Kitendo cha Wanachama wa Yanga SC Kumzomea Katibu Mkuu wa TFF ni Kukosa Heshima

Ghazwat

JF-Expert Member
Oct 4, 2015
23,718
66,262
Ni Kitendo cha kusikitisha sana kimejiri leo kwenye Mkutano Mkuu wa Yanga ndani ya Ukumbi wa DYCCC Chang'ombe, kumzomea Katibu Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania TFF, Wilfred Kidao ambaye alikuwa Mwakilishi kutoka katika Shirikisho hilo.

Kwakweli hiki Kitendo si cha kistaarabu, ni Kitendo cha kihuni kwenye Mkutano wenye Heshima na Mustakabari wa Soka la Tanzania tena mbele ya viongozi wengine waalikwa ambao wanaheshimika sana nchini akiwemo mgeni rasmi Rais Mstaafu Jakaya Kikwete, na ni kukosa heshima kwa mamlaka yenye dhamana ya kuongoza mpira nchini Tanzania.

Viongozi wa Yanga acheni kupelekeshwa na mihemko ya mashabiki wasiojielewa. Kwani haya ndo matunda ya Makamu/Kiti kuita Press Conference na kuaminisha Mashabiki na Wanachama kwamba timu inaonewa madai ambayo hata Rais Mstaafu Kikwete alipinga kwenye Kubwa Kuliko (Yanga Day).

Mpira ni mchezo wa wazi Uwanjani, mnataka TFF wafanye nini? Wafunge mabao wao badala ya Sarpong ama mnataka TFF wasajili wachezaji wenye viwango wao badala ya Engineer? Au mnataka TFF waandae timu badala ya Viongozi?

Kwakweli Viongozi Jitafakarini, kisha mpige hatua mbele na muombe radhi kwa Katibu Mkuu Wilfred Kidao pamoja na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania.
 
Kile mtu akipandacho ndicho atakachovuna

Ukipanda ubaya utavuna ubaya, usitegemee kuvuna machungwa kutoka mti wa mchongoma

Hizo ni feedback kwa TFF, wajichunguze wanakosea wapi ilikupata uhalali kwa wanamichezo wote, hususani wapenzi wa soccer.
 
Hapo watakuwa wamevunja kanuni ya 9.3 ya TFF.
Hivyo TFF itoe adhabu ya kuwafungia au wote wapigwe faini.

Udikiteta huwa hautatui matatizo

Feedback ni kuamsha, ni indicator ni ujumbe kwamba kuna mambo hayaendi vizuri . Sasa TFF IJITATHIMINI KWANINI UMATI UWAZOMEE.

TFF wanapaswa kulichukulia positively vinginevo hawatatengeza bali watahalibu zaidi.
 
Udikiteta huwa hautatui matatizo

Feedback ni kuamsha, ni indicator ni ujumbe kwamba kuna mambo hayaendi vizuri . Sasa TFF IJITATHIMINI KWANINI UMATI UWAZOMEE.

TFF wanapaswa kulichukulia positively vinginevo hawatatengeza bali watahalibu zaidi.
Wakiitwa kujitetea si ndio watasema sababu ya utovu wa nidhamu. Labda ni ile assist ya Bernard Morison kule Songea imewauma.

Hivyo faini itawahusu
 
Wakiitwa kujitetea si ndio watasema sababu ya utovu wa nidhamu. Labda ni ile assist ya Bernard Morison kule Songea, au Ally Mayai kuenguliwa kwenye uchaguzi. Hivyo bado faini itawahusu

Wakati mwengine sio vema sana kuhoji watoto uwakutapo home hawana furaha nakuanza kutoa vipigo.

Kujichunguza, kutafiti nakutafuta majibu sahihi nijukumu lako.

Otherwise utatengeneza mgogoro ambao unaweza kukuathili wewe binafsi na familia yako. Yaani ukaaibika na kudhalilika
 
Write your reply...MPAKA SASA SIMBA NDIO CLUB PEKEE AFRICA YENYE VIPORO.... APO NDIO UTAJUA KWA NINI WAMEZOMEWA
 
Write your reply...MPAKA SASA SIMBA NDIO CLUB PEKEE AFRICA YENYE VIPORO.... APO NDIO UTAJUA KWA NINI WAMEZOMEWA

Screenshot_20210627-191100.png
 
Kwanini Tff wajichinguze,wakati ukweli unajulikana,misimu mitatu nyuma yanga wameshindwa kujenga kikosi imara,wanasajili mwanzo wa msimu na Kisha kikibomoa kikosi katikati msimu.Ukweli mchungu menejimenti ya Yanga na mashabiki wa Yanga mjitathimini,mnapenda UwOnGo MtAmU kuliko UkWeli mchungu.Yanga hawana kikosi Cha ushindani,Jambo ambalo wamefaulu viongozi wa Yanga ni kueneza Propaganda kwa mashabiki wao.
Kile mtu akipandacho ndicho atakachovuna

Ukipanda ubaya utavuna ubaya, usitegemee kuvuna machungwa kutoka mti wa mchongoma

Hizo ni feedback kwa TFF, wajichunguze wanakosea wapi ilikupata uhalali kwa wanamichezo wote, hususani wapenzi wa soccer.
 
Back
Top Bottom