FiQ
JF-Expert Member
- Feb 11, 2011
- 477
- 76
Hata wafanye nini CDM rocks, Hakuna asiejua kazi inayofanywa na cdm, huyo mwandishi na hao waliomtuma wameonyesha ni jinsi gani harakakat za cdm zinawakosesha watawala usingizi! Cdm rocksSijaona jipya lolote katika kitabu hicho endapo hayo uliyoeleza ndiyo yaliyomo ndani!
Kama nitanunua kitabu hicho, basi ni kwa nia ya kukiweka kwenye museum yangu, ili watoto wa wanangu waje waone bongo za baadhi ya binadamu zilivyokuwa katika karne hizi za mwanadamu kujivua MAGAMBA kama mjusi-kafiri!
Habari za madai ya 'Uchaga' wa cdm tumezisikia toka mwanzo wa dahari, na hivyo hakuna kitakachonivutia tena kwa suala hilo...na mbaya zaidi ni kuwa tulishajua wanaoeneza maneno hayo kuwa wana nia gani!
Naamini pia (japo mleta mada hajasema hapa) kuwa watakuwa wameongelea juu ya Ukatoliki wa Mbowe, Slaa, au mwinginewe yeyote, maana hizi ndizo hoja na propaganda za wenzetu...hawana la kusema zaidi ya hayo!
Binafsi naamini kitabu hiki kimeandikwa kama mtaji wa kisiasa wa watu fulani(kwa kumtumia na kumlipa fedha mjingamjinga mmoja), na namna ya kujaribu kuiteteresha cdm, jambo ambalo naona ni utoto na KIDUKU ya kipumbavu!
Hata vichaa wanajua kuwa cdm ina uongozi unaokubalika kitaifsa, na ndiyo maana ikasajiliwa na mamlaka husika, sasa mambo ya kudai kuwa inaendeshwa kama kampuni ya mtu binafsi ni ubunifu na usanii wa sanaa-mfu!
Najua kuwa mtakiuza kitabu hicho kwa bei ya kutupa hata kugawa bure ili mradi lengo lenu litimie, lakini kwasasa naogopa mtakuwa mnafanya kazi bure, maana watu wanaelewa vizuri zaidi kwa kujionea wenyewe matendo ya viongozi wao, na kwa asilimia 95 washajua mbinu za MWOVU!
NAWASILISHA!