choga mkuu
JF-Expert Member
- Apr 11, 2016
- 283
- 110
Ifikie kipindi tuelewe kuwa Elimu hii tunayoipata hapa nchi inapaswa kufumuliwa ili kuruhusu vitu halisi vinavyoendana na mazingira na wakati kuingizwa...... Leo PROF LIPUMBA analilia uenyekit Wa chama ,tena chama chenyewe ni cha upinzani ,na upinzani wenyewe ulivyo mugumu ktk nchi zinazoendelea kama Tanzania ni aibu kubwa.... Hiii inaonesha kuwa elimu tunayoipata inatengeneza watu wasioweza kujiajili maana hawana ujuzi stahiki .... Na hiii imethibitishwa na Lipumba Haruna Mwenyewe ambaye ni Msomi mkubwa Wa uchumi Duniani..sio Tanzania, ni duniani..... Elimu yetu imatengeneza WATAFTA AJIRA na si WATENGENEZA AJIRA... Kuna wakuu Wa mikoa walisikika wakituambia tujiajiri Mara tumalizapo masomo lakini wao walipofukuzwa kazi wakaanza kulia kwamba hawana pa kujishikiza... Dr Lutengwe aliyekuwa Mkuu Wa mkoa Morogoro yeye alilia kabsa baada ya kufukuzwa kazi...... Naiomba serikali ifanyie marekebisho elimu yetu ,tuache kukalilisha kanuni za Archimedes za miaka 500 iliyopita, tusome yanayotuhusu.... Watumishi waserikali nao ni waoga mwisho hawataki kusema maana wanaogopa kutumbuliwa bila uoga,,,, karibun kwa mawazo