Kisheria ikoje hii, tunaweza kuwa na magereza binafsi?

Ncha Kali

JF-Expert Member
Sep 19, 2019
14,501
26,997
Nimewaza tu, wala msinipuuze!

Pengine ni hizi changamoto za ajira, au pengine ni katika kuwaza uwekezaji ‘nje ya boksi’ kama tunavyohubiriwa. Basi nimepata kuwaza hii kama fursa, tupeane taratibu na miongozo ya kisheria.

Kama ilivyo kwenye huduma zingine za kijamii, mfano Afya, Elimu, Usafirishaji, Mawasiliano n.k kuna mashirika ya serikali na binafsi.

Na hata kwenye ulinzi kuna majeshi ya serikali na vikosi vya kampuni binafsi, lengo ni lile lile kutoa huduma katika ubora unaokidhi viwango tarajiwa.

Basi nimewaza upande wa magereza (jela), tunaweza kuwa na uwekezaji katika sekta hii (Private Prisons). Lengo ni kuleta ushindani na kuboresha huduma, mradi tupate miongozo kuhusu vigezo vya kuzingatia.

Kuhusu i namna kwa gani tutanufaika, hili linabaki siri kwa sasa. Itoshe tu kusema tutajiendesha kama asasi zingine zisizo za kiserikali, hivyo tutajipatia ujiko kutoka kwa wahisani!

Tutapokea wafungwa kutokana na hukumu halali za kimahakama zetu, pia tutakuwa na wanasheria ili kutoa msaada kwa wahitaji, wateja wetu pamoja na wengine.

Hii itasaidia kujenga ufahamu juu uraia, na kujiepusha na uvunjifu wa sheria.

Gereza ni kwa ajili ya kurekebisha tabia, hivyo pamoja na huduma bora kwa wafungwa ni lazima tuzingatie lengo mahsusi la uwepo wake.

Wafungwa watafundishwa kazi za uzalishaji kipindi watumikiapo vifungo vyao, hii itasaidia kuwapatia kipato cha kuendesha maisha na familia zao zisizo na hatia wakati na hata baada ya kifungo.

Wasalaamu,

Ncha Kali.
 
hii ni idea nzur lakn kutokana na chain of command hapa bongo nadhan ili kuwa na magereza binafsi basi itahitaji kuwa na vituo vya polis binafs, na mahakama binafsi.
 
Kwaiyo mzee baba mfungwa anaenda kufungwa alaf analipia au sio
 
Huduma za magereza zikiboreshwa zaweza kuchochea uharifu, umewaza hilo?

Vigezo na masharti kuzingatiwa, sheria za nchi ziko pale na mahakama zitatenda haki... hata kwenye kwenye uharifu sio kwa sababu ya ubora wa magereza.

Inawezekana!
 
Umewaza vizuri ila nasikia kuna gereza fulani huko daslamu lina cell zina hadhi ya ki V.I.P yaani huko unapiga usingizi kama uko nyumbani.. nadhani kwa hoja yako itawafanya watu wafanye uhalifu huku washaweka oder ya kuja kula bata kwenye gereza lako.
 
Hatuhitaji magereza binafsi ila viwanda vingi binafsi.

Anyway ni vigumu kuwa na gereza binafsi maana magereza mengi duniani huwa chini ya tawala za nchi husika ila unaweza kuwa na kampuni binafsi ya ulinzi itakayotoa huduma za kulinda wafungwa gerezani (baadhi ya nchi hufanya hivi).
 
Hatuhitaji magereza binafsi ila viwanda vingi binafsi.

Anyway ni vigumu kuwa na gereza binafsi maana magereza mengi duniani huwa chini ya tawala za nchi husika ila unaweza kuwa na kampuni binafsi ya ulinzi itakayotoa huduma za kulinda wafungwa gerezani (baadhi ya nchi hufanya hivi).

Hapa umenipa mwanga kiasi, niseme tu asante sana!
 
Umewaza vizuri ila nasikia kuna gereza fulani huko daslamu lina cell zina hadhi ya ki V.I.P yaani huko unapiga usingizi kama uko nyumbani.. nadhani kwa hoja yako itawafanya watu wafanye uhalifu huku washaweka oder ya kuja kula bata kwenye gereza lako.

 
Back
Top Bottom