Kitabu kipya: Dola, Kanisa na Tatizo la Udini Tanzania

Tafuta kitabu cha Padri Sivallon kinaitwa Kanisa Katoliki na Siasa za Tanzania bara , utajua kanisa ni nini
Gavana,
Hivyo vitabu viwili hapo chini vilitaabisha sana Kanisa kwa kuwa yale yaliyoandikwa ndani ya kitabu yalidhihirisha mipango ambayo haikutakiwa ifahamike.

Ilipokuja kufahamika athari yake ikawa hakuna tena la kufanya siri zote ziko nje.

Hatua ambayo ilichukuliwa ni kwa kitabu cha Sivalon kisichapwe tena na cha Bergen kisiingizwe tena Tanzania.

Mna nini cha kutisha ndani ya vitabu hivi?

Prof. Njozi katika kitabu chake, ''Mwembechai Killings...'' (2002) alisherehesha vizuri vitabu hivi.

Yawezekana hii ndiyo sababu ya kitabu chake kupigwa marufuku.

Nasoma matusi na kejeli najisemea hawa ni watu kama mimi lakini wao wako upande ambao unanufaika hawawezi kuwa na fikra kama zangu muhimu kwangu ni kutuliza akili na kujaribu kufahamisha kuwa haya niandikayo si uchochezi ni tatizo la kweli ambalo iko siku litatuangamiza sisi sote kwani mficha maradhi kifo kitamfichua.

1575208830118.png


1575209008579.png
 
Mohamed Said, ]Mzee wangu Mohamed Said;
Kwanza kabisa kwa moyo wa dhati nikupe hongera kwa uthubutu wa kuendelea kuandika,na nakushauri endelea kufanya kazi hiyo hadi pale Mola wako atakapokuita,utakuwa umetuachia hazina safi sisi na vizazi vyetu.
Pili,sifurahishi sana baadhi ya maoni yatolewayo na baadhi ya watu kuhusu kitabu chako na shutuma zinazotolewa juu yako,si busara hata kidogo kukuita majina yasiyoendana na umri wala hulka yako,mfano,mchochezi,mfitinishaji nk.
Nasema si busara kwa sababu zifuatazo;

1: Wote wanaokushutumu hawajasoma kitabu chako;hata ukiwauliza wanukuu japo mstari mmoja kutoka humu kitabuni hawawezi na wala hawajui nini kilichoandikwa ndani yake.
*Busara ilikuwa ni kununua kitabu na kukisoma,ikiwa kina tatizo hoja zingejengwa juu ya contents na sio abstract ideas,ambazo mkosoaji hajui ni nini anakosoa ila tu anatumia ufundi wa maneno,hili ni kosa ndugu zangu.

2: Kutajwa kwa neno "kanisa" haiwezi kukifanya kitabu kizima tu kiwe INVALID kisa kutajwa kwa neno kanisa.Huu ni wakati wa kuwa huru kifkira na kimtazamo,ikiwa tu tutataka kusikia ama kusoma kile tu kinachoendana na mawazo yetu na kinachotufurahisha tunakuwa si viumbe huru bali wafungwa wa mawazo.

3: Kuficha historia/ukweli wa mambo mabaya/uovu uliotendwa nyuma na watu,dini,dhehebu au mtu kwa kigezo cha teknolojia hakiifanyi jamii kuwa salama bali hujenga chuki za ndani kabisa na mwisho wa siku madhara huwa mabaya zaidi ya kama ingesemwa na kukemewa hadharani na kutafuta suluhu.

4:Mimi nikiwa mkristo nakushukuru mzee wangu,nitakitafuta kitabu nitasoma,hakuna mwisho wa kujifunza na kupata maarifa hakuchagui yametolewa na nani,ana nini,anaamini nini,yuko wapi na wakati gani?..

Swali;Leo tunajifunza historia za biashara ya Watumwa (Slave trade),American civil War,Socialism,WW1 & WWII,Cold war,Jews massacre,Maji maji,nk; matukia haya yote yalishapita,lengo la kujifunza ni nini basi?.

- Je;lengo ni kutufanya tuwe waovu kama waliowafanya babu zetu watumwa na kuwafunga minyororo na kuwatumikisha?.

- Au ni kutufanya tujifunze kuuwa wanadamu wenzetu kama Hitler na Mussolini?.

Na je,kujifunza historia hii ya mzee wetu ndiyo italeta chuki na madhara kwa jamii,zaidi ya hizi za Mkwawa kukatwa kichwa na wajerumani,Au mfalme Leopolds kuwakata mikono babu zetu wenye ujuzi?.

Bila shaka kuna la kujifunza kwa mwenye kufikiri.
 
Mohamed Said,Kumbe mnazungumzia Dhehebu la Kanisa Katoliki na Sio Ukristo kwa ujumla wake yaani Madhehebu mengine Mnavyotaja Kanisa? Kama mnataka kuwataja Romani katoliki kuhusu siasa za Tanzania Bara...msihusishe Kanisa kama Ukristo wote Kiujumla...hatutaelewana
 
Rusumo,
Kuna mtu kaniuliza tafsiri ya hiyo cover.
Mimi sijui kwani usanifu wa cover kafanya publisher.

Nitamuuliza In Shaa Allah.
Kitabu hiki muombe mtu akununulie hapa Dar es Salaam.
Kitabu chako mwenyewe hujui tafsiri ya covw
er?

Hujaukiza na kupitisha?

Unaweza kuwekewa alama za Nazi kwenye cover usijue.

Ukashangaa watu hawanunui kitabu kwa nini.
 
Kitabu chako mwenyewe hujui tafsiri ya covw
er?

Hujaukiza na kupitisha?

Unaweza kuwekewa alama za Nazi kwenye cover usijue.

Ukashangaa watu hawanunui kitabu kwa nini.
Kiranga,
Hapana sijapata kuandika kitabu nikashauriwa kuhusu cover.
Kawaida baada ya kukamilika uhariri kitabu kinachapwa.

Mimi sijashughulishwa na cover ya kitabu.

Unadhani kwa kiwango changu cha uandishi na watu wanaochapa kazi zangu kama Oxford University Press, Ibn Hazm Media Centre, Abantu Publications wanaweza wakaweka picha ya Auschwitz kwenye cover ya kitabu?

Vitabu niandikavyo vyote vina mauzo mazuri.

Alhamdulilah kama uonavyo hapa mkiona jina langu mnavyojazana kunisikiliza na vitabu ni hivyo hivyo.
 
Kumbe mnazungumzia Dhehebu la Kanisa Katoliki na Sio Ukristo kwa ujumla wake yaani Madhehebu mengine Mnavyotaja Kanisa? Kama mnataka kuwataja Romani katoliki kuhusu siasa za Tanzania Bara...msihusishe Kanisa kama Ukristo wote Kiujumla...hatutaelewana
Sajosojo,
Kumbe bado mchanga sana katika elimu hii?

Nakushauri kama unataka kujadili somo hili soma kwanza historia ya Tanganyika na jifunze lugha ya uandishi.
 
Mohamed Said, Ni kosa kubwa sana kutoshirikishwa katika cover muandishi.

Umeulizwa cover lina maana gani, hujui.

Hujui kitu cha kwanza kabisa watu wanachoona kuhusu kitabu chako kina maana gani.

Hapo unaonesha kukosa umakini.

Mtu anaweza kukuzushia lolote kuhusu hilo covwr, ukashindwa kutetea hoja zaidi ya "appeal to authority" kutaja majina ya publishwrs, which is a very weak argument.
 
Kiranga,
Kiranga,
Nina kitabu kingine kinakuja na cover hainishughulishi nawaachia wataalamu wa publisher kwani naamini watafanya kazi nzuri.

Mimi ninachojua ni kuandika miswada tu mambo ya cover kweli kabisa sijui na wala sijaona haya ya kutaka kujua cover ya kitabu changi itakuwaje.

Katika miaka yangu 21 ya uandishi ni leo ndiyo nasikia msomaji anauliza cover ya kitabu changu.

Labda kwa kuwa kitabu chenyewe kilivyo maudhui yake.
Msomaji hasomi kitabu anahangaika na cover.
 
Mohamed Said, ]Cover ni kitu cha kwanza kabisa wasomaji watakachokiona.

Na hivyo, kuelewa maana yake ni nini ni kitu muhimu.

Unaweza kuwekewa, kwa bahati mbaya au kwa makusudi symbolism yenye maana mbaya.

Ikiwa hivyo, ni bora kugundua hilo kabla vitabu hajijachapishwa kuliko vitabu vikishachapishwa kwa maelfu.

Anything less is dereliction of duty. Leaving things to chance. Trusting authority.
 
Sioni tatizo la udini Tanzania bali naona tatizo litakaloletwa na wachokonoa udini Tanzania.., popote pale watu wanapoweka issues za utofauti wa wao na sisi kuliko kuweka wazi vile vinavyotuunganisha mwisho wake sio kujenga ni kubomoa..

Aliyisema nchi isiwe na dini na kila mtu na imani yake atekeleze huko huko kwa manufaa yake na waumini wake, alikuwa na busara sana.., tukianza kila mtu kudai (sijui tunadai nini) kwa ajili ya imani zetu tutakuwa hatuwatendei haki wale wasio wa imani zetu
 
@Kiranga,Kiranga,
Mimi si mjuzi kama hao wanaochapa vitabu vyangu.

Kwangu kitabu kitakuwa na rangi gani au cover gani si muhimu.

Tafadhali nakuomba unielewe.
 
Sioni tatizo la udini Tanzania bali naona tatizo litakaloletwa na wachokonoa udini Tanzania.., popote pale watu wanapoweka issues za utofauti wa wao na sisi kuliko kuweka wazi vile vinavyotuunganisha mwisho wake sio kujenga ni kubomoa..

Aliyisema nchi isiwe na dini na kila mtu na imani yake atekeleze huko huko kwa manufaa yake na waumini wake, alikuwa na busara sana.., tukianza kila mtu kudai (sijui tunadai nini) kwa ajili ya imani zetu tutakuwa hatuwatendei haki wale wasio wa imani zetu
Keyser,
Hayo usemayo ndilo lilikuwa tegemeo la wale waliojitolea kupigania uhuru kwa nafsi na mali zao.

Hali haikuja kuwa hivyo.
 
Kiranga,
Mimi si mjuzi kama hao wanaochapa vitabu vyangu.

Kwangu kitabu kitakuwa na rangi gani au cover gani si muhimu.

Tafadhali nakuomba unielewe.
Kwanza kabisa, uamuzi ni wako na nimekuelewa. Sina nia ya kubadilisha uamuzi wako.

Ila, muandishi kuonesha lack of curiosity hivyo ni alarming.

Ujumbe ninaoupata hapa ni kwamba huna curiosity ya kutosha kutaka kujua cover la kitabu chako mwenyewe lina maana gani.

Na kwangu mtu ambaye ninapenda kuwa na attention to intricate detail, hilo si jambo zuri.

Kwako wewe si kitu muhimu.
 
Kiranga,
Naam sishughulishwi na muonekano wa kitabu.
Mie si ''alarmist.''

Hii ndiyo mara yangu ya kwanza katika miaka 21 ya uandishi wa vitabu kuulizwa cover na msomaji.

1575221955500.png


1575222024436.png
 
Mohamed Said,
Labda hizo cover hazikuwa ambigous na hii ni vinginevyo.., sasa mtu akuulize cover inahusu nini wakati anaona ni picha ya Nyerere ?
 
Mohamed Said, Labda kwa sababu wasomaji wako wengi ni kama wewe, hawana attention to detail.

Na unaposema wewe si alarmist, maudhui ya vitabu vyako yanaweza kukufanya uitwe si tu alarmist, bali pia petty alarmist pia.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom