Kisutu: Mahakama yatupilia mbali hoja za Meya wa Dar es Salaam kutaka asalie madarakani, yasema hoja za mwombaji hazina miguu ya kusimamia

Huyo akatafute kazi nyingine asilete ujuaji mwisho akalala mlupango na Mahakama imeshaitupilia mbali kesi yake!

Wee ni poyoyo tu unayeshabikia upumbavu huu wa ukiukwaji wa sheria na taratibu za Utawals bora!
Hivi huyu Mhe.Mwita angelikuwa ni wa CCM tungeshuhudia huu upumbaf unaoendelea hapa? Makosa yote ni maigizo tu ili kujustify huu uhuni!
Jiulize kwanini Tume ya uchunguzi wa tuhuma dhidi ya Mstahiki Meya Mwita imeundwa na RC Paul Makonda…!
 
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imesema haiwezi kuzuia Meya wa DSM,Isaya Mwita kuondolewa kwenye nafasi yake kwa sababu hakuna uthibitisho wa uwepo wa kikao cha kumuondoa madarakani wala hasara atakayoipata endapo akiondolewa.

Yasema mwombaji hajatoa sababu za msingi za kukidhi vigezo vitatu vya kwanini abaki kwenye nafasi hiyo.

Hakimu asema maombi yamekosa ushahidi kuwa kulikuwa na kikao kinachokusudia kumwondoa madarakani.

“Mahakama hii inatupilia mbali hoja za kutaka muombaji (Mwita) kubaki madarakani kwa sababu hoja za Wakili wa muombaji hazina miguu ya kusimamia kwa kushindwa kufata vigezo ikiwemo uwepo wa kikao cha kutaka kumtoa madarakani”- Hakimu Janeth Mtega.

Uamuzi wa Mahakama kusema haiwezi kuzuia Mwita kuondolewa kwenye Umeya unatokana na maombi yake ambayo aliyawasilisha Jan 6, 2020 ya kutaka kuzuia Kikao cha Baraza la Madiwani wasijadili ajenda ya kumng’oa, kesi ya msingi ya mchakato wa kumuondoa kukiuka Utaratibu imepangwa Jan 13.

Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es Salaam Isaya Mwita amesema kikao Cha Jana hakikua na uhalali wa kumuondoa madarakani hivyo jumatatu nitaripoti kazini kama kawaida.

"Nakusudia kuwashtaki wote waliohusika kufoji saini ya Diwani ambaye yupo nje ya nchi na mmoja wa washtakiwa Hawa atakuwa Kigogo mkubwa tu katika Jiji la Dar es Salaam" Isaya Mwita Meya wa Jiji la Dar es Salaam.

Leo asubuhi nimeripoti ofisini japo mkurugenzi ananipa gari sijui shida nini hivyo nimemuandikia Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam aniletee gari kwa haraka mno" Mstahiki Meya wa Jiji Isaya Mwita.


Pia soma
- Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Isaya Mwita Meya anyang’anywa gari, ofisi yafungwa. Adai kuwa yeye bado ni Meya halali
Huyu hakimu anafikiri kwa kutumia kile kitu cha kati. Huwezi kuwa na ubongo ukasema hakuna hasara atakayoipata! Tumuulize mbona kumpindua Rais ni kosa la jinai? Kwani akipinduliwa rais anapata hasara gani? Kile cha kati kinafikiri kweli!
 
Lakini pia mahakama ipo sahihi sana kusema,haiwezi kuzuia kikao cha kumuondoa kwa sababu hata akiondolewa hapati hasara yoyote!! Hapo ndo nimepapenda kweli..!! Kwani mwita anapata hasara gani akiondolewa kuwa MEYA!.?0
Uchu tu wa madaraka
Jana kapanda bajaji kawahi ofisi halafu kajipiga mapicha eti yupo ofisini
Kuna maana gani kukaa ofisini kazi haziji,na saini zote zimeshaondolewa benki
 
Nimesoma na kusikia kupitia vyombo vya habari kuwa akidi haikutimia wakati wa kumuondoa Mstahiki Meya wa Dar es Salaam. Kuna sheria taratibu za kumwondoa Mstahiki Meya yeyote lakini kama sheria, taratibu na kununi hazikufuatwa mimi naona waanze mchakato upya. Mstahiki Meya atakapoenda Mahakamani na akasikilizwa na sheria zikafuatwa basi Mstahiki Meya atawabwaga chini. Ninashauri sheria, taratibu na kanuni zifuatwe kumuondoa Mstahiki Meya madarakani.
 
Kama ni kweli basi Mkurugenzi ataonekana kituko kuongoza kikao cha maamuzi ambacho akidi haijafikia
 
Hakika inashangaza sana kuona Upigaji kura wa kutokuwa na imani na Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es salaam ukigubikwa na vurugu na kugushi jina na saini ya Diwani aliyopo nje ya nchi lakini Waziri mwenye dhamana na Tamisemi akiwa kimya.Ni vema suala hilo likatolewa ufafanuzi wa kina na Waziri ili kuondoa Sintofahamu iliyowakumba Wananchi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mahakama ilitoa kesi ya hawali ya meya kuwa na hofu kuondolewa.hapakuwepo na ushaidi ulionyesha kuwa meya walitaka kumuondoa.Yeye bado ni meya kwa kuwa hata hii waliyo kaa kikao cha kumuondoa kwa nguvu kimekiuka kanuni na sheria kwa kuwa hakukidhi idadi ya wajumbe ya 2/3
 
Mpango mkakati wa shetani bado unaendelea kutamalaki ktk nchi ya Mungu, tusali na kuomba sana kwani hakuna aliye salama.
 
Back
Top Bottom