Kisheria nani ana mamlaka ya kuwaetua Wakurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa, Wilaya na Miji?

Jamaa anatamani hata ateue mabalozi wa nyumba kumi.
It is very true.

Jamaa ameamua kuendesha nchi kwa staili ya ONE MAN SHOW.

Katiba ya nchi na sheria mbalimbali za nchi zishawekwa kapuni.

Hebu nitoe mifano michache tu ili tupate picha namna gani nchi ambavyo haiendeshwi tena kwa misingi ya sheria.

Jamaa alimpendekeza yule mdada kada mkubwa wa Chama chake akakalie kigoda kule jumba la kutunga sheria kule Dom na kesho yake akapita kwa kishindo kukalia kigoda kule Dom!

Matokeo yake hiko chombo kimeondokana kabisa na kuwa chombo cha kuwakilisha wananchi na badala yake kimegeuka kuwa vikao vya NEC.......

Jamaa akatangaza hadharani kuvipiga marufuku vyama vyote vya siasa vya upinzani visifanye shughuli zozote za siasa hadi 2020,lakini akatoa 'ruksa' kwa chama chake kuendelea kufanya shughuli za kisiasa na Jeshi la Polisi lisiwabughuzi na Jeshi la Polisi limeitii amri hiyo bila kujali kuwa insisigina Katiba ya nchi..........

Tusije shangaa before 2020 jamaa akawa tayari keshairejesha hii nchi kwenye single party system...

Let us wait and see. Kwa Magu anything can happen.
 
Hapana, Wakurugenzi wanateuliwa na Waziri mwenye dhamana ya Serikali za Mitaa. Zamani Waziri mwenye dhamana hiyo alikuwa ni Waziri Mkuu kwa sababu ilikuwa ikiitwa Ofisi ya Waziri Mkuu - TAMISEMI. Kwa sasa, Rais ameiondoa chini ya Waziri Mkuu na ameipeleka Ofisini kwake na inaitwa Ofis ya Rais - TAMISEMI. Tafsiri yake ni kwamba Rais ndiye mwenye dhamana ya Serikali za Mitaa na sio Waziri Mkuu tena. Hivyo, Rais ambaye ni mwenye dhaman ya TAMISEMI ndo anapaswa kuteua Wakurugenzi. Nawasilisha wakuu!!!
Unaweza kuwa uko sawa, lakini ebu mtu yeyote atuwekee ushahidi wa maandishi au kifungu cha kanuni kinachompa Rais mamlaka ya kuwateua, maana haitoshi tu wizara ikiwekwa chini ya ofisi ya Rais basi Rais anafanya anavyotaka bila kuwepo maelekezo ya kimaandishi.
Maana kama ndiyo hivyo kuna siku Rais ataweka wizara ya mambo ya ndani na wizara ya elimu chini ya ofisi yake kisha akateua ma RPC na maOCD na maofisa elimu wa mikoa na wilaya na hata maheadmaster wa shule tubaki kuroroma tu na kusema wizara ziko chini ya ofisi yake.
 
Kila kitu ccm kinawezekana.
It is very true.

Kwa CCM hata jambo ambalo utaliona ni IMPOSSIBLE kwao watalifanya kuwa POSSIBLE....

Ndiyo maana hata hili la kuteua more than 90% kwenye nafasi nyeti za DED kuwa ni makada wa CCM nalo limewezekana!
 
Hao ni vijana waliopigania chama wamekumbukwa. Hakuna cha uweledi wala ubobezi; kilichoangaliwa ni ukada
 
Mimi kwa uelewa wangu Mhe. Rais ana mamlaka ya kuwateua Wakurugenzi wa MAJIJIJI tu. Wakurugenzi wa Manispaa, Wilaya na Miji wanateuliwa na Mhe.Waziri Mkuu. Mimi nashauri kama ndiyo utaratibu basi wenzetu wa Utumishi wa Umma hawakumshauri Mhe.Rais kwa kufuata sheria, taratibu na kanuni kitu ambacho ni dosari kubwa sana. Lazima nchi iongozwe kwa kufuata sheria, taratibu na kanuni.
Hapo zaman wakati tamisemi iko chini ya ofiso ya waziri mkuu ilikua mteuzi n waziri mkuu lakn kwa sasa tamosemi iko chini ya ofc ya Rais so mteuzi wa nafasi hzo ni Rais
 
Hapo zaman wakati tamisemi iko chini ya ofiso ya waziri mkuu ilikua mteuzi n waziri mkuu lakn kwa sasa tamosemi iko chini ya ofc ya Rais so mteuzi wa nafasi hzo ni Rais
Kwahiyo siku akiweka wizara ya mambo ya ndani ktk ofisi ya raisi basi Ma Rpc, OcD atawateua yeye pia?
 
Hapana, Wakurugenzi wanateuliwa na Waziri mwenye dhamana ya Serikali za Mitaa. Zamani Waziri mwenye dhamana hiyo alikuwa ni Waziri Mkuu kwa sababu ilikuwa ikiitwa Ofisi ya Waziri Mkuu - TAMISEMI. Kwa sasa, Rais ameiondoa chini ya Waziri Mkuu na ameipeleka Ofisini kwake na inaitwa Ofis ya Rais - TAMISEMI. Tafsiri yake ni kwamba Rais ndiye mwenye dhamana ya Serikali za Mitaa na sio Waziri Mkuu tena. Hivyo, Rais ambaye ni mwenye dhaman ya TAMISEMI ndo anapaswa kuteua Wakurugenzi. Nawasilisha wakuu!!!
Hawatakuelewa mkuu.....ila ndo ukweli

wanajifanya hawaioni hii comment yako kwa sababu wana majibu yao kichwani
 
Hapana, Wakurugenzi wanateuliwa na Waziri mwenye dhamana ya Serikali za Mitaa. Zamani Waziri mwenye dhamana hiyo alikuwa ni Waziri Mkuu kwa sababu ilikuwa ikiitwa Ofisi ya Waziri Mkuu - TAMISEMI. Kwa sasa, Rais ameiondoa chini ya Waziri Mkuu na ameipeleka Ofisini kwake na inaitwa Ofis ya Rais - TAMISEMI. Tafsiri yake ni kwamba Rais ndiye mwenye dhamana ya Serikali za Mitaa na sio Waziri Mkuu tena. Hivyo, Rais ambaye ni mwenye dhaman ya TAMISEMI ndo anapaswa kuteua Wakurugenzi. Nawasilisha wakuu!!!
Sio sahihi hoja hii, wakurugenzi wa halmashauri za miji na wilaya wanateuliwa na Waziri mwenye dhamana chini ya Sheria namba 7 na 8 za 1982. Na Sheria pia hasa namba 8 inaeleza juu ya wakurugenzi wa majiji.
Mabadiliko ya miundo ya wizara hayabadili wala kufanya marekebisho katika Sheria za bunge, bali bunge lenyewe. Mimi sijaona marekebisho ya Sheria hizi yaliobadili mfumo wa uendeshaji wa hizi mamlaka nchini.

Sheria inamtaka huyo Waziri mwenye dhamana kwa kushirikiana na Rais kuteua wakurugenzi "in consultation with the President". Pamoja na hayo sioni shida katika watu walioteuliwa wala kuhoji uteuzi wake huenda isiwe sawasawa, watanzania tunataka maendeleo sio malumbano.
 
Jamani rais yupo sahihi. Serikali iliyopita tamisemi ilikuwa chini ya waziri mkuu. Ila kwa mabadiliko yaliyofanywa na JPM hiyo wizara kwa sasa ipo chini ya Ofisi ya Rais.
Tuache kulalamika kila kitu bila kuwa na data za uhakika.
 
Swali lako ungeliuliza hivi naomba kufahamishwa ni nani mwenye mamlaka ya kuteua wakurugenzi ingetosha kuliko maelezo marefu shutuma na lawama... baada ya mabadiliko ya wizara TAMISEMI iliondolewa chini ya ofisi ya waziri mkuu (hapo kabla wakurugenzi wote walijibika kwa waziri mkuu) na kupelekwa ofisi ya Rais kwa hiyo hata uteuzi unafanywa na ofisi ya Rais
Mimi kwa uelewa wangu Mhe. Rais ana mamlaka ya kuwateua Wakurugenzi wa MAJIJIJI tu. Wakurugenzi wa Manispaa, Wilaya na Miji wanateuliwa na Mhe.Waziri Mkuu. Mimi nashauri kama ndiyo utaratibu basi wenzetu wa Utumishi wa Umma hawakumshauri Mhe.Rais kwa kufuata sheria, taratibu na kanuni kitu ambacho ni dosari kubwa sana. Lazima nchi iongozwe kwa kufuata sheria, taratibu na kanuni.
 
Jamani rais yupo sahihi. Serikali iliyopita tamisemi ilikuwa chini ya waziri mkuu. Ila kwa mabadiliko yaliyofanywa na JPM hiyo wizara kwa sasa ipo chini ya Ofisi ya Rais.
Tuache kulalamika kila kitu bila kuwa na data za uhakika.
Laws are not amended by implication (automatically)!
 
Mimi kwa uelewa wangu Mhe. Rais ana mamlaka ya kuwateua Wakurugenzi wa MAJIJIJI tu. Wakurugenzi wa Manispaa, Wilaya na Miji wanateuliwa na Mhe.Waziri Mkuu. Mimi nashauri kama ndiyo utaratibu basi wenzetu wa Utumishi wa Umma hawakumshauri Mhe.Rais kwa kufuata sheria, taratibu na kanuni kitu ambacho ni dosari kubwa sana. Lazima nchi iongozwe kwa kufuata sheria, taratibu na kanuni.
Bado una donge tu? Utapata kiharusi mkuu fanya kazj,watu wamesuateuliwa,ndio imetoka hiyo
 
Swali lako ungeliuliza hivi naomba kufahamishwa ni nani mwenye mamlaka ya kuteua wakurugenzi ingetosha kuliko maelezo marefu shutuma na lawama... baada ya mabadiliko ya wizara TAMISEMI iliondolewa chini ya ofisi ya waziri mkuu (hapo kabla wakurugenzi wote walijibika kwa waziri mkuu) na kupelekwa ofisi ya Rais kwa hiyo hata uteuzi unafanywa na ofisi ya Rais
Mabadiliko hayo yametokea lini mkuu, maana sikuwa na habari hiyo.
 
Hapana, Wakurugenzi wanateuliwa na Waziri mwenye dhamana ya Serikali za Mitaa. Zamani Waziri mwenye dhamana hiyo alikuwa ni Waziri Mkuu kwa sababu ilikuwa ikiitwa Ofisi ya Waziri Mkuu - TAMISEMI. Kwa sasa, Rais ameiondoa chini ya Waziri Mkuu na ameipeleka Ofisini kwake na inaitwa Ofis ya Rais - TAMISEMI. Tafsiri yake ni kwamba Rais ndiye mwenye dhamana ya Serikali za Mitaa na sio Waziri Mkuu tena. Hivyo, Rais ambaye ni mwenye dhaman ya TAMISEMI ndo anapaswa kuteua Wakurugenzi. Nawasilisha wakuu!!!
Uko sahihi Mkuu. Nadhani watu bado wanadhani iko chini ya Waziri Mkuu. Hoja yao ingekuja wakati Halmashauri inahamishiwa Ofisi ya Rais wangetakiwa kuliona hili mapema. All in All uchaguzi ulitakiwa kuzingatia zaidi ya Sheria ( Rais ndio mwenye dhamana), Kanuni na Taratibu zilitakiwa zifuatwe na kama hazikufuatwa basi it was/ is wrong na bado kuna nafasi ya kurudia mchakato pamoja ya kuwa inaweza waathiri waliochaguliwa lakini kwa sasa Taifa kwanza mbele, wao wapewe nafasi zinazowastahili.
 
Back
Top Bottom