Kisiasa Mbowe anaweza kuwa ni rafiki mzuri wa Dkt. Magufuli kuliko Job Ndugai

johnthebaptist

JF-Expert Member
May 27, 2014
83,853
141,772
Ukifuatilia kwa makini mwenendo wa Freeman Mbowe utagundua kuwa ni mtu anayejua anachokifanya. Tofauti na wanasiasa wengi ambao hutenda mambo kwa kubahatisha, kinafiki na wakati mwingine wakitaka waonekane wanausapoti uongozi wa juu.

Ukiangalia utendaji wa Mbowe kama KUB amekuwa upande wa serikali zaidi japo hili huwezi kulibaini kiurahisi. Tofauti na Dr Slaa alipokuwa akimsaidia KUB Hamad Rashid , Mbowe hajawahi kuibua hoja yoyote nzito ya kuibana serikali.

Hata kwenye kipindi cha maswali ya papo kwa hapo kwa waziri mkuu ambapo kanuni zinampa upendeleo KUB kuuliza swali la kwanza mara nyingi Freeman huwa hayupo bungeni.

Mambo ni mengi hata kumuengua Dkt. Slaa kinyemela 2015 na kumleta Lowassa ulikuwa ni mkakati wa kutaka kuhakikisha mtu makini hagombei.
Ikumbukwe hapa ni Mbowe huyu huyu aliyemtoa Dkt. Slaa bungeni ili agombee urais ilhali akijua kabisa huwezi kumshinda Rais wa CCM anapogombea muhula wa pili. Lengo la Mbowe lilikuwa ni kupunguza nguvu ya Dr Slaa kwani umaarufu wake aliujengea zaidi bungeni.

Niseme tu kwa kifupi, Mbowe na hata Zitto Kabwe wanaweza kuwa ni marafiki " wazuri" wa Dr Magufuli kuliko Ndugai na Musukuma.

Maendeleo hayana vyama!
 
Mbowe hajawahi kuibua hoja yoyote nzito ya kuibana serikali.

Unaweza ukawa uko sahihi kwa kiasi fulani ila ukweli ni kwamba hoja nzito za kuibana Serikali kwa kipindi hiki cha awamu ya tano, hazipo. Mbowe ni mtu makini, na hivyo asingependa kuongea hewa. Labda angekuwa huyu mwingine mgombea wao u-rais mtarajiwa

Pamoja na hayo ikumbukwe pia kuwa system ya uongozi wa Nchi (siyo Serikali) au dola, ina watu watatu tu juu, yaani Rais, Spika na Jaji Mkuu. Kama tuseme kuna sehemu ambayo una uhakika kabisa kuwa ulishindwa kumuelewa Job Ndugai, basi atakuwa alikuwa anafanya utafiti kwa ajili ya kumpelekea feedeback za utafiti huo, mmojawapo wa hao wenzake wawili. Nadhani hata Katiba ya Nchi yetu inasema kuwa Rais na Makamu wa Rais wanapokuwa wako nje ya Nchi, yaani wote wawili wanakuwa hawapo kwa wakati mmoja, ni Spika au Jaji Mkuu anayeweza ku-kaimu nafasi ya u-Rais. Zaidi ni kuwa Mkuu wa KUB hayupo kwa ajili ya kuibomoa Serikali, bali kuijenga na ujenzi huo naamini kabisa kuwa hauwezi kulingana na ule wa Ofisi ya Spika kwa sababu KUB kwa upande mwingine ni mpinzani wa Chama chenye Serikali iliyopo madarakani, wakati Ofisi ya Spika, ni msimamizi wa Serikali iliyopo madarakani, bila kujali ni ya chama kipi cha Siasa
 
Tilapia na nyumba ya tai vipo jirani sana kwa kweli. Na watu wanamiliki tilapia tangu enzi hizo,na tcha mmoja hivi alipewa rum maalum kwa ajili yake free kwa mwaka mzima na kwa maisha yake yote. Tcha na mmiliki wa tilapia ni wa1.
 
Ukifuatilia kwa makini mwenendo wa Freeman Mbowe utagundua kuwa ni mtu anayejua anachokifanya. Tofauti na wanasiasa wengi ambao hutenda mambo kwa kubahatisha, kinafiki na wakati mwingine wakitaka waonekane wanausapoti uongozi wa juu.

Ukiangalia utendaji wa Mbowe kama KUB amekuwa upande wa serikali zaidi japo hili huwezi kulibaini kiurahisi. Tofauti na Dr Slaa alipokuwa akimsaidia KUB Hamad Rashid , Mbowe hajawahi kuibua hoja yoyote nzito ya kuibana serikali.

Hata kwenye kipindi cha maswali ya papo kwa hapo kwa waziri mkuu ambapo kanuni zinampa upendeleo KUB kuuliza swali la kwanza mara nyingi Freeman huwa hayupo bungeni.

Mambo ni mengi hata kumuengua Dkt. Slaa kinyemela 2015 na kumleta Lowassa ulikuwa ni mkakati wa kutaka kuhakikisha mtu makini hagombei.
Ikumbukwe hapa ni Mbowe huyu huyu aliyemtoa Dkt. Slaa bungeni ili agombee urais ilhali akijua kabisa huwezi kumshinda Rais wa CCM anapogombea muhula wa pili. Lengo la Mbowe lilikuwa ni kupunguza nguvu ya Dr Slaa kwani umaarufu wake aliujengea zaidi bungeni.

Niseme tu kwa kifupi, Mbowe na hata Zitto Kabwe wanaweza kuwa ni marafiki " wazuri" wa Dr Magufuli kuliko Ndugai na Musukuma.

Maendeleo hayana vyama!
Tatizo Mbowe ana marafiki wawili tuu.
Lucy Mukya na ruzuku
 
Kama kuna ka ukweli fulani hivi ukiunganisha dots fulani
Ila dots zimekuwa nyingi ndizo zinazofanya Habari hii iwe parl fulani hivi
 
Back
Top Bottom