KISANDU-Tusifuate mkumbo tukomae kifikra.

Baba Clara

Member
May 10, 2011
94
27
Kuna watu bwana wanajifanya wapenzi wakuu wa vyama bila hata kujua mustakabali wa Taifa lao, Tanzania leo hii kuna magazeti mengi sana(hard newz) na yale ya udaku, mina zungumzia magazeti ya hard newz ambapo wanaojiona wanaharakati ndio hupenda kusoma na kuwadharau wanao soma magazeti ya udaku. ifahamike kuwa yapo magazeti ni mali za vyama, serikali na watu binafsi mfano ona magazeti haya kwa itikadi zake gazeti la UHURU(ccm), gazeti la FAHAMU(cuf ), Tanzania daima(itikadi ya cdm), HABARILEO(serikali), NIPASHE(mtu binafsi) na mengine mengi. Basi kuna watu sijui ni kwasababu ya ulimbukeni wa siasa, akikukuta unasoma gazeti fulani kisa si la chama fulani utaitwa msaliti, au ukiwa unasoma gazeti ambalo si la chama chochote kisa yeye halipendi basi hataki usome gazeti hilo kisa linabeba habari nyingi ama za chama fulani au za serikali, na ukikutwa unasoma gazeti la udaku utaonekana kirazaaaa kabisa na mwanasiasa duni. Nilichojifunza mimi hatuna uelewa wa vyombo vya habari na matumizi yake katika jamii kwa masuala mbalimbali, kama wewe uko chama fulani unawajibika kusoma magazeti yote ya vyama vingine ili ujue wanasema nini na wapi wanawahadaa wananchi ili utoe msimamo sahihi kwani si watu wote wana vyama, si wote wanapenda kusoma magazeti ya hardnewz mimi mdogo wangu hapendi kabisa kusikia magazeti hayo ila ukimwambia magazeti ya udaku stori zote utazipata na hayahaya ya udaku ndio yanayowabeba sana wanasiasa na kuwauuza kisiasa maana wanawake na vijana walio wengi hata watoto walio chini ya miaka 18 wanasoma sana,kunapo kuwa na habari ya kisiasa hata moja ina wika zaidi kuliko Hardnewz, nisawa na watu wengi wanapenda RADIO za FM kuliko za AM, ona Cloudsfm,timesfm n.k zinavyoweza kutoa habari kwa urais kuliko hata TBC radio. Tusifuate mkumbo hebu tukomae kifikra. KISANDU2015
 
Back
Top Bottom