Kisa cha Waziri na Nyuki

fired

Senior Member
Apr 4, 2021
151
310
UBISHI SI MZURI.

Waziri wa ufugaji katembelea mradi wa NYUKI, alipofika getini Mlinzi akamwambia haruhusiwi mtu kuingia kwa sasa. Waziri kwa hasira akamjibu Mlinzi kwani hujui mimi ni nani huku akimwonesha kitambulisho

Mlinzi kwa utii, akamwambia haya ingia mheshimiwa. Baada ya muda mfupi, Waziri alisikika akiita Mlinzi, Mlinzi NYUKI wamenivamia-Mlinzi AKAJIBU waoneshe kitambulisho huenda HAWAKUJUI WEWE NI NANI
 
Back
Top Bottom