Uchaguzi 2020 Kitendo cha Tundu Lissu kukubalika Kanda ya Ziwa kwa kiwango hiki inaashiria nini?

Hizo ndizo picha halisi zikinazo onyesha joto analolipata kanda hii. Hizo zingine za kwao ni za kubumba. Leo alikuwa afanye mkutano katika viwanja vya shule ya msingi Mabatini, wilaya ya Ilemela mkoa Mwanza. Hakuna hata mtu mmoja aliyehudhuria, mkutano ukaahirishwa. Lakini kesho tutaoneshwa mafuriko aliyoyapata Ilemela jijini Mwanza. Figisu tupu.
Hiyo ndio demokrasia sio ukubalike sehemu zote.Sasa sikilizia mziki wake kwani unafikiri Chadema hawawezi kuandika mabango? Najua wataishia lockup! Ila wataandika.
 
Wewe ni mbumbumbu kabisa wa siasa za Kanda ya Ziwa tafuta video clips za 2015 za Lowassa then uje utuambie ilikuaje hakupata hata mbunge mmoja Mkoani Geita wakati kulikuwa na mafuliko?? Subiri tarehe 28/10/2020 ndiyo utajua!
Tena hadi Msukuma, mbunge wa Geita alitua na helikopta yake Arusha kwenye uwanja alikokuwa akifanya kampeni Lowasa akijifanya ameenda kumuunga mkono kumbe ameenda kumchora tu! Lowasa alishuka kwenye jukwaa la kampeni na kwenda kumpokea Msukuma kwenye hiyo chopa ya Msukuma! Yaani hawa watu wana matani hadi utafurahi!
 
Tumeshawaambia hadi tumechoka picha zenu za kuchakachua za kitengo chenu cha uchakahuaji CHADEMA tumezichoka.Mwacheni Lowasa apumzike picha zake za mikutano yake mlizochakachua inatosha.
Mkuu hata TV huna, kweli jpm kafukarisha wengi
 
Kwanza nataka nikuambie hizo picha zinazotembea mitandaoni siyo hali halisi ilivyokuwa pale Geita leo naona wameziedit ndiyo maana nasema tusubiri October 2020 tutaona nani ni kidume!
Suala siyo picha hizo, bali ni ukweli kuwa waathirika wakubwa wa utawala wa Magufuli ni wasukuma. Mifugo, mashamba, uvuvi, vitambulisho nk vyote hivi wasukuma wameonja joto la Jiwe. Sasa mpigieni kura sisi tutawafuta machozi!
 
Halafu nasika huyu mwamba enzi za JK akiitwa Polisi, huyo Polisi atakayefika home kwake anamlamba vibao. Amri nyingi za Serikali alizipinga huyo mwamba, ndio maana Mheshimiwa Magufuli alimwonesha jeuri ya Serikali.
Kweli kabisa huyo jamaa alikuwa mafia wa kiwango cha juu Sana Ila Magu kamnyoosha ile mbaya.
 
Acha uongo sehemu gani alisema hivyo. Kwanza watu waliohudhuria mikutano ya Rais Magufuli ni wengi kuliko wa Lissu na Mwanza mlisema hivyo lakini Magufuli alifunika kabisa. Lakini msema kweli ni tarehe 28/10/2020.
Alisema hayo akiwa Geita tena kwa kisukuma!
 
Maufuli alifunika kwa kusomba watu na malori pamoja na wanafunzi na walimu ambao kwa siku hiyo alipiga marufuku kwenda shule
 
Wewe unajidanganya, Lisdu hawezi shinda uraisi hizo kampeini uchwara unazofanya hapa jamii forum unapoteza muda bora ukojoe ukalale, ni JPM tu hadi 2025
Labda niandike nilichokificha ili uelewe vizuri uzi huu , kabla ya ujio wa Lissu watu wa Geita walikuwa wanatangaziwa kwa kisukuma kwamba Kuhudhuria mkutano wa Lissu ni Usaliti , ikiwa kama Magufuli anatakiwa kiasi unachokisema ilikuwaje jambo hili litangazwe kwa umma ? hata hivyo wananchi wamepuuza kinyama
 
Hiyo ndio demokrasia sio ukubalike sehemu zote.Sasa sikilizia mziki wake kwani unafikiri Chadema hawawezi kuandika mabango? Najua wataishia lockup! Ila wataandika.
Ni dalili mbaya sana. Haijawahi kutokea kwenye kampeni yo yote nchini kwetu mgombea urais kuzomewa kiasi hicho. Jana Mbowe naye kazomewa sana jimboni kwake Hai lakini picha za kubumba zikaonesha mafuriko! Yaani mwaka huu CDM ndiyo basi!
 
Ni dalili mbaya sana. Haijawahi kutokea kwenye kampeni yo yote nchini kwetu mgombea urais kuzomewa kiasi hicho. Jana Mbowe naye kazomewa sana jimboni kwake Hai lakini picha za kubumba zikaonesha mafuriko! Yaani mwaka huu CDM ndiyo basi!
Ungekuwa Kagera wala usingeandika hivi kuzomewa kwa wanasiasa ni kitu cha kawaida
 
Nilikuwepo kweli huu mkutano kumsnina meko ameenda na maji, Baba yake Mzee LOFA naye alishatangulia Nani atamsaidia??? Mpaka SASA ninavyoandika hapa wananchi wamejaaa hapa Kilimanjaro hotel hawataki kuondoka!
 
Suala siyo picha hizo, bali ni ukweli kuwa waathirika wakubwa wa utawala wa Magufuli ni wasukuma. Mifugo, mashamba, uvuvi, vitambulisho nk vyote hivi wasukuma wameonja joto la Jiwe. Sasa mpigieni kura sisi tutawafuta machozi!

Kuna kila ukweli kwa baadhi ya unayo sema, lakini nyinyi sio wafatiliaji wa data wazuri.

Kuna ongezeko la wanaoenda shule za msingi na sekondari za kata kwa kanda nzima watoto 750,000 kwa ngazi ya shule za msingi na sekondari, jee mnajua ni Maendeleo gani yatatokea baada ya miaka kumi ?

Jee Mabadiliko gani tuyategemee, hasa maendeleo na vurugu itakayo kuja kielimu baada ya miaka ishirini ?.
 
Mimi naomba tarehe 29 na 30 mwezi ujao muwepo humu! Nina kuhakikishia hapa hakuna mkoa wowote wala jimbo lolote ambalo Lissu atashinda kwa ujumla wa Kura dhidi ya Magufuli tena uko kanda ya Ziwa ndio usiseme kabisa!

Mimi naomba usije ukalimbia jukwaa!
Kamwe Lissu awezi mshinda Magufuli kwenye jimbo lolote wala mkoa wowote hapa Tanzania!

Najua sasa hivi utonielewa lakini tarehe 30 utanielewa! Kamwe Kamwe tena uko kanda ya Ziwa Lissu hatoweza kupanda ushindi hata ule unao mkaribia Magufuli hata chembe!

Naomba tuombe Mungu atuweke hai hadi tarehe 28 hakika tutaona na tutarudi hapa kusimuliana!
wewe ni Mungu au ni mungu?
 
Sitaki kukuharibia siku, kwa taarifa tuu, Kuna association moja inafanya kazi overdrive. Mpaka 28th October, 2020 usishangae kwa matokeo yeyote.
Hii kitu ilikuwa akilini mwangu juu ya mawaziri na hii ndiyo naisema itakuja ilete mapinduzi ya kiutawala watu washangae..!
 
Kuna kila ukweli kwa baadhi ya unayo sema, lakini nyinyi sio wafatiliaji wa data wazuri.

Kuna ongezeko la wanaoenda shule za msingi na sekondari za kata kwa kanda nzima watoto 750,000 kwa ngazi ya shule za msingi na sekondari, jee mnajua ni Maendeleo gani yatatokea baada ya miaka kumi ?

Jee Mabadiliko gani tuyategemee, hasa maendeleo na vurugu itakayo kuja kielimu baada ya miaka ishirini ?.
Kwa mujibu wa wataalam wa magonjwa ya akili , mtu yeyote anayedhani ana akili kuliko wote huyo ni kichaa , yaani wewe Maghembe wa milimani ndio unajua sana mambo kuliko kamati kuu ya chadema !
 
Hiyo ni protest(sijui maana kwa kiswahili) au salamu wanatuma kwa Serikali kama wameachwa nyuma. Wananchi wa huko hawaendi spidi moja na kasi ya uchumi wa kati.
 
Back
Top Bottom