Kisa cha Zuwena Ali

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,474
39,987
Moyo ulianza kunienda kwa kasi, viganja vilianza kulowa jasho, na koo lilinikauka nilipokuwa nikikata kona kuingia katika eneo la Hospitali ya Bombo, mjini Tanga. Moyo wangu ulikuwa umegubikwa na ubaridi utadhani alfajiri katika mji wa Makambako kule Iringa. Nilishikwa na huzuni, hofu, na nilihisi kuchanganyikiwa. Akili yangu ilikuwa ikinizunguka utadhani mkokoteni wa kisambaa. Nikifikiri mara milioni ni kitu gani ningekifanya tofauti kukwepa ukweli ambao ulikuwa unanikabili. Nilikuwa natembea kama akili zimeniruka nilipoingia katika geti za hospitali hiyo na hatimaye kwenye wodi ya kina mama. Nilikaribishwa hospitalini hapo na Nesi aliyevalia sare nyeupe na kikofia cheupe chenye mistari ya rangi ya hudhurungi.

“Tafadhali nifuate” Aliniambia Nesi Fatma Ally, ambaye alikuwa amevaa beji yenye jina lake. Walikuwa wananitarajia kwani Nesi Fatma aliniambia walikuta namba yangu ya simu na jina langu kwenye pochi ya mgonjwa.

Bila kufanya ajizi au kuuliza maswali nilimfuata kwa haraka huku miguu yangu nikiihisi kunitetema utadhani miti ya mianzi ipagwapo na upepo. Tuliingia katika Wodi namba tatu ambayo madirisha yake yaliangalia bahari ya ya Hindi. Vitanda vya wagonjwa vilipangwa kinadhifu na wodi nzima ilikuwa inang’ara kufuatia matengenezo ya hivi karibuni kutoka msaada wa serikali ya Ujerumani. Toka mbali niliweza kuona ngalawa na mitumbwi ikipita, wavuvi wakiendelea na uvuviw, na upeo wa mbali wa bahari hiyo niliweza kuona meli iliyotia nanga katika Gati ya Ras Kazone.

Sista Fatma (kama manesi wanavyoitwa) alinielekeza hadi kitanda namba 11 kilichokuwa kwenye kona. Nilisogea na moyo wangu nusura unitoke kwani mpenzi wangu wa moyoni, wa ubani wangu na aliyekuwa nuru ya maisha yangu alikuwa amelala chali akizungukwa na mipira na machine za kila aina zilizomsaidia kunusuru maisha yake.

“Mbona hamjamuweka kule chumba cha dharura jamni” Nilimuuliza dada Fatma huku donge limenikaba shingoni na sauti ya kutetemeka.

“Ndiko ametokea huko, na baada ya hali yake kutuwama ndo ameletwa huku, ni ghali sana kukaa huko na sisi hatukujua ni nani atamlipia” Alinijibu.

“Hivyo ina maana kama nikilipa bili anaweza kupewa uangalizi huo” Nilimuuliza huku nikishika mfuko wangu kushoto kuashiria kuwa pochi siyo tatizo.

“Swadakta, kaka hela inafanya miujiza hapa” bila haya wala kigugumizi alinijibu tena. Nikagundua kuwa hapo hapendwi mtu ila pochi tu. Nikafanya hima kuzungumza na Nesi na Daktari wa zamu, na baada ya nusu saa hivi Zuwena Zuberi Ali alihamishwa toka chumba cha jumla na kuwekwa katika chumba cha Uangalizi maalumu tena cha binafsi. Nilimuita Daktari wa Zamu na kwa aibu zangu zote za Kingoni, nikamkatia kitita cha shilingi elfu ishirini kuhakikisha kuwa Zuwena anapata “uangalizi maalumu”. Alinihakikishia itakuwa hivyo.

Niliingia na kukaa pembeni ya kitanda chake, alikuwa hana ufahamu wowote na alikuwa akipumua kwa mashine. Tumbo lake la ujauzito lilikuwa limekaa kama mlima wa Usambara. Sikujua kama alihisi uwepo wangu au la. Niliushuka mkono wake nikiukanda taratibu, machozi yalianza kunitoka nikikumbuka jinsi nilivyokutana na binti huyo wa Kitanga miezi karibu tisa iliyopita. Nesi aliondoka hapo chumbani akiniacha mimi na mpenzi wangu Zuwena. Nilizama katika dimbwi la mawazo na sala, nikimuomba Mungu amrejeshee uzima ili nikiri wazi pendo langu kwake. Katika dimbwi hilo la mawazo nilijikuta nimeanza safari ya kumbukumbu, ambayo barabara yake ilikuwa imenyoka kama barabara ya Uhuru ile iendayo Pangani ambayo inaigawa wilaya ya Tanga katika pande za Mashariki na Magharibi.

* * *

Niliwasili katika mji wa Tanga siku ya Ijumaa kwa basi la Zafanana nikitokea Arusha ambako ndiko nilikozaliwa na kukulia. Baada ya kuhitimu kozi yangu ya Uhasibu toka Chuo cha Uhasibu Mbeya nilipata kibarua katika Ofisi ya Mamlaka ya Mkonge kama Mhasibu Msaidizi Daraja la III. Ilikuwa ni mara yangu ya kwanza kufika Tanga. Nilikuwa na hamu ya kufika Tanga kuanza ajira yangu ya kwanza. Safari ilikuwa nzuri na kwa hakika abiria wote wengi wao wakiwa ni wafanyabiashara walikuwa wametulia muda mrefu wa safari. Wengi wao walikuwa wanafuatilia burudani ya muziki wa kikongo kwenye video iliyokuwa nyuma ya kiti cha dereva.

Tulipokuwa tunakaribia kufika stendi ya Basi nilianza kuagana na dada wa Kichotara ambaye alikuwa ameketi upande wangu wa kulia, dirishani. Tulifahamiana kwa masaa machache tangu apande basi pale Moshi. Katika safari nzima hatukuzungumza sana kwani muda mwingi yeye alikuwa amelala na mimi nilikuwa nikijisomea kitabu cha riwaya cha Ben R. Mtobwa – Tutarudi na Roho Zetu?. Tulipata nafasi ya kunywa chai pamoja pale Same na nilimkaribisha mlo wa mchana tulipofika Korogwe, lakini yeye alikataa alitaka nimuagizie tu nyama choma. Nilifanya hivyo.

Aliniambia kuwa yeye anaitwa Zuwena Zuberi Ali na alikuwa anarudi nyumbani kwao Tanga baada ya safari ya kibiashara toka Arusha na Moshi. Nilimuambia habari zangu kuwa na mimi ilikuwa ni mara ya kwanza kufika Tanga. Nilimuuliza habari za mji wa Tanga na hasa kuhusu majini na uchawi. Watu wa Tanga walikuwa wanasifika kwa fani hizo. Hakunipa maelezo mengi, lakini kila alipoongea nami uso wake uliangaza utadhani mbalamwezi.

“Utafikia wapi au hujui bado?” Aliniuliza.

“Sijui, labda kama kuna hoteli hapo karibu na stendi” Nilimjibu.

“Zipo hoteli nyingi tu karibu na stendi au nje kidogo” Alinijibu huku akiendelea kunitajia baadhi ya majina ya hoteli na mahali zilipo. Alitaja majina ya Guest House maarufu mjini hapo kama “Kwetu ni Kwao” na “Sisi kwa Sisi” ambazo zilikuwa zinamilikiwa na mfanyabiashara maarufu mjini hapo aitwaye Bw. Kindoroko (ndiye yule yule mwenye Hoteli ya Kindoroko ya Moshi karibu na tawi la Benki ya MNB)

Tulipofika kituoni nilichukua mizigo yangu na nilianza kuteremka. Nikatembea hadi upande wa pili wa stendi ambako kulikuwa na taxi nyingi zilizokuwa zinangojea wateja. Kabla sijaamua nipange taxi ipi, taxi moja wapo ya rangi ya kijani ilisogea karibu yangu. Ulipofunguliwa mlango wa abiria, Zuwena alikuwa ameketi na akaniashiria niingie.

“Mwanakijiji, njoo ntakupeleka kwenye Hoteli nzuri” Aliniambia

“Bajeti yangu mimi ni ndogo dada” Nilimuambia

“Usiwe na wasiwasi, siyo ghali sana na kwa vile utakaa kwa muda, bila shaka watakupa viwango vya chini vya malipo” Alinibu. Nilifikiri kwa sekunde kama kumi hivi na kuamua kuingia kwenye hilo gari.

Hoteli ya Baobab iko karibu kilomita kumi toka Tanga mjini pembeni mwa barabara ya Pangani. Hoteli hiyo iliyogusa ufukwe wa bahari ya Hindi ilikuwa ni ya kupendeza na iliyovutia watalii wengi. Binafsi sikupanga kufikia kwenye hoteli yenye hadhi kama hiyo. Zuweni alinitaka nisubiri kidogo ili aende kuangalia kama kuna chumba au la. Alisema yeye ni mfanyabiashara na hiyo siyo mara ya kwanza yeye kutafutia wageni wake mahali hapo. Alirudi na habari njema kuwa kuna chumba ambacho watakikodisha kwangu kwa bei nafuu kweli. Nilifurahi sana na kumshukuru. Zuwena alinisaidia kuingiza mizigo yangu katika chumba hicho kizuri kilichoangalia bahari ya Hindi. Hoteli yenyewe iliezekwa vigae na juu yake makuti. Kulikuwa na njia za sakafu hadi baharini na zilikuwa zimepambwa na magamba ya chaza (oyster shells). Tuliagana na mimi nilimshukuru sana na katika kumwonyesha shukrani yangu nilimkaribisha akipata nafasi kesho anitembelee tuweze kula chakula cha mchana pamoja. Alisita kidogo lakini kwa shingo upande alikubali.

Kesho yake jioni nikiwa nimetulia chumbani nikiangalie vichekesho vya televisheni ya Kenya nilijikuta naamshwa na mlio wa mlango ukigongwa. Nilipofungua mlango macho yangu nusura yanidondoke na taya langu nililizuia lisije gota sakafani. Nilidhani nimebahatika kutembelewa na malaika. Uzuri wa Zuwena ulikuwa wazi mbele yangu. Alivalia sketi fupi ya jeans iliyoonyesha umbo lake la namba nane. Alikuwa amevalia tisheti ya rangi nyeusi yenye maneno “Don’t Touch” kifuani. Alivalia mkufu wa dhahabu ulioning’inia vyema shingoni kwake na alimachisha na hereni za duara za dhahabu. Nywele zake nyeusi zilizojisokota zilionyesha kuwa huyu binti alichangiwa damu Aliziacha nywele zidondoke mabegani mwake.

“Ah.. Mwanakijiji mbona kama umeona mzuka” Alinizibua toka katika mawazo machafu yaliyonivamia sekunde hizo chache.

“Mzuka? Tuambiane ukweli mapema, hivi wewe ni jini au mwanadamu?” Nilimuuliza nikiwa nimeshikwa na kigugumizi cha ghafla.

“Inategemea jini ni mtu wa namna gani” Alinijibu huku akiniangusha tabasamu na kuzungusha macho yake kwa madaha. Nikajua mtoto wa kinyakyusa nimepatikana. Nilimkarisha ndani kwenye sebule ya chumba hicho. Tuliamua kuagiza chakula na kwa kweli sikuwa na hamu ya kutoka chumbani hapo. Watanga wasije kuniloga. Ilikuwa yapata saa saba na nusu hivi tulipomaliza kula na kuhamia kwenye sofa. Tukaanza kupiga soga za hapa na pale. Tukazidi kufahamiana na kuchekeshana. Baada ya kuzungumza kwa muda mrefu tukajikuta hatuna maneno mengi ili kuangaliana na kuchekeana. Kulikuwa na hali ya mahaba hewani na sote tulijua hilo. Swali lilikuwa ni nani arushe ndoana ya kwanza.

“Mbona unaniangalia sana kifuani” Bila ya kutegemea alinirushia hilo swali.

“Nimeipenda tisheti yako” Nilimwambia, nikijua kuwa nimemwongopea.

“Tisheti peke yake?” alinihoji.

“ah Zuwena jibu langu litanifanya nihukumiwe au niwekwe huru?” nilimuuliza kabla sijamjibu kiukweli.

“Inategemea na jibu lenyewe” aliniambia. Aliisema sentensi hiyo huku kwa bahati “mbaya” akijifanya kukaa vizuri, na pale pale akanipiga picha!

“Zuwena, napenda kukuangalia toka utosini hadi unyayo na kila ninachokiona ninakipenda” Nilimwambia. Nilihisi joto limeanza kunipanda na ashki isiyo kifani ikinivamia. Nilijizuia nilipokuwa nimeketi.

“Hata mimi napenda kukuangalia Mwanakijiji, wewe ni nadhifu sana na very handsome” Aliniambia huku akiinamisha kichwa chake kwa aibu. Nilisikia mbingu zimefunguka na pepo imenishukia. Nilijisogeza alipokaa. Aliniangalia na kutabasamu kidogo. Niliweka mkono wangu kwenye mapaja yake huku nikiyapapasa taratibu. Akayabana kwa ghafla. Nikasogea karibu zaidi. Nikamsogelea kumnong’oneza kitu. Nikamnong’oneza jambo na nilipomaliza kusema miguu yake ilikuwa imepanuliwa. Nilizungusha mkono wangu wa kulia mgongoni kwake nikamvutia karibu yangu na mkono wa kushoto ukiendelea kumpapasa. Tulianza kurushiana mabusu ya nguvu. Akauinua mguu wake wa kulia kuuweka juu ya meza ndogo. Mkono wangu wa kushoto ukaanza kumvinjari kwenye malango ya nyumba ya uanamke wake. Alikuwa ameanza kuloa. Nilianza kumcheze kwa taratibu na kwa ufundi huku nikimbusu.

Bila kufanya kuonyesha aibu sana alianza kuutumia mkono wake wa kulia kunifungua mkanda wangu. Akaiteremesha zipu yangu taratibu. Nilikuwa nimeshapata “mwamko” wa nguvu. Alianza kuingiza mkono wake ndani ya chupi yangu. Alizungusha kiganja cha mkono wake kwenye mtarimbo wangu. Nilisikia joto la vidole vyake laini. Pole pole alimchomoa mzee na akaanza kumchezea taratibu. Ilikuwa ni kuchezeana na kubusiana.

“Ah Mwanakijiji, natamani hii” Alisema huku akiashiria kwa kumtingisha mzee.

“Hata mimi natamani hii” Nilisema hivyo huku nikikichovya kidole cha kati katika kisima cha mapenzi yake. Aliruka kidogo na kuguna.

Niliinuka na kusimama mbele yake. Nikaanza kumchojoa chupi yake huku yeye mwenyewe akifungua zipu ya sketi yake. Nikaviteremsha vyote pamoja. Nilipokuwa nateremsha sketi yeye mwenyewe alivua tisheti yake na sidiria. La haula wa la kwata!! Huyu binti alikuwa ni mzuri na sikujua nilistahili kitu gani mimi kuwa naye hapo. Nikasimama mbele yake na yeye naye akaanza kuteremsha suruali yangu. Na mimi nikamaliza kwa kulitupilia mbali shati langu. Na kabla sijasema hili wala lile, Zuwena akanichukua mdomoni mwake na kuanza kuninyonya kiufundi huku akivingirisha ulimi wake.

“ah.. tamu sana hii” Nilimwambia huku nikilalama kimapenzi

Hakusema kitu (hakuweza kusema) aliniangalia na kwa macho yake nilijua alifurahia hilo. Alifanya hivyo kwa muda kidogo na nilipoona niko hatarini kushusha nikamwondoa pole pole. Akiwa bado amekaa kwenye sofa nilimsogeza kwenye kona na kupanua miguu yake.

“njoo baby njoo” alinialika.

Nilianza kumwingia taratibu na mara baada ya kuzama nilianza kumkatikia kama vile miye mwehu. Aliyajibu mapigo yangu tena kwa kuzungusha kiuno chake haraka zaidi yangu halafu anajirusha juu kukutana nami. Ilikuwa ni watu wawili waliopagawa. Nilimpa akanipa, hatukunyimana kitu. Nikaanza kumwingia kwa nguvu zaidi nikichomeka na kuchomoa. Zuwena alijibu hilo pia. Kwa karibu nusu saa tulipeana mahaba na mapenzi. Kama vile kulipuka kwa kibo na mawezi ndivyo sote tulijikuwa tunafika kileleni kwa pamoja. Kucha zake ndefu zilikita mgongoni mwangu huku tukijikamua kushusha nyege zetu. Yeye alikuwa ni mpiga kelele, kwani alipiga ukelele ambao hadi leo hii bado naukumbuka. Nikakaa nikiwa nimekumbatia kwenye sofa. Baada ya muda tulipitiwa na usingizi.

Tulipoamka jua lilikuwa limeanza kutua. Tukaenda kuoga maana tulikuwa tumelowa jasho.

“Zuwena Mpenzi” Nilimuita hivyo bila hata ya kufikiri. “Unataka kwenda kutembea ufukweni?” Nilimuuliza.

“Ndiyo” alinijibu. Baada ya kumaliza kuoga na kuvaa nguo nyepesi tukaamua kwenda kutembea ufukweni mwa bahari. Harufu ya maji ya chumvi ilitufikia na upepo mwanana ulikuwa ukitupepea huku tukiendelea kubarizi. Tulikuwa tumeshikana kiuno huku tukitomasana na kucheka. Roho zetu zilikuwa zimekutana. Giza kidogo lilipoanza kuingia tulikaa kando ya bahari tukisikiliza mlio wa mawimbi. Nilikuwa nimelala chali kwenye mchanga na Zuwena pembeni yangu. Tukaangalia nyota zikianza kuangaza. Hakukuwa na mtu yeyeto mwingine aliyebakia hapo ufukweni.

“Naona nitaipenda Tanga” Nilimwambia kwa sauti ya upole.

“Naona nimeanza kukupenda Mwanakijiji” Aliniambia. Nilimjibu na mimi pia nimeanza kumdondokea kimapenzi.

Zuwena akaja kukaa juu yangu, akaiteremsha taratibu kaptula yangu hadi maeneo kwenye miguu. Nilikuwa nimedinda tena. Na yeye akavua chupi yake na kuiacha ining’inie kwenye mguu mmoja. Akainama kunibusu huku mkono wake wa kushoto aiuongoza uume wangu kumwingia. Akajiteremsha taratibu hadi nilipozama ndani yake. Akaanza kukatika tena. Niliingiza mikono yangu chini ya shati lake na kuanza kumchezea matiti yake. Alinipa raha tena na safari hii ilikuwa ni zamu yangu kujibu mapigo yake. Tukaendelea kufanya mapenzi hadi yeye alipofika kilele, ndipo na mimi nikajiachia. Tukabaki tumekumbatiana hivyo huku tukifurahia upepo wa bahari ya Hindi.

Kwa mbali tuliona mtu mwenye tochi akija upande wetu. Tuliamka hapo na kuvaa nguo zetu na kuelekea hotelini. Tulikula chakula cha jioni pamoja. Kwenye saa tatu za usiku Zuwena aliondoka kurudi kwao.

* * *
Mapenzi yetu yaliendelea hivyo kwa muda wa miezi hiyo yote na siku za karibuni baada ya kugundua kuwa Zuwena ni mja mzito nilikuwa na hamu sana ya kukutana na familia yake. Wazazi wake nao walitaka wajue ni nani baba ya mtoto. Hakuwaambia ukweli mara moja alikuwa akiwazungusha zungusha. Tulikuabaliana aje kunichukua kunipeleka kwao maeneo ya New Nguvumali nikutane na wazazi wake. Niliona lolote litakalokuwa ni lazima tuweke penzi letu hadharani. Alikuwa anakaribia kujifungua na itakuwa ni jambo la maana kama atawaambia ukweli wazazi wake.

Siku moja kabla yake Zuwena alinipigia simu majira ya saa tatu za usiku huku akilia kwa nguvu. Aliniambia kuwa wazazi wake hawataki kukutana nami na wamemtaka avunje uhusiano wetu. Aliamua kuniambia ukweli kuwa yeye ni mtoto wa Shehe mmoja maarufu na tajiri sana wa Mkoa wa Tanga na hawakuwa tayari mtoto wao azae na Mkristu au kuolewa na Mkristu. Alikiri kuwa ananipenda na yuko tayari kuja kuishi nami na hayuko tayari kuacha wazazi wake kumchagulia mtu wa kumpenda. Nilijikuta na mimi naanza kulia. Nikamwambie asubiri kesho yake ili akipata nafasi niende kukutana pale Mariner’s Inn karibu na Kituo cha Polisi cha Central Chumbageni. Ukweli ni kuwa hakusubiri kwani usiku wa saa sita, alitoroka nyumbani kwao akipewa usafiri na rafiki zake wawili ili wamlete kwangu. Kwa bahati mbaya walipata ajali ya gari kwenye Mzunguko wa barabara ya Ishirini kwenye njia panda ya kwenye Makorola na ile inaelekea kiwanda cha Chuma. Marafiki zake wale wawili walikufa papo hapo. Zuwena alijeruhiwa vibaya na hali yake haikujulikana itakuwaje.

* * *

Mawazo yangu yalikatishwa na Daktari aliyeingia hapo akiwa na kibao cha kuandikia.

“Bwana Mwanakijiji?” Aliniuliza.

“Ndiyo Dokta” Nilimjibu nikisimama na kumpa mkono.

“Nina habari mbaya” Alianza kusema, “Ni bora uketi” aliniambia

Niliketi. Daktari aliniambia kuwa Zuwena alikuwa kwenye koma na hakuna uwezekano wa kuwa mzima tena. Pia aliniambia kuwa wakati wakifanya vipimo vyao waligundua kuwa hali ya mtoto bado ni mzima. Akaniambia kama niko tayari kuwapa ruhusa wamfanyie upasuaji wa C-Section ili wamtoe mtoto kwani alikuwa ameshafikia miezi karibu tisa. Niliwapa ruhusa. Moyo uliniuma nilishindwa kujizuia nikaanza kulia kama mtoto mdogo. Nilimsogelea Zuwena, na nilikiri pendo langu kwake milele na jinsi binti huyo wa kitanga alivyobadilisha maisha yangu. Niliendelea kubwabwaja kwa uchungu mkubwa.

“Zuwena Nakupenda sana na nitaendelea kukupenda” Nilimwambia.

Ghafla Zuwena alifumbua macho yake. Nikasogea karibu yake zaidi kusikia.

Na yeye akaninong’oneza kitu. Na baada ya kusema alichosema alifumba macho na kuvuta pumzi yake ya mwisho huko mashine zikianza kulia kuonyesha kuwa moyo wake umeanza kuacha mapigo. Alikimbizwa kwenye chumba cha upasuaji ambako mtoto wa kiume alizaliwa, siku mama yake anafariki. Wakati huo wazazi wa Zuwena na wenyewe ndiyo walikuwa wamefika tu pale.

Niliamka na bila hata ya kuwasalimia niliondoka hospitali ya Bombo huku nikilia na hasira ikiwa imenipanda kichwani. Niliingia ndani ya gari langu Peagout 504 Pick UP mali ya Mamlaka ya Mkonge na kuanza kukanyaga mafuta. Kama vile ilikuwa siku ya uchuro radio Tanzania walianza kupiga wimbo ule wa wana OSS wakiwa chini ya Marijani Bin Rajab;

Zuwena ningempata wapi ee
Zuwena mwingine sawa na yeye
Mtoto aliyeumbika mwenye umbo la kupendeza
Zuwena Zuwena kweli nampenda


Mwisho
 
kwa hiyo wewe kwa hasira zako hukwenda kumzika mpenzi wako????

Kumbuka hasira hasara.
 
inaelekea unaamini sana "love at first sight?" hadithi zako nyingi zinafundisha ukimuona mtu unampenda hapo hapo afu kesho yake mnafanya ngono!!!hii inatufundisha nini?
 
Huyu hana tofauti nayule mungwana anayehubiri ukimwi kwenye vyombo vyake vya habari wakati yeye ni mzinzi. Soma hadithi zake kujifurahisha nawala sio kupata fundisho.
 
Hivi mmesoma maana na kazi za fasihi? Mwanakijiji hadithi tamu sana.ila mkuu una mzaha?
But kachukue mwanao mkuu! he he he
 
inaelekea unaamini sana "love at first sight?" hadithi zako nyingi zinafundisha ukimuona mtu unampenda hapo hapo afu kesho yake mnafanya ngono!!!hii inatufundisha nini?


Inatufundisha kuwa ukimdondokea mtu kwa ghafla subiri, vinginevyo utaumizwa.
 
Huyu hana tofauti nayule mungwana anayehubiri ukimwi kwenye vyombo vyake vya habari wakati yeye ni mzinzi. Soma hadithi zake kujifurahisha nawala sio kupata fundisho.

Usipopata kujifunza katika hadithi zangu (inategemea kujifunza nini) basi umeshindwa kuburudika. Hakuna hadithi ambayo nimeandika isiyo na funzo. Wewe ukibakia kwenye suala ngono peke yake utamiss big picture.... Hebu jaribu kujiuliza Kisa cha Zuwena kinatuasa nini na kinatupa mafunzo gani katika maisha? Hiyo ndiyo kazi ya fasihi simulizi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom