Kisutu: Kesi ya Erick Kabendera yaendelea. Jamhuri yaweka kisiki Erick kushiriki msiba wa mama yake mzazi

Hili kosa la kukwepa kodi ilikuwaje Makonda yeye hakushitakiwa pamoja na ushaidi wa wazi ulokuwapo kwenye ishu ya makontena
 
Kwani alizaliwa peke yake? Lini mshitakiwa aliwahi ruhusiwa kwenda kwenye mazishi? Au hii iwe special kwa huyu, mwandishi habari? Wakulima je? Wafugaji je?
Tusiishie kusikitika, tuepuke kujiingiza kwenye mambo ya kujitakia. Kulikuwa na kila njia ya kuachana na hayo lakini naona alijivunia ushujaa.
Nakuombea siku uko ndani gerezani, mama yako au baba yako wanafariki, na usiruhusiwe kwenda kuwaaga.

Sent using Unataka kujua ili iweje
 
Kwa nafasi yake raisi ana uwezo wa kila aina kuangalia afya ya mama yake mzazi.

Lakini wakati anaomboleza kifo cha dada yake (Monica) kitu kilichokuwa kinamsumbua nani ataziba pengo la Monica sio kwamba hana ndugu wengine. Isipokuwa Monica ndio mtoto ambae mama yao kamzoea na aliekuwa akimtegemea kwa mambo mengi ya kila siku including emotional support ata kama Magu ndio anagharamia.

Kwa ivyo huo uchungu raisi nae anaujua, usimfanyie mtu kitu ambacho wewe usingependa kufanyiwa.

Uwezi kumfunga mtoto wa mwenzako kwa kosa ambalo madhara yake ni makelele tu ambayo hayana impact zozote kwa serikari, kama adhabu sijui ipi itazidi hili kumsababishia kifo cha mama yake na kumzika pia wamnyime kuna watu wana roho mmbaya,
 
Kwani alizaliwa peke yake? Lini mshitakiwa aliwahi ruhusiwa kwenda kwenye mazishi? Au hii iwe special kwa huyu, mwandishi habari? Wakulima je? Wafugaji je?
Tusiishie kusikitika, tuepuke kujiingiza kwenye mambo ya kujitakia. Kulikuwa na kila njia ya kuachana na hayo lakini naona alijivunia ushujaa.
Umejibu vizuri,watanzania siku zote huwa wanalenga kupata huruma ni sawa na tabia za bati huwa linawahi kupata joto na kuwahi kupoa
 
Mkuu tetea uovu maana uko mezani kwa mfalme na sahani yako imejaa mlo wa kutosha, na namna nzuri ya huo mlo ili uweze kushuka utakavyo ni pamoja na kujenga hoja ya kuutetea huo uovu. Hata akina Mwigulu, Nape, Januari nk walikuwa wanatetea uovu enzi za JK wakiwa mezani kwenye mlo kama ww. Ila hiyo warmup inayowakuta hivi sasa akili imewarudia.
Hili linafanya watu wawe na chuki na viongoz wao

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa kila aliye,still kuwa mfungwa hakumzuii mtu kunyimwa haki za msingi

haki za msingi ndio zipi zinazolindwa ukiwa jela?

hata kuzaa ni haki ya msingi

Kabendera aachiwe akazae kisha arudi?

Huyu mwandishi kafanyiwa dhulma, na hayuko peke yake, lakini kuachiwa kwenda kuzika huwa hakuna anaepewa fursa hiyo

mimi natetea usawa hata kwenye kuonewa, tuonewe kwa usawa

unamuachia Kabendera kwani Rugemarila hajafiwa? Namtumia Rugemarila kama mfano wa prominent detainee, na sijui kama kafiwa lakini tunajuaje hajafiwa na mama, mke, mtoto, kaka, kipindi chote hiki ????

yani mahabusu woooote waliotiwa kizuizini awamu hii kwa kesi za dhulma hakuna aliyefiwa na mamaake?

hivi nyinyi hamna ndugu walioko humu majela ya Tanzania, hamuwaulizi? hamuwatembelei wakawaambia?
 
Kuna kitu sijaelewa ati mahakama yako haina mamlaka..... Sasa kwanini kesi iko hapo mahakamani??
Erick Kabendera mwandishi wa Kujitegemea wa Habari za uchunguzi inaendelea leo Mahakama ya Kisutu.

Kabendera anashtakiwa kwa Makosa matatu ikiwemo kukwepa Kodi, Utakatishaji Fedha na kujihusisha na genge la uhalifu.


UPDATES

MAHAKAMA YAOMBWA KABENDERA KUMUAGA MAMAKE


HOJA SITA ZA UPANDE WA UTETEZI KWANINI KABENDERA APEWE RUHUSA KUSHIRIKI MAZIKO YA MAMA YAKE

Jopo la mawakili wa Mwandishi wa habari wa kujitegemea Erick Kabendera, wakiongozwa na Wakili Jebra Kambole wamewasilisha hoja sita mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama ya Kisutu Janet Mtega kwa mshitakiwa kupatiwa ruhusa chini ya ulinzi ili aweze kushiriki Katika maziko au kutoa heshima za mwisho kwa mama yake aliyefariki hivi karibuni.

1. Kutoa heshima za mwisho ni haki ya msingi ya binadamu. Wakili ameeleza kuwa Kabendera ana haki ya kuwa na kuheshimu familia pamoja na haki ya faragha hivyo kuna umuhimu kwa Kabendera kushiriki Katika kutoa heshima za mwisho kwa mama yake.

2. Erick Kabendera anatakiwa adhaniwe kuwa hajatenda kosa mpaka pale mahakama itakapothibitisha kuwa ametenda kosa na kumzuia kushiriki mazishi itakuwa ni adhabu ya Kinyama kwa Kabendera.

3. Tangu Mshitakiwa amekamatwa hajaonesha nia ya kutoroka au kutaka kufanya vurugu hivyo hakuna uwezekano wa mtuhumiwa kutoroka Kama atapatiwa ruhusa

4. Mashitaka anayokabiliwa nayo mshitakiwa hayahusiani na uvunjifu wa amani hivyo Mahakama itilie maanani ombi Hilo

5. Kama Mahakama ilitoa amri aende mahabusu hivyo Mahakama Ina uwezo wa kuamua ombi hilo kwani kama mshitakiwa pia aliweza kupelekwa mahakamani haitashindikana kumpeleka kanisani kumuaga mama yake.

6. Ruhusa ya Kabendera kuhudhuria mazishi Jamhuri haiwezi kuathirika



MAJIBU YA UPANDE WA SERIKALI

Jamhuri yampa pole nyingi kwa msiba wa mama yake mzazi, Bibi Verdiana Mjwahuzi. Pia Jamhuri imepinga hoja za utetezi wakidai Mahakama haina Mamlaka wala DPP hajaipa mamlaka ya kutoa maamuzi hayo.

Wakili wa Serikali, Simon Wankyo amesema...

"Hata sisi tuna masikitiko makubwa na tunampa pole nyingi Kabendera kwa kufiwa na mama yake mzazi, lakini mahakama isifungwe mikono kwa maombi yaliyowasilishwa ya kutaka mshtakiwa kushiriki Msiba.”

Mheshimiwa Hakimu katika macho ya kisheria mahakama yako haina mamlaka ya kusikiliza maombi hayo kwa sababu kesi hii ni ya uhujumu uchumi, licha ya kuwa hata sisi tuna masikitiko makubwa lakini tunaiomba Mahakama yako isifungwe mikono.”



Pia soma

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom