Kitendo cha Rais kuagiza 'Viboko' wapelekewe maji ni kielelezo cha kufa kwa taasisi zetu

Quinine

JF-Expert Member
Jul 26, 2010
21,271
47,271
TANAPA, TAWA na Waziri husika walikuwa wapi.

Akiwa kwenye ziara Mkoani Katavi rais John Pombe Magufuli aliagiza Mamlaka ya Hifadhi za Wanyamapori nchini (TAWA) kuchimba bwawa na kujaza maji kwa ajili ya viboko wanaoishi katika Hifadhi ya Taifa ya Katavi.

“Ninawaagiza TAWA kuanzia kesho wapeleke maji wachimbe bwawa wajaze maji. Wanyama hao wanatuingizia fedha nyingi, kwa nini tushindwe kuwatunza,” alisema Rais Magufuli.

Najiuliza, hadi kufikia hali hiyo Waziri wa Maliasili na Utalii alikuwa wapi, hao TAWA na TANAPA walikuwa wapi.

Ndio kusema taasisi husika hazikuona kuwa hilo ni tatizo hadi rais aingilie kati, je kama asingepita sehemu hiyo Viboko wangeendelea kuteseka? Viongozi hao wamepewa madaraka, wamepewa vitendea kazi wana kila kitu na kila mwezi wanapokea mshahara kwa kazi hiyo walikuwa wapi kulishughulikia.

Ni wakati sasa kwa wahusika kuwajibika kwa kumsaidia rais kuliko kusubiri rais awajibike kwao.
 
Sikiliza ndugu kupeleka maji kwemye bwawa la viboko bila idhini ya mkuu, unataka watu watumbuliwe na kupewa kesi ya uhujumu uchumi, unajua bei ya water bowser moja Kwa umbali ule ni kiasi Gani,na kujaza bwawa inachukua zaidi ya water bowse Mia mbili au Tatu, sasa Nani kwenye utawala huu anaweza kujichukulia mamlaka ya kutumia fedha kiasi hicho Kwa kitu ambacho sio rahisi kuwa audited bila maagizo kutoka juu embu acheni masihara nyie watu
 
Kwan wanapeleka bowser au wanachimba
Sikiliza ndugu kupeleka maji kwemye bwawa la viboko bila idhini ya mkuu, unataka watu watumbuliwe na kupewa kesi ya uhujumu uchumi, unajua bei ya water bowser moja Kwa umbali ule ni kiasi Gani,na kujaza bwawa inachukua zaidi ya water bowse Mia mbili au Tatu, sasa Nani kwenye utawala huu anaweza kujichukulia mamlaka ya kutumia fedha kiasi hicho Kwa kitu ambacho sio rahisi kuwa audited bila maagizo kutoka juu embu acheni masihara nyie watu
 
sasa Nani kwenye utawala huu anaweza kujichukulia mamlaka ya kutumia fedha kiasi hicho Kwa kitu ambacho sio
Hujataja hicho kiasi? twambie ni kiasi gani tukusaidie, hata hivo kinachotakiwa ni mawazo ya kufanya kitu wala sio fedha
 
Unajua sheria za Uhifadhi zinasemaje kuhusu uingizwaji wa Vyakula vya Wanyama au Maji? Je ecolojia inaruhusu, Tungeacha nature ichukue mkondo wake ndio ecolojia inavyoenda. Lkn kwakuwa Ushauri wa Mhe.Rais ulilenga kuokoa maisha ya wale Boko ni Maagizo. So tuache kubeza bila kujiridhisha na hayo
 
Back
Top Bottom