1 litre of water = 1 kg
1 litre of mercury = 13.3 kg
Maarifa gani? Mbona wewe umeandika "Wanahangamia" au na wewe umekosa maarifa na je umehangamia!!!!😃😃
mimi nina story ya kweli kwenye milima ya morogoro (maeneo ya mikese ile ya kulia kama unaenda Moro). ni kweli na ya kusisimua sana. ila mpaka mwisho sikufanikiwa ila nilikuja kujua siri nyingi za mali za wakoloni katika milima ile. Unasemaje unaweza kuiweka youtube?. Ilikuwa jeuri yangu niaota ndoto nikamsimulia kaka mmoja Freedom Tommorrow akanipa tafsiri ya kweli na tafsiri ilinisaidia sana jinsi ya kuingia katika mapango marefu ila sikufanikiwa kama aliyenitafsiria ndoto alivyoniambia,Ungekuwa karibu ningekufanyia interview katika kipindi changu cha simulizi za maisha. YouTube
Hii stori ni nzuri mno.
Tuletee mkuu itutoe ushambaNitakuja na simulizi ya baba mwenye nyumba yangu bythen aliyetapeliwa hizi mambo
Mwaga stori hiyo mkuumimi nina story ya kweli kwenye milima ya morogoro (maeneo ya mikese ile ya kulia kama unaenda Moro). ni kweli na ya kusisimua sana. ila mpaka mwisho sikufanikiwa ila nilikuja kujua siri nyingi za mali za wakoloni katika milima ile. Unasemaje unaweza kuiweka youtube?. Ilikuwa jeuri yangu niaota ndoto nikamsimulia kaka mmoja Freedom Tommorrow akanipa tafsiri ya kweli na tafsiri ilinisaidia sana jinsi ya kuingia katika mapango marefu ila sikufanikiwa kama aliyenitafsiria ndoto alivyoniambia,
Kwanini uyo Jamaa hamkumwambia mashartiMiaka 5 iliopita nilipata tamaa ya kutafuta rupia lkn wkt naendelea nikaskia kuhusu mekyuri.
Bei ya mekyuri ilinishtua sana ilinipa tamaa ya kwenda kutafuta
Mekyuri inapatikana kwenye mapango ya nyoka wakubwa ili uipate ni lzm nyoka atoke nje
Nilikutana na mzee mmoja huko milima ya Usambara akasema ipo sehemu na alishatoa mwanzo akadhurumiwa na Dada mmoja wa Kenya kwahio Kama nataka twende lkn malipo ni mpk tutoe mzigo
Masharti unatakiwa usilale na mwanamke na usiage unaenda wapi. Nilitimiza masharti
Lkn kwasababu skua mzoefu na mazingira alitafutwa kijana mwengine tukaelezana akakubali na akasema ataingia yeye. Akaelezwa masharti akakubali.
Siku ikafika tukaenda eneo la tukio hakika panatisha Sana. Tulivyofika tulikuta jiwe kubwa lenye tundu kubwa kuzama ndani.
Mzee akakita fimbo pembeni zaidi ya pango Kisha akapaka dawa mdomo na kumwaga dawa eneo lile.
Alivyopiga mluzi tu ebwana bonge la nyoka mithiri ya tairi la trekta lile kubwa. Alivyotoka nyoka yule alifika kwenye ile fimbo akatulia.
Kijana akaambiwa ingia kachote mzigo tuondoke.
Jamaa akaingia zilivyopita dk 2 aisee mashine ikajikunjua ikawa inarudi kwenye pango na jamaa bado yupo ndani
Ilibaki story jamaa hajatoka tena tuliskia kelele kwa mbali sana
Tukaondoka na kufika nyumbani tukamkuta mke wake anasema jamaa kamuaga anaenda kutafuta mekyuri. Mzee akajua jamaa alivunja miiko.
Hakika tangu siku hio naogopa sana kila nkikumbuka tukio hilo
Utajiri ni mgumu aisee