Kisheria hakuna ndoa kwa kuishi na mwanamke/ mwanaume kwa miezi 6

Mgeni wa Jiji

JF-Expert Member
Jul 27, 2017
7,697
12,878
Habari wana JF

Leo naomba kuongelea au kuliwekea ufafanuzi jambo moja ambalo limekuwa likielezwa vibaya au kimakosa na watu wengi wengine wakiwa ni viongozi hadi wa kiserikali.

Suala hilo ni swala la je, ni ndoa kiserikali baada ya kuishi na mwanamke au mwanaume nyumba moja kama wapenzi?

Hili suala hata huku sio geni wapo waliolielezea ama kwenye uzi kamili au komenti katika uzi.

Jibu kwa swali hili ni kuwa HAKUNA NDOA kisa mmeishi nyumba moja na mwanaume au mwanamke kwa miezi sita au zaidi. Ndio HAKUNA NDOA.

Hili linaweza likakushitua kwani umeshawahi kusikia na hata kuaminishwa na viongozi wa kiserikali kama ustawi au dawati la jinsia na hata baadhi ya wabunge bungeni kwa nyakati tofauti (inashangaza sana).

Jambo ambalo huwa lipo baada ya kuishi kimahusiano katika nyumba moja kwa miezi sita au zaidi ni UWEPO WA FIKIRIO LA NDOA hii sio ndoa bali ni fikirio tu na fikirio hili halina nguvu ya ndoa.

Kwanini ni FIKIRIO LA NDOA na sio NDOA?, jibu ni rahisi kabisa. Swala hili ni fikirio kwani sio ndoa na kwavile watu hao wanaishi pamoja basi hujengeka fikra kuwa pengine wataoana.

Fikirio hili limewekwa mahususi kwa ajili ya kumlinda hasa mwanamke kwani mwanamke akiishi na mwanaume kwa muda huu kisha mwanaume akaoa mwanamke mwingine basi mwanamke huyu anao uwezo wa kushitaki na kudai fidia kwa kupotezewa muda (japo wote wanaweza kuwa wamepotezeana muda)

Fikiro hili la ndoa kamwe haliwezi kufanya kazi kama ndoa na mwanamke au mwanaume aliyepo kwenye hadhi ya FIKIRIO LA NDOA hawezi kudai maslahi ya ndoa hata mara moja akafanikiwa Mahakamani.

Sasa tupate ufahamu juu ya jambo ambalo huonesha uwepo wa ndoa halali.

Ndoa yoyote ili iwe ndoa halali Tanzania ni sharti.iwe imesajiliwa kwa msajili wa ndoa na kupewa cheti cha ndoa cha serikali, hapa nisisitize sio cheti cha kanisa lako au msikiti wako ni cheti cha serikali. Upo mtindo wa sasa unakuta taasisi ya kidini ina cheti chao hasa makanisa ya kiroho, rafiki hapa kuwa makini sana hakikisha unapata cheti cha serikali.

Ndoa ili iwe halali ni sharti ifungishwe na mtu aliyepewa mamlaka ya kufungisha ndoa. Hapa tufahamu kuwa sio kila kiongozo wa kidini anao uwezo wa kufungisha ndoa halali, hakikisha anayefungisha ndoa yenu anayo hayo mamlaka.

Kwa vile uzi huu sio kwa ajili ya kupima uhalali wa ndoa kisheria basi itoshe kuishia hapo juu ya swala hili.

Turudi kwenye jambo litakalokuonesha kuwa hapa kuna ndoa.

Kitu kitakachokuonesha na kuthibitisha uwepo wa ndoa kama nilivyosema ni cheti halali cha ndoa cha serikali.

Hivyo hata ndoa za kimila zinapaswa kusajiliwa kwa msajili wa ndoa mara baada ya kufungwa.

Kuna kasumba imejitokeza watu waliosogezana wakaanza kuishi pamoja kujiita wapo kwenye ndoa ya kimila, hakuna ndoa ya kimila ya hivyo na watu hao sio wana ndoa hata wakiishi miaka 20 pamoja.

Mwisho kabisa ndoa haiwi ndoa kwa muda mlioishi pamoja bali ndoa huwa ndoa baada ya kusajiliwa kwa msajili wa ndoa.

Ahsanteni na mafikirio mema ya hali zenu.
 
Inaamana jirani yako miezi 6 si anajua nyie ni wanandoa msio na cheti.
ikitokea lolote anasema nini wakati mmekaa zaidi ya miezi sita na kuendelea pika pakua.

Huyu ni mke au mume tu ingekuwa wiki ingekuwa jina lengine
 
Kwahiyo uwezo wako wa kufikiri umeishia hapo?
Kwanini Mkuu au kuna mwanamke hutaki ajue kuwa atakushitaki kwa kupa tarajio la ndoa kisha kumpotezea muda wake 😂😂. Nisamehe tu Mkuu ila nafanya japo huu wajibu mdogo kwa jamii
 
Unaweza kuongeza zaidi mkuu
Fikirio la Ndoa - Neno sahihi ni DHANA YA NDOA
Tafsiri ni kuwa watu wa nje watawaona hawa wanaoishi pamoja kuwa ni wanandoa isipokuwa kama wao wenyewe (WANANDOA) watapinga DHANA hiyo kuwa hawaishi kama wanandoa, yaani mfano kwa miaka yote waliyoishi pamoja labda wanapigana sana, hawalali chumba kimoja na kitanda kimoja nk

Dhana ya Ndoa huhesabika pale watt wanapoishi pamoja kama mke na mume kwa kipindi cha MIAKA 2 na kuendelea
 
  • Thanks
Reactions: _ID
Fikirio la Ndoa - Neno sahihi ni DHANA YA NDOA
Tafsiri ni kuwa watu wa nje watawaona hawa wanaoishi pamoja kuwa ni wanandoa isipokuwa kama wao wenyewe (WANANDOA) watapinga DHANA hiyo kuwa hawaishi kama wanandoa, yaani mfano kwa miaka yote waliyoishi pamoja labda wanapigana sana, hawalali chumba kimoja na kitanda kimoja nk

Dhana ya Ndoa huhesabika pale watt wanapoishi pamoja kama mke na mume kwa kipindi cha MIAKA 2 na kuendelea
Shukrani kwa kusahihisha Mkuu, barikiwa.
 
Fikirio la Ndoa - Neno sahihi ni DHANA YA NDOA
Tafsiri ni kuwa watu wa nje watawaona hawa wanaoishi pamoja kuwa ni wanandoa isipokuwa kama wao wenyewe (WANANDOA) watapinga DHANA hiyo kuwa hawaishi kama wanandoa, yaani mfano kwa miaka yote waliyoishi pamoja labda wanapigana sana, hawalali chumba kimoja na kitanda kimoja nk

Dhana ya Ndoa huhesabika pale watt wanapoishi pamoja kama mke na mume kwa kipindi cha MIAKA 2 na kuendelea
Sio Dhana ni Dhanio la ndoa.
 
Habari wana JF

Leo naomba kuongelea au kuliwekea ufafanuzi jambo moja ambalo limekuwa likielezwa vibaya au kimakosa na watu wengi wengine wakiwa ni viongozi hadi wa kiserikali.

Suala hilo ni swala la je, ni ndoa kiserikali baada ya kuishi na mwanamke au mwanaume nyumba moja kama wapenzi?

Hili suala hata huku sio geni wapo waliolielezea ama kwenye uzi kamili au komenti katika uzi.

Jibu kwa swali hili ni kuwa HAKUNA NDOA kisa mmeishi nyumba moja na mwanaume au mwanamke kwa miezi sita au zaidi. Ndio HAKUNA NDOA.

Hili linaweza likakushitua kwani umeshawahi kusikia na hata kuaminishwa na viongozi wa kiserikali kama ustawi au dawati la jinsia na hata baadhi ya wabunge bungeni kwa nyakati tofauti (inashangaza sana).

Jambo ambalo huwa lipo baada ya kuishi kimahusiano katika nyumba moja kwa miezi sita au zaidi ni UWEPO WA FIKIRIO LA NDOA hii sio ndoa bali ni fikirio tu na fikirio hili halina nguvu ya ndoa.

Kwanini ni FIKIRIO LA NDOA na sio NDOA?, jibu ni rahisi kabisa. Swala hili ni fikirio kwani sio ndoa na kwavile watu hao wanaishi pamoja basi hujengeka fikra kuwa pengine wataoana.

Fikirio hili limewekwa mahususi kwa ajili ya kumlinda hasa mwanamke kwani mwanamke akiishi na mwanaume kwa muda huu kisha mwanaume akaoa mwanamke mwingine basi mwanamke huyu anao uwezo wa kushitaki na kudai fidia kwa kupotezewa muda (japo wote wanaweza kuwa wamepotezeana muda)

Fikiro hili la ndoa kamwe haliwezi kufanya kazi kama ndoa na mwanamke au mwanaume aliyepo kwenye hadhi ya FIKIRIO LA NDOA hawezi kudai maslahi ya ndoa hata mara moja akafanikiwa Mahakamani.

Sasa tupate ufahamu juu ya jambo ambalo huonesha uwepo wa ndoa halali.

Ndoa yoyote ili iwe ndoa halali Tanzania ni sharti.iwe imesajiliwa kwa msajili wa ndoa na kupewa cheti cha ndoa cha serikali, hapa nisisitize sio cheti cha kanisa lako au msikiti wako ni cheti cha serikali. Upo mtindo wa sasa unakuta taasisi ya kidini ina cheti chao hasa makanisa ya kiroho, rafiki hapa kuwa makini sana hakikisha unapata cheti cha serikali.

Ndoa ili iwe halali ni sharti ifungishwe na mtu aliyepewa mamlaka ya kufungisha ndoa. Hapa tufahamu kuwa sio kila kiongozo wa kidini anao uwezo wa kufungisha ndoa halali, hakikisha anayefungisha ndoa yenu anayo hayo mamlaka.

Kwa vile uzi huu sio kwa ajili ya kupima uhalali wa ndoa kisheria basi itoshe kuishia hapo juu ya swala hili.

Turudi kwenye jambo litakalokuonesha kuwa hapa kuna ndoa.

Kitu kitakachokuonesha na kuthibitisha uwepo wa ndoa kama nilivyosema ni cheti halali cha ndoa cha serikali.

Hivyo hata ndoa za kimila zinapaswa kusajiliwa kwa msajili wa ndoa mara baada ya kufungwa.

Kuna kasumba imejitokeza watu waliosogezana wakaanza kuishi pamoja kujiita wapo kwenye ndoa ya kimila, hakuna ndoa ya kimila ya hivyo na watu hao sio wana ndoa hata wakiishi miaka 20 pamoja.

Mwisho kabisa ndoa haiwi ndoa kwa muda mlioishi pamoja bali ndoa huwa ndoa baada ya kusajiliwa kwa msajili wa ndoa.

Ahsanteni na mafikirio mema ya hali zenu.
Naomba kufahamu,ikiwa ulifunga ndoa ya serikali na katika cheti kuna kipengele cha ndoa ya mke mmoja au wengi,tick ikawekwa kwenye mke mmoja.Je,kama utahitaji kuongeza mke mwingine wa ndoa yaani ndoa ya wake wengi unafanya nini??

Thanks in advance!
 
In
Naomba kufahamu,ikiwa ulifunga ndoa ya serikali na katika cheti kuna kipengele cha ndoa ya mke mmoja au wengi,tick ikawekwa kwenye mke mmoja.Je,kama utahitaji kuongeza mke mwingine wa ndoa yaani ndoa ya wake wengi unafanya nini??

Thanks in advance!
Unaachana na huyo mkeo kwa talaka halafu unamuoa tena upya na kwenye cheti kipya unaacha lile neno huenda ikawa ya wake wengi
 
  • Thanks
Reactions: _ID
Mgeni ...ungejikalia kimya nani angejua wewe mjinga au usiyefahamu lolote juu ya ndoa au ungekuja kutaka kufahamu juu ya ndoa
 
Tatizo ni Kila mtu (+mgeni wa Jiji kujiona ni mwanasheria)...Ona sasa kituko kilichoandikwa humu.
 
Fikirio la Ndoa - Neno sahihi ni DHANA YA NDOA
Tafsiri ni kuwa watu wa nje watawaona hawa wanaoishi pamoja kuwa ni wanandoa isipokuwa kama wao wenyewe (WANANDOA) watapinga DHANA hiyo kuwa hawaishi kama wanandoa, yaani mfano kwa miaka yote waliyoishi pamoja labda wanapigana sana, hawalali chumba kimoja na kitanda kimoja nk

Dhana ya Ndoa huhesabika pale watt wanapoishi pamoja kama mke na mume kwa kipindi cha MIAKA 2 na kuendelea
Sawa
 
Habari wana JF

Leo naomba kuongelea au kuliwekea ufafanuzi jambo moja ambalo limekuwa likielezwa vibaya au kimakosa na watu wengi wengine wakiwa ni viongozi hadi wa kiserikali.

Suala hilo ni swala la je, ni ndoa kiserikali baada ya kuishi na mwanamke au mwanaume nyumba moja kama wapenzi?

Hili suala hata huku sio geni wapo waliolielezea ama kwenye uzi kamili au komenti katika uzi.

Jibu kwa swali hili ni kuwa HAKUNA NDOA kisa mmeishi nyumba moja na mwanaume au mwanamke kwa miezi sita au zaidi. Ndio HAKUNA NDOA.

Hili linaweza likakushitua kwani umeshawahi kusikia na hata kuaminishwa na viongozi wa kiserikali kama ustawi au dawati la jinsia na hata baadhi ya wabunge bungeni kwa nyakati tofauti (inashangaza sana).

Jambo ambalo huwa lipo baada ya kuishi kimahusiano katika nyumba moja kwa miezi sita au zaidi ni UWEPO WA FIKIRIO LA NDOA hii sio ndoa bali ni fikirio tu na fikirio hili halina nguvu ya ndoa.

Kwanini ni FIKIRIO LA NDOA na sio NDOA?, jibu ni rahisi kabisa. Swala hili ni fikirio kwani sio ndoa na kwavile watu hao wanaishi pamoja basi hujengeka fikra kuwa pengine wataoana.

Fikirio hili limewekwa mahususi kwa ajili ya kumlinda hasa mwanamke kwani mwanamke akiishi na mwanaume kwa muda huu kisha mwanaume akaoa mwanamke mwingine basi mwanamke huyu anao uwezo wa kushitaki na kudai fidia kwa kupotezewa muda (japo wote wanaweza kuwa wamepotezeana muda)

Fikiro hili la ndoa kamwe haliwezi kufanya kazi kama ndoa na mwanamke au mwanaume aliyepo kwenye hadhi ya FIKIRIO LA NDOA hawezi kudai maslahi ya ndoa hata mara moja akafanikiwa Mahakamani.

Sasa tupate ufahamu juu ya jambo ambalo huonesha uwepo wa ndoa halali.

Ndoa yoyote ili iwe ndoa halali Tanzania ni sharti.iwe imesajiliwa kwa msajili wa ndoa na kupewa cheti cha ndoa cha serikali, hapa nisisitize sio cheti cha kanisa lako au msikiti wako ni cheti cha serikali. Upo mtindo wa sasa unakuta taasisi ya kidini ina cheti chao hasa makanisa ya kiroho, rafiki hapa kuwa makini sana hakikisha unapata cheti cha serikali.

Ndoa ili iwe halali ni sharti ifungishwe na mtu aliyepewa mamlaka ya kufungisha ndoa. Hapa tufahamu kuwa sio kila kiongozo wa kidini anao uwezo wa kufungisha ndoa halali, hakikisha anayefungisha ndoa yenu anayo hayo mamlaka.

Kwa vile uzi huu sio kwa ajili ya kupima uhalali wa ndoa kisheria basi itoshe kuishia hapo juu ya swala hili.

Turudi kwenye jambo litakalokuonesha kuwa hapa kuna ndoa.

Kitu kitakachokuonesha na kuthibitisha uwepo wa ndoa kama nilivyosema ni cheti halali cha ndoa cha serikali.

Hivyo hata ndoa za kimila zinapaswa kusajiliwa kwa msajili wa ndoa mara baada ya kufungwa.

Kuna kasumba imejitokeza watu waliosogezana wakaanza kuishi pamoja kujiita wapo kwenye ndoa ya kimila, hakuna ndoa ya kimila ya hivyo na watu hao sio wana ndoa hata wakiishi miaka 20 pamoja.

Mwisho kabisa ndoa haiwi ndoa kwa muda mlioishi pamoja bali ndoa huwa ndoa baada ya kusajiliwa kwa msajili wa ndoa.

Ahsanteni na mafikirio mema ya hali zenu.
Dah hapa akili imevurugika kumbe mambo yalivyo!.
 
Habari wana JF

Leo naomba kuongelea au kuliwekea ufafanuzi jambo moja ambalo limekuwa likielezwa vibaya au kimakosa na watu wengi wengine wakiwa ni viongozi hadi wa kiserikali.

Suala hilo ni swala la je, ni ndoa kiserikali baada ya kuishi na mwanamke au mwanaume nyumba moja kama wapenzi?

Hili suala hata huku sio geni wapo waliolielezea ama kwenye uzi kamili au komenti katika uzi.

Jibu kwa swali hili ni kuwa HAKUNA NDOA kisa mmeishi nyumba moja na mwanaume au mwanamke kwa miezi sita au zaidi. Ndio HAKUNA NDOA.

Hili linaweza likakushitua kwani umeshawahi kusikia na hata kuaminishwa na viongozi wa kiserikali kama ustawi au dawati la jinsia na hata baadhi ya wabunge bungeni kwa nyakati tofauti (inashangaza sana).

Jambo ambalo huwa lipo baada ya kuishi kimahusiano katika nyumba moja kwa miezi sita au zaidi ni UWEPO WA FIKIRIO LA NDOA hii sio ndoa bali ni fikirio tu na fikirio hili halina nguvu ya ndoa.

Kwanini ni FIKIRIO LA NDOA na sio NDOA?, jibu ni rahisi kabisa. Swala hili ni fikirio kwani sio ndoa na kwavile watu hao wanaishi pamoja basi hujengeka fikra kuwa pengine wataoana.

Fikirio hili limewekwa mahususi kwa ajili ya kumlinda hasa mwanamke kwani mwanamke akiishi na mwanaume kwa muda huu kisha mwanaume akaoa mwanamke mwingine basi mwanamke huyu anao uwezo wa kushitaki na kudai fidia kwa kupotezewa muda (japo wote wanaweza kuwa wamepotezeana muda)

Fikiro hili la ndoa kamwe haliwezi kufanya kazi kama ndoa na mwanamke au mwanaume aliyepo kwenye hadhi ya FIKIRIO LA NDOA hawezi kudai maslahi ya ndoa hata mara moja akafanikiwa Mahakamani.

Sasa tupate ufahamu juu ya jambo ambalo huonesha uwepo wa ndoa halali.

Ndoa yoyote ili iwe ndoa halali Tanzania ni sharti.iwe imesajiliwa kwa msajili wa ndoa na kupewa cheti cha ndoa cha serikali, hapa nisisitize sio cheti cha kanisa lako au msikiti wako ni cheti cha serikali. Upo mtindo wa sasa unakuta taasisi ya kidini ina cheti chao hasa makanisa ya kiroho, rafiki hapa kuwa makini sana hakikisha unapata cheti cha serikali.

Ndoa ili iwe halali ni sharti ifungishwe na mtu aliyepewa mamlaka ya kufungisha ndoa. Hapa tufahamu kuwa sio kila kiongozo wa kidini anao uwezo wa kufungisha ndoa halali, hakikisha anayefungisha ndoa yenu anayo hayo mamlaka.

Kwa vile uzi huu sio kwa ajili ya kupima uhalali wa ndoa kisheria basi itoshe kuishia hapo juu ya swala hili.

Turudi kwenye jambo litakalokuonesha kuwa hapa kuna ndoa.

Kitu kitakachokuonesha na kuthibitisha uwepo wa ndoa kama nilivyosema ni cheti halali cha ndoa cha serikali.

Hivyo hata ndoa za kimila zinapaswa kusajiliwa kwa msajili wa ndoa mara baada ya kufungwa.

Kuna kasumba imejitokeza watu waliosogezana wakaanza kuishi pamoja kujiita wapo kwenye ndoa ya kimila, hakuna ndoa ya kimila ya hivyo na watu hao sio wana ndoa hata wakiishi miaka 20 pamoja.

Mwisho kabisa ndoa haiwi ndoa kwa muda mlioishi pamoja bali ndoa huwa ndoa baada ya kusajiliwa kwa msajili wa ndoa.

Ahsanteni na mafikirio mema ya hali zenu.
Sahihi kabisa! Tena sasa hivi watu wanalipa mahari na kujiita wanandoa,kitu ambacho sio sahihi, unaweza usilipe mahari mukafunga ndoa ikatambulika popote pale! Unaweza ukalipa Mahari musifunge ndoa,musitambulike popote pale! Kikubwa watu wafunge ndoa zitambulike kokote kule,sio kufunga ndoa zinazotambulika kijiji fulani tu.
 
9 Reactions
Reply
Back
Top Bottom