Kitendawili: Je ni tunda gani muonekano wake wa nje unatisha ila ndani tamu?

Tetramelyz

JF-Expert Member
Apr 25, 2014
4,351
12,396
Kitendawili hiki ni maalumu kwa wale Magreatest Thinkers wanaopendelea na wenye uzoefu wa kula matunda. Ila kama wewe suala la kula matunda mpaka uandikiwe na daktari huwezi kujibu iki kitendawili hata ukipewa miaka mia. Kwahiyo wala husijisumbue kujaribu kutoa jibu utachekesha hata walionuna

Katika matunda yote matamu yanayofaa kuliwa na mwanadamu. Utamu wa tunda unalingana na muonekano wa nje wa tunda lenyewe. Ebu chukulia mfano matunda kama Zabibu (Blackberies), Apples, Passion, Strawberies n.k.
Na hii ni kanuni ya asili ya matunda karibia yote duniani yanayofaa kuliwa na mwanadamu

Lakini kuna tunda moja tu ambalo muonekano wake wa nje na utamu wake wa ndani havilingani kabisa. Na tunda ili linapingana na kanuni ya asili ya matunda. Ingekua utamu wa tunda unalingana na muonekano wake. Tunda hili la ajabu usingelitamani kulila. Manake khaaaa muonekano wake wa nje unatisha lakini...UTAMU wake wa ndani maajabu!

Je tunda ili la ajabu ni tunda gani?🤔
 
Hilo ni Doriani
Heri muonekano wa nje kuliko ile harufu ya duliani inavyochefua! Hata wanakoyaheshumu kama nini nchi kama Malaysia, Thailand na Myanmar kuna tangazo Airport kuwa huruhusiwi kuliingiza kwenye ndege.
 
Back
Top Bottom