Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,558
- 217,854
Mungu ibariki Tanzania ukipenda mwenyewe .
Hivi mnategemea siku moja MNYETI atapandishwa kizimbani ?Mbona orodha ya waliopokea fedha za Rugamalila ni ndefu lakini waliopelekwa mahakamani ni wa kuokoteza?
Hiyo ndiyo tafsiri sahihiHayo ni mazingaombwe ya Taasisi ya Kutetea na Kukuza Rushwa nchini. Ukiwauliza wengine mbona hamjawagusa na huyu ana kesi ya kujibu mbona mmemuachia huru? watakujibu ni maagizo toka mamlaka za juu AKA Ikulu au watang'aa macho. Serikali ya majizi, mafisadi na pia yanayopenda rushwa ndivyo ilivyo Mkuu.
Hivi Ruttashobolwa wa JF naye ni Super Intelligent black man .............. Au yeye siyo Mhaya!!?The Hayas is a version of super intelligent black man! Wahaya ni Wazungu weusi! Ukizaliwa Mhaya alafu ukawa kilaza, ujue una mkosi!
Mnyarwanda huyo mhaya wapi!Hivi Ruttashobolwa wa JF naye ni Super Intelligent black man .............. Au yeye siyo Mhaya!!?
Awamu hii hawatashinda kesi hata moja tu ya Ufisadi ............................!!Sasa wamemuachia, ajaribu kuja Upinzani tutaona wanavyomvua nguo.
Nafkiri anamaanisha hivyo, ngoja aje mwenyeweKua mzalendo ni pamoja na kuwaonea watu hata kama hawana hatia?
Ruge na seth watamuita yule mkulu mstaafu Kama shahidi wao maana yeye alishasema fedha hizo syo za umma....hapo Mapema sana kesi kwishaaa....Awamu hii hawatashinda kesi hata moja tu ya Ufisadi ............................!!
Kesi za chuki au visasi huwezi shinda ............... Kinachoendela ni kuwakomoa tu kwa kuwalaza Ukonga.Ruge na seth watamuita yule mkulu mstaafu Kama shahidi wao maana yeye alishasema fedha hizo syo za umma....hapo Mapema sana kesi kwishaaa....
Kama ile kesi ya mahalu?
Ova
Tatizo ni wanasheria wa serikali, prosecutors, hawawezi wasilisha na kutetea hoja zao!Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imemuachia huru aliyekuwa Mkurugenzi wa Huduma za Sheria wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Rugonzibwa Mujunangoma aliyekuwa akikabiliwa na shtaka la kupokea rushwa ya Sh 323 milioni toka kwa James Rugemalira fedha ambazo ni sehemu ya zilizotoka kwenye Akaunti ya Tegeta Escrow.
Hakimu Mkazi Mwandamizi, Victoria Nongwa amemuachia huru Rugonzibwa leo Alhamisi baada ya Mwendesha Mashtaka Mwandamizi wa Takukuru, Leonard Swai kuomba kesi hiyo iondolewe mahakamani hapo chini ya kifungu cha 98 (a) cha Sheria ya Makosa ya Jinai (CPA) na Mahakama kuridhia.
Rugonzibwa alifikishwa na Takukuru mahakamani hapo kwa mara ya kwanza Januari 14, 2015 akikabiliwa na shtaka la kupokea rushwa ya Sh 323 milioni toka kwa Rugemalira fedha ambazo ni sehemu ya zile Akaunti ya Tegeta Esrow.
Hata hivyo baadaye alibadilishiwa hati ya Mashtaka na kusomewa upya ambayo hayakuonyesha tena kuwa fedha zilizopokelewa na Mujunangoma toka kwa Rugemalira ni sehemu ya fedha za Akaunti ya Tegeta Escrow.
Kupitia hati hiyo mpya, Rugonzibwa alikuwa akidaiwa kuwa Februari 5, 2014 akiwa mtumishi wa Serikali kama Mkurugenzi wa Huduma za Sheria wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, alipokea rushwa ya Sh Sh323 milioni kupitia akaunti yake namba 00120102602001 iliyopo kwenye Benki ya Mkombozi .
Alidaiwa kuwa alipokea kiasi hicho cha fedha kutoka kwa Rugemalira, ambaye ni mshauri huru wa kitaalamu, mkurugenzi wa VIP na mkurugenzi wa zamani wa Kampuni ya Kufua Umeme ya IPTL kama tuzo kwa kushughulikia mambo ya ufilisi wa muda wa kampuni hiyo.
Baada ya kusomewa mashtaka hayo, alikana na upelelezi wa kesi hiyo ulikuwa umekwisha kamilika.
CHANZO: Mwananchi