Ileje
JF-Expert Member
- Dec 20, 2011
- 8,784
- 12,226
Hatuwezi kujisifu kuwa hii ni demokrasia bali ni fujo na ukosefu wa mwelekeo na sera za Taifa. Hadi sasa kama Taifa hatujui kama tunafuata ujamaa au ubepari.
Viongozi huandaliwa, hufunzwa na kulelewa. Haiwezekani mtu anakurupuka usingizini akiwa na matongotongo machoni anachukuwa fomu ya kuwania uspika! Hii ni hatari kubwa kwa mustakabali wa Taifa kwani tutakuja kupata viongozi wehu ilimradi tu kwa ushabiki wa kipumbavu wakapata kura za kutosha.
Aidha tamaa ya watu wengi kupata manufaa ya kiuchumi na kuondokana na umaskini uliotopea ndiyo kishawishi kikubwa kuwania nafasi za uongozi katika siasa. Wakati umefika tufanye jitihada za kuondokana na umaskini huu ili watu wengi wajikite katika shughuli za kuzalisha mali na kuinua uchumi vinginevyo Taifa litaangamia na kuishia kugombana sisi kwa sisi.
Wakati umefika tuache kufanya nafasi za uongozi wa kisiasa kama ajira za kujipatia utajiri na badala yake ziwe nafasi za kujitolea. Hii ifanyike kwa vyama vyote vya siasa tuwe na viongozi wanaokerwa na maisha duni ya watu na siyo wanaotaka kujineemesha kiuchumi. Hivi sasa tumefika mahali ambapo vijana wote wanataka kuwa viongozi wa kisiasa na siyo wavuja jasho!
TUJISAHIHISHE!
Viongozi huandaliwa, hufunzwa na kulelewa. Haiwezekani mtu anakurupuka usingizini akiwa na matongotongo machoni anachukuwa fomu ya kuwania uspika! Hii ni hatari kubwa kwa mustakabali wa Taifa kwani tutakuja kupata viongozi wehu ilimradi tu kwa ushabiki wa kipumbavu wakapata kura za kutosha.
Aidha tamaa ya watu wengi kupata manufaa ya kiuchumi na kuondokana na umaskini uliotopea ndiyo kishawishi kikubwa kuwania nafasi za uongozi katika siasa. Wakati umefika tufanye jitihada za kuondokana na umaskini huu ili watu wengi wajikite katika shughuli za kuzalisha mali na kuinua uchumi vinginevyo Taifa litaangamia na kuishia kugombana sisi kwa sisi.
Wakati umefika tuache kufanya nafasi za uongozi wa kisiasa kama ajira za kujipatia utajiri na badala yake ziwe nafasi za kujitolea. Hii ifanyike kwa vyama vyote vya siasa tuwe na viongozi wanaokerwa na maisha duni ya watu na siyo wanaotaka kujineemesha kiuchumi. Hivi sasa tumefika mahali ambapo vijana wote wanataka kuwa viongozi wa kisiasa na siyo wavuja jasho!
TUJISAHIHISHE!