Kiswahili Kitapotea na Kuzaliwa Lugha nyingine endapo hatutabadilika Watumiaji wa Lugha hii adhimu.

Phinna

Member
May 31, 2017
12
6
Habari wana jf

Ni matumaini yangu sote tunaendelea vizuri na majukumu yetu mbalimbali yanayotukabili. Lakini pia hatukosi muda wa kukutana hapa jamvini na kupeana mambo kadha wa kadha.

Leo hii mimi napenda kuongelea mwenendo wa lugha yetu hii adhimu ambayo imetufanya kuwa na utambulisho wetu katika mataifa mengine kutokana na kuitumia sana kama lugha yetu ya taifa. Nayo si lugha nyingine bali ni lugha ya Kiswahili. Mwenendo wa watumiaji wa lugha hii hasa hapa kwetu Tanzania ambapo naweza kupaita ndiyo makao makuu ya lugha hii, ndipo Kiswahili kimeanza kuharibiwa tena kwa kasi ya ajabu.

Kila lugha ina nahau zake, misemo yake na hata methali zake, lakini jambo linaloshangaza sana tumeanza kuona vya kwetu havifahi na kuanza kurukia yaliyoko kwenye lugha ngeni. Hapa chini naorodhesha baadhi ya makosa ambayo nadiriki kuyaita ni ya makusudi kabisa ambayo yanaweza kusababisha kupotea kwa uhalisia wa Kiswahili kutokana na kuharibiwa sarufi yake.

1: Neno "pelekea"-Kisarufi neno hili linamaana nyingi. Neno hili ni mnyumbuliko wa neno peleka. Lakini sasa linatumika kwa maana ya "sababisha", jambo ambalo si sahihi. Wamegeuza maneno ya Kiingereza "lead to" ambayo tafsiri yake sahihi ni sababisha watu wakatafsiri neno lead kwa Kiswahi pasipo kujua kuwa "lead to" ni clause ambayo kwa Kiswahili ni sababisha.

Ni jambo la kawaida sasa kumkuta mtu hata kama ni msomi wa kiwango gani, mwana habari au mwandishi wa vitabu naye akitumia lugha hii "hiki ndicho kilichompelekea kukamatwa" badala ya "hiki ndicho kilichosababisha akamatwe".

2: All in all- Nimewasikia watu wengi wakihangaika kutafsiri maneno hayo kwa Kiswahili. Utamsikia mtu anasema "yote katika yote". Hivi kweli tangu shule ya msingi hadi ya upili, umewahi kukutana na maneno kama hayo katika Kiswahili? Au tukifika Chuo Kikuu ndiyo tunatengeneza Kiswahili kipya?

3: Kuna lugha nyingine sasa inazaliwa tena na kukuwa kwa kasi. Sijui lugha hii itaitwa je! Eti unamkuta mtu anaongea kwa madaha kweli kweli, "atleast angalau", "sorry samahani", "infact kwa kweli". Hii ni Lugha gani?

4: Kuna tatizo ambalo sasa ndiyo limeanza kuwa sugu kama malaria, nalo ni kuchanganya herufi. Panapotakiwa kuweka "r" mtu anaweka "l" na kinyume chake. Athirika mtu anaandika adhirika. Hivi hata kama wewe unatokea kaskazini, ndivyo ulivyofundishwa darasani?

Jamani nawaombeni Waswahili wenzangu, tuipende lugha yetu isije kupotea ikazaliwa lugha mpya isiyokuwa na maana. Nakumbuka hayati Baba wa Taifa aliwahi kusema wasomi ndiyo watu wa kwanza kukiharibu Kiswahili. Kuchanganya lugha si alama ya usomi. Ni hayo tu jamani.
 
Asante kwa elimu hii namba 1 na mbili inanihusu,msichoke kutufundisha kiswahili sanifu.
 
4: Kuna tatizo ambalo sasa ndiyo limeanza kuwa sugu kama malaria, nalo ni kuchanganya herufi. Panapotakiwa kuweka "r" mtu anaweka "l" na kinyume chake. Athirika mtu anaandika adhirika. Hivi hata kama wewe unatokea kaskazini, ndivyo ulivyofundishwa darasani?
Matumizi ya "h" yananichanganya kabisa mf "ana" mtu anaandika "hana", "haji" inaandikwa "aji".
 
Hakika. Mimi naomba nimuongelee huyu Jibaba toto maarufu kama Le Mutuz. Huyu anachangia kwa kiasi kikubwa kuharibu Kiswahili chetu.

Utakuta anaandika;
Nafwaaaz
Nachekaaz
Najambaaz
Lebebeeez

Sasa mtu unabaki kushangaa, hii ni lugha gani?... Kama anashindwa aandike Kingereza tu.
 
Hakika. Mimi naomba nimuongelee huyu Jibaba toto maarufu kama Le Mutuz. Huyu anachangia kwa kiasi kikubwa kuharibu kiswahili chetu.

Utakuta anaandika;
Nafwaaaz
Nachekaaz

Sasa mtu unabaki kushangaa, hii ni lugha gani?...
 
Utakuta mtu ,neno Hindi (zao ) anaita Muhindi.Mfano.Badala ya kusema,"nataka Hindi moja la kuchoma'' mtu husema,"nataka muhindi mmoja wa kuchoma''.Vijitu vya Dar hivyo
 
Sifa ya luga ni kuzalisha misamiati mipya na kukua kulingana na mazingira na kizazi
 
Hakika. Mimi naomba nimuongelee huyu Jibaba toto maarufu kama Le Mutuz. Huyu anachangia kwa kiasi kikubwa kuharibu Kiswahili chetu.

Utakuta anaandika;
Nafwaaaz
Nachekaaz
Najambaaz
Lebebeeez

Sasa mtu unabaki kushangaa, hii ni lugha gani?... Kama anashindwa aandike Kingereza tu.
huyo kashindikana
 
Hakika. Mimi naomba nimuongelee huyu Jibaba toto maarufu kama Le Mutuz. Huyu anachangia kwa kiasi kikubwa kuharibu Kiswahili chetu.

Utakuta anaandika;
Nafwaaaz
Nachekaaz
Najambaaz
Lebebeeez

Sasa mtu unabaki kushangaa, hii ni lugha gani?... Kama anashindwa aandike Kingereza tu.
Anakiharibu au ndio anakikuza?
 
Hayo makosa ya lugha na mi ni mmojawapo. Hapo kwenye at lest angalau sijakuelewa naomba ufafanuzi
 
Mngekuwa mnatoa na mifano kwa wenzetu mfano kwa lugha ya kiingereza kuwa ni njia gani hutumia kuzuia mambo kama hayo ili lugha yao isipotee kama inawezekana kuzuia?
 
Hayo makosa ya lugha na mi ni mmojawapo. Hapo kwenye at lest angalau sijakuelewa naomba ufafanuzi
Maana haiwezi kuwa maana hadi mwenye maana ajue maana halisi ya maana kwakuwa neno maana litabaki kuwa maana daima.,.pole mkuu
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom