Kisutu: Kesi ya Erick Kabendera yaendelea. Jamhuri yaweka kisiki Erick kushiriki msiba wa mama yake mzazi

Chachu Ombara

JF-Expert Member
Dec 11, 2012
5,897
10,358
Kisutu.PNG

Awali:


Erick Kabendera mwandishi wa Kujitegemea wa Habari za uchunguzi inaendelea leo Mahakama ya Kisutu.

Kabendera anashtakiwa kwa Makosa matatu ikiwemo kukwepa Kodi, Utakatishaji Fedha na kujihusisha na genge la uhalifu.

Kabendera.jpg

UPDATES

MAHAKAMA YAOMBWA KABENDERA KUMUAGA MAMAKE


HOJA SITA ZA UPANDE WA UTETEZI KWANINI KABENDERA APEWE RUHUSA KUSHIRIKI MAZIKO YA MAMA YAKE

Jopo la mawakili wa Mwandishi wa habari wa kujitegemea Erick Kabendera, wakiongozwa na Wakili Jebra Kambole wamewasilisha hoja sita mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama ya Kisutu Janet Mtega kwa mshitakiwa kupatiwa ruhusa chini ya ulinzi ili aweze kushiriki Katika maziko au kutoa heshima za mwisho kwa mama yake aliyefariki hivi karibuni.

1. Kutoa heshima za mwisho ni haki ya msingi ya binadamu. Wakili ameeleza kuwa Kabendera ana haki ya kuwa na kuheshimu familia pamoja na haki ya faragha hivyo kuna umuhimu kwa Kabendera kushiriki Katika kutoa heshima za mwisho kwa mama yake.

2. Erick Kabendera anatakiwa adhaniwe kuwa hajatenda kosa mpaka pale mahakama itakapothibitisha kuwa ametenda kosa na kumzuia kushiriki mazishi itakuwa ni adhabu ya Kinyama kwa Kabendera.

3. Tangu Mshitakiwa amekamatwa hajaonesha nia ya kutoroka au kutaka kufanya vurugu hivyo hakuna uwezekano wa mtuhumiwa kutoroka Kama atapatiwa ruhusa

4. Mashitaka anayokabiliwa nayo mshitakiwa hayahusiani na uvunjifu wa amani hivyo Mahakama itilie maanani ombi Hilo

5. Kama Mahakama ilitoa amri aende mahabusu hivyo Mahakama Ina uwezo wa kuamua ombi hilo kwani kama mshitakiwa pia aliweza kupelekwa mahakamani haitashindikana kumpeleka kanisani kumuaga mama yake.

6. Ruhusa ya Kabendera kuhudhuria mazishi Jamhuri haiwezi kuathirika



MAJIBU YA UPANDE WA SERIKALI

Jamhuri yampa pole nyingi kwa msiba wa mama yake mzazi, Bibi Verdiana Mjwahuzi. Pia Jamhuri imepinga hoja za utetezi wakidai Mahakama haina Mamlaka wala DPP hajaipa mamlaka ya kutoa maamuzi hayo.

Wakili wa Serikali, Simon Wankyo amesema...

"Hata sisi tuna masikitiko makubwa na tunampa pole nyingi Kabendera kwa kufiwa na mama yake mzazi, lakini mahakama isifungwe mikono kwa maombi yaliyowasilishwa ya kutaka mshtakiwa kushiriki Msiba.”

Mheshimiwa Hakimu katika macho ya kisheria mahakama yako haina mamlaka ya kusikiliza maombi hayo kwa sababu kesi hii ni ya uhujumu uchumi, licha ya kuwa hata sisi tuna masikitiko makubwa lakini tunaiomba Mahakama yako isifungwe mikono.”


Soma:
 
Kwani alizaliwa peke yake? Lini mshitakiwa aliwahi ruhusiwa kwenda kwenye mazishi? Au hii iwe special kwa huyu, mwandishi habari? Wakulima je? Wafugaji je?
Tusiishie kusikitika, tuepuke kujiingiza kwenye mambo ya kujitakia. Kulikuwa na kila njia ya kuachana na hayo lakini naona alijivunia ushujaa.
 
Jamhuri haina huruma na raia wake

Sent using Jamii Forums mobile app

Katika utawala huu wa Magufuli, Tanzania imekuwa ni Taifa la kidikteta lisilojali Utu,Haki,Usawa na Sheria kwa raia wake.
Anayotendewa Erick ni zaidi ya Unyama na Ukaburu ulokuwa unafanywa na Makaburu wa enzi za Utawala wa weupe wachache nchini Afrika Kusini.

Mtu kafiwa na mamake mzazi tena kuna uwezekano mkubwa kifo cha mama huyu kitakuwa kimechangiwa na Utawala huuhuu! Huu ni ukatili wa hali ya juu sana.

RIP Mama Mujahwuzi na pole sana Erick! Mungu ndiye atakayekulipia kwa watesi wako.
 
Kwani alizaliwa peke yake? Lini mshitakiwa aliwahi ruhusiwa kwenda kwenye mazishi? Au hii iwe special kwa huyu, mwandishi habari? Wakulima je? Wafugaji je?
Tusiishie kusikitika, tuepuke kujiingiza kwenye mambo ya kujitakia. Kulikuwa na kila njia ya kuachana na hayo lakini naona alijivunia ushujaa.

Mkuu tetea uovu maana uko mezani kwa mfalme na sahani yako imejaa mlo wa kutosha, na namna nzuri ya huo mlo ili uweze kushuka utakavyo ni pamoja na kujenga hoja ya kuutetea huo uovu. Hata akina Mwigulu, Nape, Januari nk walikuwa wanatetea uovu enzi za JK wakiwa mezani kwenye mlo kama ww. Ila hiyo warmup inayowakuta hivi sasa akili imewarudia.
 
Mkuu tetea uovu maana uko mezani kwa mfalme na sahani yako imejaa mlo wa kutosha, na namna nzuri ya huo mlo ili uweze kushuka utakavyo ni pamoja na kujenga hoja ya kuutetea huo uovu. Hata akina Mwigulu, Nape, Januari nk walikuwa wanatetea uovu enzi za JK wakiwa mezani kwenye mlo kama ww. Ila hiyo warmup inayowakuta hivi sasa akili imewarudia.
Mjibu vizuri alichosema, je kuna utaratibu wa kisheria kwa mfungwa au mahabusu wa kutolewa gerezani na kwenda kushiriki msiba au tukio lolote?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimewaza hivi, niko upande wa Erick na sipendi jinsi watu wanavyobambikiwa kesi ili kuwakomoa lakini anajua hasa nini alikuwa anakifanya, labda nia yake ilikuwa nzuri lakini alivyofanya haikuwa yenye kupendeza. Yeye mwenyewe anajua hatari iliyokuwa inaweza kumkabili na hata mtakumbuka siku aliyochukuliwa kwake, ukweli alikuwa anapotea ila alikuwa 'amejiandaa' ndio mpaka leo yupo.

Mnakumbuka vifo vya maafisa kama wa tatu Wizara ya mambo ya nje kitengo Misaada kutoka EU? Walikufa ndani muda mfupi sana?

Na mmeona jinsi wanachama wa EU na US kupitia balozi zao wanavyolifatilia kwa umakini hii suala la mashtaka dhidi ya Erick na hata kuonyesha Sympathy kwa msiba wa mama yake?

Nimewaza tu

huko baadae nadhani tutashtakiana sana
 
Kwani alizaliwa peke yake? Lini mshitakiwa aliwahi ruhusiwa kwenda kwenye mazishi? Au hii iwe special kwa huyu, mwandishi habari? Wakulima je? Wafugaji je?
Tusiishie kusikitika, tuepuke kujiingiza kwenye mambo ya kujitakia. Kulikuwa na kila njia ya kuachana na hayo lakini naona alijivunia ushujaa.

Unajuaje kama huwa hawaendi hao wakulima na wafugaji?
 
Umeshasema mshtakiwa kwa maana bado hajakutwa na hatia.
Vipi ikitokea akaachiwa huru kwa kukosekana ushahidi wa kumtia hatiani.
Usiwe unajitoa ufaham tu mwenzio amefiwa na bi mkubwa wake!
Kwani alizaliwa peke yake? Lini mshitakiwa aliwahi ruhusiwa kwenda kwenye mazishi? Au hii iwe special kwa huyu, mwandishi habari? Wakulima je? Wafugaji je?
Tusiishie kusikitika, tuepuke kujiingiza kwenye mambo ya kujitakia. Kulikuwa na kila njia ya kuachana na hayo lakini naona alijivunia ushujaa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwani alizaliwa peke yake? Lini mshitakiwa aliwahi ruhusiwa kwenda kwenye mazishi? Au hii iwe special kwa huyu, mwandishi habari? Wakulima je? Wafugaji je?
Tusiishie kusikitika, tuepuke kujiingiza kwenye mambo ya kujitakia. Kulikuwa na kila njia ya kuachana na hayo lakini naona alijivunia ushujaa.
Mtuhumiwa inaruhusiwa... Mfungwa inaruhusiwa. Endapo akiwa eneo ambalo linafikiwa kirahisi.

Ila hapa kwetu inaangaliwa usalama zaidi wa mtuhumiwa/mfungwa na maofisa waliosindikiza.

Kifupi inakuw haiwezekani, japo kwenye karatasi za mwongozo wa bwana jela, kuna hicho kipengele. Kwenye haki za wafungwa na watu waliokizuizini.

Nimewahi kuona mara mbili katika umri wangu, japo sijui kama mahakama ilihusika ili wao waage.
 
Kwani alizaliwa peke yake? Lini mshitakiwa aliwahi ruhusiwa kwenda kwenye mazishi? Au hii iwe special kwa huyu, mwandishi habari? Wakulima je? Wafugaji je?
Tusiishie kusikitika, tuepuke kujiingiza kwenye mambo ya kujitakia. Kulikuwa na kila njia ya kuachana na hayo lakini naona alijivunia ushujaa.

Mkuu tetea uovu maana uko mezani kwa mfalme na sahani yako imejaa mlo wa kutosha, na namna nzuri ya huo mlo ili uweze kushuka utakavyo ni pamoja na kujenga hoja ya kuutetea huo uovu. Hata akina Mwigulu, Nape, Januari nk walikuwa wanatetea uovu enzi za JK wakiwa mezani kwenye mlo kama ww. Ila hiyo warmup inayowakuta hivi sasa akili imewarudia.
Hivi huyu Patriot ndio yule aliyekuwa kiongozi wa vijana CDM then akaunga juhudi na kupewa UDISII?
 
Hatuombeani mabaya ila itatafsirika vipi mchana huu kila mwendesha mashtaka aliyepo hapo kabla ya kusimamia hiyo "Jamhuri" kila mmoja akapata ujumbe kwenye simu yake "mama yako na mkeo wameaga dunia kwa kugongwa na gari la mkaa"?
Wataendelea kusubiri SAA za kesi kutajwa tena?
Mnaweza kuona ni hadithi, lakini Mungu akitaka kutoa fundisho anatoa tuu. Kitabu cha Kutoka Mungu alimwadhibu Farao kwa watoto wazaliwa wa kwanza kufa nchi nzima usiku mmoja kwa sababu ya moyo mgumu wa mtu mmoja.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom