Hayati Bibi Titi Mohamed alipojiunga na TANU alimshauri Hayati Nyerere alifunze Kiswahili, binafsi nimekuwa nikijiuliza na kuduwaa kwa hili, maana Wakoloni kuanzia Wajeremani walijifunza na kufundisha Kiswahili .
JF ni jamvi la kuuliza na kupata habari, kwa hiyo naomba kuuliza, kiwango cha ufahamu wa lugha ya Kiswahili kwa mtu aliyekuwa na kiwango cha kisomo cha Hayati Mwalimu Nyerere au Kiswahili alichokitaja Hayati Bibi Titi ni kitu kingine tofauti kabisa? Naamini kuna watu wengi sana Tanzania waliomfahamu Mwalimu kama mwalimu wakati akiwa TBR na Pugu, hivi, Kiswahili chake kilikuwa hoi kiasi hicho.Nitashukuru kusikia zile hotuba za awali za Mwalimu wakati wa TAA na TANU kabla ya tamko la Bibi Titi.
JF ni jamvi la kuuliza na kupata habari, kwa hiyo naomba kuuliza, kiwango cha ufahamu wa lugha ya Kiswahili kwa mtu aliyekuwa na kiwango cha kisomo cha Hayati Mwalimu Nyerere au Kiswahili alichokitaja Hayati Bibi Titi ni kitu kingine tofauti kabisa? Naamini kuna watu wengi sana Tanzania waliomfahamu Mwalimu kama mwalimu wakati akiwa TBR na Pugu, hivi, Kiswahili chake kilikuwa hoi kiasi hicho.Nitashukuru kusikia zile hotuba za awali za Mwalimu wakati wa TAA na TANU kabla ya tamko la Bibi Titi.