Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,562
- 217,871
Taarifa kutoka Mahakama ya Hakimu Mkaazi Kisutu inasema kwamba Kada wa Chadema, Mkulima wa bamia, mfanyabiashara na Mtunzi mahiri wa vitabu vya ujasusi, Yerricko Nyerere ambaye ni mkazi wa Kigamboni, leo amehukumiwa kifungo cha miaka mitatu Jela ama kulipa faini ya Shilingi milioni 5 za Kitanzania kwa kosa la uchochezi.
Mungu mbariki Yerricko, Mungu ibariki Chadema.
====
Yericko Nyerere AHUKUMIWA KWENDA JELA.
Leo 23/03/2021mahakama ya hakimu mkazi kisutu, imemuhukumu, Yericko Nyerere kifungo cha miaka mitatu jela au faini ya shilingi milioni tano (Tsh.5,000,000/=) katika kesi ya Uchochezi No 188/2017 ambayo ilihusu maneno yake kufuatia maazimio ya Baraza Kuu Chadema 2017 kuhusu UKUTA, Katiba Mpya na Tume huru ya uchaguzi.
Muda huu Yericko Nyerere anapelekwa Gerezani Kama mfungwa.
======
UPDATES: 1630HRS
======
Yericko Nyerere ameachiwa huru baada ya kufanikiwa kupata Milioni 5 ya faini. Wanachadema wamefanikiwa kuchanga kiasi hicho cha hela ndani ya saa moja.
Yeriko alikabiliwa na kesi ya kuchapisha maneno yenye nia ya uchochezi kupitia mtandao wa kijamii wa Facebook iliyoko katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam.
Hayo yalibainishwa na Wakili wa Serikali, Clara Charwe, wakati akimsomea Yericko maelezo ya awali mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam, Respicius Mwijage.
Katika maelezo hayo, Yericko alikubali maelezo yake binafsi ambayo ni jina lake, yeye ni mfanyabiashara na kwamba alishtakiwa.
Yericko anadaiwa kuwa Mei 28, 2017 kwa nia ya kuwachochea Watanzania, alichapisha maneno kupitia mtandao wa kijamii wa Facebook yasemayo:
“Maazimio ya Baraza Kuu yalikuwa (1) Katiba Mpya (2) Tume Huru (3) Bunge (4) Haki ya Kikatiba ya kuishi (Ben Saanane) (5) Haki ya Kikatiba ya kukutana na kuzungumza (Mikutano ya Hadhara ya Kisiasa) Hayo ndio yatahubiriwa katika Operesheni Ukuta.
“Baraza Kuu limeridhia kwa kauli moja kwamba vita rasmi ya kulikomboa taifa imezinduliwa na kama wewe Mtanzania unaogopa kulitetea taifa hili, ni bora ukakaa kando, nenda huko CCM ambako michemsho na supu vipo kwa wingi… kufa kwetu ni ukombozi wa Tanzania…
“Yaani sasa tunarejesha siasa za jino kwa jino, uso kwa uso, mguu kwa mguu, weka mguu niweke ugoko… Ni mwisho kuishi kinyonge, ni mwisho kulalamika, ni mwisho watu wetu kutekwa au kuuawa, ni mwisho watu wetu kuzuiwa kufanya mikutano ya hadhara… Tunasema sasa ni single touch double manifestational.” Mwisho wa kunukuu.
Pia soma: DAR: Yericko Nyerere akamatwa akiwa nyumbani kwake. Wachukua simu na laptop
Mungu mbariki Yerricko, Mungu ibariki Chadema.
====
Yericko Nyerere AHUKUMIWA KWENDA JELA.
Leo 23/03/2021mahakama ya hakimu mkazi kisutu, imemuhukumu, Yericko Nyerere kifungo cha miaka mitatu jela au faini ya shilingi milioni tano (Tsh.5,000,000/=) katika kesi ya Uchochezi No 188/2017 ambayo ilihusu maneno yake kufuatia maazimio ya Baraza Kuu Chadema 2017 kuhusu UKUTA, Katiba Mpya na Tume huru ya uchaguzi.
Muda huu Yericko Nyerere anapelekwa Gerezani Kama mfungwa.
======
UPDATES: 1630HRS
======
Yericko Nyerere ameachiwa huru baada ya kufanikiwa kupata Milioni 5 ya faini. Wanachadema wamefanikiwa kuchanga kiasi hicho cha hela ndani ya saa moja.
Yeriko alikabiliwa na kesi ya kuchapisha maneno yenye nia ya uchochezi kupitia mtandao wa kijamii wa Facebook iliyoko katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam.
Hayo yalibainishwa na Wakili wa Serikali, Clara Charwe, wakati akimsomea Yericko maelezo ya awali mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam, Respicius Mwijage.
Katika maelezo hayo, Yericko alikubali maelezo yake binafsi ambayo ni jina lake, yeye ni mfanyabiashara na kwamba alishtakiwa.
Yericko anadaiwa kuwa Mei 28, 2017 kwa nia ya kuwachochea Watanzania, alichapisha maneno kupitia mtandao wa kijamii wa Facebook yasemayo:
“Maazimio ya Baraza Kuu yalikuwa (1) Katiba Mpya (2) Tume Huru (3) Bunge (4) Haki ya Kikatiba ya kuishi (Ben Saanane) (5) Haki ya Kikatiba ya kukutana na kuzungumza (Mikutano ya Hadhara ya Kisiasa) Hayo ndio yatahubiriwa katika Operesheni Ukuta.
“Baraza Kuu limeridhia kwa kauli moja kwamba vita rasmi ya kulikomboa taifa imezinduliwa na kama wewe Mtanzania unaogopa kulitetea taifa hili, ni bora ukakaa kando, nenda huko CCM ambako michemsho na supu vipo kwa wingi… kufa kwetu ni ukombozi wa Tanzania…
“Yaani sasa tunarejesha siasa za jino kwa jino, uso kwa uso, mguu kwa mguu, weka mguu niweke ugoko… Ni mwisho kuishi kinyonge, ni mwisho kulalamika, ni mwisho watu wetu kutekwa au kuuawa, ni mwisho watu wetu kuzuiwa kufanya mikutano ya hadhara… Tunasema sasa ni single touch double manifestational.” Mwisho wa kunukuu.
Pia soma: DAR: Yericko Nyerere akamatwa akiwa nyumbani kwake. Wachukua simu na laptop
Neno la Shukrani baada ya kunusurika kwenda Segerea!
SHUKRANI Jana ilikuwa siku ngumu sana kwangu baada ya kuhukumiwa na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu chini ya Hakimu Kasian Matembele kwenda jela miaka mitatu au kulipa faini ya pesa taslimu shilingi milioni tano katika kesi No 188/2017 kosa la kuchapisha maneno ya uchochezi mitandaoni, Lakini...
www.jamiiforums.com