Kitabu cha Rais Samia Suluhu kina picha na dibaji ya Hayati Magufuli

Waziri wa madini

JF-Expert Member
Jun 12, 2019
379
464
Kuelekea utekelezaji wa mipango na mikakati ya ilani ya uchaguzi ya chama Cha mapinduzi 2020_2025 .

Serikali ya awamu ya sita ni lazima iendeleze itikadi na falsafa za awamu ya tano na sababu kuu ni kwamba Kura za wananchi walizopata serikali ya CCM katika uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2020 zilitokana na ilani ya uchaguzi ambayo chama Cha CCM waliinadi,lakini pia asilimia kubwa ya Watanzania waliipa dhamana serikali ya CCM kuongoza nchi hii kwa sababu ya Imani kubwa waliyokuwa nayo juu ya aliyekuwa Rais John pombe Joseph Magufuli na aliyekuwa Mgombea mwenza wake ambaye ndiye Rais wetu wa awamu ya sita Mama Samia Suluhu Hassan.

Matarajio na matumaini ya wananchi ni kwamba Rais aliyepo madarakani kwa vyovyote vile ataendeleza Yale yote mazuri yaliyofanywa na serikali ya awamu ya tano kwa sababu na yeye alikuwa miongoni mwa watendaji wakuu waserikali hiyo,lakini pia watayaenzi na kuyalinda Mambo yote mema aliyotufanyia aliyekuwa Rais wetu Dr.Magufuli.

Kila kasoro iliyojitokeza katika utendaji wq serikali ya awamu ya tano ukweli wa Mambo Rais wetu wa Sasa na serikali nzima inapaswa kurekebisha kwa sababu ni wajibu wao kikatiba na ikizingatiwa na wao walikuwa sehemu ya serikali hiyo iliyopita.Haifai kila lawama na jambo baya anabebeshwa mpendwa wetu tu Hayati Magufuli.

Mpendwa wetu amekwenda na Sasa ni awamu ya sita.

Awamu ambayo matumaini yetu ni makubwa na Imani yetu haina Shaka juu ya serikali yetu chini ya Rais jemedari Mama Samia Suluhu Hassan.

Wahenga wana msemo usemao kila zama na kitabu chake na Kuna mbunge kutoka mtama ametukumbusha usemi huu kuwa Sasa tumwache mama aandike kitabu chake,ni kweli kabisa Ila lazima tukumbuke kitabu Cha mama katika kava lake la nje Kuna sura ya mpendwa wetu Rais Magufuli lakini hata dibaji ya kitabu hicho iliiandikwa kwa mkono wa Rais Magufuli .

Hitimisho,tunajenga nyumba moja haipaswi kugombea fito serikali ni ya CCM na Siku zote CCM ni Ile ile.Wale wapinga maendeleo na maadui wataifa letu hawana nafasi mbele ya serikali ya CCM.

#KAZIIENDELEE​


FB_IMG_16184854608321000.jpg
 
Mkuu nimeishia hapa:

"Serikali ya awamu ya sita ni lazima iendeleze itikadi na falsafa za awamu ya tano"

Lazima?!

Wajameni mbona kupangiana? Haya si ndiyo aliyoyakataa mwendazake?
Hatupangiani ila ilani ndio inawataka hivyo ni lazima itekelezwe
 
Mnaparuana mwenyewe akiwa kavaa miwani yake anawatazama tu kwa tararibu atachagua njia yake. Ngoja kwanza tumalize mfungo
 
Trivia:

Ukurasa wa Kitabu namba 20 unamaanisha Mwaka 2020 na ukurasa namba 21 unamaanisha mwaka 2021.

Thank me later.
 
Hatupangiani ila ilani ndio inawataka hivyo ni lazima itekelezwe

Hii ni awamu ya sita jombi. Rais wake ni mama Samia. Kwa mujibu wa katiba inayopigiwa kelele yeye ndiye mwamuzi wa nini kifanyike na hakuna kuhoji. Umeyasahau ya Burigi na airport matata kabisa ya kule kwetu?

Nakazia: niliishia kusoma nilipokuelekeza.

Huo ndiyo ulio ukweli mchungu kweri kweri.
 
kusema ukweli ili Tanzania tuendelee ni lazima tufuate falsafa na maono ya hayati Dr. JPM.
 
Hapo ndio tunapofeli, kwanini yeye aandike kitabu chake ni si watanzania tumpe maelekezo aandike kitabu kipi?
nape
makamba
Unaweza wasikia sauti zao za ndani zilizojaa giliba na, chuki na unafiki
 
Hii ni awamu ya sita jombi. Rais wake ni mama Samia. Kwa mujibu wa katiba inayopigiwa kelele yeye ndiye mwamuzi wa nini kifanyike na hakuna kuhoji. Umeyasahau ya Burigi na airport matata kabisa ya kule kwetu?

Nakazia: niliishia kusoma nilipokuelekeza.

Huo ndiyo ulio ukweli mchungu kweri kweri.
Kwani ni ilani gani tunayoitekeleza
 
Hapo ndio tunapofeli, kwanini yeye aandike kitabu chake ni si watanzania tumpe maelekezo aandike kitabu kipi?
nape
makamba
Unaweza wasikia sauti zao za ndani zilizojaa giliba na, chuki na unafiki
Hawa watu ni tatizo katika taifa letu hawafai uzuri hata Mama yetu ameshawagundua Sasa wanahaha kuji kombakomba
 
Kuelekea utekelezaji wa mipango na mikakati ya ilani ya uchaguzi ya chama Cha mapinduzi 2020_2025 .

Serikali ya awamu ya sita ni lazima iendeleze itikadi na falsafa za awamu ya tano na sababu kuu ni kwamba Kura za wananchi walizopata serikali ya CCM katika uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2020 zilitokana na ilani ya uchaguzi ambayo chama Cha CCM waliinadi,lakini pia asilimia kubwa ya Watanzania waliipa dhamana serikali ya CCM kuongoza nchi hii kwa sababu ya Imani kubwa waliyokuwa nayo juu ya aliyekuwa Rais John pombe Joseph Magufuli na aliyekuwa Mgombea mwenza wake ambaye ndiye Rais wetu wa awamu ya sita Mama Samia Suluhu Hassan.

Matarajio na matumaini ya wananchi ni kwamba Rais aliyepo madarakani kwa vyovyote vile ataendeleza Yale yote mazuri yaliyofanywa na serikali ya awamu ya tano kwa sababu na yeye alikuwa miongoni mwa watendaji wakuu waserikali hiyo,lakini pia watayaenzi na kuyalinda Mambo yote mema aliyotufanyia aliyekuwa Rais wetu Dr.Magufuli.

Kila kasoro iliyojitokeza katika utendaji wq serikali ya awamu ya sita ukweli wa Mambo Rais wetu wa Sasa na serikali nzima inapaswa kurekebisha kwa sababu ni wajibu wao kikatiba na ikizingatiwa na wao walikuwa sehemu ya serikali hiyo.

Mpendwa wetu amekwenda na Sasa ni awamu ya sita.

Awamu ambayo yetu ni matumaini ni makubwa na Imani yetu haina Shaka juu ya serikali yetu chini ya Rais jemedari Mama Samia Suluhu Hassan.

Wahenga wana msemo usemao kila zama na kitabu chake na Kuna mbunge kutoka mtama ametukumbusha usemi huu kuwa Sasa tumwache mama aandike kitabu chake,ni kweli kabisa Ila lazima tukumbuke kitabu Cha mama katika kava lake la nje Kuna sura ya mpendwa wetu Rais Magufuli lakini hata dibaji ya kitabu hicho iliiandikwa kwa mkono wa Rais Magufuli .

Hitimisho,tunajenga nyumba moja haipaswi kugombea fito serikali ni ya CCM na Siku zote CCM ni Ile ile.Wale wapinga maendeleo na maadui wataifa letu hawana nafasi mbele ya serikali ya CCM.

#KAZIIENDELEE​


View attachment 1752744
Nakusahishisa...Mama Samia ni Rais wa Sita katika Serikali ya awamu ya tano..ambayo itakoma ama kufika mwishoni mwaka 2025.
 
Kuelekea utekelezaji wa mipango na mikakati ya ilani ya uchaguzi ya chama Cha mapinduzi 2020_2025 .

Serikali ya awamu ya sita ni lazima iendeleze itikadi na falsafa za awamu ya tano na sababu kuu ni kwamba Kura za wananchi walizopata serikali ya CCM katika uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2020 zilitokana na ilani ya uchaguzi ambayo chama Cha CCM waliinadi,lakini pia asilimia kubwa ya Watanzania waliipa dhamana serikali ya CCM kuongoza nchi hii kwa sababu ya Imani kubwa waliyokuwa nayo juu ya aliyekuwa Rais John pombe Joseph Magufuli na aliyekuwa Mgombea mwenza wake ambaye ndiye Rais wetu wa awamu ya sita Mama Samia Suluhu Hassan.

Matarajio na matumaini ya wananchi ni kwamba Rais aliyepo madarakani kwa vyovyote vile ataendeleza Yale yote mazuri yaliyofanywa na serikali ya awamu ya tano kwa sababu na yeye alikuwa miongoni mwa watendaji wakuu waserikali hiyo,lakini pia watayaenzi na kuyalinda Mambo yote mema aliyotufanyia aliyekuwa Rais wetu Dr.Magufuli.

Kila kasoro iliyojitokeza katika utendaji wq serikali ya awamu ya sita ukweli wa Mambo Rais wetu wa Sasa na serikali nzima inapaswa kurekebisha kwa sababu ni wajibu wao kikatiba na ikizingatiwa na wao walikuwa sehemu ya serikali hiyo.

Mpendwa wetu amekwenda na Sasa ni awamu ya sita.

Awamu ambayo yetu ni matumaini ni makubwa na Imani yetu haina Shaka juu ya serikali yetu chini ya Rais jemedari Mama Samia Suluhu Hassan.

Wahenga wana msemo usemao kila zama na kitabu chake na Kuna mbunge kutoka mtama ametukumbusha usemi huu kuwa Sasa tumwache mama aandike kitabu chake,ni kweli kabisa Ila lazima tukumbuke kitabu Cha mama katika kava lake la nje Kuna sura ya mpendwa wetu Rais Magufuli lakini hata dibaji ya kitabu hicho iliiandikwa kwa mkono wa Rais Magufuli .

Hitimisho,tunajenga nyumba moja haipaswi kugombea fito serikali ni ya CCM na Siku zote CCM ni Ile ile.Wale wapinga maendeleo na maadui wataifa letu hawana nafasi mbele ya serikali ya CCM.

#KAZIIENDELEE​


View attachment 1752744

Kama sehemu ya 'appreciation' Kwake na hivi pia ni Hayati sasa wala sioni tatizo lolote lile la Rais Samia kutumia Picha yake hiyo.

Pamoja na kwamba Hayati tunamnanga ( tunasema ) kutokana na yale 'aliyotukwaza' ila alimuinua na Kumjenga vyema Rais Samia.

Ni jambo tu la Kibinadamu na Utu zaidi.
 
Mkuu nimeishia hapa:

"Serikali ya awamu ya sita ni lazima iendeleze itikadi na falsafa za awamu ya tano"

Lazima?!

Wajameni mbona kupangiana? Haya si ndiyo aliyoyakataa mwendazake?
NI LAZIMA AENDELEZE KWANI AKIYAACHA HATWEZI KUKUBALI..MFANO ETI AACHE UJENZI WA BWAWA LA NYERERE KISA HAPANGIWI WAKATI TUMEISHA LIPA TRILLION
 
Mkuu na wewe hujakubali kuwa awamu ya tano ilishakwenda na mwendazake na hii ni awamu ya sita?
Duh..wazee mbona wagumu kuelewa aisee..Mama Samia ataanza awamu ya Sita baada ya uchaguzi Mkuu wa 2025..kwa sasa hata Ilani ya chama chake inatamka awamu ya tano...hio 2025 atakuwa Rais wa Sita katika awamu ya Sita ...2030 akifika Rais ajaye atakuwa Rais wa Saba awamu ya Sita..so now mama Samia ni Rais wa Sita katika awamu ya tano..coz haikuisha..
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom