Kiswahili cha BBC

MJIMPYA

JF-Expert Member
Mar 27, 2011
506
271
Wakuu
Nisaidie hiki kiswahili cha BBC


Umoja wa Mataifa umeziomba pande zote katika vita vya Libya,
kuzuwia vitendo vya kulipiza kisasi.


Taarifa hiyo imetolewa baada ya kuarifiwa kuwa wanajeshi wa Kanali Gaddafi wameuwa watu, na kwamba Waafrika waliokuwa wakipigana kwa niaba ya serikali piya wameshambuliwa.

Huku kukiwa na ripoti kuwa Waafrika waliokuwa katika jeshi la Kanali Gaddafi wanauwawa, wengi wao wamekuwa wakivuka mpaka na kuingia Mali na Niger.

Inaarifiwa magari 60 yameingia Niger kutoka Libya, lakini yalizuwiliwa mjini Agadez.

Watu hao wengi ni wapiganaji wa zamani wa kabila la Tuareg, ambao walipatana na serikali ya Niger mwaka 2009.
Inaarifiwa kuwa magari 10 nayo yameingia Mali.
Mapema mwaka huu, wakuu wa Mali waliiambia BBC, kwamba Wa-Tuareg wakilipwa dola elfu 10 kujiunga na serikali ya Libya, na kila siku ya mapigano wakipata dola 1000.
Duru za mataifa ya magharibi zinasema Waafrika kama elfu 10 waliajiriwa na Gaddafi.
Sasa ndege za Nato zinarusha vikaratasi na kutoa matangazo, kuwasihi Waafrika waasi na watapokelewa kufwatana na sheria.
 
Kipo sawa tu kaka, tatizo lipo wapi?
Rahaja za Kiswahili zipo nyingi ndugu, na zote zinatambuliwa kuwa ni Kiswahili:

Mfano:
Kibajuni
Kiamu
Kifundi
Kimatondoni
Kimgao
Kimrima: spoken around Pangani, Vanga, Dar es Salaam, Rufiji and Mafia Island.
Kimvita
Kimwini
Kipate
Kipemba
Kishamba
Kisiu
Kiunguja: spoken in Zanzibar City and environs on Unguja (Zanzibar) Island. Other dialects occupy the bulk of the island.
Chichifundi
Chijomvu
Chimwiini
Kimrima
Kimvita
Kimwani
Kingare
Kitikuu
Kitumbatu
Kivumba

Remember, Modern standard Swahili is based on Kiunguja

Mfano mwingine soma ili shairi, ni Kiswahili cha Kibajuni:

NALILIA UBAJUNI

Nalilia ubajuni, ilahi achusitiri
kivakumbuka moyoni, dua dhangu hukithiri
Mungu atachuawini, achupe kula la kheri
hali dhechu masikini, dhiko kachika hatari

Kidhikumbuka dhamani, dhangu imi kunyukiya
chwaliko chuna samani, vabajuni nakwambiya
chuki-ishi mahondeni, kwa dhakula na afiya
siku hidhi masikini, mangi amechupoteya
 
standard kiswahili ni cha unguja & kikifuatiwa na mombasa na cha tanga ukiwatoa " wasambaa "
 
Kipo sawa tu kaka, tatizo lipo wapi?
Rahaja za Kiswahili zipo nyingi ndugu, na zote zinatambuliwa kuwa ni Kiswahili:

Lahaja?
Ila kiswahili sasa hivi kweli shaghalabhaghala tu. The worse it is, the better it sounds.
 
Mi nachekaga wanaposema KOROKORONI
Kwa nini wasiseme ´rumande´
Kuna misemo yao mingine ni vere vere strange kama Wadukuzi,
 
Lahaja?
Ila kiswahili sasa hivi kweli shaghalabhaghala tu. The worse it is, the better it sounds.


Kiswahili
kimepatikana kwa namna au lahaja mbalimbali. Wakati wa ukoloni wa Uingereza azimio lilitolewa kutumia Kiswahili cha Unguja kuwa Kiswahili rasmi katikaTanganyika, Kenya na Zanzibar. Waingereza walikitumia pia kama lugha ya polisi najeshi katika Uganda.Kati ya lahaja za Kiswahili ni zifuatazo:
 
Back
Top Bottom