyembe pekee, bali ni pamoja na ile sehemu ya nne ya CCM ya wale ambao waliwahi kuwa viongozi wakuu wa Chama na Serikali.

Mwinyi, Salim, Malecela, Msuya, Kawawa, Salmin, Bilali, Sozigwa, Ameir, Kificho, Kinana na Warioba, je nyie mnaoshikilia ile sehemu ya nne ya Kitenge mko wapi na wale ambao ni wafuasi wenu?

Kina Rwegasira, Mwakanjuki, Hassan Moyo, Lawrence Gama, Mang'ula na utitiri mwingine wa wanaoaminika kuwa CCM safi wako wapi? Mwandosya why hugging and hanging with the thugs? Even Jumbe, Dourado and Samata are this silent? Where are Bruno Mpangala, Hashim Mbita, Sarakikya, Ibrahim Kaduma na Sepeku?

Mnashindwaje kulitumikia Taifa na kulinda maslahi ya Taifa na Mtanzania na kuukana ufidhuli na Uchafu wa CCM kwa kutoa sauti moja ya ukali na kulazimisha zile sehemu tatu zilizobakia za Kitenge zijirudi au mjitoe kabisa CCM?

Mnakubalije pamoja na Urobo wenu kuzidiwa kete na umahiri na hizi pande tatu, Kikwete, Mkapa na Chenge ziwashinde?

Kikwete na Mtandao wake, wako wapi leo kina Lowassa,Karume, Rostam, Msabaha na wengine?

Mkapa ana nguvu gani yeye na kina Kigoda, Mramba, Sumaye, Rupia au Yona na wafuasi wao?

Mnapigwa piku hata na Chenge, Msekwa, Anna Abdallah, Karume, Nahodha, Sitta, Membe, Meghji, Nchimbi, Karamagi na Makinda?

Hivi leo wakirudi Nyerere, Karume, Wakili, Sokoine, Mnauye, Kolimba na Mzee Thabit Kombo mtawaambia nini?

CCM imegawanyika kambi nne, tatu zinalinda maslahi ya Chama na Ufisadi, kwa nini nyinyi kambi ya nne msimeguke basi mkaunda umoja wenu wa pekee na kutetea Mlalahoi?

Wikiendi njema mkiwa mnatafakari "vijisenti"!
 
Mtafuruku na huku kugawanyika kwa CCM katika pande hizzi za kusadikika nne ni kutokana na tamaa na ubinafsi.

Midhali tuchukulie wanyama pori. Fisi na mbwha ni wanyama wenye ushirikiano wa hali ya juu sana. Huwinda pamoja na wakipata wote hula pamoja na kuridhika.

CCM wao ni sawa na Simba dume. Simba dume huzengea kitoweo kilichokamatwa na simba jike na watoto, na hufukuza kila mtu na kutaka ale yeye kwanza ashibe na kuvimbiwa, ndipo wengine waweze kula japo kukidhi njaa kali ya siku.

Katika CCM kuna Simba dume wengi. Ukweli wa hali halisi ni kuwa wamekosa ushirikiano wa jinsi gani wanaweza kujineemesha. Wamekosa umoja wa Fisi na Mbweha.

Nitakuwa wa kwanza kama si wa pili au wa tatu kukiri na kukubali kuwa hakuna jamii timilifu isiyo na madoa na hakuna mamlaka yeyote katika dunia hii ambayo matakwa ya viongozi huwekwa mbele kabla ya maslahi ya wengine wafuatao.

Hata wakija CUF na Chadema, najua tutakuwa na kelele nyingi, lakini natumaini wao watakuwa kama Fisi au Mbweha na kuwa na ushirikiano.

Kuwepo kwa Masimba dume wengi katika CCM, kumedhihirika kutokana na mmomonyoko wa hizi "nyeti" kila siku na uwazi wa mapigano makali katika makundi yao.

Je hii ni sahihi? ningekuwa CCM ningesema si sahihi, sote tuwe kama Fisi au Mbweha tuwe na ushirikiano wa kijamaa kula na kushiba.

Lakini kama mwananchi au nyasi ambazo huumia fahali wanapopigana, ni sahihi kuwepo kwa Simba dume wengi ili ukweli udhihiri kuwa CCM haijali maswala ya Mtanzania bali ni matumbo yao.

Ndio maana nauliza, je hakuna hata kakundi ka Mafisi na Mbweha ambao watajali maslahi ya wengine (Wananchi) na si kula na kuvimbiwa kwa dharau na ubaradhuli?

Kwa nini wale wanaojiita CCM safi waendelee kuishi kupitia vivuli vya CCM Mafisadi? Je wanaogopa nini kujitoa kwa mshikamano wao kama Mbweha na kuwafukuza hawa Masimba Dume ambayo ni malafi?

Nasubiri vitendo!
 
Mimi siamini tena kama kuna mwana CCM wa ngazi ya kati hadi juu aliye safi. Siamini hata kidogo.
 
Mimi siamini tena kama kuna mwana CCM wa ngazi ya kati hadi juu aliye safi. Siamini hata kidogo.

Nyani,

Kuna wana CCM ambao ni safi. Tatizo lao hawajiamini kutokana na kutokuwa na uwezo kifedha kupambana na wale wachache ambao wanafedha ambao wanaendelea kuhujumu Taifa. Aidha wanaogopa nguvu za fedha za hawa mafisadi kutumika kuwaangamiza.

Hata ushindi wa Kikwete 2005, ulitokana na CCM kuwa na kutumia fedha nyingi mno na ndio maana Upinzani ukashindwa.

Sasa kwa kuwa CCM inajiendesha kama Taasisi, kuna CCM wabaya ambao wanatumia kivuli cha taasisi kujitajirisha kupindukia.

Ndio maana nasema ile robo ya CCM iliyosafi, ijitoe kwenye hili gombania goli na wananchi tutawaelewa na kuwaheshimu.
 
Sasa kama kuna ambao bado wako safi ni nini sasa kinachowakwamisha ku-speak against ufisadi publicly? I don't think speaking against it will cost money, will it?
 
Sasa kama kuna ambao bado wako safi ni nini sasa kinachowakwamisha ku-speak against ufisadi publicly? I don't think speaking against it will cost money, will it?

Swali hilo nimetoka kujiuliza nikiwa na mazungumzo na Kitila muda mfupi uliopita. I have no answer to you, than speculating kuwa jamaa wameshiba nidhamu ya woga na Fikra za Mwenyekiti!
 
Hebu fikiria kama mtu kama Malecela, Kawawa, Kinana, na wengine ambao tunadhani si mafisadi wakitoa statement that strongly condemns ufisadi na mafisadi by mentioning or not mentioning any names....just think about how important and far-reaching that would be...
 
ebu jamani kila mtu a-google CORRUPTION INVOLVED JERSEY ISLAND ENGLAND hapo kuna infor kibao kuhusu vijisenti.
 
Kweli tunasema mengi kuhusu watu kufumbia macho maovu ila nadhani kutoka na tamko la kuwa against na hawa jamaa inabidi ujipange si kidogo.Inadibi ujue itakuwaje baada ya hapo,kwanza jinsi gani utaendelea kuwa hai?wachache wamepoteza uhai kwa kuhoji!sasa sijuhi ni coincedence to au ndio hivyo.Kwa hiyo umakini unahitajika kufanya hilo.
Hapa inabidi kuwa na mtandao wa wanao pinga maovu na system yao ya kujilinda wasidhulike.Sio mtandao kama huu uliopo madarakani wa kutaka tu na wao watawale NO.Maana isije ukawa mpinzani tu kwa kuwa wewe ujapewa fungu lako sasa unataka na wewe upate chance hiyo.

Woga wa kupoteza maslahi tumeuzungumzia katika thread moja hapa kuwa ndio ugonjwa mkubwa,uwoga wa kupoteza cheo ndio unafanya taasisi mbalimbali kuingiliwa ktk maamuzi yao .People afraid of changes ,Woga huu hauna maana na ndio tatizo lenyewe.
Lakini inabidi tubadilike kama wote tutakuwa si waoga watafukuza wangapi?Na hii sasa ndio tutaita changes in TZ na ndio mwanzo wa maendeleo ya kweli.
 
Nyani,

Kuna wana CCM ambao ni safi. Tatizo lao hawajiamini kutokana na kutokuwa na uwezo kifedha kupambana na wale wachache ambao wanafedha ambao wanaendelea kuhujumu Taifa. Aidha wanaogopa nguvu za fedha za hawa mafisadi kutumika kuwaangamiza.

Hata ushindi wa Kikwete 2005, ulitokana na CCM kuwa na kutumia fedha nyingi mno na ndio maana Upinzani ukashindwa.

Sasa kwa kuwa CCM inajiendesha kama Taasisi, kuna CCM wabaya ambao wanatumia kivuli cha taasisi kujitajirisha kupindukia.

Ndio maana nasema ile robo ya CCM iliyosafi, ijitoe kwenye hili gombania goli na wananchi tutawaelewa na kuwaheshimu.

Hebu nitajie jamani wanaCCM japo watatu ambao ni wasafi kati ya waliowahi kushika madaraka ya juu ya chama au serikali kati ya 1995 mpaka leo. Mi siamini kama Chama Cha Mafisadi kinaweza kutoa Malaika

Asha
 
Hebu nitajie jamani wanaCCM japo watatu ambao ni wasafi kati ya waliowahi kushika madaraka ya juu ya chama au serikali kati ya 1995 mpaka leo. Mi siamini kama Chama Cha Mafisadi kinaweza kutoa Malaika

Asha

Da Asha maneno yako ni kweli - kwa nini katika Wtz zaidi ya ml 35 tutegemee hicho kakikundi kadogo cha CCM ndio walete mabadiliko, mimi naamini kuna Wtz makini kabisa waliokuwa hawajakunywa maji ya bendera ya CCM wanaweza kututoa katika janga hili ama kama bado tutakuwa na mawazo kuwa CCM ndio chama cha kutuongoza milele ila makosa ni ya wachache tu basi tumekwisha, kwani CCM ni genge la watu wachache ambao wameweka maslahi yao mbele na kuwadanganya wafuasi wao kuwa wanashika hatamu lakini hawana tafauti na Mafioso na ukiingia hisia zote za kibinadamu zinakuondoka.
 
Hebu nitajie jamani wanaCCM japo watatu ambao ni wasafi kati ya waliowahi kushika madaraka ya juu ya chama au serikali kati ya 1995 mpaka leo. Mi siamini kama Chama Cha Mafisadi kinaweza kutoa Malaika

Asha


Asha,

Je tafsiri yako ya Usafi ni ipi? Maana najiuliza watu kama Msuya, Salim na Mwandosya si safi?
 
Asha,

Je tafsiri yako ya Usafi ni ipi? Maana najiuliza watu kama Msuya, Salim na Mwandosya si safi?

Sina uhakika kama Cleopa Msuya anastahili kuwepo kwenye kwenye hiyo list. Labda badala yake umuweke Spika wa zamani ambaye ni makamu mwenyekiti wa sasa Pius Msekwa.
 
Asha,

Je tafsiri yako ya Usafi ni ipi? Maana najiuliza watu kama Msuya, Salim na Mwandosya si safi?
Rev. hao wote sio safi nakuambia.
Maana wako kwenye CC na NEC na bado hawausemi ubaya wanaouona kwa nguvu zao au kujitoa kwenye huo uchafu tukawaelewa.
Huwezi kuishi ndani ya jalala ukatamba kuwa wewe msafi. Hata kidogo.
 
Okay, back to CCM again, what are the camps within CCM and how will each one play part in the 2015 elections? Can the open disharmony within CCM continue to tank the ship and provide opportunity for opposition to seize the moment?
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom