Kitendo cha makumi ya watu kujitokeza kuwania nafasi moja tu uspika kimedhihirisha kuwa Taifa hili halina dira wala halijitambui

Ileje

JF-Expert Member
Dec 20, 2011
8,759
12,175
Hatuwezi kujisifu kuwa hii ni demokrasia bali ni fujo na ukosefu wa mwelekeo na sera za Taifa. Hadi sasa kama Taifa hatujui kama tunafuata ujamaa au ubepari.

Viongozi huandaliwa, hufunzwa na kulelewa. Haiwezekani mtu anakurupuka usingizini akiwa na matongotongo machoni anachukuwa fomu ya kuwania uspika! Hii ni hatari kubwa kwa mustakabali wa Taifa kwani tutakuja kupata viongozi wehu ilimradi tu kwa ushabiki wa kipumbavu wakapata kura za kutosha.

Aidha tamaa ya watu wengi kupata manufaa ya kiuchumi na kuondokana na umaskini uliotopea ndiyo kishawishi kikubwa kuwania nafasi za uongozi katika siasa. Wakati umefika tufanye jitihada za kuondokana na umaskini huu ili watu wengi wajikite katika shughuli za kuzalisha mali na kuinua uchumi vinginevyo Taifa litaangamia na kuishia kugombana sisi kwa sisi.

Wakati umefika tuache kufanya nafasi za uongozi wa kisiasa kama ajira za kujipatia utajiri na badala yake ziwe nafasi za kujitolea. Hii ifanyike kwa vyama vyote vya siasa tuwe na viongozi wanaokerwa na maisha duni ya watu na siyo wanaotaka kujineemesha kiuchumi. Hivi sasa tumefika mahali ambapo vijana wote wanataka kuwa viongozi wa kisiasa na siyo wavuja jasho!

TUJISAHIHISHE!
 
... watakwambia ni ukomavu wa demokrasia ndani ya chama japo kuna baadhi ya nafasi fomu ni moja tu! Demokrasia ya kununua fomu kwenye baadhi ya nafasi ila sio kuhoji wala kukosoa maagizo ya wakubwa! Demokrasia ya kusikilizia mkubwa anasema nini halafu wengine wote tunaunga msafara uelekeo huo huo kama nyumbu wa Serengeti.
 
Ni kupanuka na kukua kwa demokrasia. Kwa nafasi ambazo bado fomu inatolewa moja, hayo maeneo ndiyo tunahitaji improvement.
 
Spika wa maelekezo kutoka juu ndiye ategemewae. Hao wengine wanaosha nyota zao tu
 
Wakati umefika tuache kufanya nafasi za uongozi wa kisiasa kama ajira za kujipatia utajiri na badala yake ziwe nafasi za kujitolea. Hii ifanyike kwa vyama vyote vya siasa tuwe na viongozi wanaokerwa na maisha duni ya watu na siyo wanaotaka kujineemesha kiuchumi. Hivi sasa tumefika mahali ambapo vijana wote wanataka kuwa viongozi wa kisiasa na siyo wavuja jasho!
Tumefanya siasa kuwa ndio ajira inayolipa na ndio maana tunaona Maprofessor , Doctors , Engineers na wataalam wengi wanaacha taaluma zao ambazo zingesaidia kuendeleza nchi na kukimbilia kwenye siasa. Yote hii ni kwasababu sera zetu zinawatukuza wanasiasa na kuwapa malupulupu mengi tofauti na watalaam wetu.

Kama renumeration ya wataam wetu ingekuwa ya kuridhisha yaani tungekuwa tunawalipa mishahara ya mizuri sidhani kama wangekuwa wanakimbilia mjengoni kuitikia NDIOOOOOOOOOOO!!!

Huko kwenye siasa hawatumii akili zao vilivyo na mara nyingine wanakuwa zombies; kufuata maelekezo bila tafakuli za kina!
 
Tumefanya siasa kuwa ndio ajira inayolipa na ndio maana tunaona Maprofessor , Doctors , Engineers na wataalam wengi wanaacha taaluma zao ambazo zingesaidia kuendeleza nchi na kukimbilia kwenye siasa. Yote hii ni kwasababu sera zetu zinawatukuza wanasiasa na kuwapa malupulupu mengi tofauti na watalaam wetu.

Kama renumeration ya wataam wetu ingekuwa ya kuridhisha yaani tungekuwa tunawalipa mishahara ya mizuri sidhani kama wangekuwa wanakimbilia mjengoni kuitikia NDIOOOOOOOOOOO!!!

Huko kwenye siasa hawatumii akili zao vilivyo na mara nyingine wanakuwa zombies; kufuata maelekezo bila tafakuli za kina!
Mama amesema wale lakini wasivimbiwe, wajipimie! Sasa mtu ataacha kukimbilia huko?
 
Hatuwezi kujisifu kuwa hii ni demokrasia bali ni fujo na ukosefu wa mwelekeo na sera za Taifa. Hadi sasa kama Taifa hatujui kama tunafuata ujamaa au ubepari.

Viongozi huandaliwa, hufunzwa na kulelewa. Haiwezekani mtu anakurupuka usingizini akiwa na matongotongo machoni anachukuwa fomu ya kuwania uspika! Hii ni hatari kubwa kwa mustakabali wa Taifa kwani tutakuja kupata viongozi wehu ilimradi tu kwa ushabiki wa kipumbavu wakapata kura za kutosha.

Aidha tamaa ya watu wengi kupata manufaa ya kiuchumi na kuondokana na umaskini uliotopea ndiyo kishawishi kikubwa kuwania nafasi za uongozi katika siasa. Wakati umefika tufanye jitihada za kuondokana na umaskini huu ili watu wengi wajikite katika shughuli za kuzalisha mali na kuinua uchumi vinginevyo Taifa litaangamia na kuishia kugombana sisi kwa sisi.

Wakati umefika tuache kufanya nafasi za uongozi wa kisiasa kama ajira za kujipatia utajiri na badala yake ziwe nafasi za kujitolea. Hii ifanyike kwa vyama vyote vya siasa tuwe na viongozi wanaokerwa na maisha duni ya watu na siyo wanaotaka kujineemesha kiuchumi. Hivi sasa tumefika mahali ambapo vijana wote wanataka kuwa viongozi wa kisiasa na siyo wavuja jasho!

TUJISAHIHISHE!
Kasoro wewe tu mtoa post...watz kama tuliweka alarm kuwa spika aking'oa mguu tu watu tunaziba nafasi hivi nami naenda kuchukua fomu maana sio kwa jua hii la utosi mtaani.
 
Ni ishara ya ukomavu na ukuaji wa demokrasia ndani ya CCM. Kuna Chama sitokitaja lakini kilifanya jambo la aibu sana
 
Hatuwezi kujisifu kuwa hii ni demokrasia bali ni fujo na ukosefu wa mwelekeo na sera za Taifa. Hadi sasa kama Taifa hatujui kama tunafuata ujamaa au ubepari.

Viongozi huandaliwa, hufunzwa na kulelewa. Haiwezekani mtu anakurupuka usingizini akiwa na matongotongo machoni anachukuwa fomu ya kuwania uspika! Hii ni hatari kubwa kwa mustakabali wa Taifa kwani tutakuja kupata viongozi wehu ilimradi tu kwa ushabiki wa kipumbavu wakapata kura za kutosha.

Aidha tamaa ya watu wengi kupata manufaa ya kiuchumi na kuondokana na umaskini uliotopea ndiyo kishawishi kikubwa kuwania nafasi za uongozi katika siasa. Wakati umefika tufanye jitihada za kuondokana na umaskini huu ili watu wengi wajikite katika shughuli za kuzalisha mali na kuinua uchumi vinginevyo Taifa litaangamia na kuishia kugombana sisi kwa sisi.

Wakati umefika tuache kufanya nafasi za uongozi wa kisiasa kama ajira za kujipatia utajiri na badala yake ziwe nafasi za kujitolea. Hii ifanyike kwa vyama vyote vya siasa tuwe na viongozi wanaokerwa na maisha duni ya watu na siyo wanaotaka kujineemesha kiuchumi. Hivi sasa tumefika mahali ambapo vijana wote wanataka kuwa viongozi wa kisiasa na siyo wavuja jasho!

TUJISAHIHISHE!
Naunga mkono hoja.
 
Hadi Dr. Msukuma, mzee wa wediwide open viza naye anautaka uspika, hii inaonyesha ni nmana gani hiyo nafasi inavyodhalilishwa. Kwa nchi za wenzetu nafasi kama hizo unakuta zina watu wake ambao wanajulikana na asilimia kubwa ya raia na hata ndani ya viongozi wenyewe wanajua kwamba hii nafasi ni fulani na fulani, ambao unaweza kuta hawafiki hata watano.
 
Sasa ulitaka w achukue fomu wangapi, au ulitaka mchakato wakumtafuta speaker uwaje, Maan umeongea tu maneno matupu mbona ww hujaonesha kuwa njia sahihi iweje
 
Sasa ulitaka w achukue fomu wangapi, au ulitaka mchakato wakumtafuta speaker uwaje, Maan umeongea tu maneno matupu mbona ww hujaonesha kuwa njia sahihi iweje
Njia sahihi ni kuweka vigezo sahihi vya kila nafasi na siyo kujua na kusoma kiswahili tu!
 
7 Reactions
Reply
Back
Top Bottom