Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,807
- 11,969
Kesi namba 458 ya Jamhuri dhidi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Jamii Media, Maxence Melo na mwenzake Mickie William inayohusu kuendesha mtandao (JamiiForums.com) bila kutumia Kikoa cha do.TZ imeendelea leo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.
Katika Kesi hiyo ambapo Watuhumiwa hao wanashtakiwa pia kwa kuzuia upelelezi wa Polisi kwa kutokutoa taarifa za Mteja aliyeandika taarifa kuhusu Benki ya CRDB imeendelea mbele ya Hakimu Huruma Shaidi.
Kwa siku ya leo, upande wa Jamhuri umewakilishwa na Wakili Gloria huku upande wa utetezi ukiwakilishwa na Wakili Benedict Alex.
Wakili wa Jamhuri amesema, shahidi wa mwisho wanayemtegemea hawajampata bado na hivyo kuomba muda mfupi zaidi ili waweze kuwasiliana na Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) kujua shauri hili litaendeleaje.
Shahidi huyo, Tully Mwambapa anayetokea CRDB amekuwa akisubiriwa tangu Agosti 01, 2019 ambapo upande wa Jamhuri ulisema ungemleta kwa ajili ya kutoa ushahidi wake.
Tangu hapo shauri hili limekuwa likiahirishwa mara kwa mara kwa kukosekana kwa shahidi huyo huku sababu kadha wa kadha zikitolewa.
Katika shauri hili mara ya mwisho shahidi kusikilizwa ilikuwa ni Novemba 12, 2018 ambapo Mpelelezi Kitengo cha Upelelezi wa Makosa ya Mtandaoni kutoka Makao Makuu ya Polisi (HQ), Inspekta Beatrice Majule alikuwa ndiye shahidi
Baada ya Wakili wa Jamhuri kuomba muda zaidi Wakili wa Utetezi alikubali na Hakimu Shaidi kuahirisha shauri hilo hadi mwakani mnamo Januari 28
Zaidi, soma;
Sent using Jamii Forums mobile app
Katika Kesi hiyo ambapo Watuhumiwa hao wanashtakiwa pia kwa kuzuia upelelezi wa Polisi kwa kutokutoa taarifa za Mteja aliyeandika taarifa kuhusu Benki ya CRDB imeendelea mbele ya Hakimu Huruma Shaidi.
Kwa siku ya leo, upande wa Jamhuri umewakilishwa na Wakili Gloria huku upande wa utetezi ukiwakilishwa na Wakili Benedict Alex.
Wakili wa Jamhuri amesema, shahidi wa mwisho wanayemtegemea hawajampata bado na hivyo kuomba muda mfupi zaidi ili waweze kuwasiliana na Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) kujua shauri hili litaendeleaje.
Shahidi huyo, Tully Mwambapa anayetokea CRDB amekuwa akisubiriwa tangu Agosti 01, 2019 ambapo upande wa Jamhuri ulisema ungemleta kwa ajili ya kutoa ushahidi wake.
Tangu hapo shauri hili limekuwa likiahirishwa mara kwa mara kwa kukosekana kwa shahidi huyo huku sababu kadha wa kadha zikitolewa.
Katika shauri hili mara ya mwisho shahidi kusikilizwa ilikuwa ni Novemba 12, 2018 ambapo Mpelelezi Kitengo cha Upelelezi wa Makosa ya Mtandaoni kutoka Makao Makuu ya Polisi (HQ), Inspekta Beatrice Majule alikuwa ndiye shahidi
Baada ya Wakili wa Jamhuri kuomba muda zaidi Wakili wa Utetezi alikubali na Hakimu Shaidi kuahirisha shauri hilo hadi mwakani mnamo Januari 28
Zaidi, soma;
Kisutu, Dar: Hukumu ya Kesi namba 456 ya Jamhuri dhidi ya JamiiForums kutolewa Januari 22, 2020
===== UPDATE: Hakimu Simba ameshindwa kusoma hukumu Desemba 06, 2019 na hivyo hukumu hiyo itasomwa January 22, 2020 ==== Wakuu, Kesho, Desemba 06, 2019 kutakuwa na hukumu ya mojawapo ya kesi zilizofunguliwa na Jamhuri dhidi ya Mkurugenzi wa Jamii Media Co. Ltd na mwanahisa, Mike William...
www.jamiiforums.com
Sent using Jamii Forums mobile app