Kitanzi cha gawio

Malata Junior

JF-Expert Member
Nov 29, 2011
3,102
2,538
Rais Samia Suluhu Hassan amefichua Siri iliyokuwa imefichika kuhusu gawio kwa serikali yaliyokuwa yakitolewa na baadhi ya mashirika na taasisi za umma huku yakiwa yamepata hasara.

Mkuu huyo wa nchi amesema viongozi wa mashirika hayo walikuwa wakikopa fedha benki na kupeleka gawio serikalini ili kuonesha yanatengeneza faida wakati yalikuwa yakijiendesha kwa hasara.

Hali hiyo ilijitokeza katika uongozi wa awamu ya tano ambapo mashirika ya umma yalitakiwa kutoa gawio serikalini,hali iliyozua maswali kwa yale yaliyotoa gawio ilhali yamepata hasara.

Rais Samia amesema viongozi wa mashirika hayo walikuwa wakihangaika huku na kule kuingia benki kukopa kulinda vibarua vyao,ikifika tarehe wahusika hao wanakuja na cheki zao wanatoa gawio lakini ukweli uzalishaji ni ziro.

======

Rais Samia Suluhu Hassan amefichua siri iliyokuwa imefichika kuhusu mali ya gawio kwa Serikali yaliyokuwa yakitolewa na baadhi ya mashirika na taasisi za umma huku yakiwa yamepata hasara.
Mkuu huyo wa nchi amesema viongozi wa mashirika hayo walikuwa wakikopa fedha benki na kupeleka gawio serikalini ili kuonyesha yanatengeneza faida, wakati yalikuwa yakijiendesha kwa hasara.

Hali hiyo ilijitokeza katika uongozi wa Serikali ya awamu ya tano ambapo mashirika ya umma yalitakiwa kutoa gawio serikalini, hali iliyozua maswali kwa yale yaliyotoa gawio hilo ilhali yamepata hasara.

Rais Samia alitoboa siri hiyo jana Ikulu jijini Dar es Salaam, wakati akiwaapisha wakuu wa mikoa, makatibu tawala na kushuhudia viongozi wa taasisi na mashirika ya umma wakila kiapo cha maadili.

Kauli ya Rais Samia ni ya kwanza kuelezea mchezo huo ambao hata Ripoti za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa miaka ya hivi karibuni imekuwa ikibainisha baadhi ya mashirika kujiendesha kwa hasara.

Katika kile unachoweza kusema ni kuwaweka kitanzi, alisema kinachohitajika sasa kufanyika ni jitihada kubwa kuhakikisha mashirika hayo yanaleta tija kwa Taifa.

“Kwa wale wa mashirika, ukweli ni kwamba mashirika yetu hayafanyi vizuri, machache sana yanayofanya vizuri, kwa hiyo tumewapeleka huko kasimamieni ili yafanye kazi vizuri,” alisema.

Akisisitiza eneo hilo, Rais Samia aliyekuwa makamu wa Rais katika awamu ya tano, alisema, “mimi najua miaka iliyopita kuna kipindi maalumu mashirika yalikuwa lazima yanatakiwa yatoe gawio.”

“Kwa kuwa yalikuwa hayafanyi vizuri, wengi wenu mlikuwa mnahangaika huku na kule kuingia benki kukopa kulinda vibaru a vyenu, ikifika terehe husika hao wanakuja na cheki zao wanatoa gawio lakini ukweli uzalishaji ni ziro.”

Aliwataka wakuu wa mashirika yanayofanya vibaya kujirekebisha kwa kuwa hatakuwa tayari kuwavumilia na hatasita kufanya mabadiliko kila atakapoona mambo hayaendi sawa.

Katika hoja hiyo, Dk Donath Olomi ambaye ni mtaalamu wa uchumi na biashara alisema baadhi ya watu wanaokopa ili kulipa gawio wanajua kufanya hivyo si sahihi lakini wanalazimika kulinda vibarua vyao na kuwa gawio linatakiwa litokane na faida.

Profesa Haji Semboja kutoka Chuo kikuu cha Zanzibar alisema moja ya makosa yanayofanyika ni viongozi wa mashirika hayo, wakiwemo wakurugenzi, kuteuliwa na Serikali badala ya kufuata mchakato unaotakiwa wa watu kuomba kazi na kufanyiwa mchujo.

Katika hilo, Kiongozi wa ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe alisema, “ilikuwa inajulikana dhahiri baadhi ya mashirika yalikuwa yanadanganya katika kutoa gawio. Rais kathibitisha tu jambo ambalo wengi tulikuwa tunajua.”
Zitto aliyewahi kuwa mwenyekiti wa kamati ya Bunge ya mashariki ya umma (PAC) alisema, “mashirika ya umma yaweza kuwa chachu kubwa ya maendeleo iwapo Serikali ikiamua yawe hivyo.”

“Mashirika pia yawe huru kuweka fedha zake kwenye benki wazitakazo ili yawe na uhuru wa kusimamia fedha zao,” Zitto aliongeza.”

Wengine matumbo joto
Rais Samia pia alidokeza kwamba kuna mabadiliko mengine ya viongozi yanakuja kwa ngazi ya wakuu wa wilaya, wakurugenzi wa halmashauri , miji, majini na manispaa pamoja na makatibu tawala wa wilaya.
Katika hotuba yake alimtaka Waziri wa Tamisemi, Innocent Bashungwa kuwaandaliwa mafunzo maalumu ya kuwakumbusha wajibu wao.

“Tumefanya tathmini ya makundi yote, maDC (wakuu wa wilaya), wakurugenzi, maDas (makatibu tawala wa wilaya), wote, kwa vyovyote vile tutegemee kuna mabadiliko,” alisema Rais Samia.
“Kwa hiyo kila watakaoingia wafanyiwe mafunzo kama watakayofanyiwa wakuu wa mikoa, kila ngazi kwa aina yake ya mafunzo.”

Alisisitiza lengo la mafunzo hayo ni kukumbushana wajibu wa kazi zao ili mtu yoyote asiseme hakujua alipashwa kufanya nini.

Huduma kwa wananchi
Rais Samia alitumia fursa hiyo kuwasisitiza wakuu wa mikoa na makatibu tawala kujitoa kwa dhati kuwahudumia wananchi kwa kuwa ndiyo jukumu walilokula kiapo kulitekeleza.

“Nendeni mkawahudumie wananchi kwa moyo safi. Huna pengine pa kuhudumia ni Tanzania na ukifanya vizuri Mungu anakunyanyua anakupeleka pazuri, ukifanya vibaya ipo siku ubaya wako utajulikana na utaadhirika,” alisema.

“Mwakilishi wa Rais katika mkoa asiwe na rafiki, kwenda kutengeneza mtandao wa marafiki halafu kazi kwa wananchi hakuna, hilo halikubaliki, hatukuwateua kufanya hayo,” alisema.

Akizungumza kwa sauti ya chini na yenye kutoa ujumbe wa msisitizo, Rais Samia alisema, “tumewatuma mkatumikie wananchi, kafanyeni hivyo bila kuchoka. Kama Rais halali hadi saa tisa usiku wewe usingizi unautoa wapi, mnatuma meseji hadi usiku najibu ina maana silalali, sasa kama mimi silali wewe usingizi unaupataje.”

Magwanda ‘out’
Samia ambaye ni amiri jeshi mkuu, alitoa maagizo kwa wakuu wa mikoa ambao ni wanajeshi na polisi waachane na magwanda kwanza.

“…kwa makanali hatuwatarajii mkivaa kombati wakati mkitekeleza majukumu ya wakuu wa mikoa, ziwekeni pembeni mtazivaa mkirudi jeshini,” alisema.

Kwa miaka ya karibuni umekuwepo mtindi wa viongozi wa kisiasa au watendaji walioteuliwa kutoka jeshini kuvaa magwanda yao ya kijeshi katika utekelezaji wa majukumu yao.

Chanzo: Gazeti la mwananchi
 
Rais Samia Suluhu Hassan amefichua Siri iliyokuwa imefichika kuhusu gawio kwa serikali yaliyokuwa yakitolewa na baadhi ya mashirika na taasisi za umma huku yakiwa yamepata hasara.
Mkuu huyo wa nchi amesema viongozi wa mashirika hayo walikuwa wakikopa fedha benki na kupeleka gawio serikalini ili kuonesha yanatengeneza faida wakati yalikuwa yakijiendesha kwa hasara.
Hali hiyo ilijitokeza katika uongozi wa awamu ya tano ambapo mashirika ya umma yalitakiwa kutoa gawio serikalini,hali iliyozua maswali kwa yale yaliyotoa gawio ilhali yamepata hasara.
Rais Samia amesema viongozi wa mashirika hayo walikuwa wakihangaika huku na kule kuingia benki kukopa kulinda vibarua vyao,ikifika tarehe wahusika hao wanakuja na cheki zao wanatoa gawio lakini ukweli uzalishaji ni ziro.

Chanzo: Gazeti la mwananchi
Kama ilivyo kwa sasa jinsi halmashauri na majiji yanavyojinasibu kwa kukusanya kodi kubwa na kuvuka malengo ilihali mambo ni magumu.

Au wanavyotoa takwimu hewa za chanjo ya covid ili kuwaridhisha wafadhili.
Na jinsi wnavyomrubuni mama anaupiga mwingi wakati hali ya maisha si shwari!
Nchi hii kila kitu ni fake, hakuna uhalisia. Kuanzia historia na kila kitu!
Mambo mengine mi naona ni bora kukaa tu kimya
 
Amenikumbusha jibu la Adam alipoulizwa na MUNGU Kwa nn umefanya kitu nilichokukataza,Adam akajibu "si huyu mwanamke uliyenipa" akamtuoia MUNGU lawama

Ni asili ya binadamu kujitetea na kuwafanya wengine ndy wamekosea zaidi pale anaponyooshewa kidole.Enzi hayo mambo yanafanyika mama si alikuwepo kwenye huo mtumbwi Ila Leo hii anakuja na lawama Kwa mtangulizi wake ( wakati yeye alikuwa makamu).Mtu anakopa mabilioni ya hela na Gavana wa BOT asimsanue mkuu kuna janjajanja inafanyika.Lengo kumuimpress Nani? Mkuu?

Bin' Adam hajawahi kubadilika...
 
Rais Samia Suluhu Hassan amefichua Siri iliyokuwa imefichika kuhusu gawio kwa serikali yaliyokuwa yakitolewa na baadhi ya mashirika na taasisi za umma huku yakiwa yamepata hasara.

Mkuu huyo wa nchi amesema viongozi wa mashirika hayo walikuwa wakikopa fedha benki na kupeleka gawio serikalini ili kuonesha yanatengeneza faida wakati yalikuwa yakijiendesha kwa hasara.

Hali hiyo ilijitokeza katika uongozi wa awamu ya tano ambapo mashirika ya umma yalitakiwa kutoa gawio serikalini,hali iliyozua maswali kwa yale yaliyotoa gawio ilhali yamepata hasara.

Rais Samia amesema viongozi wa mashirika hayo walikuwa wakihangaika huku na kule kuingia benki kukopa kulinda vibarua vyao,ikifika tarehe wahusika hao wanakuja na cheki zao wanatoa gawio lakini ukweli uzalishaji ni ziro.

======

Rais Samia Suluhu Hassan amefichua siri iliyokuwa imefichika kuhusu mali ya gawio kwa Serikali yaliyokuwa yakitolewa na baadhi ya mashirika na taasisi za umma huku yakiwa yamepata hasara.
Mkuu huyo wa nchi amesema viongozi wa mashirika hayo walikuwa wakikopa fedha benki na kupeleka gawio serikalini ili kuonyesha yanatengeneza faida, wakati yalikuwa yakijiendesha kwa hasara.

Hali hiyo ilijitokeza katika uongozi wa Serikali ya awamu ya tano ambapo mashirika ya umma yalitakiwa kutoa gawio serikalini, hali iliyozua maswali kwa yale yaliyotoa gawio hilo ilhali yamepata hasara.

Rais Samia alitoboa siri hiyo jana Ikulu jijini Dar es Salaam, wakati akiwaapisha wakuu wa mikoa, makatibu tawala na kushuhudia viongozi wa taasisi na mashirika ya umma wakila kiapo cha maadili.

Kauli ya Rais Samia ni ya kwanza kuelezea mchezo huo ambao hata Ripoti za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa miaka ya hivi karibuni imekuwa ikibainisha baadhi ya mashirika kujiendesha kwa hasara.

Katika kile unachoweza kusema ni kuwaweka kitanzi, alisema kinachohitajika sasa kufanyika ni jitihada kubwa kuhakikisha mashirika hayo yanaleta tija kwa Taifa.

“Kwa wale wa mashirika, ukweli ni kwamba mashirika yetu hayafanyi vizuri, machache sana yanayofanya vizuri, kwa hiyo tumewapeleka huko kasimamieni ili yafanye kazi vizuri,” alisema.

Akisisitiza eneo hilo, Rais Samia aliyekuwa makamu wa Rais katika awamu ya tano, alisema, “mimi najua miaka iliyopita kuna kipindi maalumu mashirika yalikuwa lazima yanatakiwa yatoe gawio.”

“Kwa kuwa yalikuwa hayafanyi vizuri, wengi wenu mlikuwa mnahangaika huku na kule kuingia benki kukopa kulinda vibaru a vyenu, ikifika terehe husika hao wanakuja na cheki zao wanatoa gawio lakini ukweli uzalishaji ni ziro.”

Aliwataka wakuu wa mashirika yanayofanya vibaya kujirekebisha kwa kuwa hatakuwa tayari kuwavumilia na hatasita kufanya mabadiliko kila atakapoona mambo hayaendi sawa.

Katika hoja hiyo, Dk Donath Olomi ambaye ni mtaalamu wa uchumi na biashara alisema baadhi ya watu wanaokopa ili kulipa gawio wanajua kufanya hivyo si sahihi lakini wanalazimika kulinda vibarua vyao na kuwa gawio linatakiwa litokane na faida.

Profesa Haji Semboja kutoka Chuo kikuu cha Zanzibar alisema moja ya makosa yanayofanyika ni viongozi wa mashirika hayo, wakiwemo wakurugenzi, kuteuliwa na Serikali badala ya kufuata mchakato unaotakiwa wa watu kuomba kazi na kufanyiwa mchujo.

Katika hilo, Kiongozi wa ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe alisema, “ilikuwa inajulikana dhahiri baadhi ya mashirika yalikuwa yanadanganya katika kutoa gawio. Rais kathibitisha tu jambo ambalo wengi tulikuwa tunajua.”
Zitto aliyewahi kuwa mwenyekiti wa kamati ya Bunge ya mashariki ya umma (PAC) alisema, “mashirika ya umma yaweza kuwa chachu kubwa ya maendeleo iwapo Serikali ikiamua yawe hivyo.”

“Mashirika pia yawe huru kuweka fedha zake kwenye benki wazitakazo ili yawe na uhuru wa kusimamia fedha zao,” Zitto aliongeza.”

Wengine matumbo joto
Rais Samia pia alidokeza kwamba kuna mabadiliko mengine ya viongozi yanakuja kwa ngazi ya wakuu wa wilaya, wakurugenzi wa halmashauri , miji, majini na manispaa pamoja na makatibu tawala wa wilaya.
Katika hotuba yake alimtaka Waziri wa Tamisemi, Innocent Bashungwa kuwaandaliwa mafunzo maalumu ya kuwakumbusha wajibu wao.

“Tumefanya tathmini ya makundi yote, maDC (wakuu wa wilaya), wakurugenzi, maDas (makatibu tawala wa wilaya), wote, kwa vyovyote vile tutegemee kuna mabadiliko,” alisema Rais Samia.
“Kwa hiyo kila watakaoingia wafanyiwe mafunzo kama watakayofanyiwa wakuu wa mikoa, kila ngazi kwa aina yake ya mafunzo.”

Alisisitiza lengo la mafunzo hayo ni kukumbushana wajibu wa kazi zao ili mtu yoyote asiseme hakujua alipashwa kufanya nini.

Huduma kwa wananchi
Rais Samia alitumia fursa hiyo kuwasisitiza wakuu wa mikoa na makatibu tawala kujitoa kwa dhati kuwahudumia wananchi kwa kuwa ndiyo jukumu walilokula kiapo kulitekeleza.

“Nendeni mkawahudumie wananchi kwa moyo safi. Huna pengine pa kuhudumia ni Tanzania na ukifanya vizuri Mungu anakunyanyua anakupeleka pazuri, ukifanya vibaya ipo siku ubaya wako utajulikana na utaadhirika,” alisema.

“Mwakilishi wa Rais katika mkoa asiwe na rafiki, kwenda kutengeneza mtandao wa marafiki halafu kazi kwa wananchi hakuna, hilo halikubaliki, hatukuwateua kufanya hayo,” alisema.

Akizungumza kwa sauti ya chini na yenye kutoa ujumbe wa msisitizo, Rais Samia alisema, “tumewatuma mkatumikie wananchi, kafanyeni hivyo bila kuchoka. Kama Rais halali hadi saa tisa usiku wewe usingizi unautoa wapi, mnatuma meseji hadi usiku najibu ina maana silalali, sasa kama mimi silali wewe usingizi unaupataje.”

Magwanda ‘out’
Samia ambaye ni amiri jeshi mkuu, alitoa maagizo kwa wakuu wa mikoa ambao ni wanajeshi na polisi waachane na magwanda kwanza.

“…kwa makanali hatuwatarajii mkivaa kombati wakati mkitekeleza majukumu ya wakuu wa mikoa, ziwekeni pembeni mtazivaa mkirudi jeshini,” alisema.

Kwa miaka ya karibuni umekuwepo mtindi wa viongozi wa kisiasa au watendaji walioteuliwa kutoka jeshini kuvaa magwanda yao ya kijeshi katika utekelezaji wa majukumu yao.

Chanzo: Gazeti la mwananchi
Hivi kwanini taasisi ya urais isishtakiwe kwa makoso ya yule fedhuli?
Wapo majahili wamebaki waliomshauri wakamatwe wajibu hoja haraka.
 
Niseme kitu kimoja Magufuli alitaka wawajibike

Hata NGO kama kanisa katoliki ni Non profit organisation

Non Profit organisation sio kwamba ni mashirika yasoyotengeneza faida la hasha!! Uongo.Yanatengeneza faida lakini faida ile inatumika kuongeza huduma zaidi hazitumiki kwenye gawio

Mfano kanisa katoliki ni NGO ambayo ni Non Profit Organisation lakini shule zake ada inasoma mamilioni. Na zinapata faida lakini faida zile wanazirudisha kuboresha zaidi shule zao na kutungua nyingine mpya nzuri nk

Magufuli kuna watu hawamwelewi alichoka kuwa sawa shirika halitakiwi kutoa gawio lakini linajiendesha kea hasara Serikali kila siku inatakiwa ipeleke pesa wajiendeshe!! Ndio akawakomalia leteni gawio vinginevyo nawatumbua wajinga nyie ndio wakaanza kukimbizana

Non Profit organisation or Company maana yake sio loss making organisation au company. Ni kuwa Profit wapatazo wanarudisha kuongeza mtaji na ku improve haziendi kwenye gawio

Kinana kaungana na Magufuli kasema mashirika yote yanayotegemea tozo yafutwe!! Naunga mkono hoja hawaelewi nini maana ya Non Profit Organisation au Company hata iwe kampuni ya Serikali wafutwe

Haiwezekani Serikali iwe kutwa inachukua pesa za walipa kodi tu kuwapa gharama za uendeshaji

Magufuli alikuwa na madhaifu mengi lakini hili la kuwakomalia watoe gawio ilikuwa kuwaamsha kuwa wake up mjiendeshe kwa faida msichukue kodi za wananchi wanyonge

Kinana very Bright kaja na very aggressive decision kali kuliko ya Magufuli kuwa wategemea tozo kujiendesha wajiandae mashirika yao kufa

Magufuli was right ila alikuwa too moderate

Kinana yuko more Radical kuliko Magufuli kuhusu hiyo issue na mu support hundred percent
 
Niseme kitu kimoja Magufuli alitaka wawajibike

Hata NGO kama kanisa katoliki ni Non profit organisation

Non Profit organisation sio kwamba ni mashirika yasoyotengeneza faida la hasha!! Uongo.Yanatengeneza faida lakini faida ile inatumika kuongeza huduma zaidi hazitumiki kwenye gawio

Mfano kanisa katoliki ni NGO ambayo ni Non Profit Organisation lakini shule zake ada inasoma mamilioni. Na zinapata faida lakini faida zile wanazirudisha kuboresha zaidi shule zao na kutungua nyingine mpya nzuri nk

Magufuli kuna watu hawamwelewi alichoka kuwa sawa shirika halitakiwi kutoa gawio lakini linajiendesha kea hasara Serikali kila siku inatakiwa ipeleke pesa wajiendeshe!! Ndio akawakomalia leteni gawio vinginevyo nawatumbua wajinga nyie ndio wakaanza kukimbizana

Non Profit organisation or Company maana yake sio loss making organisation au company. Ni kuwa Profit wapatazo wanarudisha kuongeza mtaji na ku improve haziendi kwenye gawio

Kinana kaungana na Magufuli kasema mashirika yote yanayotegemea tozo yafutwe!! Naunga mkono hoja hawaelewi nini maana ya Non Profit Organisation au Company hata iwe kampuni ya Serikali wafutwe

Haiwezekani Serikali iwe kutwa inachukua pesa za walipa kodi tu kuwapa gharama za uendeshaji

Magufuli alikuwa na madhaifu mengi lakini hili la kuwakomalia watoe gawio ilikuwa kuwaamsha kuwa wake up mjiendeshe kwa faida msichukue kodi za wananchi wanyonge

Kinana very Bright kaja na very aggressive decision kali kuliko ya Magufuli kuwa wategemea tozo kujiendesha wajiandae mashirika yao kufa

Magufuli was right ila alikuwa too moderate

Kinana yuko more Radical kuliko Magufuli kuhusu hiyo issue na mu support hundred percent
Kwahio kwa maana nyingine wakurugenzi wa mashirika walikuwa wanaendeshewa mashirika yao kwa gharama za raia ilihali mashirika hayo yanakamua tozo toka kwa raia hao hao 😂😂😂 inashangaza mno eti shirika linajiendesha kwa hasara wakati linakusanya hela toka kwa raia.
 
Ile kitu sijui Magufuli alikuwa anam fool nani? Eti unapokea dividend kutoka UDSM? MNH? Wanazalisha nini na wanaingiza nini?

Hivi ndiyo vitu ambavyo wafuasi wa Mwendazake wanasema Mama anapwaya. Nafuu wendelee kusema viatu havimtoshi kuliko ku-brain wash watu kwa takwimu za UWONGO

Kuna wakati TTCL walitowa dividend ya Tsh 2.1 Bilion mnamo March 2019, halafu after two months wakapeleka andiko Serikalini la kutaka guarantee wakope Tsh 360 Billion. That was madness
 
Kwahio kwa maana nyingine wakurugenzi wa mashirika walikuwa wanaendeshewa mashirika yao kwa gharama za raia ilihali mashirika hayo yanakamua tozo toka kwa raia hao hao 😂😂😂 inashangaza mno eti shirika linajiendesha kwa hasara wakati linakusanya hela toka kwa raia.
Uko sahihi

Mfano makanisa huanzishwa kwa mtaji wa sadaka za waumini kama Non Profit organisation mfano kanisa katoliki

Lakini it doesn't mean kuwa wabishi tu kwa sadaka sababu wasingeweza ku expand dunia nzima

Ndio maana sadaka zile wakipata hawabweteki hufungua miradi kibao iwe shule,vyuo,Hospitali ,biashara eg Msimbazi centre Dar ,mashamba nk Profit making enterprises zenye leseni na kodi wakilipa
Profit wapatazo hawagawani huzitumia for Non Profit Organisation activities Expansion na kuprovide better services etc na hao wanaijua hayo ni mapadri na masista waliosoma elimu tu ya dini

How comes jitu limesomea Uchumi na Business administration lina hadi Masters degree au PhD linategemea Tozo au Ruzuku kujiendesha na halijui maana ya Non Profit Organisation au Company? Hopeless kabisa

Magufuli aliwakomalia kuwa you hopeless haujielewi hata hapo upo unatakiwa kufanya nini.Nipe gawio mjinga wewe
 
Ile kitu sijui Magufuli alikuwa anam fool nani? Eti unapokea dividend kutoka UDSM? MNH? Wanazalisha nini na wanaingiza nini?

Hivi ndiyo vitu ambavyo wafuasi wa Mwendazake wanasema Mama anapwaya. Nafuu wendelee kusema viatu havimtoshi kuliko ku-brain wash watu kwa takwimu za UWONGO

Kuna wakati TTCL walitowa dividend ya Tsh 2.1 Bilion mnamo March 2019, halafu after two months wakapeleka andiko Serikalini la kutaka guarantee wakope Tsh 360 Billion. That was madness
Hatari kweli kweli... uongo umehalalishwa hii nchi.
 
Kwahio kwa maana nyingine wakurugenzi wa mashirika walikuwa wanaendeshewa mashirika yao kwa gharama za raia ilihali mashirika hayo yanakamua tozo toka kwa raia hao hao 😂😂😂 inashangaza mno eti shirika linajiendesha kwa hasara wakati linakusanya hela toka kwa raia.
Kifupi hakuna Non Profit Organisation au Company yeyote duniani zinazoweza survive kwa donations za donors, au sadaka au Ruzuku au tozo forever.

Zile zinakuwa seed Capital tu sio Surviving money or donations!!! That will last forever!! Kuendesha Non Profit organisation or Company wanatakiwa kujiongeza
 
Uko sahihi

Mfano makanisa huanzishwa kwa mtaji wa sadaka za waumini kama Non Profit organisation mfano kanisa katoliki

Lakini it doesn't mean kuwa wabishi tu kwa sadaka sababu wasingeweza ku expand dunia nzima

Ndio maana sadaka zile wakipata hawabweteki hufungua miradi kibao iwe shule,vyuo,Hospitali ,biashara eg Msimbazi centre Dar ,mashamba nk Profit making enterprises zenye leseni na kodi wakilipa
Profit wapatazo hawagawani huzitumia for Non Profit Organisation activities Expansion na kuprovide better services etc na hao wanaijua hayo ni mapadri na masista waliosoma elimu tu ya dini

How comes jitu limesomea Uchumi na Business administration lina hadi Masters degree au PhD linategemea Tozo au Ruzuku kujiendesha na halijui maana ya Non Profit Organisation au Company? Hopeless kabisa

Magufuli aliwakomalia kuwa you hopeless haujielewi hata hapo upo unatakiwa kufanya nini.Nipe gawio mjinga wewe
Umenichekesha sana hapo kwenye lina phd linategemea tozo...😀
Halafu linaogopa kukusanya kwenye mashirika?!

Mwananchi wa kawaida anatengenez faida gani hadi ailipe serikali tozo? Yaani nchi hii kuna mambo yanatia hasira basi tu!
 
Ile kitu sijui Magufuli alikuwa anam fool nani? Eti unapokea dividend kutoka UDSM? MNH? Wanazalisha nini na wanaingiza nini?

Hivi ndiyo vitu ambavyo wafuasi wa Mwendazake wanasema Mama anapwaya. Nafuu wendelee kusema viatu havimtoshi kuliko ku-brain wash watu kwa takwimu za UWONGO

Kuna wakati TTCL walitowa dividend ya Tsh 2.1 Bilion mnamo March 2019, halafu after two months wakapeleka andiko Serikalini la kutaka guarantee wakope Tsh 360 Billion. That was madness
TTCL kushindwa kutoa gawio ni uzembe. Mbona makampuni kama Halotel, Airtel nk yameikuta na yanaendelea vizuri tu?
 
Ile kitu sijui Magufuli alikuwa anam fool nani? Eti unapokea dividend kutoka UDSM? MNH? Wanazalisha nini na wanaingiza nini?
Unaijua BICO? Unaijua Mlimani City? Unajua kuna vyuo vikuu hapa nchini vinajiendesha kwa ada za wanafunzi tu? Ada hiyo hiyo wanalipa mishahara na gharama nyingine za uendeshaji. Lakini vyuo kama UDSM wanalipiwa mishahara, wanapewa OC kwa ajili ya gharama za uendeshaji na pesa za ujenzi wanapelekewa. Huoni kuwa kulikuwa na sababu kuwafanya wawajibike zaidi hata kwa kuambiwa walipe gawio?
 
Kuna wakati TTCL walitowa dividend ya Tsh 2.1 Bilion mnamo March 2019, halafu after two months wakapeleka andiko Serikalini la kutaka guarantee wakope Tsh 360 Billion. That was madness
Kati ya shirika ambalo niliwaona ni vilaza ni TTCL, unajua kuna kipindi watumishi wote wa umma wanastatili kupata airtime allowance walitakiwa kuwa na laini za TTCL? Nao ni watu ambao wana watu wengi nyuma yao. Kiasi kwamba kama wangewekea kivutio fulani wangewataka wategemezi wao watafute laini za TTCL. Kwa kufanya hivyo TTCL ingejikuta inapata wateja sawa na akina voda na tigo. Lakini ajabu hao TTCL licha ya hiyo favour bado inazidiwa wateja na Halotel.
 
TTCL kushindwa kutoa gawio ni uzembe. Mbona makampuni kama Halotel, Airtel nk yameikuta na yanaendelea vizuri tu?
Kifupi Serikali itafute mapadri na masista wa katoliki wawakalishe chini seminar viongozi wote wakuu wa mashirika ya Serikali Non Profit Government companies wawape elimu nini maana ya Non Profit Government organisation

It seems wako hopeless na hiyo knowledge hawana

Mama Samia wasiliana na Kanisa katoliki wazoefu wa uendeshaji wa Non Profit Organisation au companies dunia nzima wawape seminar hao wajinga ambao Serikali imewapa nafasi za kuwa mabosi wakati vichwani hamna kitu wanadhani Non Profit organisation or Company huhitaji kupata Profit!!!

Au vinginevyo teua mapadri na masista wa Katoliki waongoze hizo taasisi za hao wasiojielewa .Kaombe Kanisa Katoliki wakupe mapadri,masista au mabruda. Wanao kibao

Benki kuu ya Kenya baada ya kuona ufisadi benki ya Kenya unatisha Kenyatta alikimbilia kanisa katoliki wamupe mtu ndio wakampa Bruda wa kikatoliki Gavana wa sasa wa Benki kuu ya Kenya

Msiojua Bruda ni nani ni kama Sista wa kikatoliki .Sista anakuwa mwanamke na Bruda Mwanaume.Wote ni watumishi permanent wa kanisa walioapa kutoa au kuolewa au kuwa na familia
 
Rais Samia Suluhu Hassan amefichua Siri iliyokuwa imefichika kuhusu gawio kwa serikali yaliyokuwa yakitolewa na baadhi ya mashirika na taasisi za umma huku yakiwa yamepata hasara.

Mkuu huyo wa nchi amesema viongozi wa mashirika hayo walikuwa wakikopa fedha benki na kupeleka gawio serikalini ili kuonesha yanatengeneza faida wakati yalikuwa yakijiendesha kwa hasara.

Hali hiyo ilijitokeza katika uongozi wa awamu ya tano ambapo mashirika ya umma yalitakiwa kutoa gawio serikalini,hali iliyozua maswali kwa yale yaliyotoa gawio ilhali yamepata hasara.

Rais Samia amesema viongozi wa mashirika hayo walikuwa wakihangaika huku na kule kuingia benki kukopa kulinda vibarua vyao,ikifika tarehe wahusika hao wanakuja na cheki zao wanatoa gawio lakini ukweli uzalishaji ni ziro.

======

Rais Samia Suluhu Hassan amefichua siri iliyokuwa imefichika kuhusu mali ya gawio kwa Serikali yaliyokuwa yakitolewa na baadhi ya mashirika na taasisi za umma huku yakiwa yamepata hasara.
Mkuu huyo wa nchi amesema viongozi wa mashirika hayo walikuwa wakikopa fedha benki na kupeleka gawio serikalini ili kuonyesha yanatengeneza faida, wakati yalikuwa yakijiendesha kwa hasara.

Hali hiyo ilijitokeza katika uongozi wa Serikali ya awamu ya tano ambapo mashirika ya umma yalitakiwa kutoa gawio serikalini, hali iliyozua maswali kwa yale yaliyotoa gawio hilo ilhali yamepata hasara.

Rais Samia alitoboa siri hiyo jana Ikulu jijini Dar es Salaam, wakati akiwaapisha wakuu wa mikoa, makatibu tawala na kushuhudia viongozi wa taasisi na mashirika ya umma wakila kiapo cha maadili.

Kauli ya Rais Samia ni ya kwanza kuelezea mchezo huo ambao hata Ripoti za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa miaka ya hivi karibuni imekuwa ikibainisha baadhi ya mashirika kujiendesha kwa hasara.

Katika kile unachoweza kusema ni kuwaweka kitanzi, alisema kinachohitajika sasa kufanyika ni jitihada kubwa kuhakikisha mashirika hayo yanaleta tija kwa Taifa.

“Kwa wale wa mashirika, ukweli ni kwamba mashirika yetu hayafanyi vizuri, machache sana yanayofanya vizuri, kwa hiyo tumewapeleka huko kasimamieni ili yafanye kazi vizuri,” alisema.

Akisisitiza eneo hilo, Rais Samia aliyekuwa makamu wa Rais katika awamu ya tano, alisema, “mimi najua miaka iliyopita kuna kipindi maalumu mashirika yalikuwa lazima yanatakiwa yatoe gawio.”

“Kwa kuwa yalikuwa hayafanyi vizuri, wengi wenu mlikuwa mnahangaika huku na kule kuingia benki kukopa kulinda vibaru a vyenu, ikifika terehe husika hao wanakuja na cheki zao wanatoa gawio lakini ukweli uzalishaji ni ziro.”

Aliwataka wakuu wa mashirika yanayofanya vibaya kujirekebisha kwa kuwa hatakuwa tayari kuwavumilia na hatasita kufanya mabadiliko kila atakapoona mambo hayaendi sawa.

Katika hoja hiyo, Dk Donath Olomi ambaye ni mtaalamu wa uchumi na biashara alisema baadhi ya watu wanaokopa ili kulipa gawio wanajua kufanya hivyo si sahihi lakini wanalazimika kulinda vibarua vyao na kuwa gawio linatakiwa litokane na faida.

Profesa Haji Semboja kutoka Chuo kikuu cha Zanzibar alisema moja ya makosa yanayofanyika ni viongozi wa mashirika hayo, wakiwemo wakurugenzi, kuteuliwa na Serikali badala ya kufuata mchakato unaotakiwa wa watu kuomba kazi na kufanyiwa mchujo.

Katika hilo, Kiongozi wa ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe alisema, “ilikuwa inajulikana dhahiri baadhi ya mashirika yalikuwa yanadanganya katika kutoa gawio. Rais kathibitisha tu jambo ambalo wengi tulikuwa tunajua.”
Zitto aliyewahi kuwa mwenyekiti wa kamati ya Bunge ya mashariki ya umma (PAC) alisema, “mashirika ya umma yaweza kuwa chachu kubwa ya maendeleo iwapo Serikali ikiamua yawe hivyo.”

“Mashirika pia yawe huru kuweka fedha zake kwenye benki wazitakazo ili yawe na uhuru wa kusimamia fedha zao,” Zitto aliongeza.”

Wengine matumbo joto
Rais Samia pia alidokeza kwamba kuna mabadiliko mengine ya viongozi yanakuja kwa ngazi ya wakuu wa wilaya, wakurugenzi wa halmashauri , miji, majini na manispaa pamoja na makatibu tawala wa wilaya.
Katika hotuba yake alimtaka Waziri wa Tamisemi, Innocent Bashungwa kuwaandaliwa mafunzo maalumu ya kuwakumbusha wajibu wao.

“Tumefanya tathmini ya makundi yote, maDC (wakuu wa wilaya), wakurugenzi, maDas (makatibu tawala wa wilaya), wote, kwa vyovyote vile tutegemee kuna mabadiliko,” alisema Rais Samia.
“Kwa hiyo kila watakaoingia wafanyiwe mafunzo kama watakayofanyiwa wakuu wa mikoa, kila ngazi kwa aina yake ya mafunzo.”

Alisisitiza lengo la mafunzo hayo ni kukumbushana wajibu wa kazi zao ili mtu yoyote asiseme hakujua alipashwa kufanya nini.

Huduma kwa wananchi
Rais Samia alitumia fursa hiyo kuwasisitiza wakuu wa mikoa na makatibu tawala kujitoa kwa dhati kuwahudumia wananchi kwa kuwa ndiyo jukumu walilokula kiapo kulitekeleza.

“Nendeni mkawahudumie wananchi kwa moyo safi. Huna pengine pa kuhudumia ni Tanzania na ukifanya vizuri Mungu anakunyanyua anakupeleka pazuri, ukifanya vibaya ipo siku ubaya wako utajulikana na utaadhirika,” alisema.

“Mwakilishi wa Rais katika mkoa asiwe na rafiki, kwenda kutengeneza mtandao wa marafiki halafu kazi kwa wananchi hakuna, hilo halikubaliki, hatukuwateua kufanya hayo,” alisema.

Akizungumza kwa sauti ya chini na yenye kutoa ujumbe wa msisitizo, Rais Samia alisema, “tumewatuma mkatumikie wananchi, kafanyeni hivyo bila kuchoka. Kama Rais halali hadi saa tisa usiku wewe usingizi unautoa wapi, mnatuma meseji hadi usiku najibu ina maana silalali, sasa kama mimi silali wewe usingizi unaupataje.”

Magwanda ‘out’
Samia ambaye ni amiri jeshi mkuu, alitoa maagizo kwa wakuu wa mikoa ambao ni wanajeshi na polisi waachane na magwanda kwanza.

“…kwa makanali hatuwatarajii mkivaa kombati wakati mkitekeleza majukumu ya wakuu wa mikoa, ziwekeni pembeni mtazivaa mkirudi jeshini,” alisema.

Kwa miaka ya karibuni umekuwepo mtindi wa viongozi wa kisiasa au watendaji walioteuliwa kutoka jeshini kuvaa magwanda yao ya kijeshi katika utekelezaji wa majukumu yao.

Chanzo: Gazeti la mwananchi
Si kweli, hiyo mikopo walikuwa wanakopa benki za wapi ilihali mashirika yalizuiwa kukopa? Kama Rais anajua kilichokuwa kinafanyika ni uongo kwa nini asiwaondoe hao waliokuwa wanafanya hivyo? Maana hiyo ni jinai kabisa, au anafurahia kuretain watu waongo km viongozi wa mashirika..wakikosea atapata wapi ujasiri wa kuwawajibisha km makosa waliyofanya hapo nyuma ameyafumbia macho, kwa sababu hawamdanganyi Rais tu, wanatukosea sisi sote..sidhani km ni kweli jambo hili.
 
Kifupi Mama Samia azingatie ushauri wa Makamu Mwenyekiti Kinana kufuta Non Profit government organisation or companies

Ila namuomba Mama Samia Awape miezi sita tu waje na strategy za ku turn their companies as Profit making organisations zisizotegemea Ruzuku

Mheshimiwa Kinana nakuheshimu ushauri wako uko sahihi mia kwa mia wa kuyafuta mashirika yote tegemea tozo na Ruzuku nawaombea kwako grace period ya miezi sita itakayogawanyika kama ifuatavyo

Ndani ya miezi mitatu kuanzia September mosi walete mpango mkakati wa namba atakavyo turn around hizo Company kwa hela ruzuku hizo hizo walizopewa kwenye bajeti iliyopitishwa ruksa kufanya mabadiliko ya matumizi as long as Serikali haita inject new money.Miezi mitatu ni ya kuangalia implementation.

Wakishindwa wazo lako Mheshimiwa Kinana lifanyiwe kazi haraka futa

Kama ni la Serikali linajifanya jeuri binafsisha tangaza mnada sokoni uzia private sector
 
Back
Top Bottom