figganigga
JF-Expert Member
- Oct 17, 2010
- 25,492
- 54,890
Mmiliki wa Blog ya 8020 Fashion, Shamim Mwasha na Mume wake, Abdul Nsebo maarufu Abdukandida wamefikishwa katika mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakikabiliwa na tuhuma ya kukutwa na dawa za kulevya aina ya heroin.
Picha kapiga Mohammed Ibrahim wa Michuzi TV
======
TUHUMA ZA KUKUTWA NA GRAMU 232.70 ZA HEROINE ZAWAFIKISHA KORTNI SHAMIM NA MUMEWE
Na Karama Kenyunko
MMILIKI wa Blog ya 8020 Fashion, Shamim Omary Mwasha (41) na mume wake, Abdul Nsembo(45) wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwa wakikabiliwa na tuhuma za kusafrisha dawa za kulevya aina ya Heroine Hydrochloride zenye uzito wa gramu 232.70.
Akisoma hati ya mashtaka leo Mei 13, 2019 Wakili wa Serikali, Costastine Kakula amedai mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Mfawidhi, Steven Mhina kuwa washtakiwa wametenda kosa hilo Mei 1,2019 wakiwa huko Mbezi beach, Wilaya ya Kinondoni, jijini Dar es Salaam.
Imedaiwa kuwa siku ya tukio washtakiwa hao walikutwa na gramu 232.70. za Dawa za kulevya kinyume na sheria ya uhujumu uchumi.
Hata hivyo, washtakiwa hawakuruhusiwa kujibu kitu chochote mahakamani hapo kwa kuwa mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu haina mamlaka ya kusikiliza kesi ya uhujumu uchumi mpaka Mahakama Kuu ama kwa kupata Kibali kutoka kwa DPP.
Kwa mujibu wa upande wa mashtaka upelelezi wa shauri hilo bado haujakamilika.
Wakili wa utetezi, Hajra Mungula ameuomba upande wa mashtaka kukamilisha upelelezi haraka ili hatua nyingine iweze kuendelea licha ya kwamba Leo ndiyo siku ya kwanza kwa kesi hiyo kusomwa Mahakama hapo.
Kesi imeahirishwa hadi Mei 27, 2019 kwa kutajwa na kuangalia kama upelelezi umekamilika au la.
Zaidi, soma:
Picha kapiga Mohammed Ibrahim wa Michuzi TV
======
TUHUMA ZA KUKUTWA NA GRAMU 232.70 ZA HEROINE ZAWAFIKISHA KORTNI SHAMIM NA MUMEWE
Na Karama Kenyunko
MMILIKI wa Blog ya 8020 Fashion, Shamim Omary Mwasha (41) na mume wake, Abdul Nsembo(45) wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwa wakikabiliwa na tuhuma za kusafrisha dawa za kulevya aina ya Heroine Hydrochloride zenye uzito wa gramu 232.70.
Akisoma hati ya mashtaka leo Mei 13, 2019 Wakili wa Serikali, Costastine Kakula amedai mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Mfawidhi, Steven Mhina kuwa washtakiwa wametenda kosa hilo Mei 1,2019 wakiwa huko Mbezi beach, Wilaya ya Kinondoni, jijini Dar es Salaam.
Imedaiwa kuwa siku ya tukio washtakiwa hao walikutwa na gramu 232.70. za Dawa za kulevya kinyume na sheria ya uhujumu uchumi.
Hata hivyo, washtakiwa hawakuruhusiwa kujibu kitu chochote mahakamani hapo kwa kuwa mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu haina mamlaka ya kusikiliza kesi ya uhujumu uchumi mpaka Mahakama Kuu ama kwa kupata Kibali kutoka kwa DPP.
Kwa mujibu wa upande wa mashtaka upelelezi wa shauri hilo bado haujakamilika.
Wakili wa utetezi, Hajra Mungula ameuomba upande wa mashtaka kukamilisha upelelezi haraka ili hatua nyingine iweze kuendelea licha ya kwamba Leo ndiyo siku ya kwanza kwa kesi hiyo kusomwa Mahakama hapo.
Kesi imeahirishwa hadi Mei 27, 2019 kwa kutajwa na kuangalia kama upelelezi umekamilika au la.
Zaidi, soma:
Shamim Mwasha, mumewe mbaroni Dar kwa tuhuma za kukutwa na dawa za kulevya
Mamlaka ya Kupambana na Kuzuia Dawa za Kulevya Tanzania (DCEA) imemkamata mfanyabiashara, Abdul Nsembo maarufu Abdukandida na mkewe, Shamim Mwasha kwa tuhuma ya kukutwa na dawa za kulevya aina ya heroin. Wanandoa hao wanadaiwa kukutwa na dawa hizo zenye uzito wa zaidi ya gramu 400 nyumbani kwao...
www.jamiiforums.com