Kitendo alichofanya Huyu Traffic, ameifanya siku yangu iwe hivi...

Bill Lugano

JF-Expert Member
Aug 20, 2018
1,186
6,398
Unaamka asubuhi unawasha gari lako kama ni Range, BMW, Benz, Ford, Audi au Jeep... ambalo jana ulipeleka service wakakagua kila kitu wakamwaga oil na kufanya service nzuri kwa garage za ukweli ambazo unawaachia gari na funguo unaondoka wanakupigia simu au wanakuletea ulipo na INVOICE. unalipa maisha yanaendelea.

So leo ndo umeamka asubuhi gari jana hiyo hiyo uliwaambia wakujazie mafuta TOTAL au PUMA maana hivi ndo vituo vyenye mafuta yanayokubali kwenye gari zako.kwa hiyo ipo full tank. leo unaamka tu unakunywa soup na chapati nne unakunywa na VITAL MALT baridi unawasha gari yako safi kabisa maana walishaosha huko huko.

Umejipulizia perfume nzuri ya bei ya kawaida tu 400,000 -700,000 umevaa kawaida una pens, na raba simple chini, mkononi una saa ya silver na umevaa tshirt nyepesi. gari yako haidawi kitu yaani hata aje kukagua nani hakukuti na kosa. unachukua pesa kiasi unaweka kwenye wallet tsh 350,000 ili angalau zitoshe kwenye wallet halafu nyingine 650,000 unaziweka kwenye gari kwenye ule mkebe wa siri garini. hasa kama unatumia Benz SUV nadhani kwa wenye kutumia hizi gari watakuwa wameuelewa ulipo.huu hata waosha magari huwa hawajui kama upo.

Unaingia barabarani.... huna wasiwasi.unakula muziki taratibu.unaona tu wenye gari za toyota hasa vits,ist,passo and the like wanavyokukwepa wakiogopa kuligusa gari lako. wenye daladala wanasimama na kupita kwa mbali sana na hawataki kabisa kukuchomekea. unajua sometime hata haya magari mnayoendesha yanavutia fujo za wanaendesha dala dala...? uwe na BMW, BENZ,JEEP, FORD and the like then uone kama utachomekewa na wenye daladala au boda boda. mimi nina ushahidi sijawahi chomekewa hata siku moja.

Iwe naendesha Range mojawapo katika zile mbili, iwe naendesha Ford Ranger, iwe naendesha Hii Benz SUV au iwe naendesha VW Tourage. sijawahi chomekewa hata siku moja. na huwa naendesha kwa nidhamu nikifuata sheria zoote barabarani.

Sasa katika hali hiyo traffic ananisimamisha mimi niwe na waswas wa nini? kawaida yangu huwa wakinisimamisha nasimama natulia namsubiri aje hata mlango sifungui. akija nashusha kioo kidogo tu huku natizama mbele namsikiliza. akitaka leseni nampa anaangalia anarudisha mara nyingi huwa wanajikuta hawana cha kusema wananambia tu 'habari za kazi boss' jibu langu huwa fupi sana 'nzuri'

Basi unamwona tu traffic hana la kusema anauma uma maneno then ananambia haya nenda.

HILI LA LEO NDO SABABU YA KUANDIKA HAYA.

Nimeamka kama hivyo nlivyoelezea huko juu. nimefika mitaa ya hapa Fire askari akanipiga mkono. sikufanya hiyana mtu hakatai wito. anakataa aliloitiwa. nikasimama pembeni kama nilivyotakiwa. akaja askari (wa kiume) moja kwa moja akaja dirishani nikashusha kioo kidogo akanisalimia 'habari boss' nikamjibu tu 'nzuri'

Akanambia samahani .. kijana mwenzio nipo vibaya ingawa ni mwisho wa mwezi lakini pesa yoote imeshia kulipa madeni na majukumu mengine naomba unisaidia chochote ndugu yangu nikapate hata soup'

Niseme wazi sijawah mwonea huruma trafiki kama ambavyo leo imenitokea. nilitoa mkanda nikatoa wallet nikahesabu tshe 200,000 nikampatia. jamaa hakuamini. alitamani kabisa anikumbatie. nlikataa na nikamwambia asitie shaka ile si rushwa so hamna haja ya kuficha ficha maana alikuwa anaogopa. nikamwachia biznez card yangu. akanitajia namba yake.... nimeagana naye kiurafiki kabisa.

Jamaa aliomba pesa direct... hakunikagua kagua kunitafutia makosa... hakunipiga beat aliomba kiume. nami nlijisikia heshima kumpatia.hivyo ndivyo siku njema inavyonza unaanza kwa kutengeneza marafiki. kwa kusaidia wenye shida. kwa kuona unaheshimiwa.

Siku kama hii mara nyingi huisha vizuri sana.... natoka ofisini saa saba kamili naelekea white sands kama kuna mwana jamiiforums atakuwa huko naomba tuwasiliane ningependa tuonane na kufahamiana. maana sometime watu huwa wanatamani tufahamiane. ni jambo jema sema inategemeana na mtu mwenyewe yukoje. kama upo huko tuwasiliane ili tujue tutafahamiana vipi maana pia nakuwa makini sana ktk ku make new friends.


NAJUA KUNA WATU MTAKWAZIKA,MTAUMIA NA KUTESEKA SANA. POLENI. KILA MTU ATA SHARE EXPERIENCE YA MAISHA YAKE. USITAKE NIZUNGUMZIE MAISHA YA SHIDA WAKATI SIIFAHAMU SHIDA.WEWE ZUNGUMZIA SHIDA NTAJIFUNZA KWAKO.TUSIPANGIANE MAISHA. YOU EAT WHAT YOU HAVE ....
 
Law of Attraction
download.jpg
download.jpg
 
unaamka asubuhi unawasha gari lako kama ni Range, BMW, Benz, Ford, Audi au Jeep... ambalo jana ulipeleka service wakakagua kila kitu ukamwaga oil na kufanya service nzuri kwa garage za ukweli ambazo unawaachia gari na funguo unaondoka wanakupigia simu au wanakuletea ulipo na INVOICE. unalipa maisha yanaendelea.

so leo ndo umeamka asubuhi gari jana hiyo hiyo uliwaambia wakujazie mafuta TOTAL au PUMA. kwa hiyo ipo full tank. leo unaamka tu unakunywa soup na chapati nne unakunywa na VITAL MALT baridi unawasha gari yako safi kabisa maana walishaosha huko huko.

umejipulizia perfume nzuri ya bei ya kawaid tu 400,000 -700,000 umevaa kawaida una pens, na raba simple chini, mkononi una saa ya silver na umevaa tshirt nyepesi. gari yako haidawi kitu yaani hata aje kukagua nani hakukuti na kosa. unachuku pesa kiasi unaweka kwenye wallet tsh 350,000 ili angalau zitoshe kwenye wallet halafu nyingine 650,000 unaziweka kwenye gari kwenye ule mkebe wa siri garini. hasa kama unatumia Benz SUV nadhani kwa wenye kutumia hizi gari watakuwa wameuelewa ulipo.huu hata waosha magari huwa hawajui kama upo.

unaingia barabarani.... huna wasiwasi.. unaon tu wenye gari za toyota hasa vits,ist,passo and the like wanavyokukwepa wakioga kuligusa gari lako. wenye daladala wanasimama na kupita kwa mbali sana na hawataki kabisa kukuchomekea. unajua sometime hata haya magari mnayoendesha yanavutia fujo za wanapendesha dala dala...? uwe na BMW, BENZ,JEEP, FORD and the like then uone kama utachomekewa na wenye daladala au boda boda. mimi nina ushahidi sijawahi chomekewa hata siku moja.

iwe naendesha Range mojawapo katika zile mbili, iwe naendesha Ford Ranger, iwe naendesha Hii Benz SUV au iwe naendesha VW Tourage. sijawahi chomekewa hata siku moja. na huwa naendesha kwa nidhamu nikifuata sheria zoote barabarani.

sasa katika hali hiyo traffic ananisimamish mimi niwe na waswas wa nini? kawaida yangu huwa wakinisamisha nasimama natulia namsubiri aje hata mlango sifungui. akija nashusha kioo kidogo tu huku natizama mbele namsikiliza. akitaka leseni nampa anaangalia anarudisha mara nyingi huwa wanajikuta hawana cha kusema wananambia tu 'habari za kazi boss' jibu langu huwa fupi sana 'nzuri'

basi unamwona tu traffic hana la kusema anauma uma maneno then ananambia haya nenda.

HILI LA LEO NDO SABABU YA KUANDIKA HAYA.

nimeamka kama hivyo nlivyoelezea huko juu. nimefika mitaa ya hapa Fire askari akanipiga mkono. sikufanya hiyana mtu hakatai wito. anakataa aliloitiwa. nikasimama pembeni kama nilivyotakiwa. akaja askari (wa kiume) moja kwa moja akaja dirishani nikashusha kioo kidogo akanisalimia 'habari boss' nikamjibu tu 'nzuri'

akanambia samahani .. kijana mwenzio nipo vibaya ingawa ni mwisho wa mwezi lakini pesa yoote imeshia kulipa madeni na majukumu mengine naomba unisaidia chochote ndugu yangu nikapate hata soup'

niseme wazi sijawah mwonea huruma trafiki kama ambavyo leo imenitokea. nilitoa mkanda nikatoa wallet nikahesabu tshe 200,000 nikampatia. jamaa hakuamini. alitamani kabisa anikumbatie. nlikataa na nikamwambia asitie shaka ile si rushwa so hamna haja ya kuficha ficha maana alikuwa anaogopa. nikamwachia biznez card yangu. akanitajia namba yake.... nimeagana naye kiurafiki kabisa.

jamaa aliomba pesa direct... hakunikagua kagua kunitafutia makosa... hakunipiga beat aliomba kiume. nami nlijisikia heshima kumpatai. hivyo ndivyo siku njema inavyonza unaanza kwa kutengeneza marafiki. kwa kusaidia wenye shida. kwa kuona unaheshimiwa.

siku kama hii mara nyingi huisha vizuri sana.... natoka ofisini saa saba kamili naelekea white sands kama kuna mwana jamii forums atakuwa huko naomba tuwasiliane ningependa tuonane na kufahamiana. maana sometime watu huwa wanatamani tufahamiane. ni jambo jema sema inategemeana na mtu mwenyewe yukoje. kama upo huko tuwasiliane ili tujue tutafahamiana vipi maana pia nakuwa makini sana ktk ku make new friends.


NAJUA KUNA WATU MTAKWAZIKA. POLENI. KILA MTU ATA SHARE EXPERIENCE YA MAISHA YAKE. TUSIPANGIANE MAISHA. YOU EAT WHAT YOU HAVE ....
Aisee! mambo ni mengi sana duniani!!
 
124 Reactions
Reply
Back
Top Bottom