Kiswahili ni lugha bora kwa wanafunzi wa Tanzania

Ibnu Ayoub

Member
Mar 4, 2011
78
0
Napendekeza masomo yote yanayofundishwa katika mashule na vyuo vyote Tanzania yafundishwe kwa lugha ya taifa ili kuongeza idadi ya wanaofaulu na uelewa juu ya wanachojifunza. Kusoma kwa kiswahili kuanzia darasa la kwanza mpaka la saba halafu unapoingia kidato cha kwanza unaanza kusoma masomo yote kwa kiingereza huku ni kuumizana na kupotezeana muda wana Jamii, Mnapoandamana kuhusu Maisha bora msilisahau na hili.Hakika wanafunzi wanaumia sana kwa kukariri kuliko kuelewa.
 
Hapa ninakuunga mkono Mkuu. Sera ya Tanzania ya lugha imepotoka. Nakumbuka tangu mwaka 1969 Serikali ilitangaza nia ya kukifanya Kiswahili sio lugha ya Taifa tu bali lugha ya kufundishia, alkini sera hii daima haikutekelezwa badala yake tunawasumbua wanafunzi. Tunawaumisha vichwa wanafunzi wetu ambao inawabidi wafikirie katika Kiswahili wakati wanapokumbana na swali katika lugha ya Kiingereza. Mtoto hujifunza zaidi katika lugha yake ya kwanza. Faida yake watoto wanakuwa wepesi wa kufahamu na wabunifu kwa kutumia lugha yao kuliko kutumia lugha ya kigeni. Hapa hatusemi kuwa Kiingereza kiwachwe, bali kisomeshwe kama lugha ya pili tangu miaka ya mwanzo ya elimu.

Wanaotetea Kiingereza wanadai kuwa Kiswahili hakijitoshelezi. Hii si kweli. Taasisi ya uchunguzi wa Kiswahili imekuwa ikisanifisha Kiswahili kwa muda mrefu katika nyanja zote na tayari kuna makabrasha kwa makabrasha ya maandishi yaliyokaa katika makabati bila ya kupelekwa kwa watumiaji.

Kiswahili kina utajiri mkubwa na ulaini wa kulibadilisha neno lolote la lugha ya kigeni (hasa kutoka Kiingereza tunachoking'ang'ania) na kulitohoa kukidhi matamshi, maana na maandishi ya Kiswahili.

Wakati umefika kukifanya Kiswahili lugha ya kufundishia viwango vyote vya ellimu.
 
Hapa ninakuunga mkono Mkuu. Sera ya Tanzania ya lugha imepotoka. Nakumbuka tangu mwaka 1969 Serikali ilitangaza nia ya kukifanya Kiswahili sio lugha ya Taifa tu bali lugha ya kufundishia, alkini sera hii daima haikutekelezwa badala yake tunawasumbua wanafunzi. Tunawaumisha vichwa wanafunzi wetu ambao inawabidi wafikirie katika Kiswahili wakati wanapokumbana na swali katika lugha ya Kiingereza. Mtoto hujifunza zaidi katika lugha yake ya kwanza. Faida yake watoto wanakuwa wepesi wa kufahamu na wabunifu kwa kutumia lugha yao kuliko kutumia lugha ya kigeni. Hapa hatusemi kuwa Kiingereza kiwachwe, bali kisomeshwe kama lugha ya pili tangu miaka ya mwanzo ya elimu.

Wanaotetea Kiingereza wanadai kuwa Kiswahili hakijitoshelezi. Hii si kweli. Taasisi ya uchunguzi wa Kiswahili imekuwa ikisanifisha Kiswahili kwa muda mrefu katika nyanja zote na tayari kuna makabrasha kwa makabrasha ya maandishi yaliyokaa katika makabati bila ya kupelekwa kwa watumiaji.

Kiswahili kina utajiri mkubwa na ulaini wa kulibadilisha neno lolote la lugha ya kigeni (hasa kutoka Kiingereza tunachoking'ang'ania) na kulitohoa kukidhi matamshi, maana na maandishi ya Kiswahili.

Wakati umefika kukifanya Kiswahili lugha ya kufundishia viwango vyote vya ellimu.

Umesema kweli Mamamia
 
Pia wakumbuke kuwa hata Kiingereza wanachokikomalia huko Ulaya zama hizo hakikuwa lugha ya vyuo. Mpango mzima ulikuwa Kilatini... Waingereza wakaona haja ya kubadili mfumo ili uwafae, nashangaa sisi. Unakuta kutwa kucha wanafunzi wanakariri point, ukisoma maelezo, utumbo mtupu!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom