Ibnu Ayoub
Member
- Mar 4, 2011
- 78
- 0
Napendekeza masomo yote yanayofundishwa katika mashule na vyuo vyote Tanzania yafundishwe kwa lugha ya taifa ili kuongeza idadi ya wanaofaulu na uelewa juu ya wanachojifunza. Kusoma kwa kiswahili kuanzia darasa la kwanza mpaka la saba halafu unapoingia kidato cha kwanza unaanza kusoma masomo yote kwa kiingereza huku ni kuumizana na kupotezeana muda wana Jamii, Mnapoandamana kuhusu Maisha bora msilisahau na hili.Hakika wanafunzi wanaumia sana kwa kukariri kuliko kuelewa.