Kisima cha maji cha TZS 269 Milioni hakijawahi kutoa maji huko Mpanda

Hivi punde

JF-Expert Member
Apr 1, 2017
2,554
8,552
Licha ya kuchimbwa na kugharimu Sh268.9 milioni, kisima kilichopo Kijiji cha Ngomalusambo wilayani Mpanda, hakijawahi kutoa maji.
Kisima hicho kilichojengwa kwa miaka miwili kati ya mwaka 2013 hadi 2015 ili kuhudumia wananchi 1,600 waliopo kwenye kijiji hicho hawajawahi kunufaika nacho.


Akieleza sababu za changamoto za visima vingi kutotoa maji licha ya kukamilika kwake kama ilivyokusudiwa, leo (Jumatano) Naibu Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Seleman Jaffo amesema hujuma za wananchi dhidi ya miundombinu hiyo zinachangia kukithiri kwa changamoto hiyo.


Akijibu swali la Mbunge wa Mpanda Vijijini, Moshi Kakoso juu ya kutonufaika kwa wananchi wake na mradi huo, naibu waziri huyo amesema hatua stahiki zimechukuliwa.


"Mradi umeshindwa kutoa huduma kutokana na kuibwa kwa betri ya pampu. Kukabiliana na changamoto hiyo, halmashauri imenunua betri mpya na kuifunga," amesema Jaffo.

JAFOOOO.jpg

Licha ya hilo, serikali imesema Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda ina mpango wa kuchimba kisima kingine mwaka ujao wa fedha baada ya kisima kilichopo kupoteza uwezo wake.
 
Licha ya kuchimbwa na kugharimu Sh268.9 milioni, kisima kilichopo Kijiji cha Ngomalusambo wilayani Mpanda, hakijawahi kutoa maji.
Kisima hicho kilichojengwa kwa miaka miwili kati ya mwaka 2013 hadi 2015 ili kuhudumia wananchi 1,600 waliopo kwenye kijiji hicho hawajawahi kunufaika nacho.


Akieleza sababu za changamoto za visima vingi kutotoa maji licha ya kukamilika kwake kama ilivyokusudiwa, leo (Jumatano) Naibu Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Seleman Jaffo amesema hujuma za wananchi dhidi ya miundombinu hiyo zinachangia kukithiri kwa changamoto hiyo.


Akijibu swali la Mbunge wa Mpanda Vijijini, Moshi Kakoso juu ya kutonufaika kwa wananchi wake na mradi huo, naibu waziri huyo amesema hatua stahiki zimechukuliwa.


"Mradi umeshindwa kutoa huduma kutokana na kuibwa kwa betri ya pampu. Kukabiliana na changamoto hiyo, halmashauri imenunua betri mpya na kuifunga," amesema Jaffo.

View attachment 531877
Licha ya hilo, serikali imesema Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda ina mpango wa kuchimba kisima kingine mwaka ujao wa fedha baada ya kisima kilichopo kupoteza uwezo wake.
Kinahitaji maombi ya hali ya juu ama kitoe maji au kirudishe fedha. Lazima kichague moja tu.
 
pesa nyingi sana wakati kwa pesa hizi sisi tunaweza chimba visima mpanda yote ikawa ni maji kwenda mbele



njooni tuwachimbie visima kwa bei nafuu kabisa sawa na bureee bureee


VODA - 0766438286

TIGO - 0714453589

AIRTEL - 0686733292

KARIBUNI SANA SISI UNAKUNYWA MAJI BAADA YA MASAAA TU
FB_IMG_1581630757790.jpeg
FB_IMG_1581630796479.jpeg
FB_IMG_1581630747727.jpeg
FB_IMG_1571570655054.jpeg
limpeza_furos3.jpeg
FB_IMG_1571571550301.jpeg
FB_IMG_1575396254090.jpeg
images-38.jpeg
FB_IMG_1574751684266.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom