MwanajamiiOne
Platinum Member
- Jul 24, 2008
- 10,470
- 6,562
Wandugu habari
Najua VC alishawahi kulileta hili hapa ila naomba tuliangalie kwa jicho lingine!!
Nimelikuta kwenye mjadala mmoja huko
........eti kwenye kitcheni parties mwanamwali hufunzwa jinsi ya kumtunza mume na ndoa yake. Among things ambazo hufundishwa ni eti anatakiwa ampikie, amfulie, amuogeshe, hata akikosea ye aombe msamaha, ampigie magoti,akitupa soxy sebuleni au meza ya kulia yeye aokote tu akafue,akilala sebuleni amuache tu ila yeye kama mke bora kuhama chumba ni MWIKO hata kama ameudhiwa kiasi gani,akirudi saa tisa usiku asimuulize kitu,ampakulie,amuogeshe,na ampe sex at any time T anapotaka mume na sio akitaka yeye mke,asimbishie,akikuta sms za wanawake, akae kimya AVUMILIA TU ndio ukubwa ndio ndoa, akikuta condom kwenye mifuko ya suruali akae kimya na kama imemuuma sana basi asubiri mr akienda kazini asubuhi alia weeee ili akirudi awe ameshakuwa ok and normal,haya tena azoee kummbembeleza tuu na mengi tu yafananayo na hayo.
Wengine wanaambiwa eti wanawake wanaojifanya wajanja wote wako mtaani na talaka zao ila wale wajinga na wanaokubali kuwanyenyekea waume zao ndo wako ndani ya ndoa wanadunda..kwamba ukipigwa futa machozi cheka baadae ongea na mumeo kitandani..na kadhalika..sijui mume akija na rafiki zake akaamua kukuchamba bila sababu kaa kimya wakiondoka bana sauti muulize na mnyuke kwa kufanya naye (best performance)!!...
Kama ni kweli yanafundishwa haya kwenye vicheni pati basi ningekuwa mwanaume ningeziunga mkono.