Kitendo cha Membe kutomjibu Bashe ni hekima na busara au kapuuza?

kwitega

Senior Member
Apr 10, 2012
166
49
Hivi karibuni, Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM na Baraza Kuu la vijana Hussein Bashe alizungumza na waandishi wa habari na kumshambulia Waziri wa Mambo ya Nje Bernard Membe kuwa ni mnafiki, asiyefaa hata kwa ubalozi wa nyumba kumi na akaapa kupiga kampeni ili Waziri huyo asichaguliwe kuwa Mjumbe wa NEC kupitia kapu. Hata hivyo jitihada za kutaka Membe asichaguliwe, zilishindwa kwani alishinda japo Bashe alijitokeza na kubeza ushindi huo kuwa ni mdogo na kazidiwa na makada vijana ikiwa ni pamoja na Januari Makamba.

Kisha akabainisha kuwa anamuunga mkono Edward Lowassa anayetajwa kuwania urais 2015 kupitia chama hicho. Wengi tulitarajia kumuona Membe akiibuka kumjibu Bashe lakini siku zinaenda, hatuoni Membe akifanya hivyo. Sasa nauliza, je ukimya wa Membe;


1. Unaonyesha kuwa kampuuza Bashe na maneno yake?

2. Unaonyesha busara na hekima?

3. Unaonyesha uvumilivu?

4. Kamuogopa Bashe?
 
Ajibu nini wakati ni kweli membe ni mnafiki,mtu wa majungu,ni kweli anabebwa na familia ya ikulu,hana uwezo wa kuwa rais,.ogopa mtu wa majungu na mpenda fitina ni muuwaji kuliko mchawi.
 
Ni Sawasawa tu na Lowasa kuwapuuza akina Makonda je

1. Unaonyesha kuwa kampuuza Makonda na Nape kwa maneno yao?

2. Unaonyesha busara na hekima?

3. Unaonyesha uvumilivu?

4. Kamuogopa Makonda na Nape?
 
nadhani hajampuuza, anampeleka mahakamani kwa mujibu wa kimemo chake kwenda kwa swahiba wake na aliyekuwa kampeni meneja wake kwenye uchaguzi ule, mbunge wa Nzega, Dkt. hamis Kigwangala kama kinavyosomeka kwenye post nyingine hapa JF
 
Back
Top Bottom