Kisutu: Watanzania 100 walioondoka Nchini bila vibali warudishwa na kupandishwa kizimbani

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,797
11,959


WATANZANIA 100 wamepewa adhabu ya kutofanya kosa ndani ya miezi sita baada ya kupatikana na hatia ya kutenda kosa la kutoka ndani ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania na kwenda Afrika Kusini bila kufata utaratibu wa uhamiaji.

Raia hao ni Laurence Omary, Sultani Ditutu, Nassoro Lingumbulu, Abdul Masoud, Waziri Waziri, Dotto Abdallah na wenzao 94 ambao walipewa adhabu hiyo leo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu Thomas Simba.

Katika kesi hiyo, wakili wa serikali Godfrey Ngwijo, akisaidiana na Sitta Shija, wamedai kuwa, washitakiwa hao wanadaiwa kutenda kosa hilo Julai 3 mwaka 2020 katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Kambarage Nyerere Wilaya ya Ilala, Dar es Salaam.

Ilidaliwa kwamba, wakiwa raia wa Tanzania walibainika kutoka nje ya Tanzania katika tarehe zisizofahamika bila kufata utaratibu wa kiuhamiaji na kuelekea Afrika Kusini.
20200707_174239.jpg
 
KwaTanzania
Wamerudi Wakati Mzuri
Tupo Uchumi Wa Kati
Uchaguzi Mkuu
Watulie Tuijenge Nchi Ya Asali Na Maziwa Amani Tele
 
Hao wanatoroka nyumbani hawaujui ule usemi usemao rudi nyumbani kumenoga..😜

Halafu hapo kimasihara tu utakuta kuna mpelelezi ndani yao..!
Mi nawaitaga wambea,viherehere..😅
 
Sijaelewa Kwahiyo wamekamatwa Airport wakiwa wanarudi. Immigration South Africa hawakuwashika kwa kuoverstay Visa zao lakini wamekuja kushikwa bongo.

Yani unakamatwa kwenu wakati ulioverstay nchi ya watu. Sikuwaji jua Kuna hiyo Sheria
 
Sijaelewa Kwahiyo wamekamatwa Airport wakiwa wanarudi. Immigration South Africa hawakuwashika kwa kuoverstay Visa zao lakini wamekuja kushikwa bongo.

Yani unakamatwa kwenu wakati ulioverstay nchi ya watu. Sikuwaji jua Kuna hiyo Sheria
Maajabu ya inchi hii....mambo ya ajabu ajabu kabisa...hivi unamshikilia mtu katoroka wakati kaondoka na passport halali na umemgongea exit....kama amepitisha muda wa kuishi huko south Africa,, huku Tanzania inawahusu nn? au serikali ya Tanzania imelipia gharama shilingi ngapi kuwaleta vijana nyumbani? hii inchi hii?
 
Maajabu ya inchi hii....mambo ya ajabu ajabu kabisa...hivi unamshikilia mtu katoroka wakati kaondoka na passport halali na umemgongea exit....kama amepitisha muda wa kuishi huko south Africa,, huku Tanzania inawahusu nn? au serikali ya Tanzania imelipia gharama shilingi ngapi kuwaleta vijana nyumbani? hii inchi hii?
Hii nchi wajinga ndiyo wengi, pale immigration wamejaa wazee wabishi,upuuzi mwingi,wivu umewajaa
Unaomba pass unaulizwa maswali mengi yasiyo na msingi
 
Kuna wajinga humu JF wakiambiwa Diaspora wanajua ndio hawa. Utasikia hawa Diaspora hawana maana, warudi nyumbani waone wenzao tumenunua magari tukiwa hapa hapa Bongo. Wanataka uraia pacha wa nini, sio wazalendo!

1594141174323.png
 
Maajabu ya inchi hii....mambo ya ajabu ajabu kabisa...hivi unamshikilia mtu katoroka wakati kaondoka na passport halali na umemgongea exit....kama amepitisha muda wa kuishi huko south Africa,, huku Tanzania inawahusu nn? au serikali ya Tanzania imelipia gharama shilingi ngapi kuwaleta vijana nyumbani? hii inchi hii?
Usijifanye unajua kila kitu wewe karai , wangekuwa na hizo nyaraka unazozisema hakuna raia anaweza kufukuzwa Africa kusini ... Ukiona umerudishwa utakuwa ulienda kinyume na taratibu na lazima uhukumiwe.


Muwe mnauliza hata kwa majiran zenu kabla ya kutapika Jamii forum
 
Back
Top Bottom