green rajab
JF-Expert Member
- Oct 16, 2015
- 11,173
- 35,499
Niagazie na andazi moja au bajiaMiaka 5 iliopita nilipata tamaa ya kutafuta rupia lkn wkt naendelea nikaskia kuhusu mekyuri.
Bei ya mekyuri ilinishtua sana ilinipa tamaa ya kwenda kutafuta
Mekyuri inapatikana kwenye mapango ya nyoka wakubwa ili uipate ni lzm nyoka atoke nje
Nilikutana na mzee mmoja huko milima ya Usambara akasema ipo sehemu na alishatoa mwanzo akadhurumiwa na Dada mmoja wa Kenya kwahio Kama nataka twende lkn malipo ni mpk tutoe mzigo
Masharti unatakiwa usilale na mwanamke na usiage unaenda wapi. Nilitimiza masharti
Lkn kwasababu skua mzoefu na mazingira alitafutwa kijana mwengine tukaelezana akakubali na akasema ataingia yeye. Akaelezwa masharti akakubali.
Siku ikafika tukaenda eneo la tukio hakika panatisha Sana. Tulivyofika tulikuta jiwe kubwa lenye tundu kubwa kuzama ndani.
Mzee akakita fimbo pembeni zaidi ya pango Kisha akapaka dawa mdomo na kumwaga dawa eneo lile.
Alivyopiga mluzi tu ebwana bonge la nyoka mithiri ya tairi la trekta lile kubwa. Alivyotoka nyoka yule alifika kwenye ile fimbo akatulia.
Kijana akaambiwa ingia kachote mzigo tuondoke.
Jamaa akaingia zilivyopita dk 2 aisee mashine ikajikunjua ikawa inarudi kwenye pango na jamaa bado yupo ndani
Ilibaki story jamaa hajatoka tena tuliskia kelele kwa mbali sana
Tukaondoka na kufika nyumbani tukamkuta mke wake anasema jamaa kamuaga anaenda kutafuta mekyuri. Mzee akajua jamaa alivunja miiko.
Hakika tangu siku hio naogopa sana kila nkikumbuka tukio hilo
Utajiri ni mgumu aisee