Kitabu gani ambacho kimewahi kubadilisha maisha yako na unatamani wengine tukisome?

Kila kitabu nilichokisoma katika hatua husika kimebadili hiyo hatua hatimaye maisha.

Primary nilisoma vitabu nikafaulu, maisha yalibadilika(nilianza maisha ya boarding tofauti na maisha ya nyumbani)

Olevel nilisoma vitabu nikafaulu(nikaenda A-level maisha yakabadilika)

A-level nilisoma vitabu(Chand, BS, Nelkon, N.k) nikafaulu nikaenda Chuo(maisha yakabadilika, nikala boom la asilimia zote)

Chuo nilisoma vitabu nikafaulu, nikaingia kitaa(maisha yakabadilika)

Hii ndio namna vitabu vilivyobadili maisha yangu.
 
Chuo nilisoma vitabu nikafaulu, nikaingia kitaa(maisha yakabadika)
Hatua hii inatakiwa uanze na moja, Sababu mitaala yetu haitufanyi kuweza kujitegemea bali kuwa tegemezi,

kuna elimu tunakosa fiqQ anaiita kitaaOlojia , ambapo yule uliye mwacha kidato cha nne na akaingia mtaani kusaka maisha ndio huyo leo ana unafuu kimaisha.

Hii sentensi (hapo juu)niliyoandika kwa jicho la kawaida hutoweza kuona mantinki yake, Ila waweza kujiuliza hili swali, Je ni matajiri wangapi wameajiriwa? jibu ni hapana, hawajaajiriwa bali wamejiajiri.
 
Hatua hii inatakiwa uanze na moja, Sababu mitaala yetu haitufanyi kuweza kujitegemea bali kuwa tegemezi,

kuna elimu tunakosa fiqQ anaiita kitaaOlojia , ambapo yule uliye mwacha kidato cha nne na akaingia mtaani kusaka maisha ndio huyo leo ana unafuu kimaisha.

Hii sentensi (hapo juu)niliyoandika kwa jicho la kawaida hutoweza kuona mantinki yake, Ila waweza kujiuliza hili swali, Je ni matajiri wangapi wameajiriwa? jibu ni hapana, hawajaajiriwa bali wamejiajiri.
Mkuu nakuelewa sana.

Ni kweli wapo wengi niliowaacha katika hizo hatua zangu na wapo mbele kimafanikio kuliko mimi.

Mabadiliko/mafanikio yaliyolengwa hapa ni ya mtu mmoja bila kulinganisha na mtu mwingine hata kama yawe ni madogo.

Namna hiyo ndivyo nilivyoeleza kuhusu mimi.
 
soon ntatoa kitabu changu kiitwacho "my life my voice"
1573612325511.jpeg
 
Eti hamna app ya kusoma vitabu vya fasihi? MW natumia AnyBooks lakini yenyewe haina vitabu vya kisw
Kuna kipindi nilitafuta sana app za vitabu vya fasihi, sikuwai fanikiwa hata, hivyo sina uhakika kama hizo app zipo.
Kuna riwaya nilikuwa natafuta za Kezilahabi (Nagona, Mzingire na Kichwa maji), sikuzipata hewani
"Sorry for delaying response"
 
Back
Top Bottom