‪KISUTU, DAR: Mahakama yawapa dhamana Viongozi 6 wa CHADEMA bila kuwepo mahakamani. Kutoka gerezani Aprili 3, 2018...

hii sinema nimeipenda maana wamejua kitaa raia mori ipo juu zaidi ya povu la Kia kwenye glass wakajua wakisema dhamana ni mpk tare 3 lazima kuwake moto wakabidi wawape dhamana ila wadhaminiwa walie Pasaka ndani

Bora nusu Shari kuliko Shari nzima
 
Angalia wanaoondoka CHADEMA wanatoa picha gani? wanaobaki ndo hao ninaosema..... Data zako ni mgando, watu wanatoka na wanaendelea kutoka, wao wanaona ujinga uliopo huko. Umeweka data mgando, dunia ina move mbele, inaenda mbele hao wa 2015 si wote wamebaki huko, wengi wameondoka ...tumia akili kufikiri.

Rafiki bado nakusisitiza kujitazama kwenye kioo ujione kama uko sawa kifikra.....

Just see what you have said....

Sasa ndugu kama hiyo dunia ina "move mbele", si maana yake ni hiyo hiyo ambayo hao pamoja na wewe mnaikalia ? Au ni ya kwako tu wewe ndiyo inayo "move mbêle ?"

Kumbuka tu kuwa the movement of the people to join political parties is always irréversible...... they go out.... they come in !!

Sina hakika kama umenielewa hapa. Kama hujaelewa, nifuate.....
 
Mimi sijazaliwa uingereza wala sina uhusiano na familia ya malkia hicho kingereza nilichoandika nimejitahidi kinatosha kama hujaelewa shauri yako kwani wewe umeolewa na familia ya malkia wa uingereza?
Washauri ccm wenzako waache wizi wa Mali za umma na UFISADI kwa ujumla. Wananchi mmewafanya sehemu ya kuchumia vipato
 
Leo Mwenyekiti wa Chadema Mhe Freeman Mbowe pamoja na viongozi waandamizi wa Chadema wanatarajia kufikishwa Mahakama ya Kisutu Kwa ajili kusikiliza shauri la dhamana leo

======
UPDATES:
======

04:00pm > Hakimu Mashauri baada ya kusikiliza hoja zilizowasilishwa na upande wa Jamhuri na utetezi amesema Aprili 3, 2018 washtakiwa waletwe mahakamani wasaini bondi wakishakuwa huru ndiyo zoezi zima la taarifa ya kukata rufaa kama Jamhuri ilivyoonyesha nia litafanyika.

03:20pm > Upande wa Jamhuri (mashtaka) wamesema hawajaridhishwa na uamuzi wa kutoa dhamana na watakata rufaa. Hii ni kwa mujibu wa wakili wa Jamhuri, Faraja Nchimbi. Wanasema kuwa usalama wa umma unaweza kuwa shakani kwa washtakiwa kuwa huru mtaani.

Hakimu amekubaliana na Wakili Kibatala kuwa mawakili wa Jamhuri hawakuwa na hoja za msingi wa kisheria kupinga dhamana kwa washtakiwa.

03:00pm > Hatimaye Hakimu ametoa dhamana kwa washtakiwa! Kila mshtakiwa anatakiwa kuwa na wadhamini wawili ambao watasaini bondi ya Sh. Milioni 20 na wawe na barua toka kwa viongozi wao wa vijiji ama S/Mtaa na wawe na nakala za vitambulisho vyao.

Watatakiwa kuripoti Polisi kila Alhamisi (Central Police)

02:25pm > Wakili wa Jamhuri anamuomba mkuu wa Logistics za kuleta wafungwa Kisutu, aliyemtaja kwa jina moja la Shaban aeleze sababu za watuhumiwa kutofika mahakamani. Shaban anasema asubuhi aliwasiliana na mkuu wa gereza la Segerea ambaye alisema gari limeharibika.

2:08pm > Hakimu na Mawakili wa pande zote wanaelekea kwenye Ukumbi wa Mahakama. Ukumbi umeshajaa watu tayari. Ni wazi kuna uamuzi flani utatolewa hapa...

2:00pm > Hakimu amewaita mawakili. Waendesha mashitaka hawapo, aijulikani wameenda kula au vipi...

1:50pm > Waziri Mkuu mstaafu, Edward Lowassa amerejea mahakamani akiwa na Ndg. Mgeja. Amefika na kunong’onezana kitu na Wakili Kibatala

View attachment 728573
View attachment 728574

1:20pm > Vurugu nje ya mahakama ya Kisutu now, mtu mmoja amezongwa na kulazimishwa kuondoka kwenye makusanyiko wa wanachama wa CHADEMA.

"Huyooooo huyoooo, ondoka hapa, wewe kibaraka, hatukutaki, ondoka," kelele zimesikika wakimtimua mtu huyo.

Inadaiwa na wanachama hao wa CHADEMA kuwa mtu huyo ni "kibaraka" wa CCM na wengine wakimtuhumu kuwa mwanausalama.

Mtu huyo kaondoka kwa kukimbia akielekea katikati ya jiji.

12:26pm > Wakili Kihwelo ameiambia JamiiForums kuwa Hakimu Mashauri ameamua kusoma uamuzi mdogo, wawepo watuhumiwa ama wasiwepo, kuhusu dhamana ya Mbowe na wenzake. Hatua hii inakuja baada ya Mawakili wa Mbowe na wenzake kwenda kwa Hakimu Mkuu Mkazi, Wilbard Mashauri.

12:01pm > Hadi muda ni kuwa watuhumiwa wote wakiongozwa na Mh. Freeman Mbowe ambao wapo gerezani Segerea waliokuwa waletwe Kisutu, hawajatokea. Inadaiwa gari hakuna na lililopo ni bovu!

11:50am > Askari wenye silaha za kivita wameanza kuitana, wanajikusanya. Hatujui walikuwa wanapanga nini. Baadae wamesambaa; baadhi wameelekea getini huku wengine wakijipanga tena kuzunguka viunga vya mahakama.

11:45am > Mawakili wa Jamhuri - Patrick Mwita, Mutalemwa Kishenyi na Mawakili wa washitakiwa Peter Kibatala na Hekima Mwasipu wameingia ofisini kwa Hakimu Mkuu Mkazi, Wilbard Mashauri.

11:34am > Baadhi ya Viongozi wa juu wa CHADEMA waliokuwa wamefika mahakamani wameondoka mahakamani Kisutu. Wanaenda kushiriki msiba wa marehemu Kimesela ambaye anazikwa makaburi ya Kinondoni jijini Dar.

11:30am > Wananchi na makada wa CHADEMA wameanza kukosa uvumilivu baada ya kuzuiliwa nje ya lango kuu la mahakama na Polisi. Wameanza kuimba nyimbo za kudai haki, Wakili Kibatala amewasihi waondoke lakini dalili hazionyeshi kama wataondoka eneo hili.

11:20am > Mpaka muda huu, Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe na wenzake watano, hawajafikishwa katika eneo la Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar. Tetesi zinadai kuna mikakati ya kuhakikisha wanakula Pasaka wakiwa gerezani. Kisingizio kinachodaiwa kutumika ni kuwa “Magereza hawana gari la kuwaleta mahakamani”

======
Katika Picha:

> Waziri Mkuu Mstaafu na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, Edward Lowassa afika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kufuatilia mwenendo wa kesi inayowakabili viongozi wakuu wa chama hicho, akiwamo Mwenyekiti wake, Freeman Mbowe.

View attachment 728388
==========
> Waandishi wa habari na wananchi wengi wamefika mahakamani ambapo ulinzi leo umeimarishwa sana. Kulikuwa na kesi ya Ugaidi hivyo inapelekea watu kuzuiliwa.

> Jeshi la Polisi limeimarisha zaidi ulinzi katika Mahakama ya Kisutu, baadhi ya wafuasi wa CHADEMA na wananchi wamezuiwa kuingia, wamekusanyika nje ya mahakama.

View attachment 728403

> Waziri Mkuu mstaafu, Frederick Sumaye pia amewasili mahakamani hapa kushuhudia kitakachotokea.

View attachment 728417

> Baadhi ya wanachama wa CHADEMA, viongozi na wananchi wakiwa ndani ya chumba cha mahakama kusubiri shauri la Mbowe na wenzake

View attachment 728420
Ni shangwe tupu, dah kikundi hiki cha waharifu wanaspend pasaka wakiwa kolokoloni, hahahaha, Mungu ni kubwa. Tena wakithibitika na hatia wafungwe kabisa.
 
Magufuli ukimaliza uraisi wako tegemea kupata shida ata kama utamrithisha mwanao, makosa yako hayatakuacha salama
Hahahah, wewe zombe zombe tu. Dkt Magufuli ni mtu safi anapendwa sana na watanzania, tunampenda sana tena sana, tupo tayari kufa kwa ajili yake, Mungu amlinde kabisa ili ainyoshe nchi, vibaraka wote lazima Mwenyezi Mungu awaue kama alivyopata kunena Shehe wa Mkoa Dar.
 
Nina swali la kuuliza. Hivi kama ukipata dhamana bila kuletwa Mahakamani, Je utaratibu wa REMOVAL ORDER hauwezi kutumika?.
 
Hata mm ningewish iwe ivyo alaf chama kiachiwe kina LEMA kama hapajageuka libya hapa siyo mimi
Ausha lema aliwekwa ndani miezim sita hakukgeuka libya.Arusha kumemshinda ndo aweze nchi? Sema ana mikelele kama Lisu na Sugu tu .Hao watatu ndio wanaongoza kwa mikelele sasa hivi mwingine aliyeanza kujitutumia mikelele ni Heche.
 
Mh. Mbowe alidhani bado kuna kundi kubwa la wafuasi nyuma yake. Masikini hakujua kundi kubwa aliondoka nalo Dkt Slaa. Mh. Mbowe alidhani kuwa iwapo atatiwa mikononi mwa vyombo vya sheria kwa sababu ya kuvunja sheria basi wananchi wataandamana mitaa yote ya Tanzania, yaani alidhani watu hawatakula, alidhani watu watamlilia, hahaha, tumeshuhudia akienda kule Segera bila hata mwananchi mmoja kuandamana, leo mpaka Pasaka ipite yupo Behind Bar, na hakuna hata tone la shabiki zake wanaolalamika zaidi ya wabeba mabox waliopo chini ya uvungu.

Chezea watanzania! Kwa sasa habari ya Mujini ni Dkt Magufuli, CCM, utawala bora, Viwanda, na kila kijana sasa anajitambua vilivyo. Tofauti na enzi zile, waliwanunulia vijana bangi, waliwanunulia viroba, waliwanunulia madawa wa kulevya, then wanawaambia tunaingia mtaani huku wakiwalipa shs 10,0000, na wengine kuwasafirisha ili kuandamana, ila mpaka sasa hizo mbinu kwishaaa kabisa.
 
Gari la magereza kwa mara ya kwanza limeharibika kushindwa kuwafikisha watuhumiwa mahakamani.dhamana yao ilikuwa wazi lakini bado wameng'ang'aniwa.imewapendeza wao wenye mamlaka kuhakikisha wanashiriki mateso ya kristo pamoja

Kwa kuwa serikali itafungua ofisi zake mara baada ya Yesu kufufuka,nao watatolewa mpaka Yesu afufuke.

Nawatia moyo.wasikate tamaa.tunajua hayo yanawapata kwa maslahi ya wengi.waliofanya kwa maslahi yao walipotiwa msukosuko walinyamaza kimya

Kama wewe ni kiongozi wa upinzani hujawahi kutuhumiwa kitu na kukamatwa katika zama hizi, basi ujue huna madhara katika vita ya kupigania democrasia
 
Chadema na wafuasi wake mitandaoni....mnasikitisha sana na sijui kwanini mnajipa matumain hewa wa kuutingisha utawala MAGUFULI ili hali mmechokwa na wananchi wa TANZANIA kwa kiwango cha hali ya juu sana na hili mnlijua na ndio maana sasa hivi mnacheza vizuri sana na njia mbadala za kudeal na MAGUFULI na si CCM tena kama kutekeleza mauaji..utekaji kwa umakini wa hali ya juu sana ili mwisho wa siku ionekane ni MAGULI NA SERIKALI YAKE....

Sasa nije kwenye viashiria vya kudoda so called maandamano ya 26/04 yanayo ratibiwa na CHADEMA NYUMA YA PAZIA...Rejea tamko la MSIGWA juu ya haya maandamo na MSIGWA ni mjumbe wa kamati kuu...vishiria vyenyewe ni..

Hivi kweli semeni ukweli..Ni nchi gani Africa kiongozi mkubwa wa upinzani anawekwa ndani na ananyimwa dhamana kizembe kiasi hiki afu wafuasi wake hata they dont even bother kuonyesha kuguswa kwenye....Kihuhalisia kama ingekuwa ni CHADEMA ya Enzi za slaa kwa yaliyo watokea viongozi wa CHADEMA wiki hii pasingekalika lazima tungeona purukushani za maana nchi nzima...Lakini ni nziiiii...

Kuwekwa kwa LEMA ndani kizembe zembe kwa miezi kadhaa hivi kweli kwa Arusha ya hizo wasingekubali hili...mbona pangechimba.ila ukweli ni kwamba CHADEMA mmechokwa ndani ya nchi hii..

So called rais wa mbeya leo hii anaonja utamu wa magereza na wakazi wa mbeya WANAENDELEA na shughuli zao as if Nothing happened...Aiseeeh haya ni maajabu kweli maana si kwa niwajuavyo wafuasi wa CHADEMA kwenye jiji la mbeya mostly enzi z Dr SLAA...

Kushindwa kinondoni na siha kizembe kizembe kama msemavyo(ILA KWENYE KUSHINDWA HAYA MAJIMBO UKWELI MNA UJUA) still wafuasi wenu hatujaona hata mmoja kaonyesha kupingana na huu usgindi wa CCM...Rejea CHADEMA ya enzi hizo mfano Masha na WENJE nyamagana....

Idadi ya wabunge ba madiwani mpaka sasa ni aibu ukilinganisha na idadi kabla ya 2018.....sasa kamaviongozi wanakimbia vipi kuhusu WANACHAMA....?
 
Watafanyiwa figisu sana ila muda utaongea na ipo siku watakua huru! Tuwaombee ili watesi wao wawafanyie tahfifu!
 
Jibu hoja.
hoja gani za kipuuzi! Et umeona wapi kiongozi mkubwa wa upinzani ananyimwa dhamana, hivi unamjua beseje? Si ni wa afrika!? Kwanza ulitaka wafuasi wa chama wafanyeje? Wavunje sheria kama unavyotaka wewe? Yaani wewe raha yako ulitaka uone wafuasi wa chadema waingie na geti pale kisutu? Kama ni hivyo basi jifikirie upya wallah huna ishu!
 
Back
Top Bottom