Kiswahili cha Tanga [kimtangata] na lahaja za kimwambao

Abunwasi

JF-Expert Member
Jun 25, 2009
5,486
3,468
TANGA KWETU
Ni ukweli usiopingika kuwa wazungumzaji wazuri wa lugha ya kiswahili ni watu wa pwani, jambo hili limechangiwa na sababu kadha wa kadha lakini kubwa ni sababu za kihistoria na maingiliano ya watu wa pwani na jamii za kale za waarabu waliofika na kufanya makazi katika ukanda huu miaka mingi iliopita, maingiliano hayo ndio chanzo cha kuzawa lugha hii ya kiswahili.

Neno swahili linatokana na neno la kiarabu ساحل "saahil" lenye maana ya Pwani au mwambao au ufukwe, hivyo waswahili "سواحليون"(sawahiliyun) nii wakaazi wa wa ukanda wa pwani. Kama ilivyo katika lugha nyingine mzungumzaji mmoja anaweza kutafautiana na mwingine, mtindo huu wa kuzungumza wenye utafauti hujumuisha matumizi ya maneno tafauti na matamshi tafauti (lafudhi), utafauti huu baina ya wazungumzaji wa lugha moja huitwa " lahaja" na lugha moja huweza kuwa na lahaja mbalimbali.

Mji wa tanga na mwambao wake ni katika wazungumzaji wazuri wa kiswahili kinachovutia kukiskiza. Lahaja hizi za kiswahili cha mji wa tanga huitwa kimtang'ata (kiswahili cha Tanga) na kimrima (kiswahili cha mwambao wa Tanga).
sifa kubwa ya lahaja hizi ni uzungumzaji wake wa kasi ya wastani usio wa haraka kama lahaja ya kipemba, na usio wa taratibu sana kama lahaja ya kiamu (kiswahili cha Lamu). Lakini pia wazungumzaji wake hupenda sana kufupisha vitenzi wakati wa kuvitamka, Kama kusema naja badala ya ninakuja, napika, nachoka, naenda.

Mfano wa utumiaji wa maneno yanayoweza kumtambulisha haraka mswahili wa Tanga ni kama odo" mama mdogo"
ngogwe "nyanya chungu" uono. Kimrima nacho ni lahaja ya kiswahili cha mwambao wa Tanga. Kiswahili hiki khaswa huzungumzwa maeneo ya digo kama vile Moa, Vanga, Pangani, Mwarongo, Tongoni, Kwale, Vyeru, Monga na Kichalikani, baadhi hukiita kiswahili cha kidigo kutokana na wazungumzaji wake kuzungumza kwa madaha ya kidigo.
lahaja nyengine za kiswahili za mwambao ni kama kiamu, Kisiu, kipate kingozi, kibajuni, Kibarawa na kimvita, kiunguja na kipemba.

Baraza ya kiswahili la tanzania limechagua lahaja ya kiunguja kuwa ndio lahaja ya kiswahili sanifu(fasaha).
Image may contain: sky, cloud, ocean, outdoor and water
Image may contain: sky, ocean, tree, cloud, outdoor, nature and water
Image may contain: one or more people, ocean, sky, outdoor, nature and water
 
Abunwasi,

Wale wa kwenye R wanaweka L au L wanaweka R waje tuwaone!

Halafu wanajitia wanajua Kiswahili kwelikweli!

Bongo tuna safari ndefu sana,

hadi Kiswahili tunachotegemea tuwe wakali ndio kwanza tunakiharibu!
 
Kiswahili cha tanga, kiswahili cha mombasa.. Haswa haswa mombasa, wanawake wao nikiwasikia huwa wananivuruga kweli.

Kipindi nipo chuo dit pale ilikuwa daily usiku lazima niende kula msosi kariakoo kuna mtaa mmama alikuwa anauza msosi so wale watu wanaotoka kenya hasa mombasa wakishuka na gari zao hula pale.. Ilikuwa nikienda pale kuwasikiliza tu wanavyongea..
 
Hata kingereza kinatamkwa tofauti kulingana na utamaduni wa watu
Wale wa kwenye R wanaweka L au L wanaweka R waje tuwaone!

Halafu wanajitia wanajua Kiswahili kwelikweli!

Bongo tuna safari ndefu sana,

hadi Kiswahili tunachotegemea tuwe wakali ndio kwanza tunakiharibu!
 
Kiswahili cha tanga, kiswahili cha mombasa.. Haswa haswa mombasa, wanawake wao nikiwasikia huwa wananivuruga kweli.

Kipindi nipo chuo dit pale ilikuwa daily usiku lazima niende kula msosi kariakoo kuna mtaa mmama alikuwa anauza msosi so wale watu wanaotoka kenya hasa mombasa wakishuka na gari zao hula pale.. Ilikuwa nikienda pale kuwasikiliza tu wanavyongea..
Kiswahili kitumikacho Mombasa ni Kimvita
 
Wale wa kwenye R wanaweka L au L wanaweka R waje tuwaone!

Halafu wanajitia wanajua Kiswahili kwelikweli!

Bongo tuna safari ndefu sana,

hadi Kiswahili tunachotegemea tuwe wakali ndio kwanza tunakiharibu!
Unayosema ni kweli kabisa. Siku hizi waongeao kiswahili sanifu ni wanyarwanda,wakenya ambao wamejifunza kiswahili darasani Kwani hata unguja hivi sasa utakuta wapo wanaochanganya R and L.
 
Abunwasi,
Makala nzuri ila marekebisho kidogo maalim wangu, Kiswahili kilisanifiwa mnamo miaka ya 1930, na kiunguja mjini ikateuliwa na kufanywa kuwa lahaja rasmi ya Kiswahili. Waliokiteuwa hawakuwa Baraza la Kiswahili la Tanzania Bali ni enzi Za ukoloni.
 
Ahsante kwa kunijuza mkuu.

Kina tofauti gani na kiswahili cha tanga, unguja, pemba na huku kwetu bara.!?
Kwenye visiwa hivi viwili , kuna lahaja nyingi kiasi ukiachilia udogo sale, Pemba, kijulikanacho kama kipemba ila pia kuna kikojani (Kijani ni kisiwa kidogo huko Pemba). Unguja , kitumbatu (na lahaja zote Za kaskazini ya kisiwa husika, kimji - Kiswahili tunachosomeshwa na kutumika rasmi kwenye shughuli za kiserikali, na kimakunduchi (na lahaja zote Za kusini ya Unguja).
Kipemba hufanana kiasi fulani na lahaja ya kitanga (hutumia WA badala ya U....)
 
Makala nzuri ila marekebisho kidogo maalim wangu, Kiswahili kilisanifiwa mnamo miaka ya 1930, na kiunguja mjini ikateuliwa na kufanywa kuwa lahaja rasmi ya Kiswahili. Waliokiteuwa hawakuwa Baraza la Kiswahili la Tanzania Bali ni enzi Za ukoloni.
Ulichosema ni kweli kabisa kuwa wakoloni walivyokuja kutawala afrika ya mashariki walikuta kiswahili kimesambaa ukanda wote wa pwani ya afrika mashariki kuanzia visiwa vya pate huko kaskazini hadi sofala na comoro kusini.
Lugha hii haikuwa ikitumika bara kwani huko lugha za kikabila zilikuwa zinatumika kwenye maeneo yote mengine.
Walivyokuja wakoloni wakakuta lahaja zifuatazo mwambao :-
1. Kipate -Pate
2 Kisiu [Kisyu] Somalia
3 Kimbalanzi-Somalia
4. Kitikuu-Pate
5. Kiamu-Lamu
6. Kingozi- Pwani ya Lamu
7. Kibajuni- Pate
8. Kimvita-Mombasa [Enzi hizo kabla ya mkoloni ilikuwa lugha maarufu hasa kwa wasomi]
9. Kijomvu-Mombasa
10. Kivumba- [Kivanga]Tanga
11. Kipemba-Pemba
11. Kimtangata-Tanga
12. Kivumba-Tanga
13. Kihadimu- Unguja kusini
14. Kiunguja - Unguja mjini
15..Kihadimu[kimakunduchi [kusini unguja]
16. Kimrima [pangani,dar esalaam hadi Rufiji na Mafia
17. Kimgao-Kilwa
18. Kimafia
19 Kingazija- Comoro nako kulikuwa na lahaja za shikomor, shimaore na shinzuani]

Hizi lahaja zilikuwa ni nyingi mno [kuna nyingine nimeziacha] na mkoloni alitaka kutumia lahaja rahisi na inayoeleweka kiurahisi kwa ajili ya matumizi kwa polisi pamoja na wafanyakazi wa serikali hizo na ndiyo hapo ilipoonekana kuwa lahaja rahisi kueleweka ilikuwa kiunguja.

Ieleweke vile vile kuwa baada ya uhuru, lugha rasmi kwa Afrika ya Mashariki ilikuwa ni kingereza na Tanzania ambayo ilikuwa ni nchi ya kwanza kujitawala iliamuwa kutumia kiswahili [lahaja ya kiunguja] kama lugha rasmi kwa shughuli zote Tanganyika na baadaye Jamhuri ya Muungano.


·

·
 
Unayosema ni kweli kabisa. Siku hizi waongeao kiswahili sanifu ni wanyarwanda,wakenya ambao wamejifunza kiswahili darasani Kwani hata unguja hivi sasa utakuta wapo wanaochanganya R and L.
Walisha hao...

Kama wenzao watanga...itawajua wakiongea kwanza kabla ya mengine!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom