Beatrice Kamugisha
JF-Expert Member
- May 18, 2019
- 762
- 6,980
Upo umuhimu wa wasomi na wataalam wetu kuliangalia hili suala kwa macho mapana na kuishauri serikali. Tusione Canada wanatoa hifadhi kwa Watanzania tukakaa kimya, tujiulize tumefikaje hapa?
Ikumbuke kwa mujibu wa sheria za kimataifa ukimbizi ni hadhi unayopata baada ya wataalam kukaa na kujiridhisha kwamba unastahili.
Kama lema na familia yake wamekubaliwa hifadhi ni udhibitisho kwamba wamepita kwenye mchujo na kufaulu, wameweka ushahidi nakuishawishi Canada kuwapokea. Familia yake itaishi kwa raha na watoto watasoma vizuri zaidi ya hapa ila kila siku kwa maika dahari ya Taifa letu watabaki kusomwa kwenye hiztoria ya Taifa letu Kama tunavyowasoma akina Kambona.
Tujitafakari mara nyingine Tena, Tanzania si sehemu salama? Kama ni sehemu salama kwanini marafiki zetu wa muda mrefu Canada wanautangazia Ulimwengu kwamba tuna wakimbizi wakisiasa? Tujadiliane nao tulifute doa ili na lema na familia yake warejee nchini kuendelea na siasa.
Tulizoea haya kutokea kwa majirani zetu na tuliyakemea ikiwemo viongozi wetu waandamizi kushiriki kuwarejesha nchini kwao wakimbizi wakisiasa. Tunalo jukumu lakufuta sifa hii mbaya iliyomea na inayostawi.
Ikumbuke kwa mujibu wa sheria za kimataifa ukimbizi ni hadhi unayopata baada ya wataalam kukaa na kujiridhisha kwamba unastahili.
Kama lema na familia yake wamekubaliwa hifadhi ni udhibitisho kwamba wamepita kwenye mchujo na kufaulu, wameweka ushahidi nakuishawishi Canada kuwapokea. Familia yake itaishi kwa raha na watoto watasoma vizuri zaidi ya hapa ila kila siku kwa maika dahari ya Taifa letu watabaki kusomwa kwenye hiztoria ya Taifa letu Kama tunavyowasoma akina Kambona.
Tujitafakari mara nyingine Tena, Tanzania si sehemu salama? Kama ni sehemu salama kwanini marafiki zetu wa muda mrefu Canada wanautangazia Ulimwengu kwamba tuna wakimbizi wakisiasa? Tujadiliane nao tulifute doa ili na lema na familia yake warejee nchini kuendelea na siasa.
Tulizoea haya kutokea kwa majirani zetu na tuliyakemea ikiwemo viongozi wetu waandamizi kushiriki kuwarejesha nchini kwao wakimbizi wakisiasa. Tunalo jukumu lakufuta sifa hii mbaya iliyomea na inayostawi.