demigod
JF-Expert Member
- Jan 2, 2015
- 8,250
- 15,116
Mimi ni shabiki wa Yanga kama nijulikanavyo hapa jukwaani.
Ila nimeshangaa kinoma kuona Mwakalebela akiitisha vyombo vya habari na kuanza kulalamika kuhusu kuonewa na waamuzi viwanjani, cha ajabu zaidi anasema kuwa Yanga itajitoa kwenye ligi endapo changamoto alizozisema zikiendelea. Binafsi ninaona ni ujinga wa kiwango cha juu zaiidi kwa kiongozi mkubwa kama yule wa klabu kufanya jambo kama lile la kijinga.
Ni kweli changamoto ya uamuzi imeonekana, lakini sio sababu ya Timu kushindwa kufanya vizuri mpaka uitishe vyombo vya habari na kuanza kuwalalamikia wengine kwa makosa yao wenyewe viongozi. Kushindwa kupata matokeo mazuri recently kumetokana na machaguo ya kijinga ya mwalimu na sio kwa sababu ya kunyimwa penati.
Ushamba huu iliwahi kufanywa na Haji Manara alipokuwa anaita waandishi wa habari akiwa na Flat Screen akionyesha jinsi Simba ilivyokuwa inanyimwa penati. Sasa inakuwaje kiongozi wa juu wa hadhi yake arudie kufanya ushamba wa aina hii?
Ametukera na kutuudhi wengi.
Ila nimeshangaa kinoma kuona Mwakalebela akiitisha vyombo vya habari na kuanza kulalamika kuhusu kuonewa na waamuzi viwanjani, cha ajabu zaidi anasema kuwa Yanga itajitoa kwenye ligi endapo changamoto alizozisema zikiendelea. Binafsi ninaona ni ujinga wa kiwango cha juu zaiidi kwa kiongozi mkubwa kama yule wa klabu kufanya jambo kama lile la kijinga.
Ni kweli changamoto ya uamuzi imeonekana, lakini sio sababu ya Timu kushindwa kufanya vizuri mpaka uitishe vyombo vya habari na kuanza kuwalalamikia wengine kwa makosa yao wenyewe viongozi. Kushindwa kupata matokeo mazuri recently kumetokana na machaguo ya kijinga ya mwalimu na sio kwa sababu ya kunyimwa penati.
Ushamba huu iliwahi kufanywa na Haji Manara alipokuwa anaita waandishi wa habari akiwa na Flat Screen akionyesha jinsi Simba ilivyokuwa inanyimwa penati. Sasa inakuwaje kiongozi wa juu wa hadhi yake arudie kufanya ushamba wa aina hii?
Ametukera na kutuudhi wengi.