Steve Dii
JF-Expert Member
- Jun 25, 2007
- 6,402
- 1,254
Kwanza kabisa napenda nianze kwa kukiri kuwa Kiswahili bado ni lugha inayonipiga chenga pahala pengi. Hivyo kuna pahala pengi katika hoja yangu nitachanganya na lugha ya Kiingereza, pamoja na kwamba ningelipenda sana kuepuka. Lakini hilo lingewezekana tu kama ningelikuwa na muda na uwezo wa kupangilia na kukumbuka maneno fasaha ya kutumia.
Pia nakili kuwa hii hoja sijaifanyia utafiti madhubuti kuhakikisha kuwa ina vielelezo vya kutosha ili kuchanganua na kufafanua mifano mbalimbali ambayo inaweza kutumika kuikoleza na kuipa msingi zaidi hoja yenyewe. Ni imani yangu kuwa wale walio bobea kwenye maswala ya lugha wanaweza kuiendeleza zaidi. Shukrani.
------------------ ***** --------------
Nitaanza;
Nikisema 'ngoko' au 'nkoko' Wasukuma, Wahaya na ninaamini makabila mengine mengi ya Tanzania wataelewa kuwa ninalotaka kulitaja ni jina la ndege tumjuaye kama 'kuku' kwa Kiswahili. Si makabila ya Tanzania tu, bali Wabemba wa Zambia, Washona wa Zimbabwe, Baganda wa Uganda nao wangelielewa.
Nikisema 'nzoka' au 'nyoka' vivyo hivyo makabila mengi yenye asili ya Kibantu yatanielewa.
Sawa, lugha nyingi zinakua na kuendelea kwa kuazima maneno kutoka kwenye lugha nyingine. Na maneno mengine yanajitokeza na kukua na kukubalika kama moja ya maneno ya lugha fulani kutokana na mazingira yanayozungukuka jamii.
Maneno kama 'swahiba', 'mstakabali', na mengine mengi yenye kusikika na kutamkwa kwa lafudhi ya pwani asili yake kubwa ni kutoka Kiarabu. Na ukweli wa mambo ni kwamba chimbuko la lugha ya Kiswahili ni lugha ya Kiarabu.
Hoja yangu: Je, chimbuko la lugha yetu ambayo tumerithi, tumejifunza, tumeikuza na kuienzi ndiyo kipimo pekee cha uhalisia wa maneno tuyatumiayo katika Kiswahili chetu?
Kimfano, nasema hivi kwani leo hii nikija na neno fulani hivi kutoka katika lugha ya Kihaya na neno hilo hilo kuwa tafsiri ya kitu ambacho kinapatikana Uhayani lakini hakipatikani katika Pwani, lakini hapo hapo kitu hicho kikabahatika kuwa na tafsiri yake katika lugha ya Kiarabu; uwezekano wa neno la Kiswahili kutumia (au hata kunyambulisha tu hilo neno la Kihaya ili iwe tafsiri yake katika Kiswahili) neno la Kihaya ni mdogo kuliko ambavyo urithi au ukubalianaji wa tafsri ya neno hilo ungelikuwa ule wa kutoka kwenye neno la Kiarabu.
Sasa, hii (sijui niite dosari) favouritism ya Uarabu dhidi ya Ubantu inatokana na nini, is it the case for inferiority complex ya aina fulani hivi, elimu au nini haswa?! Kwanini tunaenzi sana maneno kutoka Kiarabu kuliko maneno ambayo yana maana ileile kutoka lugha zetu za Kibantu. Seriously, I think there is an over-arabization of Kiswahili from its conception to this day.
"Akhsanteni", "Shukrani", natanguliza "Fadhila" zangu, au basi niseme... "ndaga fijo", "mwabeja"?!
SteveD.
MICHANGO ILIYOTOLEWA NA WADAU:
Pia nakili kuwa hii hoja sijaifanyia utafiti madhubuti kuhakikisha kuwa ina vielelezo vya kutosha ili kuchanganua na kufafanua mifano mbalimbali ambayo inaweza kutumika kuikoleza na kuipa msingi zaidi hoja yenyewe. Ni imani yangu kuwa wale walio bobea kwenye maswala ya lugha wanaweza kuiendeleza zaidi. Shukrani.
------------------ ***** --------------
Nitaanza;
Nikisema 'ngoko' au 'nkoko' Wasukuma, Wahaya na ninaamini makabila mengine mengi ya Tanzania wataelewa kuwa ninalotaka kulitaja ni jina la ndege tumjuaye kama 'kuku' kwa Kiswahili. Si makabila ya Tanzania tu, bali Wabemba wa Zambia, Washona wa Zimbabwe, Baganda wa Uganda nao wangelielewa.
Nikisema 'nzoka' au 'nyoka' vivyo hivyo makabila mengi yenye asili ya Kibantu yatanielewa.
Sawa, lugha nyingi zinakua na kuendelea kwa kuazima maneno kutoka kwenye lugha nyingine. Na maneno mengine yanajitokeza na kukua na kukubalika kama moja ya maneno ya lugha fulani kutokana na mazingira yanayozungukuka jamii.
Maneno kama 'swahiba', 'mstakabali', na mengine mengi yenye kusikika na kutamkwa kwa lafudhi ya pwani asili yake kubwa ni kutoka Kiarabu. Na ukweli wa mambo ni kwamba chimbuko la lugha ya Kiswahili ni lugha ya Kiarabu.
Hoja yangu: Je, chimbuko la lugha yetu ambayo tumerithi, tumejifunza, tumeikuza na kuienzi ndiyo kipimo pekee cha uhalisia wa maneno tuyatumiayo katika Kiswahili chetu?
Kimfano, nasema hivi kwani leo hii nikija na neno fulani hivi kutoka katika lugha ya Kihaya na neno hilo hilo kuwa tafsiri ya kitu ambacho kinapatikana Uhayani lakini hakipatikani katika Pwani, lakini hapo hapo kitu hicho kikabahatika kuwa na tafsiri yake katika lugha ya Kiarabu; uwezekano wa neno la Kiswahili kutumia (au hata kunyambulisha tu hilo neno la Kihaya ili iwe tafsiri yake katika Kiswahili) neno la Kihaya ni mdogo kuliko ambavyo urithi au ukubalianaji wa tafsri ya neno hilo ungelikuwa ule wa kutoka kwenye neno la Kiarabu.
Sasa, hii (sijui niite dosari) favouritism ya Uarabu dhidi ya Ubantu inatokana na nini, is it the case for inferiority complex ya aina fulani hivi, elimu au nini haswa?! Kwanini tunaenzi sana maneno kutoka Kiarabu kuliko maneno ambayo yana maana ileile kutoka lugha zetu za Kibantu. Seriously, I think there is an over-arabization of Kiswahili from its conception to this day.
"Akhsanteni", "Shukrani", natanguliza "Fadhila" zangu, au basi niseme... "ndaga fijo", "mwabeja"?!
SteveD.
MICHANGO ILIYOTOLEWA NA WADAU:
===Historia imepinsishwa. Kamwe kiswahili si KIARABU hata siku moja ndio maana leo ukimchukua muarabu kutoka uarabuni hawezi kuongea kiswahili vivyo hivyo sisi waswahili hatuwezi kuongea kiarabu
Waarabu walikuja wakakuta tayari watu wa pwani wana kiswahili chao ila wao walilazimisha baadhi ya maneno ya kiarabu yawe sehemu ya mawasiliano na kupitia kwa baadhi ya majinga ya wakati huo ambayo yalikuwa karibu na majamaa hayo yakaona ni ufahari sana wao kutamka maneno ya kiarabu ndivyo hivyo walivyochafua Lugha yetu hadi leo.
Hiyo ni historia basi kama kuna baadhi ya mameno ambayo yalifanikiwa kupenya na kuwa sehemu ya Lugha sii mbaya kwa sababu nyakati hizo zilikuwa nyakati za giza na lugha yetu ilikuwa bado inakuwa.
Kinachonikereketa roho sasa hivi ni nyakati za mwanga, watu wamesoma, kuna maneno mengi ya kibantu lakini kuna baadhi ya watu wanaona fahari sana kuchanganya maneno ya Lugha ya kiarabu na kiingereza kwenye lugha yetu kwa makusudi ili yaonekane ama yamesoma dini saana ama yamesoma elimu nyingine kuliko watu wengine.
Nimeshangaa majuzi kuna neno ambalo linatumika wakati wa kurusha matangazo ya moja kwa moja maarufu kama LIVE siju ni mtu gani kaenda kwenye kamusi ya kiarabu na kutuletea neno MUBASHARA. Kwanza neno lenyewe ni lirefu sana na limeshindwa kuendana na neno LIVE na je kwa sasa tunashindwa kupata neno mbadala wa LIVE mpaka tukakope UARABUNI? Yaani kwenye makabila yote ya Afrika tumekosa hadi tuvuke mabara kwa hao jamaa?
===Steve Dii,
Wewe ungalijua kwamba Kiarabu ndiyo mama wa Lugha zote DUNIANI wala usingekuja na hiyo hoja.
Lugha ya kiswahili ni Mkusanyiko wa lugha kuu mbili Kibantu na kiarabu, kibantu ni 65- 70%, Kiarabu ni 20-25%, lugha zingine kama kiingereza, kireno, kihindi, kijerumani ni 3-5%-- kama 65-70% ni kibantu, je, haitoshi tu hadi tuendelee kuingiza maneno mengine ya kibantu (kihaya, kisukuma, kiha nk)??!!--- juu ya yote hiyo inawezekana kujenga ukabila na uhasama wa makabila kwani kila kabila labda linaweza kutaka maneno yake yaingizwe katika matumizi ya kiswahili (standardized into kiswahili).
Juu ya yote Hakuna hata lugha moja ya kibantu ni ya kimataifa kinyume na kiarabu ambayo ni miongoni mwa lugha kuu 5 za kimataifa hivyo kuingiza maneno ya kiarabu katika kiswahili ni njia moja ya kukifanya kiswahili kiwe chepesi kueleweka kimataifa na kufundishika na kupata kasi ya kimataifa kama kiarabu.
Kule comoro kuna lugha moja inazungumzwa na wenyeji wa huko karibu asilimia 40 ni maneno ya kiswahili,Wataalamu wa kiswahili wanasema hiyo lugha ni kipande/ mtoto wa kiswahili.
Kwa kweli kiasili Kiswahili ni lugha ya kichotara lakini hii si aibu. Lugha za kichotara zinastawi vizuri kwa sababu ni rahisi zaidi kupokea maneno mapya. Mfano mkuu ni Kiingereza ambacho ni mchanganyiko wa Kigermanik na Kifaransa cha kale; muundo wake unafanana na Kiswahili kwa sababu kuna msingi upande moja (Kiing.: Kigermanik; Kiswahili: Kibantu) na msingu huu ni sarufi pamoja na kiasi kikubwa cha msamiati halafu lugha ya pili iliyoingiza maneno mengi.
Kiingereza kiliweza kupokea kirahisi maneno mengi kutoka kote na kuimarika hivyo. Maneno ya Kisayansi ambayo tunajifunza kama "Kiingereza" si Kiingerza kiasili bado Kilatini au Kigiriki hasa ila tu Waingereza hawapigani nayo wanayapokea tu. Hapo ndipo pia nguvu moja ya Kiswahili ninavyoona na asili yake ya kichotara inasaidia sana. Kwa zaidi angalia hapa.