Kisutu: Mahakama yatupilia mbali hoja za Meya wa Dar es Salaam kutaka asalie madarakani, yasema hoja za mwombaji hazina miguu ya kusimamia

Return Of Undertaker

JF-Expert Member
Jun 12, 2012
4,572
26,868
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imesema haiwezi kuzuia Meya wa DSM,Isaya Mwita kuondolewa kwenye nafasi yake kwa sababu hakuna uthibitisho wa uwepo wa kikao cha kumuondoa madarakani wala hasara atakayoipata endapo akiondolewa.

Yasema mwombaji hajatoa sababu za msingi za kukidhi vigezo vitatu vya kwanini abaki kwenye nafasi hiyo.

Hakimu asema maombi yamekosa ushahidi kuwa kulikuwa na kikao kinachokusudia kumwondoa madarakani.

“Mahakama hii inatupilia mbali hoja za kutaka muombaji (Mwita) kubaki madarakani kwa sababu hoja za Wakili wa muombaji hazina miguu ya kusimamia kwa kushindwa kufata vigezo ikiwemo uwepo wa kikao cha kutaka kumtoa madarakani”- Hakimu Janeth Mtega.

Uamuzi wa Mahakama kusema haiwezi kuzuia Mwita kuondolewa kwenye Umeya unatokana na maombi yake ambayo aliyawasilisha Jan 6, 2020 ya kutaka kuzuia Kikao cha Baraza la Madiwani wasijadili ajenda ya kumng’oa, kesi ya msingi ya mchakato wa kumuondoa kukiuka Utaratibu imepangwa Jan 13.

Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es Salaam Isaya Mwita amesema kikao Cha Jana hakikua na uhalali wa kumuondoa madarakani hivyo jumatatu nitaripoti kazini kama kawaida.

"Nakusudia kuwashtaki wote waliohusika kufoji saini ya Diwani ambaye yupo nje ya nchi na mmoja wa washtakiwa Hawa atakuwa Kigogo mkubwa tu katika Jiji la Dar es Salaam" Isaya Mwita Meya wa Jiji la Dar es Salaam.

Leo asubuhi nimeripoti ofisini japo mkurugenzi ananipa gari sijui shida nini hivyo nimemuandikia Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam aniletee gari kwa haraka mno" Mstahiki Meya wa Jiji Isaya Mwita.


Pia soma
- Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Isaya Mwita Meya anyang’anywa gari, ofisi yafungwa. Adai kuwa yeye bado ni Meya halali
 
Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Kisutu, Dar es salaam, Janeth Mtega amesema Mahakama hiyo imeyatupilia mbali maombi ya Meya wa jiji la Dar es salaam Isaya Mwita kwa kuwa Wakili wake hakufuata baadhi ya vigezo katika kufungua madai yake.

Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es Salaam Isaya Mwita amesema kikao Cha Jana akikua na uhalali wa kumuondoa madarakani hivyo jumatatu nitaripoti kazini kama kawaida.

"nakusudia kuwashtaki wote waliohusika kufoji saini ya Diwani ambaye yupo nje ya nchi na mmoja wa washtakiwa Hawa atakuwa Kigogo mkubwa tu katika Jiji la Dar es Salaam" Isaya Mwita Meya wa Jiji la Dar es Salaam.

Leo asubuhi nimeripoti ofisini japo mkurugenzi ananipa gari sijui shida nini hivyo nimemuandikia Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam aniletee gari kwa haraka mno" Mstahiki Meya wa Jiji Isaya Mwita.

Yasema mwombaji hajatoa sababu za msingi za kukidhi vigezo vitatu vya kwanini abaki kwenye nafasi hiyo.

Hakimu asema maombi yamekosa ushahidi kuwa kulikuwa na kikao kinachokusudia kumwondoa madarakani.
=======
Rejea
 
Wale wote wanaofanya hujuma kwa upinzani kwa makusudi tuweke rekodi zao siku hi nchi ikikombolewa watajibu unless wawe wametangulia mbele ya haki.
Vipi kuhusu wale wanaohujumu nchi kwa makusudi kwa kushirikiana na adui zetu. Haki yao ni nini??
 
ifikie kipindi kuwe na usawa jaman hata ule wa kinafki ukizungumzia hilo la matumizi mabaya ya pesa, hivi kati ya nanii na huyu nani ana matumizi mabaya ya pesa za umma? mimi siasa siijui vizuri na hata ile hamu ya kuijua sina kwa kweli ila itafika kipindi wa upinzani woote wakishakuwa dhaifu kabisa hawajiwezi watarudi tena huku JF kutafta masalia na wale wanaohoji vitu ambavyo kwa fikra zao ni kama havituhusu.
 
Kwa hili ingawa siungi mkono meya kuondolewa kihuni kwa sababu ya kutoolewana na Makonda..Lkn nadhani mahakama imemtendea haki,kwa sababu aliwahi mno kwenda kufungua kesi ya hisia ya kufukuzwa.

Meya hakuwa na sababu ya kufungua kesi ya mahakama kuzuia kikao cha kumuondoa,bora hata angeweka zuio la kikao chenyewe kwamba ni kikao batili ukizingatia yy ndo mwenyekiti wa vikao vyote.

Lakini pia mahakama ipo sahihi sana kusema,haiwezi kuzuia kikao cha kumuondoa kwa sababu hata akiondolewa hapati hasara yoyote!! Hapo ndo nimepapenda kweli..!! Kwani mwita anapata hasara gani akiondolewa kuwa MEYA!.?0

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kila mara Rais wa JMT amekuwa akisisitiza kuwa maendeleo hayana vyama.

Yaani ni ya kwetu wote watanzania uwe Cuf au Chadema. Sasa hili la kutaka mayor wa chama flan tu ndio awe kiongozi linatoka wapi! Na kama alipata ajari na gari alikuwa anaendesha yeye? Dereva kwa nini asichunguzwe kama ni mzembe. Alafu kama hakutumia hizo bil 5.1 kwani yeye alizuia zisitumike .Madiwani na baraza zima kwa nini hawakuhoji?

Mwisho kwani akiwa mayor wa chama kingine ndio ataleta maendeleo? Na kwa nini kumchomoa mtu kw figisu figisu. Hata umeya wenyewe aliupata kwa mbinde mpaka Rais wa JMT alipotoa neno.
 
Watu mnachangia bila uelewa. Mimi binafsi nimemuelewa hakimu.. Mwita jumatatu ripoti kazini
 
Back
Top Bottom