Waziri wa madini
JF-Expert Member
- Jun 12, 2019
- 379
- 464
Kuelekea utekelezaji wa mipango na mikakati ya ilani ya uchaguzi ya chama Cha mapinduzi 2020_2025 .
Serikali ya awamu ya sita ni lazima iendeleze itikadi na falsafa za awamu ya tano na sababu kuu ni kwamba Kura za wananchi walizopata serikali ya CCM katika uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2020 zilitokana na ilani ya uchaguzi ambayo chama Cha CCM waliinadi,lakini pia asilimia kubwa ya Watanzania waliipa dhamana serikali ya CCM kuongoza nchi hii kwa sababu ya Imani kubwa waliyokuwa nayo juu ya aliyekuwa Rais John pombe Joseph Magufuli na aliyekuwa Mgombea mwenza wake ambaye ndiye Rais wetu wa awamu ya sita Mama Samia Suluhu Hassan.
Matarajio na matumaini ya wananchi ni kwamba Rais aliyepo madarakani kwa vyovyote vile ataendeleza Yale yote mazuri yaliyofanywa na serikali ya awamu ya tano kwa sababu na yeye alikuwa miongoni mwa watendaji wakuu waserikali hiyo,lakini pia watayaenzi na kuyalinda Mambo yote mema aliyotufanyia aliyekuwa Rais wetu Dr.Magufuli.
Kila kasoro iliyojitokeza katika utendaji wq serikali ya awamu ya tano ukweli wa Mambo Rais wetu wa Sasa na serikali nzima inapaswa kurekebisha kwa sababu ni wajibu wao kikatiba na ikizingatiwa na wao walikuwa sehemu ya serikali hiyo iliyopita.Haifai kila lawama na jambo baya anabebeshwa mpendwa wetu tu Hayati Magufuli.
Mpendwa wetu amekwenda na Sasa ni awamu ya sita.
Awamu ambayo matumaini yetu ni makubwa na Imani yetu haina Shaka juu ya serikali yetu chini ya Rais jemedari Mama Samia Suluhu Hassan.
Wahenga wana msemo usemao kila zama na kitabu chake na Kuna mbunge kutoka mtama ametukumbusha usemi huu kuwa Sasa tumwache mama aandike kitabu chake,ni kweli kabisa Ila lazima tukumbuke kitabu Cha mama katika kava lake la nje Kuna sura ya mpendwa wetu Rais Magufuli lakini hata dibaji ya kitabu hicho iliiandikwa kwa mkono wa Rais Magufuli .
Hitimisho,tunajenga nyumba moja haipaswi kugombea fito serikali ni ya CCM na Siku zote CCM ni Ile ile.Wale wapinga maendeleo na maadui wataifa letu hawana nafasi mbele ya serikali ya CCM.
Serikali ya awamu ya sita ni lazima iendeleze itikadi na falsafa za awamu ya tano na sababu kuu ni kwamba Kura za wananchi walizopata serikali ya CCM katika uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2020 zilitokana na ilani ya uchaguzi ambayo chama Cha CCM waliinadi,lakini pia asilimia kubwa ya Watanzania waliipa dhamana serikali ya CCM kuongoza nchi hii kwa sababu ya Imani kubwa waliyokuwa nayo juu ya aliyekuwa Rais John pombe Joseph Magufuli na aliyekuwa Mgombea mwenza wake ambaye ndiye Rais wetu wa awamu ya sita Mama Samia Suluhu Hassan.
Matarajio na matumaini ya wananchi ni kwamba Rais aliyepo madarakani kwa vyovyote vile ataendeleza Yale yote mazuri yaliyofanywa na serikali ya awamu ya tano kwa sababu na yeye alikuwa miongoni mwa watendaji wakuu waserikali hiyo,lakini pia watayaenzi na kuyalinda Mambo yote mema aliyotufanyia aliyekuwa Rais wetu Dr.Magufuli.
Kila kasoro iliyojitokeza katika utendaji wq serikali ya awamu ya tano ukweli wa Mambo Rais wetu wa Sasa na serikali nzima inapaswa kurekebisha kwa sababu ni wajibu wao kikatiba na ikizingatiwa na wao walikuwa sehemu ya serikali hiyo iliyopita.Haifai kila lawama na jambo baya anabebeshwa mpendwa wetu tu Hayati Magufuli.
Mpendwa wetu amekwenda na Sasa ni awamu ya sita.
Awamu ambayo matumaini yetu ni makubwa na Imani yetu haina Shaka juu ya serikali yetu chini ya Rais jemedari Mama Samia Suluhu Hassan.
Wahenga wana msemo usemao kila zama na kitabu chake na Kuna mbunge kutoka mtama ametukumbusha usemi huu kuwa Sasa tumwache mama aandike kitabu chake,ni kweli kabisa Ila lazima tukumbuke kitabu Cha mama katika kava lake la nje Kuna sura ya mpendwa wetu Rais Magufuli lakini hata dibaji ya kitabu hicho iliiandikwa kwa mkono wa Rais Magufuli .
Hitimisho,tunajenga nyumba moja haipaswi kugombea fito serikali ni ya CCM na Siku zote CCM ni Ile ile.Wale wapinga maendeleo na maadui wataifa letu hawana nafasi mbele ya serikali ya CCM.
#KAZIIENDELEE