Kisingizio: Daftari la Wapiga Kura, vyombo vya dola. Sababu?

Daftari la wapiga kura na vyombo vya dola vitabebeshwa lawama na labda vinastahili. Lakini katika hili CHADEMA inapaswa kutoa sababu zinazoeleweka zaidi ya visingizio.

Wanachama, wapenzi, na mashabiki wa CHADEMA wanapaswa kuwa wakali kidogo (au sana) ili chama kiweze kutoa maelezo yanayoeleweka ya kwanini matokeo haya hayakuwa mazuri kama watu walivyokuwa wanaaminishwa au kutarajia. Kuelekea uchaguzi mkuu wa 2015 CHADEMA ilitakiwa iwe inasukumwa na upepo wa ushindi lakini hali sivyo ilivyo.

Kama majibu ya kueleweka hayapo ipo haja ya haraka ya kuanza kudai watu wawajibike au wawajibishwe.

To be continued....

Ulitaka nani abebeshwe lawama? MM hivi kweli kuwa na mfumo unaowanyima watu kutumia haki yao ya kidemokrasia ya kuwapigia kura watu wanaowataka eti kwa sababu tu hawako kwenye daftari kwa nini utaratibu huo usilalamikiwe kwa matokeo ya aina yoyote ile.

The police will not escape blame as they have not exercised prudence in excuting their responsibilities. Hivi MM unawezaje kusema hoja hizi ni visingizio, watu wanachomwa mikuki, rushwa kedekede, umafya nk?

Najua haya ni maoni yako na una uhuru nayo, lakini maoni ambayo yanawaghafilisha wasomi wako si yako tena ni ya wote tafadhali jitahidi kama ambavyo umekuwa ukifanya huko nyuma kutuletea a well cooked ideas
 
Joshua Nassari sijui kwa nini aliamua kuleta taharuki kufyatua risasi ovyo wakati Chadema walikuwa kwenye ngome yao kaskazini.
 
Kwani hiyo kata ya Republic of Nauru diwani ni CUF ama CCM?
sie kama kawa tunasherehekea sana tena sana kwa kata5, CCM vipi?
CCM ni losers maana wameanza kutumia mapesa kibao kwanza kwenye kura za maoni kwenye chama chao cha wala rushwa, halafu unakuja kwenye uchaguzi unaangukia puwa!! inawauma sana.

281527_551482168211904_1540626594_n.jpg
 
Binafsi Nina kila sababu ya kukipongeza cdm kwani wamefanya kazi nzuri ukilinganishwa NA vyama vingine vya siasa, ingawa matokeo hayaendani NA matarajio,
ccm wamejificha chini ya daftari la wapigakura kwani kuna watu wengi wanepata elimu ya kupigakura lakini hawapati nafasi
 
Mkuu REMSA,
Nami huwa nashindwa kumuelewa Mzee Mwanakijij, nadhani ataka watoke ili aingie yeye, kila wakishindwa conclusion watoke, mara sasa anataka majibu mbadala, sijajua tatilo lake< siasa za USA analeta Bongo, kila siku namwambia makamanda wanafanya kazi kubwa sana ukilinganisha, mfumo wetu na mazingira yalivyo Bongo, kwanzia sheria mpaka na kila kitu.

na MMJ anafahamu Tanzania huwa tuna Watawala na si Viongozi, so kazi inayofanywa na CDM si ya kubezwa hata kidogo ni ya kupongezwa sana.

Ni kweli Mkuu ktk mazingira ya utovu wa Demokrasia hata serikali kuwa tayari kuua wananchi
wake ili mradi tu kuwazuia viongozi wa CDM wasiwaelimishe watanzania,bado wamesacrifise maisha yao
MM you have to think twice kabla hujawambia viongozi hawa wa CDM kustep down.

Thats why napata hofu kuwa wewe ni chui ndani ya ngozi ya kondoo, upo upande ambao viongozi hawa wa CDM ni hatari kwao na maslahi yao, si kweli una uchungu kwa Tz, maana hata mtoto wa primary school anajua kinachofanywa na Mbowe na Dr.Slaa.
 
MM you have to think twice kabla hujawambia viongozi hawa wa CDM kustep down.Thats why
napata hofu kuwa wewe ni chui ndani ya ngozi ya kondoo
Mkuu, nimeipenda hiyo MMJ ndio alivyo, hata wafanyeje sijawahi ona kaanzisha uzi wa kuwasifika, makamanda hawalali sie tunaona wanapambana na majitu, imagine CCM more than50 yearz wanatawala, leo tuje kuwatoa kilahisi, mpaka sasa CDM wamejitahidi na tunajivunia kuwa nao...

Ama anataka tuanzishe Chadema Halisi...?
 
Mkuu, nimeipenda hiyo MMJ ndio alivyo, hata wafanyeje sijawahi ona kaanzisha uzi wa kuwasifika, makamanda hawalali sie tunaona wanapambana na majitu, imagine CCM more than50 yearz wanatawala, leo tuje kuwatoa kilahisi, mpaka sasa CDM wamejitahidi na tunajivunia kuwa nao...

Ama anataka tuanzishe Chadema Halisi...?
Kwani hujui Mwanakijiji ni mmoja wa waasisi wa CCJ?
 
Mzee wa kijiji naomba kuchangia wazo kidogo juu ya hoja yako ambayokwa kiwango fulani inaonesha huna furaha juu ya matokeo haya! hakika hata mimi sijafurahia.
Pamoja na kutaka viongozi wetu watoe sababu za kupata matokeo hayo, basi kabla yao naomba na mimi nitoe sababu moja ya msingi.
Kwa ujumla naomba kuwakumbusha wapenzi wa cdm kuwa chama kama chama kimejiongezea wanachama siku chache kabla ya uchaguzi wa 2010 na baada ya hapo namba imeendelea kuongezeka siku hadi siku. lakini kati ya wapenzi wengi wa cdm wa sasa kumbuka walikuja kuipenda cdm wakati maboresho ya daftari la wapiga kura yakiwa yameishafanyika, hivyo hadi sasa wengi wao ni wanachama wa moyoni lakini hawawezi kupiga kura kwani sheria haiwaruhusu.
USHAURI: Kwakuwa 2014 kutakuwa na uandikishaji upya wa daftari la wapiga kura, cdm ijipange kutoa elimu ya uraia ili kila mtu aone kuwa kupiga kura ni haki yake na ili upige kura lazima ujiandikishe. NI MAONI YANGU TU.
The BOSS, POMPOO, MWITA MALANYA, MCHAMBUZI mpo hapo? karibuni

Uko sawa kaka!
 
Daftari la wapiga kura na vyombo vya dola vitabebeshwa lawama na labda vinastahili. Lakini katika hili CHADEMA inapaswa kutoa sababu zinazoeleweka zaidi ya visingizio.

Wanachama, wapenzi, na mashabiki wa CHADEMA wanapaswa kuwa wakali kidogo (au sana) ili chama kiweze kutoa maelezo yanayoeleweka ya kwanini matokeo haya hayakuwa mazuri kama watu walivyokuwa wanaaminishwa au kutarajia. Kuelekea uchaguzi mkuu wa 2015 CHADEMA ilitakiwa iwe inasukumwa na upepo wa ushindi lakini hali sivyo ilivyo.

Kama majibu ya kueleweka hayapo ipo haja ya haraka ya kuanza kudai watu wawajibike au wawajibishwe.

To be continued....
mimi na wenzangu wengi tuu hatukupiga kura na hadi sasa hakuna chaguzi ndogo tumeweza.Pia kuna watanzania sasa hivi wapo 18,19 wenye haki ya kupiga hawana hiyo nafasi,wameishia kuwa ktk kampeni tuu huku wakipata machungu ya kutokuwa sehemu ya uchaguzi.Sijui mtalisemea vipi hili?
 
Daftari la wapiga kura na vyombo vya dola vitabebeshwa lawama na labda vinastahili. Lakini katika hili CHADEMA inapaswa kutoa sababu zinazoeleweka zaidi ya visingizio.

Wanachama, wapenzi, na mashabiki wa CHADEMA wanapaswa kuwa wakali kidogo (au sana) ili chama kiweze kutoa maelezo yanayoeleweka ya kwanini matokeo haya hayakuwa mazuri kama watu walivyokuwa wanaaminishwa au kutarajia. Kuelekea uchaguzi mkuu wa 2015 CHADEMA ilitakiwa iwe inasukumwa na upepo wa ushindi lakini hali sivyo ilivyo.

Kama majibu ya kueleweka hayapo ipo haja ya haraka ya kuanza kudai watu wawajibike au wawajibishwe.

To be continued....

Mwanakijiji,

Hivyo si visingizio bali ni sababu kubwa za msingi sana.Kumbuka maeneo yote ambayo Chama kimejikitika kwa kiwango cha juu,ushindi tumechukua.

Naomba nikukumbushe tu,eneo kama Geita mwenyekiti yuko hoi hospitalini majerui zaidi ya kumi wamelazwa,utaanza kumlaumu nani na wote walikuwa kazini,Vijana kadhaa mawakala wameumizwa vibaya.

nenda shinyanga,mwenyekiti,mbunge wote wako hoi,wanachama kadhaa wamelazwa pia wako hoi,nani wakumlaumu?
jamani jamani lawama zingine ni za kuwaponda watu moyo hasa vijana wote wanaojitoa kupambana.

Unaambiwa mtu ameenda kupiga kura na sime.mwingine anafyatua risasi hewani what do you want more than that?

nawatetea makamanda wote maana najua wameumizwa kwa kiwango gani.wengi wanaugulia majeraha sasa,wake zao wamepoteza matumaini......tooooooo much.
 
lakini still bado nasisitiza hizo ni sababu,hata kura zao za ushindi zimepungua sana,jiulize kwanini?

Mimi nafikiri ni bora mjue wapiga kura walikuwa wangapi?na wangapi walipaswa kupiga kura,na hii ndiyo sababu Chadema inapambana na tume kila leo.Hawako wazi kubainisha wapiga kura kila eneo ni wangapi,bado mfumo hauko sawa.

Polisi wanawalinda kwa kuruhusu matukio bila wao kufanya kazi zao.
 
MMK at work..a man with mission.Kama alivyokomaa kuwa ufisadi si kitu kikubwa kwa CDM kushikia bango asa anajidhihirisha tena yupo katika mrengo gani.Startistics zinaonyesha idadi kubwa sana ya watu hawakupiga kura mwaka 2010,na wengi ni kwa vile daftari halikufanyia mabadiliko ya kuwajumusha watu,ununuzi wa shahada na mengine.Vijana wa iaka 18,na 19 ni wengi sana na kila mtu anajua kura zao zingekwenda wapi.MMK kaamua tuu kibishi kulifanya si muhimu suala la daftari.Na kaenda mbali kuchochea uasi ndani ya CDM.

Huyu ndiye mshauri wa kujitolea kwa CDM kutoka CCM.Sasa anajianda kuja na makala ndeefu sana kwa kile anachoamini kuwa kapata kit chenye mashiko ,akiamini kapata kitu toka ktk fikra ambcho ni worth kuandika maneno meengi sana.Mbaya zaidi ahjafanya hata research aone ktk parameters zote zinazotumika kuelezea matokeo ya chaguzi na Kwa kiasi gani zilichangia kubadili wingi wa kura kw aupande fulani huku zikiongeze upande mwingine.

Mkulu hana subira kama jamaa wa mbagala ili awahi haribu kabla haujaja uthibitisho utakaomzuia nia yake kutimia.Sasa anataka viongozi waseme nini wakati wengine wana majibu waliyojionea wenyewe?huyu ndie aliyeshindwa sema kama yeye ni mshauri au critics kasema hizo options hazitoshi.Sasa mwenye macho na fikra amtafutie nafasi yake.
 
Mwanakijiji,

Hivyo si visingizio bali ni sababu kubwa za msingi sana.Kumbuka maeneo yote ambayo Chama kimejikitika kwa kiwango cha juu,ushindi tumechukua.

Naomba nikukumbushe tu,eneo kama Geita mwenyekiti yuko hoi hospitalini majerui zaidi ya kumi wamelazwa,utaanza kumlaumu nani na wote walikuwa kazini,Vijana kadhaa mawakala wameumizwa vibaya.

nenda shinyanga,mwenyekiti,mbunge wote wako hoi,wanachama kadhaa wamelazwa pia wako hoi,nani wakumlaumu?
jamani jamani lawama zingine ni za kuwaponda watu moyo hasa vijana wote wanaojitoa kupambana.

Unaambiwa mtu ameenda kupiga kura na sime.mwingine anafyatua risasi hewani...

Kwanza nimeguswa mno na vurugu hizi katika kampen na chaguzi zetu, kwan inaonyesha bado tunasafari ndefu kuifikia ile demokrasia ya kweli.

Nazidi kuwapa pole wahanga na majeruh wa vurugu hizo, lakin mimi bado ninauliza, hivi tofauti na kutafuta mtu wa kumlaumu, hakuna hatua nyingine za kuwachukulia hao watu? Huu si wakati wa kulaumu tena na kutoa matamko ya kisiasa, tuchukue hatua
 
Mkuu, nimeipenda hiyo MMJ ndio alivyo, hata wafanyeje sijawahi ona kaanzisha uzi wa kuwasifika, makamanda hawalali sie tunaona wanapambana na majitu, imagine CCM more than50 yearz wanatawala, leo tuje kuwatoa kilahisi, mpaka sasa CDM wamejitahidi na tunajivunia kuwa nao...

Ama anataka tuanzishe Chadema Halisi...?

Time will tell,ukombozi uko mlangoni,hauzuiliwi na propaganda za watu kama MM.
 
Mzee Mwanakijiji

Mkuu,

Tathimini yako na wengine kwa haraka haraka ni rahisi kukurupuka kuwa Chadema kimeshindwa...

Hatuna sababu ya kuwa wakali wala kutafuta sababu, uzuri wanachadema tunazijua sababu,


Kwa hili ungewashauri CCM, wajitadhimini na waje na sababu kwa nini wanazidi kuporomoka...uchaguzi huu wamepoteza viti 3 vya udiwani...Chadema tumeongeza, sasa sijui nani aje na hizo sababu...

Mkuu MMK, kama Tanzania tungekuwa na Democrasia ya Kweli...Nami ningeungana nawe, kuwakosoa na kuwaponda viongozi wetu, lakini kwa jinsi uwanja wa demokrasia ulivyo, CDM wamejitahidi sana,, nikuulize kidogo tu...
1. Unafahamu kuna kesi ngapi zinazowakabili viongozi wakuu wa CDM mpaka sasa?
2. Kesi ngapi kwa mashabiki na wapenz wa Cdm mpaka sasa?
3.Kuna mashabiki wangapi wa CDM wamekufa mpaka sasa?
4.Kuna walemavu, wagonjwa, walioteswa wa CDM mpaka sasa?

MzeeMwanakijiji, Tanzania ni zaidi ya ujiavyoo..., Chadema tunawapongeza sana tena sana, endeleeni viongozi wetu tupo nyuma yenu.

hiyo ndio mission yake,mkuu ndio maana kashawishi uasi wa wanachama.Atakuja na posting ndeefu sana halafu hana tafiti yoyote inayoweza thibitisha kuwa hizo factors hazikuwa na effect au hata effect zake ni negligible.

Mbaya kasahau kuwa ingekuwa kinyume basi wanachama ndio wangelaumiwa kwa kutopiga kura.
 
Mzee Mwanakijiji

Unaweza ukaona hizo siyo sababu za CHADEMA kutoshinda kata nyingi, lakini lazima ujue CCM na CHADEMA haviko sawa kwenye uwanja wa siasa, mfumo wa sheria ulioa anzisha vyombo vya kusimamia uchaguzi vinaibeba CCM big time! Lakini pia CCM bado inatumia hila nyingi sana maeneo ambayo wananchi bado hawana muamko wa elimu ya uraia! CHADEMA imeshinda kata tano, ukiwauliza watu wa hayo maeneo watakuambia hali yao ya usalama wa maisha ilikuwaje kipindi cha uchaguzi na hata baada ya uchaguzi! Mimi nilikuwa mwathirika arusha wa kuvamiwa na kikundi cha green guard cha CCM walitupiga mawe, wakatuvunjia gari letu, Mungu alitusadia maana dereva wetu walikuwa amepigwa kichwa damu zinavuja hawezi kuona ikabidi nirukie usukani kwakuwa nilikuwa kiti cha mbele niikwepeshe gari iliyokuwa inaingia darajani, hayo yalitokea Arusha Daraja mbili. Ni vigumu mno kuyaacha haya mambo kama sababu ya kushindwa kwenye kata nyingi vitisho ni vingi na usalama wa maisha ni mdogo sana wakati wa uchaguzi na baada ya uchaguzi! Hii hali inaratibiwa kabisa na serikali kwa kuwatumia watu makatili na wanaojulikana kwa vitendo vya mauji na ujambazi kufanya matukio ya kikatili kwa kuwalipa! Na wakikamatwa wanaachiwa ndani ya dakika zisizozidi 30! Unataka kusema Mzee Mwanakijiji kuwa uwanja uko sawa hapa! Siasa za Tazania siyo za marekani. Tuna safari ndefu kufikia democrasia ya kweli! Kuna sababu gani kwa Tume hii kukaa miaka zaidi ya minne bila kuandikisha wapiga kura wapya kama siyo mbinu ya CCM kuendelea kushinda chaguzi ndogo? Kila baada ya uchaguzi huwa kunakuwa na hamasa mpya ya kisiasa kwaninini tume isitumie hiyo fursa kuandikisha wapigakura wapya? Ni uhuni usiokubalika kuacha watu mtaani wenye umri wa kupiga kura halafu hawawezi kuitumia hiyo haki yao ya kikatiba! Mimi Msimamo wangu hakuna mjadala wa kiongozi yoyote wa chadema kuwajibika, ila nawapongeza kwa kuendelea kufanya kazi kwenye mazingira magumu yasikuwa na ushindani sawa!
 
Last edited by a moderator:
Mzee Mwanakijiji unashindana na Imani potofu iliyojikita kwa mashabiki wa CHADEMA humu JF. kuna watu kama alivyosema Pasco kwamba wanajiona wao ndiyo CHADEMA zaidi hadi kupoteza uwezo wao wa kufikri kama binadamu. Hakuna anayebeza matokeo ya CHADEMA kushinda kata 5 kati ya 29 zilizokuwa zinashindaniwa, bali hoja hapa kama kweli hizo kata zilizopatikana ndiyo yalikuwa malengo ya CHADEMA?

Wakati mchakato wa Kampeni unaanza CHADEMA lengo lao lilikuwa ni kushinda Kata ngapi na je lengo hilo limefikiwa? Vingozi wa Kitaifa walioshiriki kwenye Kampeni hadhi zao zinalingana na wale wa CCM walioshiriki kwenye Kampeni hizo? Jee hata kule ambako tuliambiwa watu kama Lusinde walichafua hali ya hewa kwa maneno yao CHADEMA wameshinda? Ni nani ana hakika kwamba wote wapiga kura wapya watakaoandikishwa watakuwa ni wapiga kura wa CHADEMA?

Wakati wa uchaguzi wa UVCCM mashabiki wa humu JF wakawa wanashangaa inakuwaje kuna vijana ambao bado wako CCM kama vile itatokea siku vijana wote watakuwa CHADEMA. Na hilo nalo ni tatizo kudhani kwamba kwa kuwa tu ni kijana basi lazima awe CHADEMA au kwa kuwa ni mzee basi ni CCM!! Ni lazima kama unataka kukubalika utoke kwenye kiota chako cha mawazo mgando na uende mbele zaidi kuukabili (face the reality) ukweli kinyume cha hapo tutaishia kujilisha upepo.
 
Last edited by a moderator:
Mimi binafsi napataga shida na MM kwa nini conclusion yako huwa ni viongozi wa CDM kuachia
ngazi?Maana hata uchaguzi wa Arumeru Mashariki ulipendekeza hivyo.Je ni kweli hakuna ambayo
viongozi wa CDM wamefanya kwa ajili ya chama hata kuifanya CDM kujulikana nakukubalika na watanzania!? Kigezo
kwako kwa hawa viongozi kuwa wanajituma ni ushindi wa 100% tu!? Je ushauri huu umeutoa kwa JK ambaye
ameifikisha ccm na taifa hapo lilipo mara ngapi?hasa baada ya chaguzi zinazoendelea ndani ya chama? bila shaka
haya unayosema si visingizio bali ndio ukweli halisi.Hivi kama kata ina watu 5000 wanapiga kura watu 2000 huoni
kuwa ni tatizo!


mkuu Remsa, mi nilishamshtukia mapema! Huyu MMK ni zaidi ya unavomfikiria hapa!!
 
Back
Top Bottom