Kiswahili kinapanuka na kupasuka wakati huo huo?

Pulchra Animo

JF-Expert Member
Jun 16, 2016
3,398
2,990
Mara nyingi nisomapo makala ndefu za Kiswahili sikosi kukutana na angalau neno moja la Kiswahili linaloonekana kuwa jipya kwangu. At the same time, the same article may contain a few familiar words that do not appear to conform to the standard Swahili that I learned during my early school years. Mengi ya maneno yanayoathirika ni yale yenye herufi "h", "dh", "l" na "r" ndani yake.
Watu wanaandika, mfano,

aya wakimaanisha haya,
ivi wakimaanisha hivi,
ivyo wakimaanisha hivyo,
erufi wakimaanisha herufi,
uzuni wakimaanisha huzuni,
nazani wakimaanisha nadhani,
zuluma wakimaanisha dhuluma,
karenda wakimaanisha kalenda, n.k.

Sasa ninapoona vitu kama hivi, ninapata kigugumizi kuamini kwamba yale maneno yanayoonekana kama mapya kwangu kweli ni maneno mapya na sahihi ya Kiswahili.

What's going on? Sarufi ya Kiswahili siku hizi haifundishwi tena kwenye shule zetu au mimi nimeganda kwenye karne ya ishirini?
 
Mara nyingi nisomapo makala ndefu za Kiswahili sikosi kukutana na angalau neno moja la Kiswahili linaloonekana kuwa jipya kwangu. At the same time, the same article may contain a few familiar words that do not appear to conform to the standard Swahili that I learned during my early school years. Mengi ya maneno yanayoathirika ni yale yenye herufi "h", "dh", "l" na "r" ndani yake.
Na mdudu mwingine hatari zaidi kwa lugha yetu hii ni pale watumiaji wake kwa makusudi kabisa wanapoamua kuchanganya Kiswahili na Kiingereza. Na bila shaka, hali inageuka na kuwa ya kuogofya maradufu pale uchanganyaji huo wa Kiingereza unapofanyika katikati ya kukitetea Kiswahili! Inakuwa ni kama Mchungaji aliyesimama madhabahuni akikemea dhambi ya uzinzi wakati huo huo akionekana waziwazi na waumini jinsi anavyomtazama kwa jicho la matamanio mmoja wa waumini wa kike aliyeketi kiti cha mbele!
 
Na mdudu mwingine hatari zaidi kwa lugha yetu hii ni pale watumiaji wake kwa makusudi kabisa wanapoamua kuchanganya Kiswahili na Kiingereza. Na bila shaka, hali inageuka na kuwa ya kuogofya maradufu pale uchanganyaji huo wa Kiingereza unapofanyika katikati ya kukitetea Kiswahili! Inakuwa ni kama Mchungaji aliyesimama madhabahuni akikemea dhambi ya uzinzi wakati huo huo akionekana waziwazi na waumini jinsi anavyomtazama kwa jicho la matamanio mmoja wa waumini wa kike aliyeketi kiti cha mbele!

Sidhani kama hilo ni tatizo linaloweza kulinganishwa na uchafuzi wa maneno ya lugha fulani. It's common for writers (in any language) to borrow a word or words from another language. The rule is that the borrowed word(s) should be presented in its (their) correct form. Obviously, that doesn't violate any grammatical rules!
 
Sidhani kama hilo ni tatizo linaloweza kulinganishwa na uchafuzi wa maneno ya lugha fulani. It's common for writers (in any language) to borrow a word or words from another language. The rule is that the borrowed word(s) should be presented in its (their) correct form. Obviously, that doesn't violate any grammatical rules!
Tofautisha kati ya kuazima maneno na kuchanganya lugha!
 
Tofautisha kati ya kuazima maneno na kuchanganya lugha!
I would be OK na mtu anayechanganya kuliko anayeharbu kiswahili. Inaudhi sana ninaposoma huku jamvini maneno kama "mshahala" badala ya "mshahara", "kula" badala "kura". Ninajua kuna makabila ambayo wanashida ya kutamka maneno mengine lakini kuyaandika siku hizi imekuwa ni shida pia. Aibu !
 
I would be OK na mtu anayechanganya kuliko anayeharbu kiswahili. Inaudhi sana ninaposoma huku jamvini maneno kama "mshahala" badala ya "mshahara", "kula" badala "kura". Ninajua kuna makabila ambayo wanashida ya kutamka maneno mengine lakini kuyaandika siku hizi imekuwa ni shida pia. Aibu !
Kuchanganya nako ni kuharibu Kiswahili... mbona hili lipo wazi?! Tena ni kuharibu kwa makusudi tofauti na wale wa "r" na "l". Au mnaona hiyo si kuharibu kwavile tunachanganya na kizungu?!
 
Kingine kimechangia kuchafua kiswahili ni huu mziki wa bongo fleva, kiasi kikubwa sana,sikiliza mziki wa diamond nyimbo zake nyingi kuongeza neno ga mfano alikuja atasema alikujaga, Si peke yake tu Rais wenu baba nanii nayeye licha ya kuwa alikuwa Mwalimu pia kiswahili hajui,
Wahitimu wengi wa Primary kuanzia mwaka ya 2000 hawajui kiswahili, ndio hao badala Riziki waaandika Ridhiki, msingi wa kiswahili unatoka shule ya msingi, kuna mdogo wangu kamaliza degree juzi tu hapa lakini kiswahili tunabishana sana maana hakijui na masomo yake yote kasomea hapa hapa Tz
 
Pia ufipishaji maneno isivyo stahili inakera sana.

Sasa, unakuta imeandikwa xaxa :-/

aGgggggrrrrrrrrr!
 
Kizazi kipya kazi kweli kweli! In most cases, mtoto wa kigogo, kinyakyusa, kinyaturu, au kabila lolote lile, hana lugha yoyote anayoijua kwa ufasaha, iwe Kigogo, Kiswahili, au English! Tunaelekea wapi? Labda mimi ndiye niliyeganda kwenye karne ya ishirini!
 
Wewe ume borrow sentensi siyo word au words. Poor teacher

Sasa mbona unarudia kosa hilo hilo? Tena afadhali mimi sikufanya uchafuzi wa maneno; ya Kiswahili yamesimama na kujitosheleza na ya English vivyo hivyo! Angalia wewe "Ume" yako isivyojitosheleza.
 
Sasa mbona unarudia kosa hilo hilo? Tena afadhali mimi sikufanya uchafuzi wa maneno; ya Kiswahili yamesimama na kujitosheleza na ya English vivyo hivyo! Angalia wewe "Ume" yako isivyojitosheleza.
Hahahaaa. Mkuu nimecheka sana. Hizi zote ni juhudi za kujitetea?
 
Kuazima maneno kutoka lugha nyingine kuja kiswahili ni njia mojawapo ya uundaji wa msamiati wa kiswahili ambapo lugha uweza kukua...ila kuchanganya lugha wakati wa mazungumzo au maandishi ni kitu kungine tofauti kabisa
huweza
Ndio yale yale yanayo ongelewa hapa!!
 
Wakuu mjue katika lugha kuna kitu kinaitwa language change. Ambapo ndani yake kuna kitu kinaitwa morphological change. Hapa kwenye morphological change moja ya sababu kubwa ni factor inaitwa aesthetic factor...hapa ndo badala ya kusema hiki-hichi, haya-aya, sasa_asa etc.
Lakini pia tukumbuke kuwa hii inafanyika kwenye normal conversational environment ie informal use of lg.
Japo ni kweli kuwa language change ni hatari wakati mwingine kwenye maendeleo ya lugha kwani inaweza sababisha dead language ila ukweli ni kwamba haiepukiki.
 
Kumbuka kuwa, kuandika na kuongea lugha ya Kiswahili kwa ufasaha utatakiwa ubobee kwanye hii lugha, wengi wetu tunaandika Kiswahili cha kuongea au cha mazoea.
Lugha za makabila nazo zinachangia sana watu kukosea katika uandishi wa herufu, kuchanganya lugha ya Kingereza katikati ya Kiswahili nao ni uchafuzi mkubwa wa lugha.
 
Unajua zamani, tulipokuwa tunasoma vitabu shule ya msingi .Walimu walikuwa wanatutolea misamiati na miundo kwenye zile hadithi tulizokuwa tunasoma kwenye vitabu hivyo ,hii ilisaidia kujua misamiati mingi.
 
Kumbuka kuwa, kuandika na kuongea lugha ya Kiswahili kwa ufasaha utatakiwa ubobee kwanye hii lugha, wengi wetu tunaandika Kiswahili cha kuongea au cha mazoea.
Lugha za makabila nazo zinachangia sana watu kukosea katika uandishi wa herufu, kuchanganya lugha ya Kingereza katikati ya Kiswahili nao ni uchafuzi mkubwa wa lugha.

Kitu gani kimebadilika? Kiswahili cha kuongea au cha mazoea kimekuwepo tangu zamani. Vivyo hivyo lugha za makabila, pia! Matatizo niliyokuwa nikiyaona zamani ni kwamba mtu atalitamka neno tofauti na atakavyoliandika, kwa sababu ya athari ya lugha za makabila. Una kuta mtu, kwa mfano, anaandika neno "sasa" lakini analitamka "thatha" au neno "nchi" lakini analitamka "nji". Bottom line ni kwamba huko nyuma maneno yaliandikwa kwa usahihi, lakini yalitamkwa isivyo! Sasa hivi mtu aongeavyo ndivyo aandikavyo utadhani shule hazipo tena.
 
Mara nyingi nisomapo makala ndefu za Kiswahili sikosi kukutana na angalau neno moja la Kiswahili linaloonekana kuwa jipya kwangu. At the same time, the same article may contain a few familiar words that do not appear to conform to the standard Swahili that I learned during my early school years. Mengi ya maneno yanayoathirika ni yale yenye herufi "h", "dh", "l" na "r" ndani yake.
Watu wanaandika, mfano,

aya wakimaanisha haya,
ivi wakimaanisha hivi,
ivyo wakimaanisha hivyo,
erufi wakimaanisha herufi,
uzuni wakimaanisha huzuni,
nazani wakimaanisha nadhani,
zuluma wakimaanisha dhuluma,
karenda wakimaanisha kalenda, n.k.

Sasa ninapoona vitu kama hivi, ninapata kigugumizi kuamini kwamba yale maneno yanayoonekana kama mapya kwangu kweli ni maneno mapya na sahihi ya Kiswahili.

What's going on? Sarufi ya Kiswahili siku hizi haifundishwi tena kwenye shule zetu au mimi nimeganda kwenye karne ya ishirini?
Upuuziaji au kutokuwa makini kumeshamiri siku hizi. Sijui upotofu uko wapi, mashuleni au mitaani.
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom