Kitabu cha ucheshi

Yona F. Maro

R I P
Nov 2, 2006
4,202
218
Kuna mshikaji mmoja alikuwa kinyozi. Saluni yake ilikuwa katika ghorofa ya tatu. Kadiri siku zilivyokuwa zinakwenda wateja wakaanza kupungua na ikafika kipindi hakuna hata mtu anayekwenda kunyoa kwenye saluni yake hiyo.
Jamaa akajaribu kufanya utafiti na kwa mahesabu ya haraka haraka akaona huenda inatokana na saluni yake kuwa juu na kwamba watu wanaona uvivu kupandisha ngazi.
Basi siku moja akaamua kufanya utaratibu wa kuhamia ghorofa ya kwanza na mlangoni akaandika hivi; YULE KINYOZI ALIYEKUWA ANANYOA JUU, SASA HIVI ANANYOA CHINI KWA BEI NAFUU! Mpo hapoo?...

Shuka nikumeze


Mama mmoja alikuwa akiishi ghorofani peke yake lakini alikuwa muoga sana. Siku moja asubuhi wakati anashuka kuelekea chini akasikia sauti ikisema, Shuka nikumeze! Shuka nikumeze!
Mh! Yule mama kusikia vile moyo ukaanza kumwenda mbio akijua kwamba kuna jitu kubwa ambalo ndilo linalomwambia hivyo na kwamba kweli akishuka litammeza.
Basi akaamua kupiga simu polisi ili waje wamsaidie. Haikupita muda polisi wakafika nyumbani kwa yule mama wakiwa wamejikoki vizuri huku wakiwa na silaha nzito.
Cha ajabu sasa walipofika wakakutana na kichaa mmoja mdogo kadhoofika akiwa amelala chini ya lile ghorofa, kamasi zikimtoka mithili ya dawa ya mswaki iliyominywa huku akiimba Shuka nikumeze! Shuka nikumeze, akimaanisha kamasi zishuke azimeze! Ukitaka cheka ukitaka nuna lakini habari ndio hiyo!

Nyumba ndogo inaitwa pafyumu

Mwalimu Kibogoyo aliingia darasani kufundisha somo la Kiingereza na kabla ya kuanza kufundisha, akaanza kwa chemsha bongo ndipo alipomuuliza mwanafunzi mmoja swali, ilikuwa hivi:
Mwalimu: Nyumba ya ghorofa kwa kiingereza inaitwa Losheni, je nyumba ndogo inaitwaje?Enhe! Kifudu jibu.
Mwanafunzi: Inaitwa pafyumu
Basi darasa zima likalipuka kwa kicheko...

Ajisaidia kwenye soksi

Jamaa mmoja mkazi wa Manzese alishikwa na tumbo la kuhara ghafla maeneo ya posta.Akaingia nyumba moja akaomba kujisaidia.
Chooni kuko hivi, unaingia kuna sehemu unabonyeza kisha linatoka sinki unajisaidia kisha unabonyesha sinki linapotea. Alipoingia akatafuta shimo la choo halioni.
Akavua soksi yake akajisaidia humo kisha akatoka nayo kwenda kuitupa nje. Wakati anatoka akakutana na mwenye nyumba na mazungumzo yakawa hivi:
Mwenye nyumba: Mbona unatoka na mzigo
Jamaa:Nimemkuta panya kafa kwenye shimo la choo ndio nakwenda kumtupa
Mwenye nyumba:Hebu nimuone
Jamaa: Ananuka sana acha tu nikamtupe.
Mwenye nyumba akawa ameshtukia ishu.

Brazameni ajipaka kinyeshi

Brazameni mmoja alialikwa kwenye sherehe ya birthday.Kwa uroho jamaa akafakamia vyakula kisha baadae kuanza kucheza muziki na demu mmoja. Mara mshikaji akashikwa na tumbo la kuhara ndipo alipokwenda chooni na kujisaidia. Baada ya kumaliza haja yake, kuangalia kwenye ndoo maji ya kunawia hamna kwahiyo akaamua kutoa ‘engachifu’ yake na kujifutia kisha kuikunja vizuri na kuirudisha mfukoni.
Aliporudi ukumbini akaendelea kucheza muziki hadi kuloa jasho.
Si akajisahau na kutoa ile ‘engachifu’ aliyokwishaitumia kujisafishia chooni na kujifutia. Akijikuta amejipaka kinyesi usoni na kusababisha harufu mbaya iliyowafanya watu kumkimbia...

KAZI YA USAGAJI

Mama mmoja alikuwa na mtoto wake aitwaye Jeni. Mtoto huyo alikuwa darasa la tatu. Siku moja mwalimu wao aliwataka wanafunzi kutaja kazi wanazofanya wazazi wao na mazungumzo kati ya mwalimu na mwanafunzi huyo yalikuwa hivi:
Mwalimu: Jeni, baba yako anafanya kazi gani?
Mwanafunzi:Mwalimu
Mwalimu:Mama yako je?
Mwanafunzi:Yeye anafanya kazi ya usagaji.
Mwalimu:Heeh! We mtoto, ulijuaje kuwa mama yako anafanya kazi hiyo?
Mwanafunzi:Namuona akiifanya na shoga yake mama Kasim na mimi huwa naendaga kumsaidia ninapotoka shule.
Mwalimu kusikia hivyo akabaki ameduwaa kwani alifikiria vingine

Kibaka Atoa ya mwaka

Kibaka mmoja mzoefu alikwapua simu ya dada mmoja maeneo ya Kariakoo. Baada ya kufanikisha zoezi hilo wananchi wakaanza kumkimbiza huku baadhi wakiwa na matairi, petroli, mapanga na marungu ili wakimkamata wamuue.Yule kibaka kuona kifo kinamnyemelea akaona ajiokoe kwa kujisalimisha kituo cha polisi...

A little boy asked his father,
"Daddy, how much does it cost to get married?"
Father replied, "I don't know son, I'm still paying."

A young son asked,
"Is it true Dad, that in some parts of Africa
a man doesn't know his wife until he marries her?"
Dad replied, "That happens in every country, son."

Siku moja punda alienda kwa SIMBA 'mfalme wa mbuga' kushitaki wenziwe wanaomcheka na kumuita PUNDA, jina hili la punda hakulipenda kabisa kwa sababu wenziwe wanasema jina hilo ni kwa ujinga mwingi alonao huyo punda ndipo akaitwa punda. Mazungumzo yao yakawa hivi:

Simba: Wacha nikupe mtihani mdogo kupima akili yako kama kweli wewe ni mjanja na mwerevu kama wenzio, ukishinda mtihani huu nitakubadili jina na kukuita Farasi.
Punda: Nipime ujanja wangu na utanikuta ni mwerevu sana kushinda wenzangu.
Simba: Sawa, sasa nenda mbiooooo mpaka nyumbani kwangu ukaniangalie nipo huko au sipo nyumbani mwangu? Halafu urudi unipe jibu.
Punda: Kazi rahisi sana hiyo, nisubiri hapa nakuja sasa hivi.
Basi bwana Punda akatoka mbio hadi kwa nyumbani kwa mfalme kwenda kumwangalia kama yupo.
Kweli Punda zuzu, sasa anakwenda kumwangalia nani wakati mfalme mwenyewe amemuacha njiani.
Aliporudi mambo yakawa hivi:
Simba: Enhee vipi umenikuta?
Punda: Mh! Haupo.
Simba: Basi kama ndivyo, utaendelea kuitwa Punda hivyo hivyo kutokana na akili yako ndogo. Sasa umekwenda kwangu kunitafuta vipi wakati umeniacha hapa? Haya potea hapa haraka sana, Punda wewe! Kuanzia hapo jina la Punda linabaki kuwa hivyo hivyo!!! Tehe tehe tehe tehe.....



The Smiths were unable to conceive children and decided to use a surrogate
father to start their family. On the day the surrogate father was to
arrive, Mr. Smith kissed his wife and said, "I'm off. The man should be
here soon" Half an hour later, just by chance a door-to-door baby
photographer rang the doorbell, hoping to make a sale.

"Good morning, madam. I've come to...."
Muuza nyama [butchery]mkewe kamzalia watoto wawili mapacha,akawapa majina mmoja kamwita Kilopatra [Cleopatra] wa pili kamuita Kilonyama!!!!!

Mtu mmoja ana ugonjwa wa kusahau,kenda kumueleza daktari kuhusu ugonjwa wake wa kusahau,daktari akamuuliza; Ugonjwa wako huu umekuanza lini?
Mgonjwa: ugonjwa gani!!!!!
hehehehehh
Mtu na mkewe wanajikumbusha zamani zao walipooana,sherehe ilivyokuwa,na watu wengi waliohudhuria harusi yao,wakihadisia hayo mbele ya mtoto wao,punde mtoto kawanunia kweli na kwa hasira anawalaumu,mbona hamjanialika?????

mwanafunzi mmoja kaenda shuleni kachelewa sana ...mwalimu alivyo muuliza sababu ya kuchelewa vile akajibu kuwa mama na baba walikua wakigombana mwalimu akamwambia na imehusu nini ugomvi wa wazazi wako kukusababisha uchelewe........mwanafunzi akajibu kuwa mama alikua akitumia kiatu changu cha shule kumpigia baba ndio nilikua nakisubiria.........ha ha ha

>>>>>>>> Kissing a Woman <<<<<<<<<<<
Kissing a woman at her FOREHEAD is Respect

At her LIPS is Love
CHEEK is Heroism
NECK is Lust.


Kuna dereva mmoja wa AMBULANCE[mraibu wa mairungi] huko vitani kapewa maiti ya wanajeshi 35 awapeleke mochari ya kambini,akiwa njiani na maiti hao - akasikia taarifa ya kijeshi redioni ikitangaza kuuliwa kwa wanajeshi wao 20, hapo hapo kasimamisha gari na kufungua mlango wa nyuma na kwa ukali kuwaambia maiti; "wale 15 wanaojifanya wameuliwa wajitokeze haraka!!!" nasema haraka muteremke au mutakiona cha mtema kuni!!!!!!! munadandia eeeh!!!
Mlevi wa bangi,anavyoipenda sana bangi mpaka ameipa jina la ''Ufunguo"ili polisi wasijue anakusudia nini, hata mtoto wake kamuita ufunguo vilevile,siku moja aliletewa habari wakati yeye keshalewa bangi kibao,akaambiwa mwanao ufunguo amefariki,akawajibu;Musiwe na wasiwasi ninao spea!!!!!!.
Jamani Hasidi ni hasidi hata siku ya kufa anafanya uhasidi. Watu wawili wamehukumiwa kunyongwa,anaulizwa wa kwanza unatamani kitu gani utimiziwe kabla hujanyongwa? akasema; Natamani nimuone mamangu mzazi. Wa pili [hasidi] anaulizwa matamanio yake,akasema; Natamani mwenzangu asimuone mamake!!!!!!!.

pale wanachi wanapoamua kumfukuza mwizi mmoja ambae aliiba maeneo ya mtendeni,baada ya pirika za huku na huku walikutana na msenge mmoja na kumsimamisha na kuanza kumuuliza maswali

WANANCHI; umemuona mwizi kapita maeneo haya
MSENGE; eeeee nimemuona kapita kwangu hapa lakini nimemmwagia maji ya vumba la samaki akifika mbele tu ataliwa na paka msiwe na wasi wasi.........wananchi wote walipigwa na ganzi...........hahahaaaa heheheeeee.....
kuna mtoto mmoja mpungufu wa akili alipoona amechelewa kwao kurudi ilibidi atunge uongo ili amdangaje babake..alipofika kwao ilikuwa kama hivi.

BABA: ulikuwa wapi muda wote
MTOTO: nilikuwa namsaidia dereva wa treni kule tazara kubadilisha pancha.................heheheeeeheheeeee
jamaa mmoja katika zunguka zunguka zake aliwakuta jamaa wawili wakiongea mmoja kati yao alikuwa ni kipofu ilikuwa kama hivi

kipofu; hivi sasa hivi tupo katika mfungo wa ramadhani nini ?
jamaa: kwa nini unaniuliza hivyo kwani wewe mwenyewe hujui tupo kipindi gani
kipofu: sio hivyo kwasababu nasikia harufu ya mdomo hapa
jamaa: aaa ndio maana ukaniuliza hivyo sio nimepiga suna tu leo usijali.

kumbe jamaa alikuwa ananuka mdomo kweli aliua soo tu...hahaaaaaaa heheeeeee........
pale viongozi wa zanzibar walipokwenda ziara nchini china baada ya harakati zote ikafika muda wa kula..
vijiko na vikombe walivyokuwa wakitumia vilikuwa vya zahabu kawawa kuona vile ilibidi kimoja akiibe baada ya kuiba jumbe alimuona kumbe na yeye alikuwa anakitaka.ikabidi jumbe awaambie wachina anataka kufanya mazingara(mazingaombwe)wachina walikaa kimya na kumsubiri rais jumbe afanye mazingara,alichukua kile kijiko na kuanza kukipuliza alafu akakitia mfukoni na kusema kwa nguvu kawawa toa kijiko,kawawa kusikia vile ikabidi atoe kile kijiko...hahhaaaa heheheheee
kunakuwa na kipindi maalum pale viongozi wanapotakiwa kwenda kuangali machizi(wagonjwa wa akili).
kwa mara hii ilikuwa ni kipindi cha jumbe wakati alipoingia mental na kuanza kuzunguka huku na huku alikutana na chizi mmoja,jumbe aliwaambia wale walinzi wake mwangalieni yule chizi mnafikiri atapoa yule.yule chizi alijibu chizi mimi chizi wewe angalia umeletwa humu ndani na watu kibao wote wanakulinda wewe ao yaani anamwambia mh raisi jumbe maneno kumbe walikuwa bodyguard wake wale....hahahaaa heheeee....
Mwalimu anajaribu kuwafahamisha wanafunzi kuhusu lugha. Anasema fulani anaongea lugha nyingi,lakini "lughamama" [mother tongue] anayoongea ni kizulu. Swali; Kwanini ikaitwa lughamama?, MWANAFUNZI: Kwasababu, ni mama tu ndie anaeongea daima wakati baba hata siku moja hajapewa nafasi na mama kuongea lolote!!!!!,heheheheheheheh
Walevi wawili wamesimama mbele ya kioo,mmoja akamwambia mwenzake; Huyu mtu sijui nimemuona wapi. Mwenzake akamjibu; Huyo nimimi mjinga wewe!!!! heheheheheheheh
Mwalimu wa shule anamuuliza mwanafunzi mdogo; Babako ana miaka mingapi? Mwanafunzi akajibu; Sijuiiiii!!! Lakini kutoka zamani sana yupo kwetu nyumbani.hahahahahah
Mchezaji mpira miguu kajiunga na timu nyengine,baada ya mwezi zimekutana timu hizo mbili kwa mchezo wa kirafiki,mchezaji huyo kaifunga bao timu yake ya zamani,mpaka kufikia dakika za mwisho hawajaweza kulikomboa hilo bao-kuona hivyo mchezaji huyo huyo kaingiza bao kwa timu yake aliyojiunga,alivoulizwa kwanini umewapatia bao la kusawazisha? akajibu; sipendi kuona timu yoyote imetoka uwanjani na masikitiko!!!!!!!!! hehehehehheh HAKI SAWAAAAA.
pale msambaa na mdigo wanapokutana matani yao yanakua ni kuumbuana tu... ilikua kama hivi

mdigo> wewe angalia meno kama foleni ya madumu
msambaa> aaa tulia wewe meno kama reki
mdigo> aa hilo tu angalia domo ilo kama mfuko wa nyongeza
msambaa>naona unakwenda mbali miguu kama minazi kitamli
mdigo>duh angalia bichwa kama dume la siafu
msambaa> kama vipi tuishie hapa kwa leo tumbo kama mfuko wa saruji hahahaa heheeeee....
kuna jamaa mmoja alichoshwa sana na maisha kutokana na ulemavu wake wakua hana mkono mmoja,aliamua apande juu ya jumba la michenzani ili kwa ajili ya kujitupa(kujiua).
Baada ya kufika juu alimkuta jamaa akijisugua sugua na ukuta namaanisha anajikuna matako,jamaa aliamua kumfuata na kumuuliza..ilkua kama hiv...
mbona unajisugua sugua na ukuta
alijibu; wewe kwani unaona mimi nafanya nini hapa..
nakuona unajisugua sugua mimi nilikuja huku ili kwa ajili moja tu ya kujiua kutokana sina mkono mmoja...
alijibu; mimi mwenzio toka saa hizo napata tabu hapa nataka kujikuna matako sipati sina mikono yote na sijitupi ijekuwa wewe mkono mmoja kafanye kazi wewe jikaze....hahahaaa heheee...
Bibi mzee anasoma shule ya watu wazima{ngumbaro},mwalimu anamuuliza alama hii = inamaanisha nini?,Bibi mzee akajibu; ni11 imelala!!!! hahahahah
Dereva amegonga watu wawili,mmoja amefariki na mwengine ameumia kidogo,aliyeumia kaamka na matusi makali makali anamtupia dereva. Dereva nae kateremka na hasira akimwambia alieumia;Wewe umeumia kidogo tu na unanitusi namna hiyo?. Mtizame mwenzio kafariki dunia,wala hata hajasema lolote!!!!.hahahahahahahah
Jamaa kaulizwa;Unapenda mkeo afe?. akajibu; Laa sipendi. akaulizwa; Kwanini?; akajibu;Nahofia nisife mimi kwa furaha akisha kufa!!! hahahahahahah
Jamaa mmoja msahaulifu sana kafariki dunia, kwanini? kasahau kuvuta pumzi !!!. hahahahah
jamaaa mmoja ambaye alikuwa bingwa wa kunywa pombe za kienyeji (gongo)siku moja aliingia maeneo ya kiboje kwa mabingwa wa kutengeneza gongo
ilikuwa kama hivi...
wewe mama muuza lete mzinga mmoja..mama akauliza nani huyo alieagiza mzinga ataumaliza..walevi wengine wakasema we mpelekee tu bingwa wa mjini kaingia huyu....yule mama alimpelekea lakini ilikuwa nusu tu sio mzinga...jamaa akaaanza kutukana mimi nimekwambia mzinga mmoja..yule mama akasema kunywa hiyo kwanza ukimaliza nitaengeza....jamaaa akaanza kunywa baada yamuda wa dakika kumi tu yule jamaa alipasuka macho yaani kapofuka...majibu yaliyotoka kwa yule jamaa.....hata mkizima umeme mimi sitoki humu...hahaaaa heheeeee....
ndani ya mahakama za mitaa kunakuwa na wazee maalum ambao kazi zao kusaidia mahakama kwa ajili ya kesi ndogo ndogo za vijana..
wakati jaji anamsomea kesi jamaa mmoja alieiba kuku wawili mitaaa ya ilala mheshimiwa jaji aliwaomba wazee watoe msaada wao.wakati jaji anauliza wazee mnasemaje kuhusu huyu kijana.mzee mmoja ambaye yeye alikuwa mkubwa wao alikuwa amelala.baada jaji kuuliza tena toweni mchango mzee kwa huyu kijana itabidi aamshwe yule mzee aliyekuwa amelala,baada ya kuamka tu yule mzee alisema miaka kumi (10).
watu wote walianza kucheka na jamaa kuanza kutukana ndani ya mahakama..jamaa alifungwa kweli miaka kumi kwa kosa la kuiba kuku ...hahaaaaaa heheeeee...
kuna jamaa mmoja aliiba baiskeli alikamatwa na kupelekwa mahakamani.ililkuwa kama ifuatavyo..
jaji>mshitakiwa unashitakiwa kwa kosa la kuiba baiskeli
mshitakiwa>nakubali ila naomba nijitetee ilikuwa sio mie ni ibilisi tu yule
jaji>basi kama ibilisi wewe tutakufunga miaka miwili na ibilisi miwili wazee mpelekeni ndani yeye na ibilisi wake.......hahaaaaa heeheheee...jamaaa kala ngoma nne..
Polisi anawakuta walevi wawili wa bangi sehemu fulani,baada ya kuwatizama vizuri akawauliza kiuchokozi; kwanini wote macho yenu ni mekundu?, mmoja wao akajibu; mheshimiwa ni kwasababu sisi ni ndugu. hahahahahah
MVUTA BANGI MMOJA ANAMWAMBIA RAFIKI YAKE; JICHO LANGU LEKUNDU SANA,NIFANYEJE?. RAFIKI YAKE AKAMJIBU; LIKISHA GEUKA KUWA LA KIJANI > ANZA KUTEMBEA. hahahahahah
Jamaa kaambiwa nenda haraka kule chini ya mti utamuona mkeo ameketi pamoja na rafiki yako!!!,jamaa kusikia hivyo kenda mbiompaka chini ya mti na kumtizama huyo alieketi na mkewe na kurudi mbio.mbona umerudi mbio?rafiki yake kauliza. Jamaa akajibu nimekwenda kumuangalia alieketi na mke wangu,sio rafiki yangu na wala hata simjui!!!.hahahahah
KUNA MAJUHA WATATU WAMENUNUA MBUZI, MMOJA AKASEMA MIMI SIJUI KUCHINJA.WA PILI AKASEMA MIMI SIJUI KUCHUNA NGOZI. WA TATU AKASEMA MIMI SIJUI KUKATA NYAMA. MBUZI NAE AKASEMA {moyoni} MIMI NI MJINGA NILIEKUBALI KUWAFUATA MAJUHA NYIE!!!.hahahahah
<>KICHEKESHO KUTOKA IKULU<> SIKU MOJA RAIS HOSNI MUBARAK ALIMUITA [aliekuwa makamu wake] MHE.LUTFI ABED NAKUMUULIZA MASWALI YA KUJIGAMBA KIDOGO. LUTFI NJOO NIKUULIZE; naam Mheshimiwa Rais-niulize. Rais Hosni; Ni nani alie kiongozi bora kati yangu na Jamal Abdinaser? Bw.Lutfi akajibu;ni wewe mheshimiwa,Jamaal huyu alikuwa akiwaogopa warusi wewe huwaogopi.hahahah sawa bw.Lutfi kumbe unanijua vizuri,akasema Rais. Swali la pili Bw.Lutfi. Niulize Mhe.Rais. Ni nani aliebora mimi na Anwar Saadat?Bw.Lutfi akajibu; ni wewe mheshimiwa, Saadat huyu alikuwa akiwaogopa wamarekani mheshimiwa,lakini wewe huwaogopi.hahahah asante sana Bw.Lutfi. sasa nitakuuliza swali la mwisho,niulize mheshimiwa[hapa Bw.Lutfi keshachoshwa na maswali]. Nauliza?Rais Hosni anamuuliza Bw.Lutfi; niambie ni nani aliebora zaidi,mimi au Bw.Omar bin Al-Khataab {r.a}?. Bw.Lutfi akajibu; naam, mheshimiwa Rais,ni wewe mheshimiwa, huyu Omar bin Al-khataab anamuogopa mungu,wewe humuogopi!!!!!!!.

kulikuwa na mashindano ya watu wafupi, katika hayo mashindano mshindi wa kwanza anazawadiwa gari yenye thamani ya shilingi milioni 350 na kupewa jumba la kifahali lenye thamani ya shilingi milioni 440,watu walikusanyika kushuhudia ninani na ni kwanini ataibuka kidedea,mashindano yalianza kwa kuingia mshiriki wa kwanza ambae alikuwa mfupi kama chemli,watu walishangilia sana huku wakisema ama kweli duniani kuna watu wafupi,mshiriki wa pili aliyeingia alikuwa mfupi kama kipande cha sabuni cha shilingi mia,watu wakavunjika mbavu wakasema jamani eeeeeee kwa mtindo huu dunia imekwisha,yaani.......yaani.......yani.......yaaaani we acha tu.kabla hawajamaliza kushangaa iliingia gari aina ya benzi dereva akafungua mlango akadondosha kiberiti chini watu wakapigwa na butwaa ghafla kiberiti kikafunguka akatoka mtu amevaa suti,watu wote pale ukumbini wakajobu hundred,hahahahehehehehihihihh

mshikaji mmoja ambae ni mwana michezo wa kunyanyua vitu vizito huko visiwani zanzibar,yaani huyu jamaa alikuwa na uwezo wakunyanyua gari aina ya prado kwa mkono mmoja,yakatokea mashindano ya kunyanyua vitu vizito kwa nchi za afrika,mashindano hayo yalikuwa yanafanyikia nchini kenya,mashabiki wake walifurahi sana, siku ya siku ikafika jama akaandaliwa kwaajili ya safari kuelekea kwenye mashindano,akiwa kwenye basi njiani alimuona mtu amebeba magari aina ya isuzu matano kichwani na mkononi analikokota treni lenye mabehewa 40,alishangaa,akawauliza abiria wenzake hivi yule jamaa anakwenda wapi? wakamwambia yule anarudi toka kenya kwenye mashindano ya kunyanyua vitu vizito,ameshindwa ndiomaana anarudi,yule jamaa akaanza kulia mayoooooooooooooooooo,hehehehehehehehehheheheeeeeee
mama mmoja huko china ilikuwa anakaa kwenye jengo lenye urefu wa ghorofa laki moja na elfu hamsini,mara nyingi hupenda kukaa juu ya paa la jengo kwa mapumziko ya kawaida,siku moja akiwa huko juu ya paa akiwa amembeba mtoto wake mchanga wa miezi miwili huku akimrusharusha kwania ya kumbembeleza,ghafla akaponyoka na kudondoka chini ya ghorofa,kwa uwezo wa mungu hakupata mdhara yeyote,yule mama akatoa ripoti polisi wakaja haraka sana kwa pamoja na yule mama wakaenda kumuangalia yule mtoto kule chini,walipofika walimkuta mtu mmoja mzee sana wakashangaa na kujiuliza jamani mtoto mwenyewe yuko wapi? ghafla yule mzee akaanza kuita mama mimi hapa mwanao yaani umenisahau? yule mama akiangalia sura inakujakuja,kumbe kutokana na urefu wa lile jengo yule mtoto alikuwa anaendelea kukua njiani kabla hajafika chini,heheheheeeeeeee
Hii sio joke bali ni mkasa wa kweli, nilikuwa nikisoma darasa la sita mwaka 1966 Haile Salise School Zanzibar, na tulkuwa na kipindi cha Kilimo,mara ghafla katuingilia Abeid Amani Karume, mwalimu wetu wa kilimo kasita kutusomesha baada ya kumuona rais kuingia darasani, Abeid Karume kamuambia mwalimu andelea kusomesha, basi mwalimu akaendelea kutusomesha na kusema kuwa miti ni kama binadamu zina roho zinataka hewa na maji bila hayo haziwezi kuishi, hapo tukamuona Abedi Karume zimeshoti akaanza kumtukana mwalimu na kutuambia sisi wanafunzi kuwa huyu mwalimu mwende wazimu hana akili ati miti zina roho ? hapo hapo katoa amri mwalimu afukuzwe kazi ya uwalimu apelekwe welezo hospitali ya wenda wazimu. Masikini mwalimu wetu alikuwa mwalimu nzuri sana na kabebwa juu kwa juu mpaka welezo.
mshikaji mmoja ambaye ana ndugu yake (kaka yake)anayeishi marekani kwa miaka mingi,siku moja aliamua kumtumia zawadi ya surali na shati alizozinunua kwa bei mbaya huko mjuu,baada ya kupata mzigo huo kwa njia ya posta alikwenda nao hadi nyumbani akiwa na furaha tele,alipofika akazijaribu zikamtosha vizuri tu lakini akasema hizi nguo sizivai mpaka siku ya jumapili kanisani,hatimae jumapili iliwadia jamaa akatika viwalo vyake anaelekea zake kanisani huku anajiangalia kila mara kama amependeza,watu walimshangaa kwajinsi alivyokuwa anajipiga chabo kila wakati,basi kabla ya kufika kanisani aliingia dukani akanunua sigara akawa anavuta huku akiendelea na safari sigara ilipokwisha na kubaki kipisi akasahau na kukitia mfukoni kikiwa bado kina moto ghafla ile suruali ikaanza kuungua na kufuka moshi mtu mmoja akawa anamwambia kaka angalia suruali yako inatoka moshi,yule jamaa kwa mbwembwe akamjibu acha ushamba wewe hii suruali nimeletewa juzi tu kutoka marekani we unafikiri inatoka moshi hii, kwani we unanionaje? baada ya hatua chache akaanza kujisikia jotojoto ghafla akaanza kupiga kelele mama naunguaaaaaa,hehehehehehehehehheeeeeee
Jamaa mmoja ambaye ni mwizi maarufu sana alikamatwa na wananchi wenye hasira kali akiwa anaiba tena alikuwa amebeba fuko la hela aliloiba,wananchi waliokusanyika kwaajili ya kumkomesha mwizi huyo kwa kumtoa roho yake ili kukomesha vitendo hivyo mtaani kwao kila mmoja alikuja na silaha ya aina yake mwenye panga,rungu,sime,bunduki,na kila aina ya silaha.waliamua kumuuliza sababu ya yeye kuiba ili wajue pengine aliiba kwa bahati mbaya,andipo yule mwizi akasema jamani msiniue nikweli kabisa nimeiba lakini naomba niwaeleze jinsi ilivyokuwa,jama akasema minilikuwa napita nikaona nyumba iko wazi nikaona pengine hii ni riziki yangu niliyobarikiwa na mungu, basi ........nikanyata ........nikanyata ......nikanyata ......huku anasogea mbele wale wananchi wanamuangalia tu, ghafla akakurupuka na kuingia mitini mmoja akasikika akisema minilijua tu atakimbia huyu,heheheheheheheheeeeeee!
Mwalimu wa somo la sayansi darasa la nne aliingia darasani na kuwaambia wanafunzi kuwa leo tunajifunza sayansi juu ya umuhimu wa chakula kwa binadamu sawa watoto wanafunzi wakajibu kwa pamoja ndioooo! mwalimu,mwalimu akawauliza swali wanafunzi,binadamu tunakula chakula ili iweje? wanafunzi hawakunyoosha mikono kwakuwa hakufahamu jibu lake ila mwanafunzi mmoja ambaye ni mtukutu sana darasani akawaza kimoyomoyo na kujisemea mwenye mhh,hili swali mwalimu kauliza ni la kimtegmtego lakini mimi mtego wakr nishaujua akanyoosha mkono mwalimu akasema enhee tunaomba jibu akajibu mwalimu minaona binadamu tunakula ili tunye, darasa zima likalipuka kwa kicheko na mwalimu nae akashika kichwa na kujisemea kimoyomoyo hapa sina mwanafunzi,baada ya muda yule mwanafunzi akawageukia wenzie na akawauliza mnashangaa nini kwani kuna mtu asiyekunya humu ndani.hehehehehehehehehhehhheeeeeee!
Muuza bangi kafungua kiwanda cha kuuza gesi inayotumiwa kwa kupikia,siku ya pili kalipua kwa makusudi slenda mbili za gesi kikaungua kiwanda chake;kwanini?eti anafanya matangazo ya biashara - wateja wapajuwe kiwandani!!!.hehehehehehe
Kuna mtoto mmoja nyumbani kwao,kila siku anafundishwa awe mwenye adabu na heshima nyingi,lazima akitoka aage na akiingia nyumbani lazima agonge mlango na kusema hodi,mpaka imefikia anagonga hodi mlango wa friza na friji kabla hajaufunguwa.hahahahhahah
Jamaa mmoja kanunua simu ya mkononi,akampigia simu mdogo wake na kumwambia;ningependa unitumie message kwasababu "maandishi yako ni mazuri kuliko yangu".heheheheheheh
pale machiz wote wanapofanyiwa mitihani ili kumjua nani kapungua uchiz ili kwa ajili ya kumtoa akasalimie wazazi..mtihani wa safari hii ulikuwa kama hiv...machizi wote walikusanywa sehemu moja na kuambiwa waigize kama kuku wengi wao walikua wanawika kama jogoo wengine wanatetea lakini mmoja kati ya wale alikua katulia madaktar wakaona huyu ndo kapoa kidogo walimfata na kuanza kumuuliza maswali....vipi wewe mbona huigizi kama wenzio yule chiz aliwaambia ssshhhhhh...nataga....hahaaheheeeeee...
pale machiz wote wanapofanyiwa mitihani ili kumjua nani kapungua uchiz ili kwa ajili ya kumtoa akasalimie wazazi..mtihani wa safari hii ulikuwa kama hiv...machizi wote walikusanywa sehemu moja na kuambiwa waigize kama kuku wengi wao walikua wanawika kama jogoo wengine wanatetea lakini mmoja kati ya wale alikua katulia madaktar wakaona huyu ndo kapoa kidogo walimfata na kuanza kumuuliza maswali....vipi wewe mbona huigizi kama wenzio yule chiz aliwaambia ssshhhhhh...nataga....hahaaheheeeeee...
Mama anamuuliza mwanawe mdogo,mbona mwanangu unam-nywesha kuku maji dafi?Mtoto: ndio mama kwasababu apatetoa yai liloiva tayari.hahahahahah
kuna jamaa mmoja baada kuona maisha yanaanza kumshinda aliamua aandike barua kwa mungu ili aombe pesa baada ya kuandika aliituma kwa njia ya posta.wafanyakaz wa posta baada ya kuipokea ile barua na kuikagua walijua huyu jamaa kama kuwa chiz bas zimebakia siku kidogo wafanyakaz waliamua kumchangia huyu jamaa kabla hajadata zilipatikana kama elfu 70 na wakamtumia kwa njia ile ile ya anuani yake jamaa baada kuipokea ile barua alimshukur sana mungu kwa kumgaia ela sema akaandika barua nyengine na kumnasihi mungu mara nyengine akitaka kumtumia pesa asitumie tena posta kwani wanakuwa wizi na najua hiz zilikuwa zinafika laki lakini washaziiba......hahaaaaaaheeeeeeeee.....
Jamaa ameingia hotelini akaagiza chakula,mara akamuita waiter {dawari} na kumwambia: Nawashukuru sana kwa usafi wenu na chakulachenu humu hotelini.Waiter akamuuliza;ulijuaje mzee kama hoteli yetu na chakula chetu kisafi?.Mteja akajibu:kwasababu chakula chote kina ladha na harufu ya sabuni!!!!!.hahahahahah kaona atasifiwa!!!!
Watoto jirani walikuwa wanacheza nje ya nyumba zao,mama wa mmoja wao kafungua mlango na kumuuliza mtoto wa jirani yake hivi; wee!! Ali,mamako yupo nyumbani?, Ali:Mama Katoka. MamaJirani: Saa ngapi atarudi?, Ali: Subiri nikamuulize!!!!.heheheheheeh
kuna jamaa ashikwa na tumbo la uharo aaga kazini na kukimbilia nyumbani kwa kujisaidia aliingia ndani bila ya kusalimia na kufukuzia msalani hatimae baada kuchojoa na kuanza kukaa kwenye shimo alijamba tu hakikutoka kitu hahaaaaaheheeeeee
<<<<<BWANA NA BIBI HARUSI>>>>>> Miaka ya kwanza: Bwana ndie anaesema sana na mke ndie anaesikiliza!!!.Miaka ikipita, Mke ndie anaesema sana na bwana anasikiliza!!!!. Wakisha zaana: Wote wanasema sanaaaa na majirani ndio wanaosikilizaaaa!!!! hahahahahah..
Mwalimu wa shule anawaambia wanafunzi wake: Yeyote kati yenu kama ni mjinga na haelewi kitu aje asimame hapa mbele!!!. baada ya muda mfupi mmoja wa wanafunzi kenda simama mbele kama alivyosema mwalimu; oooh!! kumbe wewe ndio mjinga??, mwanafunzi akajibu: hapana mwalimu,mimi sio mjinga,lakini nimeona nisikuwache pekeyako umesimama mbele - ndio nikaona tusimame pamoja mwalimu!!!!! hahahahahah
Mbuzi anamuuliza mwenzake,zimepita sikukuu mbili mbona hujachinjwa?,mwenzake akamjibu: cheti changu cha kuzaliwa nimeandikwa mimi Punda!!! heheheheh
Jamaa mmoja alikuwa akilia sana katika muhadhara wa kidini.Basi kila Shekhe alipokuwa akizidi kufafanua hoja za mawaidha jamaa huyo alizidi kulia hadi baada kumalizika mawaidha ilibidi abebwe kutokana na kuzidiwa na kilio wakti wa mawaidha.

Waliombeba walishtushwa na kilio chake wakati wa muhadhara na kutaka kujua nini kilimsibu yule na jamaa nae bila kusita aliwaeleza kuwa kilio chake kilitokana na Ndevu nyingi za yule shekhe aliekuwa akitoa mawaidha kwani ndevu hizo ziliamsha kumbu kumbu ya Beberu wake ambae aliibiwa punde tu kabla ya kuja kwenye muhadhara huo.
Mkulima mmoja kwa mara ya kwanza kaja mjini na kwa bahati mbaya kaibiwa pochi lake,kenda piga ripoti kituo cha polisi,baada ya kueleza kisa chake -polisi akampa matumaini mazuri kwa kumwambia; Usiwe na wasi-wasi mzee wangu - pochi lako hata kama limefichwa chini ya ardhi tukilipata tutakupa mwenyewe.Mkulima kusikia hivyo katoka kituoni na furaha tele,kufika nje ya kituo cha polisi kwa hatua kama hamsini hivi kaona wafanya kazi wa idara fulani wanachimba kando ya bara-bara pengine ni wa umeme au ni wa idara ya maji hatujui!!, mzee mkulima kuwaona hao wafanya kazi kawatolea sauti; Wazee!! wazee!! mujuwe rangi ya pochi langu ni leusiiii na mna picha yangu humooo!!! pochi lenyewe lina zipu ya buluuu na pini katikatiiii!!!!!!! nimeshapiga ripotiiii!!! basi haya tena!!! mukalipeleke kituoniiii,wafanya kazi wanatizamana na kushangazwa na huyo babu.hehehehehehehh
Mkuu wa kikosi cha polisi cha kuwapokea wageni wa serikali anamwambia askari wa kupiga mizinga: Askari,punde akiwasili mheshimiwa rais-anza kupiga mizinga 21 ya mapokezi. Afande mheshimiwa nitafanya ulivyonituma,lakini ninauliza? kwa mfano mheshimiwa Rais akiumia kwa mzinga wa kwanza niendelee kumrushia mizinga iliyobaki 20???!!! heheheheheheh
vituko ndani ya mental pale chizi mmoja anapoamua kupanda mnazi alaf hataki kushuka ilkuwa kama ifuatavyo....

madaktari..we shuka uko juu
chiz.. sishuki
daktari mmoja akaja na panga nakuanza kusema shuka tunaukata huu..chizi sishuki..daktari mwengine akaja na shoka na mwengine akaja na trekta shuka tunaukata huu ..chiz sishukiii ng'oo baada ya kushindikana vyote hatimae akatokea chizi mwenziwe akiwa kashikilia mkasi na kufanya kama anaukata ule mnazi na kusema we chiz shuka uko naukata sasa hiv huu...hatimae chiz kushuka mbio na kuanza kulia.....wewe vunja babake..hehehehee..hahaaaa...
And They Ask Why
I Like Retirement!

Question: How many days in a week?
Answer: 6 Saturdays, 1 Sunday
Question: When is a retiree's bedtime?
Answer: Three hours after he/she falls
asleep on the couch.
Question: How many retirees to change a light bulb?
Answer: Only one, but it might take all day.
Question: What do retirees call a long lunch?
Answer: Normal.
Question: What is the best way to describe
retirement?
Answer: The never ending Coffee Break.
Question: What's the biggest advantage of
going back to school as a retiree?
Answer: If you cut classes, no one calls your
parents.
Question: Why does a retiree often say he
doesn't miss work, but misses the
people he used to work with?
Answer : He is too polite to tell the whole truth.
QUESTION: What do you do all week?
Answer: Mon. to Fri. Nothing, and on
Sat &Sun I rest!
Yuko dereva mmoja ameshitakiwa kwa kosa la kugonga na kuuwa watu 51,Polisi anamuuliza; Imekuaje ukagonga na kuuwa watu 51-wewe huoni au umelewa?,Dereva: Musee mimi tafahamisha wewe jambo mocha,yuko mutu alikuwa anapita kwa njia mbele yangu na upande wa kulia iko sherehe ya harusi,unataka mimi nipanye bipi?,Polisi akamwambia;kama upande wa kulia kuna harusi unagonga huyo mutu mumoja tu!!!. Dereva: Na mimi nimefanya vile umesema muheshimiwa nilitaka kumugonga huyo mutu lakini yeye akakimbia ndani kwa hiyo sherehe!!!,na mimi nikasema siwezi kumuacha muchinga huyu nitamugonga huko huko ndani kwa wale watu yeye amejificha kwao.

EBWANA NOMA KUNA MASAI MOJA AULIZWA JINA NA POLISI

POLISI :JINA LAKO NANI

MASAI :JINA YANGU REFU BANA
POLISI :SEMA BWANA WEWE JINA LAKO NANI
MASAI :YARRR JINA YANGU IKO KUBWA SANA BANA ITAKUPA SHIDA
POLISI :WE SEMA NAKUPA MARA YA MWISHO
MASAI :YARRR MIMI BWANA JINA YANGU TRENI

POLISI ASHIKWA NA GANZI NA KUANZA KUVUNJA HAA HAAA...HEHEEEEE VUNJA
KUNA NJEMBA MOJA YAINGIA NYUMBA YA INAYOUUZWA GONGO KALI KULIKO ZOTE DUNIANI.BAADA YA KUAGIZA NIBU YA MWANZO TU HAJA KUBWA NA NDOGO ZATOKA BILA YA KIZUIZI.AKASEMA SIO TATIZO KUBWA AKAAGIZA NUSU BAADA YA KUNYWA TU KAPOFUKA MACHO AKABAKIA KUSEMA HATA MKIZIMA UMEME SISI HATUTOKI HUMU......VUNJAAAAAA HAHA HAAA....
Msichana anamuuliza Mpenzi wake bakhili alierudi kutoka safari,umeniletea zawadi gani kutoka ng'ambo? Mvulana akamwambia mpenzi wake"nimekujia mimi mwenyewe kwako kama zawadi", mpenzi nae akamjibu; mimi sipokei zawadi rahisi.mambo hayo...hehehehehehe

KUMBE KIFAA ALIKICHUKUA MWENDAWAZIMU HAHAHAHA!!!!!!!!!!!

EH!!! KUMBE KILE KIFAA CHA UMEME ALIKICHUKUA MWANDAWAZIMU.
BAADA YA MKAGUZI WA UMEME KUKITOA NA KUKIWEKA PEMBENI.
NDIPO HAPO CHIZI ALIPOKICHUKUA BILA KUTOJUA KINA FAIDA GANI.
AKAENDA NACHO HADI KUFIKIA MELI MOJA AKAAMUA KUKIFUKIA.
KWANI ALIHISI KINAMSUMBUA MAANA HAKISEMI NA NI KIZITO SANA.
BAADA MUDA SI MREFU WATAALAMU WALIPOTOKA NDANI YA MTAMBO.
WALIONA KIFAA HAKIPO, WALISHANGAZWA SANA NA KUANZA :-
KUKITAFUTA, MARA WALIPOULIZWA WANANCHI WALIJIBU.
TULIMUONA (MWENDAWAZIMU)NA DUBWANA LINA WAYA KASHIKILIA MKONONI.
NA IMEPITA MUDA MREFU TANGU WALIKPOMUONA
MSAKE MSAKE MARA WAKAMKAMATA AKIWA AMELALA JUU YA MKUNAZI.
KIKO WAPI KILE KIFAA ULICHOCHUKUA TWENDE UKATUONESHE KILE KIFAA.
YULE CHIZI AKAJIBU SAWA LAKINI MKANINUNULIE BIRIANI YA KUKU PASSING SHOW.
AKANUNULIWA HIYO BIRIANI, KALA AMESEMA BADO SIJASHIBA NIMEKINAI TU HIVYO.
KANINUNULIENI CHIPS MAYAI PALE SLIM KIOKS MAKONTENA NA SODA YA SHANI.
AKANUNULIWA KWA KWELI HAKUTAJA, MUHESHIMIWA (.....) AKAAMURU YULE CHIZI:-
AADHIBIWE KWA KUSUMBUA WAKUBWA WAHESHIMIWA WENGINE WAKAKATAA KUMPA
ADHABU YULE CHIZI KWANI WALIJUA HEKMA NDIO ITAKAYOWASAIDIA. SIKU YA PILI
ILIKUA KAMA IFUATAVYO. TWENDE KATUONESHE KILE KIFAA ULICHUKICHUKUA JANA.
NAYE AKAJIBU NI SAWA LAKINI LEO NATAKA KWENDA KULALA TEMBO HOTEL PALE
WALIPO HAWO WATAALAM NASIKIA WAPO PALE HATA MIMI NI MTAALAM KWANINI
NILALE JUU YA MTI" HE!! HII KAZI SASA MUHESHIMIWA (....) AKALALAMA .
BAADA YA KUFIKIRIA SANA NA JINSI YA USUMBUFU WA JULE CHIZI KIJANA MMOJA
KWA JINA MAGANGA ALIELEZA KUA TABIA YA YULE CHIZI NI KUFUKIA VITU ARDHINI.
NA HUPENDELEA SANA MAENEO YA KUSINI KULE KWENYE MIEMBE MIWILI MiGOMBANI.
KUPATA HABARI ILE NAE MUHESHIMIWA FULANI AKAAMURU KUA KUTOKA ENEO LILE
HUENDA TUKAJARIBU KUCHIMBA NA TUTAKIPATA, MUDA SI MREFU MARA LIKALETWA
GARI LA KUCHIMBUA. NAYO CHIMBUA CHIMBUA IKAAZA BILA MAFANIKIO ILA HASARA.
HASARA HIYO WALIIPATA WAKULIMA KWANI MASHAMBA YAO YALIHARIBIWA VIBAYA MNO.
HIVYO NAO WAKULIMA KUDAI FIDIA NA CHIMBUA CHIMBUA KUSIMAMISHWA HAFLA.
NDIPO WALIPOMFUATA YULE CHIZI KWA MARA NYINGINE TENA NA YULE CHIZI NAE.
HAKUSEMA LOLOTE KAMA KUWA ALIKUA AKIUMWA, MARA AKAKATIZA MSICHANA MREMBO.
NDIPO YULE CHIZI ALICHANGANYIKIWA KIDOGO NAKUANZA KUPIGA MAYOWE HI HI HI HI!!!
AH!! WALE WAKUU ILIBIDI WAPATE WAZO, MARA WAKAMPELEKA YULE CHIZI BWAWANI.
KUFIKA DISCO TEQUE WAKAMPATIA MALAYA MREMBO MMOJA NA KUMPATIA CHUMBA.
CHUMBA CHA BWAWANI HOTEL AS COMLIMENTARY, AMA KWELI NYAMA HAINA CHIZI.
YULE CHIZI BAADA YA RAHA KUMKOLEA MARA ALITAJA KILE KIFAA ALIPOKIFUKIA NA
KIPO MIEMBE MIWILI KWENYE MIGOMBA MIDOGO NIMEKIFUKIA PALE NDIPO WAKUU
MARA KUSIKIA HIVYO WAKUU NAO WAKAAGIZA KIFUATWE NA MARA WAKAKIONA.
NA KUKISAFISHA NA HADI KUTANGAZA KUA UMEME UTAWASHWA SIKU SAA FULANI.
AMA KWELI NYAMA HAINA CHIZI HIVYO NDIVYO MANENO YALIVYOTAWALA JE KAMA
YULE CHIZI HAKUPATIWA MSICHANA KWA KUMLIWAZA NAZANI TUNGELIKAA TENA
ZAIDI YA MIEZI MITATU BILA YA UMEME MAANA YULE MWENDAWAZIMU AMESHAPOTEZA
KUMBUKUMBU KABISA HMM NIHATARI
kuna mwizi mmoja alikwenda kuiba maeneo flani baada ya kuruka ukuta na kufanikiwa kuingia ndani alikutana na wabeba vyuma kama sita hivi wakimwangalia yule mwizi kuona hali ile na hamna msaada wa karibu kwake ilibidi ajinadie mwenyewe na kuvunja dirisha kukimbia.......heheheeeee.....heheheeee...
jamaa mmoja bingwa wa kula pilau na kudoea harusi za watu siku moja alikutana na bingwa mwenzake...
baada ya watu pirika pirika za huku na kule hatimae sahani ya pilau ikaekwa mbele ya huyo bingwa,na watu walianza kula yule bingwa kuona mwenzake aliyeekwa nae ana speed ya kula alimpiga mkwala wacha kupiga matonge.kuona jamaa hajamjibu kitu yule bingwa aliondoa nyama zote na kachumbari pale juu ya pilau,yule mwenzake kuona vile yeye alisimama na kutia mkono mfukoni na kutoa kipande cha nguru mkavu na kuendelea kula kama kawaida.......heheeeee.....hiiiihihihihhiii.......
kuna rifa (mchezesha mpira)mmoja ambae alikua anachezesha mechi moja kali sana nchini england aliona cross moja imepigwa kali sana kuelekea kwenye lango la goli kuona ile cross ni nzuri alafu ukizingatia inakuja upande wake aliamua kuacha ujinga alitupa kipenga pembeni na kuunganisha kwa voli moja kali sana mpira wavuni aliokota kipenga chake na kukipiga ,mpira kati watu wote walishangaa na kitendo cha rifa huyo.alipoulizwa alisema aaaa taratibuni kila siku nakuchezesheni nyinyi tu........watu mbavu.....heheeeeee hihihiii hoooooo huuuuuu.....
Wanasema uchunguzi uliofanywa huko marekani ni kwamba wanaume ambao wake zao sio warembo {kwa sura na umbo} ndio walio bahatika kutopatwa na magonjwa kama presha na ma-temper{ukali} wakati mwingi na kwamba wanakuwa na bahati ya kuishi umri mrefu zaidi {mungu akipenda}.Lakini wanaume walio-owa wanawake warembo,uchunguzi umegunduwa kama ndio wao zaidi wanaugua sana magonjwa kama presha na wakati wote ni wakali hata kwa jambo dogo sana na ndio mara nyingi wanafikia kuugua hata maradhi ya moyo. Jamani wivuuuuuuu!!!!!!!
Kijana mmoja mfungwa alisikika akimtoa jasho hakimu wa mahakama kwa kumzungusha na majibu. Hakimu; Kijana unaishi wapi?. Kijana; Ninaishi na mjombangu. Hakimu; na mjombako anaishi wapi?, Kijana; anaishi na mimi. Hakimu;{ kwa ukali} Wewe na mjombako munaishi wapi?, Kijana; tunaishi pamoja nyumbani. Hakimu; hooooooooooooooooooooo!!! askari muondoe huyu kijana mbele yangu!!!!!!!.
Msichana ameketi kando ya simu yao ya nyumbani akiwa kama mwenye wasiwasi,mara dadake anaingia na kumuuliza mbona una wasiwasi na kama mwenye kubabaika,una nini?. Msichana akasema; Yupo kijana hana adabu,anatusumbuwa, kila siku anapiga simu, lakini leo mpaka sasa hajapiga sijui ana nini akhhh!!!!!!!,heheheheheh
Jamaa mmoja 'anaonesha mwenye huruma sana' kamwambia mkewe; Masikini wasichana wa Palestina,nchi yao inaharibiwa na wayahudi na wenyewe kuuliwa kila siku,laiti kama inawezekana kila mmoja wetu humu nchini aende Palestina akawaowe wasichana wao > mungu atamjaalia kheri nyingi kwa kufanya hivyo. Mkewe akamtizama mumewe,akamwambia kama unataka kweli kufanya kheri nenda Darfur ipo hapa karibu,nenda kaowe wasichana wao, Mola atakupa kheri nyingi zaidi!!!!.hahahahahh
Ma-CID wamemshika mtu huko Lamu kwa kumshuku kama ni gaidi, Mambo yakawa hivi; CID.Wewemswahili,Unaweza kuniambia What is your last operation? MSWAHILI; mimi? nimefanya operation ya bawasiri mheshimiwa!!!!.heheheheh
wavuta bangi wawili baada yakuvuta bangi zao waliamua wakae kijiwe ili wazisikilizie zile steam zao.....baada ya mudawa dakika chake tu alipita mwanamke mmoja aliyekua kapendeza kiasi flani ..yule mvuta bangi mmoja akaanza kumsifia yule mwanamke.......oya babake unaona kitu icho mtoto mguu mguu...mgongo mgongo...chuchu saa sita....yaaani si mchezo...kama unampata yule sijui inakuaje.......yule mwenzake alikua kakaa kimya akimsikiliza rafiki yake baada ya kumaliza tu kusifia, yule mwenzake akamwambia...baba unajua yule unaemsifia ni bi mkubwa wako......yule jamaa alipigwa nabutwaa.....duh inamana mama yangu yule basi faza kafaidi....heheehheeee...hihihihhihi...huhuhuhuh..
kuna jamaa mmoja aliomba lift alikua akitokea maeneo ya mwera na kuja mijini,baada ya kusimamisha gari dereva alisimama lakini alimwambia mbele kumejaa labda nyuma lakini nimemueka mbuzi..jamaa akasema hamna wasi mbuzi tu mimi nitakaa nae..jamaa alipewa lift lakini ilibidi akae na mbuzi kule nyuma...baada ya mwendo mdogo tu jamaa alianza kusinzia nakuanza kuyumba ishara ya kuanguka yule mbuzi alishtuka kuona vile....jamaa akasinzia tena na tena ilibidi yule mbuzi ajiulize huyu jamaa vipi anatangaza vita na mimi....yule jamaa kusinzia tena tu yule mbuzi na yeye akainua miguu yake ya mbele...yule jamaa kuyumba tena alikutana kichwa na kichwa na yule mbuzi.....yule jamaa ilibidi asimamishe gari ashuke hata hajafika safari yake akiwa na bonge la tenzi usoni mwake...hahaaaaaa.hehehee hihihihhiii...
vituko ndani ya mental (hospital ya wagonjwa wa akili)

mara hii pale madaktari wanapoamua kuwafanyia interview(majaribio) machizi wote wale waliokua afadhali kidogo ili watolewe wakasalimie makwao....
jaribio la leo madaktari walichora mlango mkubwa kwenye ukuta alafu wakawaruhusu machizi wote watoke..baada ya muda wale machizi wote walikimbilia ule mlango isipokua mmoja tu yeye alikua katulia....wale madaktari waliona huyu aliyebakia labda ndo kapoa kidogo ilibidi wamuite ili wamuulize maswali....
aliulizwa wewe mbona huendi kutoka nje...yule chizi alijibu mimi nawaangalia tu uo ufunguo wenyewe ninao mimi watatoka vipi wale.......hahahaaa heheeeee hihihii....
Baba aliyekuwa na hasira kwa matokeo mabaya ya mwanawe ya shule kamwambia mwanawe; Napoleon mfalme wa ufaransa alipokuwa mdogo kama wewe alikuwa akiongoza kwa masomo shuleni. Mtoto nae akamjibu babake na kumwambia; Napoleon huyo huyo alipokuwa ana umri kama wako baba alikuwa mfalme wa ufaransa,mbona wewe hujakuwa mfalme????,heheheheheh
Kuna polisi wawili wa kuzuwia fujo ambao walihamishwa kutoka kijijini kwa ujinga mwingi walionao, kwa mara ya kwanza waliingizwa kiwanja cha mpira ili kuzuwia fujo zozote kama zitatokea,Kamanda wao kawaambia mukisikia au mukimuona mtu yeyote ambae ni hatari kwa watazamaji au kwa wachezaji - mumkamate MARA MOJA. Hapo uwanjani muda sio mrefu,mtangazaji wa ndani akatangaza kwa kipaza sauti; MCHEZAJI HATARI SASA ANAINGIA UWANJANI,MAMBO MAKUBWA LEO,na wakati huo mchezaji huyo anaingia uwanjani kwa kasi sana!!! na huku nyuma yake ni hao mapolisi wawili wanamfukuza mpaka wakamkamata, eti tumeambiwa mtu yeyote ambae ni hatari tumkamate,na sisi tumesikia kwa masikio yetu kama wewe ni hatariiiiii,twendeee!!!! hahahahahah
Mama mmoja kamuacha mwanawe mchanga kwa bibi yake kwa muda wa siku mbili na yeye kaenda matangani,huku kwa bibi mtoto alikuwa analia sana,bibi kaona hamna njia nyengine ya kumnyamazisha mtoto isipokuwa ni kumnyonyesha ziwa lake mwenyewe{bibi}. Mama aliporudi kamkuta mwanawe mgonjwa mgonjwa ikabidi ampeleke hospitali akapimwe,baada ya kupimwa daktari akamwambia mama mtoto;usiwe na wasiwasi,hali ya mwanao haitishi - mwanao kanywa maziwa yaliyoisha muda wake!!!!!heheheheheheh.{ Date of expire 1960}
Rafiki yangu wadudu wamezidi,hata humu pia?duh!!,hebu nipatie spray yoyote au antivirus au shemejivirus au shangazivirus nikamalize haka
kuna mzungu mmoja katika kupiga piga picha msituni alifika katika ziwa nyara alimkuta mtoto wa kiboko akimuuliza mamake..mama kwa nini wewe una domo kubwa mama mtu alijibu aaaaa tulia mwanangu na wewe unakuja huku huku....mtoto akamuliza tena kwa iyo na mie nitakuwa na domo kama lako..mama akajibu naam mwanangu pengine kuliko ata hili..mtoto akasema kama hivyo bora mie ata nife tu....mzungu akabaki kusema kweli mungu kaumba..hahaaaaa..hihihihihh..heheeee...
kuna jamaa watatu walikutana kijiweni yaani maskani kila mmoja alianza kusimulia ndoto ambayo ameota wawili walikuwa washahadithia akabakia mmoja wakawa wanamsikiliza.....
jana masela mimi nimeota nimepata ujauzito alafu mimba ilishakuwa miezi 8 ndani ya usiku wa saa saba uchungu ulinizidi ikabidi niwahishwe hospital baada ya harakati za madokta kutaka kunizalisha kweli walifanikiwa kumpata mtoto lakini baada ya kuamka asubuhi nikuta nimejisadia haja kubwa ndani ya suruali......sasa masela nakuulizeni hii ndoto inamaanisha nini? washkaji wote walipigwa na mshangao... hahahaaaa heeheheheee hihihihhihi.......
kuna jamaa mmoja katika harakati zake za kulala aliota ndoto moja mbaya sana ikabidi amuhadithie babake asubuhi ilipofika....baba nataka nikuhadithie ndoto ambayo niliyoota jana babake akasema njoo mwanangu wewe ndio kidume ninaekutegemea humu ndani lete habari ....mtoto akaanza kusimulia jana baba niliota ndoto nimeolewa alafu baada ya kumalizika harusi wewe ukaniambia niende kwa mume wangu nichukue kila kilicho changu.....baba mtu alibaki kaduwaa tu akimalizia kusema kweli sina mtoto hapa.....hahaaaaaa heheheeee......
Jamaa mmoja kaumwa na nyoka,akacheeeeka sana.Nyoka akamuuliza unachekeshwa na nini?,akamwambia umeniuma na mimi nina UKIMWI.heheheheheheh
Mlevi wa bangi anamuuliza mwenziwe;kwanini taarifa ya habari ya leo ni ndefu sana?; akamjibu; nafikiri leo ni TOLEO LA MWISHO !!!!!!!!!!!!! heheheheheheheh
Kijana mvuta bangi na muhuni sana,wazazi wake wanajaribu kumfundisha heshima na adabu nzuri,kama vile ukitaka kuingia nyumbani lazima ugonge mlango,baadae wakasema wacha tumchunguze kama kweli anafuata mafunzo au laa, wakamuona kasimama mbele ya friza,kabla hajaufungua mlango wa friza kabisha hodiiiii. hehehehehehehh
Kuna jamaa mmoja amemtumia mkewe barua lakini hajaandika lolote,yaani karatasi safi bila maandiko yoyote,akaulizwa kwanini hujaandika kitu? akasema; nimemkasirikia mke wangu sitaki kumsemesha. hahahahahhaaahh
pale wanachi wanapoamua kumfukuza mwizi mmoja ambae aliiba maeneo ya mtendeni,baada ya pirika za huku na huku walikutana na msenge mmoja na kumsimamisha na kuanza kumuuliza maswali

WANANCHI; umemuona mwizi kapita maeneo haya
MSENGE; eeeee nimemuona kapita kwangu hapa lakini nimemmwagia maji ya vumba la samaki akifika mbele tu ataliwa na paka msiwe na wasi wasi.........wananchi wote walipigwa na ganzi...........hahahaaaa heheheeeee.....


Mvuta bangi anapiga simu anamtafuta Yona,mara kapokea simu mtu mwengine,
Mvuta bangi: Hello wewe ni Yona?
Mtu: Laa mimi sio Yona,
Mvuta bangi: kama wewe sio Kidungaz kwanini kupokea simu?????.
heheheheheheh!!!!!!

POEM OF THE MONTH >> > POEM #1 >> > >> > Roses are red, >> > Pickles are green >> > I love your legs >> > and whats between >> > >> > POEM #2 >> > Roses are red >> > Grass is green >> > Open your legs >> > And i'll https://jamii.app/JFUserGuide you clean >> > >> > POEM #3 >> > I like your style >> > I like your class >> > but most of all >> > I like your ass >> > >> > POEM #4 >> > I'm a cool girl >> > In a cool town >> > It takes a real mother fucker to put me down >> > >> > POEM #5 >> > Kissing is a habit >> > Fucking is a game >> > Guys get all the pleasure >> > Girls get all the pain >> > The guy says i love you >> > You believe its true >> > But when your tummy starts to swell >> > He says 'the hell with you' >> > 10 minutes of pleasure >> > 9 months of pain >> > 3 days in hospital >> > A baby without a name >> > The baby is a bastard >> > The mother is a whore >> > This never wouldn't have happened >> > If the rubber wouldn't have torn >> > >> > POEM #6 >> > Guys are like roses >> > Watch out for the pricks >> > >> > POEM #7 >> > Smoke a smoke >> > Not a butt >> > https://jamii.app/JFUserGuide a virgin >> > Not a slut >> > >> > POEM #8 >> > Sex is evil >> > Evil is sin >> > Sins are forgiven >> > So stick it in >> > >> > POEM #9 >> > Holy mother,full of grace >> > Bless my boyfriend's gorgeous face >> > Bless his hair that tends to curl >> > Keep him safe from all the girls >> > Bless his arms that are so strong >> > Keep his hands where they belong >> > Bless his dick,the one i sucked >> > Bless the bed,in which we fucked >> > And if my mum happened to walk in >> > Bless the shit i'd be in >> > >> > POEM #10 >> > Sex is when a guy's communication >> > Enters a girl's destination >> > To increase the population >> > For a younger generation >> > Do you get the information >> > Or do you need a demostration >> > >> > POEM #11 >> > Men are like public toilets >> > They are either engaged or full of shit >> > >> > POEM # 12 >> > If guys had their periods >> > They would have compare the size of their tampons >> > >> > POEM #13 >> > Mental anxienty >> > Mental breakdowns >> > Menstural cramps >> > Menopause..... >> > Did you ever notice how all our problems begin >> > With MEN! >> > >> > >> > POEM #14 >> > Roses are red >> > Violets are corny >> > When i think of you >> > Ohh baby i get horny >> > Eat me >> > Beat me >> > Bite me >> > Blow me >> > Suck me >> > https://jamii.app/JFUserGuide me >> > very slowly >> > If u kiss me >> > Don't be sassy >> > Use your tongue >> > And make it nasty!!!!! >> > >> > >> > POEM #15 >> > Roses are Red >> > Violets are Black >> > Why is your chest >> > As flatt as your back??
 
Ki-PDF basi hafu ukiweke kwa ku-chinipandisha yaani "download" sijui ni sawa hapa waswahilina mtanisaidia.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom